Gorgeousmimi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2010
- 9,296
- 7,688
Habari za saa hizi marafiki,
Leo tuongelee kuhusu jinsi ya kujipenda na kuwa na furaha bila kutegemea watu wengine.
Ukiwa unajitegemea kifikra ndio mwanzo wa kujitambua na kutambua mahitaji na matarjio yako kutoka kwa watu wengine.Nikisema kujitambua namaanisha kujua nini kinachokufanya uwe nafuraha,kinachokukera na kukubughudhi,majonzi yako,malengo yako,mahitaji yako na matarajio yako.
Jaribu kutoka kwenye lile eneo ambalo upo comfortable na kumiliki fikra zako,kutimiza ndoto zako na kupigana kufikia malengo yako.
Usikubali kuburzwa kifikra na mtu mwengine usifanye kitu kwasababu fulani amefanya,fanya kitu kwasababu wewe umetaka kufanya hivo,wewe ndio muamuzi wa furaha yako,si kosa kuwa mbinafsi kwa minajili ya furaha yako."Timiza ndoto zako na simamia zile zinazokufanya wewe kuwa wewe"
Ishi kwa kujifunza vitu vipya kuhusu wewe na jifunze vilevile kutoka kwa wengine,furahia maisha na jenga uelewa wa kuwa unataka kuwa mtu wa aina gani na ujipende.Furaha ni jambo kubwa na fikra zako ndio zinazoamua na kutawala hilo.
Tatizo linalowakabili wengi ni kwamba tunafikiria sana yanayojiri sasa na si ya malengo yetu ya baadae.Ni vyema kufurahia maisha ya sasa na vilevile kujijenga kifikra kwa baadae.Mabadiliko yanaanza na wewe.Pigania kwaajili ya vitu vinavyokupa ubora vinavyokupa inspiration ya kuwa mtu unayetaraji kuwa.
Hakuna aliyekamilika lakini kuna mstari mwembamba kati ya kuukubali ukweli na kuishi maisha ya kufikirika yanayotupa furaha ya muda mfupi.Usiishi kwa majuto bali kupitia kwenye makosa yako na somo ulolipata kupitia hapo.
Kitu kimoja nimejifunza ni kwamba ni kawaida kuvutiwa na watu wanaofanana na wewe.Kama wewe umevurugwa,utavutiwa na walovurugwa,kama ni mtu bora utavutiwa na watu bora.Jipe nafasi ya improvement na utaona mabadiliko.Jenga ukaribu na watu ambao wanajitambua kifikra,watakuinspire wewe kuwa mtu bora.
Jipende na utambue thamani yako."Happiness starts within you"
Wasalaam gorgeousmimi
Leo tuongelee kuhusu jinsi ya kujipenda na kuwa na furaha bila kutegemea watu wengine.
Ukiwa unajitegemea kifikra ndio mwanzo wa kujitambua na kutambua mahitaji na matarjio yako kutoka kwa watu wengine.Nikisema kujitambua namaanisha kujua nini kinachokufanya uwe nafuraha,kinachokukera na kukubughudhi,majonzi yako,malengo yako,mahitaji yako na matarajio yako.
Jaribu kutoka kwenye lile eneo ambalo upo comfortable na kumiliki fikra zako,kutimiza ndoto zako na kupigana kufikia malengo yako.
Usikubali kuburzwa kifikra na mtu mwengine usifanye kitu kwasababu fulani amefanya,fanya kitu kwasababu wewe umetaka kufanya hivo,wewe ndio muamuzi wa furaha yako,si kosa kuwa mbinafsi kwa minajili ya furaha yako."Timiza ndoto zako na simamia zile zinazokufanya wewe kuwa wewe"
Ishi kwa kujifunza vitu vipya kuhusu wewe na jifunze vilevile kutoka kwa wengine,furahia maisha na jenga uelewa wa kuwa unataka kuwa mtu wa aina gani na ujipende.Furaha ni jambo kubwa na fikra zako ndio zinazoamua na kutawala hilo.
Tatizo linalowakabili wengi ni kwamba tunafikiria sana yanayojiri sasa na si ya malengo yetu ya baadae.Ni vyema kufurahia maisha ya sasa na vilevile kujijenga kifikra kwa baadae.Mabadiliko yanaanza na wewe.Pigania kwaajili ya vitu vinavyokupa ubora vinavyokupa inspiration ya kuwa mtu unayetaraji kuwa.
Hakuna aliyekamilika lakini kuna mstari mwembamba kati ya kuukubali ukweli na kuishi maisha ya kufikirika yanayotupa furaha ya muda mfupi.Usiishi kwa majuto bali kupitia kwenye makosa yako na somo ulolipata kupitia hapo.
Kitu kimoja nimejifunza ni kwamba ni kawaida kuvutiwa na watu wanaofanana na wewe.Kama wewe umevurugwa,utavutiwa na walovurugwa,kama ni mtu bora utavutiwa na watu bora.Jipe nafasi ya improvement na utaona mabadiliko.Jenga ukaribu na watu ambao wanajitambua kifikra,watakuinspire wewe kuwa mtu bora.
Jipende na utambue thamani yako."Happiness starts within you"
Wasalaam gorgeousmimi