Hatari niliyoiona mlima Iwambi - Mbalizi MBEYA

mzee wa kasumba

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
1,432
2,892
Kwa ambao wamebahatika kupita barabara hii ya Dar - Tunduma, ukitoka Mbeya kama unaelekea Mji mdogo wa Mbalizi kuna mahala huitwa IWAMBI.

Hapa unakutana na mteremko mkali sana ambao unashuka nao hadi mjini Mbalizi.

Ajali zimekuwa nyingi hususan kufeli breki kwa magari makubwa, kuacha njia na kuingia korongoni, ajali za kugongana uso kwa uso n.k.

Mamlaka zimeliona hilo na kulidhibiti katika mtindo huu ;-

Kwamba kwa sasa magari makubwa (ya mizigo) na mabasi madogo (daladala) hupeana zamu kupita eneo hilo kupanda na kushuka.

Yaani kuna muda yanaruhusiwa magari makubwa tu, na kuna muda huruhusiwa dala dala.

SHARAUTI sana kwa mamlaka husika.

ILA

Mtihani upo kwa madereva hawa wa daladala. Yaani muda wa kuruhusiwa kwao ukifika inakuwa ni fujo + wenge kiasi kwamba panaweza kusababishwa ajali nyingine baina yao wenyewe ama hata kwa watembea kwa miguu hasa wanaovuka vivukoni.

Yaani lile suala la kuachiwa kila mtu anataka kuwa wa kwanza kuwahi abiria kituo cha mbele, basi inakuwa tafarani.

Naiomba mamlaka nayo iliangalie hili, ingawa unaweza kuona ni la kawaida, ila madhara yanaweza kutokea hapo mbeleni.

Na huu ndio mwisho wa taarifa ya habari kutoka KASUMBA FM.
 
Au hata mabasi ya mikoani kutoka Dar yakiruhusiwa hufanya fujo sana njiani. Huo ndo ubongo wa ngozi nyeusi. Wanaoitukana hii ngozi wakati mwingine nawaona wako sawa.
Mtu gari yako ipo nyuma unataka harakaharaka iwe mbele, ukitegemea nini kama siyo kuhatarisha maisha ya watu?


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Ebwana ee kumbe hata mabasi makubwa ni hovyo
 
Hivi Tanroads hawawezi kweli kuupunguza ule mlima kwa kujenga daraja halafu lile bonde libakie tu kqma kivutio cha utalii!!!
Ha ha ha nimecheka.

Mawazo hayo hata wao waliwaza hivyo, lakini wakishajitwisha mtungi (vitu) wanasahau ama kupuuza kila kitu na kuona kila mtu jukumu hilo sio lake.
 
Kwa ambao wamebahatika kupita barabara hii ya Dar - Tunduma, ukitoka Mbeya kama unaelekea Mji mdogo wa Mbalizi kuna mahala huitwa IWAMBI.

Hapa unakutana na mteremko mkali sana ambao unashuka nao hadi mjini Mbalizi.

Ajali zimekuwa nyingi hususan kufeli breki kwa magari makubwa, kuacha njia na kuingia korongoni, ajali za kugongana uso kwa uso n.k.

Mamlaka zimeliona hilo na kulidhibiti katika mtindo huu ;-

Kwamba kwa sasa magari makubwa (ya mizigo) na mabasi madogo (daladala) hupeana zamu kupita eneo hilo kupanda na kushuka.

Yaani kuna muda yanaruhusiwa magari makubwa tu, na kuna muda huruhusiwa dala dala.

SHARAUTI sana kwa mamlaka husika.

ILA

Mtihani upo kwa madereva hawa wa daladala. Yaani muda wa kuruhusiwa kwao ukifika inakuwa ni fujo + wenge kiasi kwamba panaweza kusababishwa ajali nyingine baina yao wenyewe ama hata kwa watembea kwa miguu hasa wanaovuka vivukoni.

Yaani lile suala la kuachiwa kila mtu anataka kuwa wa kwanza kuwahi abiria kituo cha mbele, basi inakuwa tafarani.

Naiomba mamlaka nayo iliangalie hili, ingawa unaweza kuona ni la kawaida, ila madhara yanaweza kutokea hapo mbeleni.

Na huu ndio mwisho wa taarifa ya habari kutoka KASUMBA FM.
Nakubali sana uandishi wako. Kumbe kuna muda unaandika point

Haya
Sharaut kwako

mzee wa kasumba
 
Kuna siku daladala ziligongana,konda alitoka mbio huku damu zinatiririka.

Chanzo Cha ajali ni vurugu za kuwahi abiria gari zikisharuhusiwa.

Nadhani hii ya magari kwenda kwa zamu imepunguza tatizo ila imezalisha tena tatizo jingine.

Sometimes daladala zinaruhusiwa pale iwambi stand zishuke,huku upande mwingine maroli yanakuwa bado hayajaisha, yanapanda mlima.
Na Mara nyingine daladala zinaruhusiwa mbalizi,zinakuja overtake Lori zinazopanda taratibu.
Ni hatari Sana.

Nature ya eneo lenyewe ,lina balaa miaka na miaka.
Kwa kweli inabidi daraja lijengwe..sijui watajengaje ila wajenge,
Lile eneo linamwaga mno damu za watu.
 
Kuna siku daladala ziligongana,konda alitoka mbio huku damu zinatiririka.

Chanzo Cha ajali ni vurugu za kuwahi abiria gari zikisharuhusiwa.

Nadhani hii ya magari kwenda kwa zamu imepunguza tatizo ila imezalisha tena tatizo jingine.

Sometimes daladala zinaruhusiwa pale iwambi stand zishuke,huku upande mwingine maroli yanakuwa bado hayajaisha, yanapanda mlima.
Na Mara nyingine daladala zinaruhusiwa mbalizi,zinakuja overtake roli zinazopanda taratibu.
Ni hatari Sana.

Nature ya eneo lenyewe ,lina balaa miaka na miaka.
Kwa kweli inabidi daraja lijengwe..sijui watajengaje ila wajenge,
Lile eneo linamwaga mno damu za watu.
Karibu niko hapa kwa Ester😂😂
 
Kuna siku daladala ziligongana,konda alitoka mbio huku damu zinatiririka.

Chanzo Cha ajali ni vurugu za kuwahi abiria gari zikisharuhusiwa.

Nadhani hii ya magari kwenda kwa zamu imepunguza tatizo ila imezalisha tena tatizo jingine.

Sometimes daladala zinaruhusiwa pale iwambi stand zishuke,huku upande mwingine maroli yanakuwa bado hayajaisha, yanapanda mlima.
Na Mara nyingine daladala zinaruhusiwa mbalizi,zinakuja overtake roli zinazopanda taratibu.
Ni hatari Sana.

Nature ya eneo lenyewe ,lina balaa miaka na miaka.
Kwa kweli inabidi daraja lijengwe..sijui watajengaje ila wajenge,
Lile eneo linamwaga mno damu za watu.
Ha ha ha

Suala la watajengaje watajua wenyewe... Kinachotakiwa WAJENGE

Mbona daraja la treni limejengwa na linadumu kama chama fulani
 
Tuwekeeni hata picha basi tufanye utalii wa ndani kwa picha.
@Chaliifrancisco
images%20(2).jpg
 
Back
Top Bottom