Harusi ndo harusi

Harusi ndo harusi

Hun

Senior Member
Joined
Oct 11, 2012
Posts
110
Reaction score
106
Wazima wadau.

Nimepigiwa simu jana na rafiki yangu analalamika kuhusu mume wake, labda kwa pamoja twaweza kumpa ushauri.

Mumewe alisimamia harusi jumamosi iliyopita ya rafiki yake, alikuwa kama maid, kulikuwa na maids wa kike pia. baada ya harusi katika pekenyua pekenyua yake ( si unajua wanawake nasi kwa kupekenyua simu tena), akakutana na msg mumewe anachat na yule maid waliopangwa wote, maongezi ya kuulizana siku ilikuwaje na nini sikukuu vipi na vitu kama hivyo.. bishosti kapanick anataka alianzishe kwa mume, nimemwambia atulizane asome mchezo utaendeleaje asiwe na papara labda ni maongezi ya kirafiki tu. nyie mnamshaurije
 
Mm nlidhani anataka kurudi kwao kumbe kulianzisha?!

Kama alimwachia mumewe asimamie harusi na wanawake wengine aendelee kuisoma namba tu wenzie wanasimamia mpk dudu
 
Simu ya mumewe aliichukua ya kazi gani, ndo akome kukagua simu ya mwenzie.

Mwambie akilianzisha ajue Maid anachukua nafasi yake
 
Mwambie mchezo huo asifanye hata kidogo namsihi sanaaaa,ni kitu kidogo lakini sio kizuri...
 
Hapo tu ndio wanawake mnakosea, siku akilianzisha ajue kwamba huyo maid ndio ataondoa stress za huyo mume wake.
 
"....Wengi wanaosimamia harusi pamoja ambao si mke na mume huishia kwenye mahusiano yasiyo rasmi...."
Mc Pilipili
 
Anatakiwa aongee na mume wake vizuri tu kwamba hizi communication sizielewi au sizipendi, kiupole tu.

Kama mume alikuwa na intention yoyote ile ataahirisha, ila asitumie ukali kabisa, atafute njia rahisi na ya upole ya kuzungumza na mumewe.

Asiache mpaka ifike mbali, afanye sasa.
 
watu wengine bwana kufunua funua tuuuu

ingekuwa mimi angekula kipigo kama cha rihanna kutoka kwa chris brown pumbafu sana
 
Back
Top Bottom