hataki mpangaji mwenye gari

Jamani MadameX na Preta wengine wana magari hawana nyumba kwa kuwa ni ya bahati nasibu lakini pia huyo baba mwenye nyumba nae ana roho ya kwanini, ndo mpaka lift hataki nadhani huo ni uzuzu na hatokuja kununua gari kwa style hii.
 
Last edited by a moderator:
Hapa naona kuna hoja moja tete.

Kwanza, wenye nyumba nji hii wamekuwa kama Miungu watu...kuna watu wanadhani ukishajenga nyumba, ukamweka mpangajim ni kama 'mjakazi' wako...wanasahau kuwa mtu akishalipa kodi mkataba ni kuwa yeye ana nyumba anaitumia, wewe unatumia pesa zake? itakuwaje mpangaji akimwambia mwenye nyumba pesa alizompa asinywee bia? au asihonge nyumba ndogo?
Ni utamaduni ambao haujabalansi niseme....

Inabidi tufike mahali tujue na kujiuliza itakuwaje kila mtu akajenga nyumba.....kingine wenye nyumba tunachosahau ni kuwa mtu anapanga kwa sababu mbali mbali na sio kwamba yeye hana nyumba anayomiliki! Imagine wale wanaohama kikazi kutoka mji mmoja hadi mwingine..atajenga nyumba ngapi?

Kwa hili huyo mzee ni kilaza, ana kijiba cha roho na mbumbumbu wa maisha, Kuwa na gari siku hizi imekuwa kama basic need hasa kwa maeneo ya mijini kusiko na usafiri wa uhakika wa public. sasa huwezi kunipangisha nyumba then unambie nisiwe na gari kisa tu wewe huna?

Kuna mmoja anasema ni kuwatia wivu wa maendeleo sijui nini...kama ni hivyo basi mwenye nyumba naye angenunua gari yake ili akamilishe 'maendeleo'...maendeleo ni nini kwani hasa?
 
Kujenga nyumba ni project ya muda wakuu, Kama sheria inasema kila mwenye gari awe na nyumba mbona hata hii project ya magufuli haitahitajika kwa jinsi jam itakavyopungua!
Na mbona kama ni kusubiri kujenga ndo uwe na gari watu watakufa bila kuenjoy raha za mwenye gari mjini hapa?

Project ya nyumba nayo ngumu maana msingi tu unaweza kukulamba 4 million bado kunyanyua ukija roofing utalamba kati ya 5 million - 10 milion depending na aina ya bati, milango, madirisha, rangi, makaro ya maji machafu na uzio, hapo si itafika zaidi ya milioni 50 kabisa wakati gari unaweza pata la mpaka 4 million na kuendelea
 
huyo baba mwenye nyumba ana wivu tu....

Hivi kila mtu akijenga nani atakuwa mpangaji.....

Ila mie ningekuwa ni mpangajiwake walllhahiiiiiiii yaani gari yangu, kodi nimoe, nichangie buku buku za paking na ulinzi, visa anifanyie then nimpe lifti? Thubutuuuu atakuwa anaiona ikipaki tu....
 
Jamani MadameX na Preta wengine wana magari hawana nyumba kwa kuwa ni ya bahati nasibu lakini pia huyo baba mwenye nyumba nae ana roho ya kwanini, ndo mpaka lift hataki nadhani huo ni uzuzu na hatokuja kununua gari kwa style hii.

Sasa wote wamepata kwa bahati nasibu, basi kama mtu anaakili si unauza gari angalau ununue kiwanja.
 
kha nyumba za kupanga sina hamu, usinikumbushe hiyo kadhia! namshukuru MUNGU nilipofika, nilishawahi kupigana na mama mwenye nyumba, kila hausgal akija mgeni anamuondosha, mwenzie nina twins ilibidi niache kazi nilee, nilipokuja kujua ni yeye anafanya mahaugal hawakai, alijua kama samaki kwao ni baharini na kamwe hutawakuta ubungo ati wamekaa, lol!

safi sana, wenye nyumba wengine viazi sana....
 
Hapa naona kuna hoja moja tete.

Kwanza, wenye nyumba nji hii wamekuwa kama Miungu watu...kuna watu wanadhani ukishajenga nyumba, ukamweka mpangajim ni kama 'mjakazi' wako...wanasahau kuwa mtu akishalipa kodi mkataba ni kuwa yeye ana nyumba anaitumia, wewe unatumia pesa zake? itakuwaje mpangaji akimwambia mwenye nyumba pesa alizompa asinywee bia? au asihonge nyumba ndogo?
Ni utamaduni ambao haujabalansi niseme....

