Kufuatia mlolongo wa matukia ya mwanandinga Haruna Moshi Boban kukataa kuichezea timu ya taifa U-23, dhidi ya Ushelisheli hivi karibuni kule Arusha imenikumbusha rekodi yake mbovu ya nidhamu.Si kule Simba tu toka nyakati hizo ila pia aliwahi kuingia na kopo la bia U/Taifa,kukacha mazoezi na hivi majuzi baada ya fainali ya Kagame Cup chap chap alibadili nguo akavaa jeans na T shirt na open shoes, baada ya kukabidhiwa medali akaivua pale pale mbele ya mgeni rasmi.Hii pia imenikubusha ni kwa nini Maximo aliwahi kusema hana nidhamu hata kidogo na humpiga chini jumla kuichazea Stars.