hata wao wakiwa wakubwa, watakuwa na tabia kama zenu! wazazi wetu maadili hamna! ukweli tuwaambie!!!

Excel

JF-Expert Member
Jul 8, 2011
19,744
10,074
wadau! mimi kwa kweli sipendi wala sipendezwi na hii tabia ya wazazi wetu kuwatukana matusi ya nguoni watoto!

yani utakuta mama mtu mzima kabisa na kanga yake kiunoni, anamporomoshea matusi maziiiiito mtoto mdogo, na hata kama asingekuwa mtoto mdogo, mzazi kuporomosha maneno machafu kama yale tena mbele ya kadamnasi si sahihi kabisa!

msishangae kabisa enyi wazazi, ndio maana watoto hao wakikua wanawapiga! na mpigwe tu! hii ni laana kwenu!

kiungo chako cha mwili unaki-quote mbele ya mtoto na kuki-refer kama tusi!!! si uungwana kabisa!! napinga hili kwa nguvu zangu zote!

pamoja na mitusi mingine mizito ya viungo vya mwili, utamkuta mzazi mtu mzima kabisa na akili zake, anamrefer mtoto wake na mbwa, mbuzi, kenge, kondoo, nguruwe, ngiri, pundamilia, nyati, fisi, nyoka, shetani na viumbe vingine vya ajabu!!

wazazi wa leo mnatisha!

jamani kama mko humu wenye tabia kama hizo, badilikeni na muwabadilisheni wenzenu pia huko mliko!

hii tabia inachosha!
 
ndugu hasa mabibi. umewahi ishi na bibi? huwa wanamatusi ya ajabu sana hawa watu
 
Jana nikitoka job nilipitia duka la dawa, ndani kulikuwa na mama na mtoto wake a boy of labda 12yrs. Kijana alikuwa amesahau kumeza dawa
Matusi yaliyoporomoshwa na hiyo mama kwa mtoto wake sikuamini. Mama akaanza kueleza mapungufu ya baba na kumlinganisha na mtoto.
Nikajiuliza nani mwenye kosa katika kuchagua baba.

My point muadhibu mtoto kwa kosa alilofanya itamjenga na atajifunza zaidi kuliko mzazi akatumia matusi
 
Back
Top Bottom