Harrier vs forester subaru

System ya brake ni failure.ndio maana zina ajali sana.Subaru ni fake.ndio maana hata kwenye WRC world rally championship wameanza kiziondoa.mbadala wake ameingia Ford focus.
 
Sitamshauri kwa sababu ya fuel consumption unless awe anataka power tu
====
comeon, mkuu napenda kukuambia kwamba natumia hiyo gari wala haitumii mafuta mengi. 11km/L ni kweli. wala usihofu kama unataka makubwa lazima uwe mkubwa. Sasa unataka anunue IST kwani ni demu?
 
Mhhh sijui sn magari bt Harrier is on a whole new level, level zake ni SUV, Subaru naona ni sedan, enewei mtu km mie mwonekano wa gari matters the most performance mara sijui spidi vya kazi gani Dar kwnyw foleni kila mahali
Subari ipi ambayo ni sedan
 
====
comeon, mkuu napenda kukuambia kwamba natumia hiyo gari wala haitumii mafuta mengi. 11km/L ni kweli. wala usihofu kama unataka makubwa lazima uwe mkubwa. Sasa unataka anunue IST kwani ni demu?

Kwanza siamini hiyo consumption rate yako, pili sijasema atumie ist wala gari yoyote ya cc chini ya 1500. Kama unaelewa ni kuwa nafananisha na gari ya cc 2000 hapa
 
Hapo kama bado unapenda ujana na unataka gari la kudumu na la familia pia basi nakushauri chukua Subaru Forester XTi(sio STi) hii ni full SUV na ina size kubwa mfano wa Rav4 hivi, hizi gari zinaaminika zaidi kwa performance, usalama kwenye ajali, size kubwa na pia utulivu barabarani.....pia zina ulaji wa kawaida wa mafuta hasa hasa 2.0 petrol na pia haziharibiki kirahisi....asikudanganye mtu kuwa Subaru zinakula sana mafuta ni wewe tu na utayochukua kama 2.0 au 2.5...mm nna subaru Forester sti mwaka wa 5 huu na nimebadilisha taa na matairi tu tena kwa kuigonga vingine vyote viko sawa
 
Mkuu Sti ina shida gani?
 
Ni kweli. Nina subaru toka mwaka 2010, watu wanashangaa bado iko bomba. Imepiga route ndefu mara kibao Tabora Tunduma. Mafuta na spare ndio bei juu. Hata hivyo, ukiweka spare , ndio utasahau kuharibika. Iimetulia barabarani iko stable sana na kukimbia ingawa wengi wanaangalia sura kuwa haivutii sana. Nyuma ( boot) pia ina nafasi kubwa kwa mizigo ya familia.
 
XTi inavutia mkuu

Hyo iko pimped na imeshushwa bumpers
 
STi iko chini pia...ila inavumilia kila kitu, unaweza fukia shimo na bado ukawa salama na sample yako na vitu vingine kama shock ups e.t.c ila utaacha bumper
Hivi subaru zote hua zina sauti ya Simba ? Namaanisha masuala mazima ya zile sounds nzito za kuvutia panapo exhaust pipe?
 
Hivi subaru zote hua zina sauti ya Simba ? Namaanisha masuala mazima ya zile sounds nzito za kuvutia panapo exhaust pipe?
Hapana mkuu, ile loudspeaker unafunga mwenyewe, inaitwa muffler kwa lugha nyepesi..... Subaru huwa hazina sauti kabisa, na inaweza washwa mbele yako hata usisikie kama imewashwa.....ndo maana nazipenda sana hizi gari maana zinakubali hali yoyote uliyonayo, kama unapenda ile sauti unafunga na inaitika kama hupendi unatoa na inakuwa silent balaa mno labda pale inapowasha radiator fan kupooza engine ndo utasikia inatoa sauti.....


Ila ukifunga muffler mkuu, ukiwasha tu linaweka heshima mkuu....pia ufunge na breather kwa ajili ya chafya na transmission performance
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…