Mal...
Sitakupa jibu la moja kwa moja bali nitakuwekea hapa sehemu za mhadhara niliotoa State University of Zanzibar (SUZA) iwe muongozo wa kutuangazia tulikotoka hadi kufikia hali hii:
‘’Sheikh Ali Saleh alikuwa alikuwa Imam wa Msikiti wa Kitumbini wakati ule wa ukoloni bila woga wowote alikuwa akitoa khutba za hamasa katika sala ya Ijumaa akiunga mkono harakati za Waarabu wa Palestine dhidi ya uonevu wa Uingereza katika mgogoro wa Mashariki ya Kati.
Mgogoro huu ingawa ulikuwa mbali sana na Tanganyika lakini ulikuwa mmoja wa migogoro iliyokuwa ikiitatanisha serikali ya kikoloni kwa kuwa Waislam wa Tanganyika tayari walikuwa wakipamba Waingereza nchini na waliona shida ya Waislam Palestine ni shida yao pia.
Hali hii ikatoa picha kuwa ni tatizo lililowahusu zaidi Waislam kuliko watu wengine.
Lakini huu ulikuwa wakati wa Waingereza wanaitawala Tanganyika.
Uhuru ulipopatikana sera ya Tanganyika na baadae Tanzania ilikuwa kuwaunga mkono wote wanaodhulumiwa duniani pamoja na Wapelestina.
Katika kupinga dhulma kokote duniani Mwalimu Nyerere akawa ameacha historia kubwa sana.
Baada ya kifo cha Mwalimu Nyerere mwaka wa 1999, pametokea ndani ya Tanzania mabadiliko makubwa yaliyogusa sehemu nyingi katika misingi ambayo ndiyo ilikuwa utambulisho wa nchi.
Mojawapo ya mabadiliko haya makubwa ni msimamo wa Tanzania kwa Israel na tatizo la Wapelestina.
Tanzania imefungua ubalozi Israel baada ya kukata uhusiano na nchi hiyo mwaka wa 1967 baada ya Vita Vya Siku Sita kati ya Israel, Misri, Iraq, Syria, Jordan and Lebanon.
Tanzania imerudisha uhusiano na Wayahudi.
Amerika ni taifa la Kikristo na ni rafiki mkubwa wa Israel lau kama Wayahudi ndiyo waliomuua Yesu, ambae wao kama Wakristo wote duniani wanamuitikadi ni ‘’Mtoto wa Mungu.’’
Kwa Wamarekani Israel ni rafiki na mshirika wake si adui abadan.
Waamerika wana marafiki katika mataifa ya Kiislam kama vile walivyokuwa pia wana maadui wengi katika mataifa ya Kiislam.
Tanzania Ukristo umedhibiti vyema serikali na una nguvu sana katika nyanja zote kuanzia serikalini kwenyewe hadi ndani ya Bunge la Jamhuri ya Tanzania.
Idadi ya Waislam ndani ya Bunge la Tanzania ni ndogo kiasi inaogopwa hata kuelezwa.
Hii nguvu na ushawishi wa Ukristo ndani ya Bunge la Tanzania unaweza kuwa moja ya sababu ya kuona Tanzania imerudisha uhusiano na Israel na balozi wake kujifaharisha na kibandiko cha Kiyahudi pale alipokwenda kujitambulisha Israel.
Zitto Kabwe alipata kusema ndani ya Bunge kuwa:
''Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau.
Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.''
(Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19).
Zitto Kabwa hakurudi Bungeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.
Hiki ni kisa kingine kwa siku nyingine.
Kwa kuhitimisha napenda kusema kuwa katika historia ya Tanzania kuwaunga mkono Palestine siku zote anatajwa Julius Nyerere hakuna mwandishi yeyote aliyepata kumtaja Sheik Ali Saleh na kusema kuwa harakati hizi zilianza zamani sana na mtu aliyezisimamia alikuwa Sheikh Ali Saleh Imam wa Msikiti wa Kitumbini.