Inabidi tufike mahali tujue na kujiuliza itakuwaje kila mtu akajenga nyumba.....kingine wenye nyumba tunachosahau ni kuwa mtu anapanga kwa sababu mbali mbali na sio kwamba yeye hana nyumba anayomiliki! Imagine wale wanaohama kikazi kutoka mji mmoja hadi mwingine..atajenga nyumba ngapi?

Kwa hili huyo mzee ni kilaza, ana kijiba cha roho na mbumbumbu wa maisha, Kuwa na gari siku hizi imekuwa kama basic need hasa kwa maeneo ya mijini kusiko na usafiri wa uhakika wa public. sasa huwezi kunipangisha nyumba then unambie nisiwe na gari kisa tu wewe huna?

Kuna mmoja anasema ni kuwatia wivu wa maendeleo sijui nini...kama ni hivyo basi mwenye nyumba naye angenunua gari yake ili akamilishe 'maendeleo'...maendeleo ni nini kwani hasa?

nimekupenda bila hela shemeji.......
 
utanunuaje gari nyumba ya kupanga......?

Hiyo hai-justify mateso ya mwenye nyumba.
Wengine tumejenga tayari, ila tumehamishwa kikazi hadi mikoani, sasa mnataka uwe tunajenga kila mahali tunakohamishiwa?
 
Hiyo hai-justify mateso ya mwenye nyumba.
Wengine tumejenga tayari, ila tumehamishwa kikazi hadi mikoani, sasa mnataka uwe tunajenga kila mahali tunakohamishiwa?

Exactly one of my points mkuu Idimi....watu wanashangaza sana aisee...
 
Last edited by a moderator:
Jaman maisha ya dar es salaam bila gari ni tabu as kwenye proffessional nyingine smartness ni muhimu sana, kwa usafiri wa daladala unaweza kwenda kwenye meeting na shati chafu tena na clients ukaonekana kituko, gari hadi million 7 to 10 unapata, but kiwanja gan itapata kwa bei hiyo harakaharaka, huyo mwenye nyumba ana matatizo ya akili but gari sio luxury need ni essential ndo maana tumenunua mapema, but kujenga needs some times, I plan to build my house around 5-7 years pole pole sasa mda huo wote nikakae wapi kama nisipopoanga.
Also nina imani kujenga sio kazi, kazi ni kupata kiwanja kizuri kwenye location unayopendelea kuishi.

Jaman magari sio utajiri,
 
Mimi nina gari na nyumba na hata mashamba.Lakini ushauri huu ni wa bure kwa vijana.Si busara kununua gari wakati huna hata kibanda.Nunua kiwanja halafu anza hata na vyumba viwili.You look sensible.
weekend hii nimetembelea jamaa zangu mitaa fulani .........amepanga na ana gari.Hiyo nyumba ina wapangaji wanne na wote wana magari y akutembelea....nyumba ina uwanja mkubwa tu wa kutosha kupaki hayo magari...kwa bahati mbaya au nzuri mwenye nyumba hana gari,bado ni mtu wa makamo na anafanya kazi...siku za hivi karibuni ameanza vituko vinavyoonekana kama ni wivu...achilia mbali kwamba huwa hataki lift za hayo magari ata kama mvua zinanyesha na amewanyima hadi wanae kuyapanda.......tabia mpya nipamoja na kudai watu walipie parking 1000 kwa siku,mara mlinzi,mara anahatarishiwa usalama wa nyumba yake,mara anakosa hewa ya kutosha kil ammoja anapewa sababu..wakat mwingine anasikika akiponda utanunuaje gari nyumba y akupanga.........huyu mzee kijana wanamheshimu sana;tunajua yupo hap aJF pia..AJIREKEBISHE au aweke madai mezani.....na wenye nyumba hapa JF mshaurini mwenzenu..........
 
Samahani dada Preta, wewe ni mchaga?

Kaka zenu nasikia ndo huwa hawaoi kabla hawajajenga kwao na mjini, ni kweli?

hahaha Bigirita chezeya kulala gheto moja na mdingi? laana hiyo!!!! Yaani unanyooka hapa, dingi naye ananyooka chumba jirani? laana na nusu yake!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom