Hapa ndo ninaposhindwa kumuelewa mwanamke

Daudi1

JF-Expert Member
Dec 14, 2013
8,774
8,661
Habari za weekend wapendwa, natumaini muwazima wa afya, naomba niende moja kwa moja kwenye lengo kuu kilichonisukuma kuongea hivyo ni huu mkanganyiko ninauona kwa hawa wanawake kwa kutokuwa na msimamo ambao sio wote ni baadhi lakin wengi wao....
Kuna jamaa yangu alikuwa na mpenz wake na Mimi nilimuita shemej kama kawaida japo sijawah kumuona live kutokana na umbali hivyo niliongea naye kwa simu tu walikuwa wanapendana na jamaa alitokea kumuelewa sana kwa kipind hicho mwanamke alikuwa na umri wa miaka 23 alikuwa chuo mwaka wa mwisho lengo lao ilikuwa mwanamke akimaliza wafanye process za ndoa lakin mwanamke alikuja kugeuka ghafla sijui nini kilimpata na jamaa alipojaribu kumuuliza hakuna na jibu lolote juu ya mabadiriko hayo,baadaye mwanamke akataka waachane huku akimrushia lawama nying jamaa kwamba hajui kuhandle Mara anamhisi na mwanamke mwingine hakuishia hapo akaonyesha kila aina ya dharau na kufikia hatua ya kumtamkia jamaa kuwa yeye ni mrembo na umri wake bado mdogo hivyo atapata mwanaume wa kuendana naye yaani mwanaume wa saizi yake.
Jamaa hakuna na namna ikabidi akubaliane na hali halisi maisha yakaendelea miaka ikasonga kumbe mwanamke alipata mwanaume mwingine mwanafunz mwenzake akampa mimba na kumtelekeza kwakuwa mwanamke amesomea kozi ya ualimu ameweza kumlea mtoto na maisha yanaendelea na jamaa yangu amepata mchumba na process zina endelea miez michache ijayo atafunga ndoa.
Sasa yule mwanamke amerudi na anataka jamaa warudiane na amuoe tena huku ajifanya anamahaba ya hali ya juu na msg nzuri za mapenzi huku akisema jamaa ni mwanaume Mwenye huruma sijui anayejal hapa ndo ninapopata mkanganyiko kwa hawa viumbe saizi ana mtoto ndo anataka jamaa amuoe Wakt hana alisema jamaa si wa hadhi yake, yaani malue lue, hivi kwanini wanawake mkipata wanaume sirias huwa mnawadharau? Kwanini?
 
Mmmmh!! Ni kutojitambua tu mkuu hamna lingine! Na umri nao unachangia!!
Kwa hiyo wakiwa na umri mdogo na akili huwa ndogo, sas basi mnapoachana msiseme nauli mbaya sasa saiz amesahau sema jamaa mpolee anamuangalia tu
 
Duuh, umenikumbusha Emmy wangu, tulikuwa vyuo tofauti tukaachana kisa masharobaro wa chuo, nikawachukia wadada wote wa chuo nikaoa form four leaver, wanawake wa chuo mabwege sana.
Dah pole sana kwa yaliyokukuta mkuu
 
Sasa yule mwanamke amerudi na anataka jamaa warudiane na amuoe tena huku ajifanya anamahaba ya hali ya juu na msg nzuri za mapenzi huku akisema jamaa ni mwanaume Mwenye huruma sijui anayejal hapa ndo ninapopata mkanganyiko kwa hawa viumbe saizi ana mtoto ndo anataka jamaa amuoe Wakt hana alisema jamaa si wa hadhi yake, yaani malue lue, hivi kwanini wanawake mkipata wanaume sirias huwa mnawadharau? Kwanini?
Mkuu hata mie hawa viumbe huwa siwaelewi kabisaaaaaa, ila huwa nafurahi sana kuwaona maana ni sinema tosha kwa sababu ya vituko vyao. Kwa hiyo kapigwa miti huko mpaka kazaa afu ndo anataka jamaa amuoe yaani alee damu ya mwanaume aliyemfanya akdharaulika!? ha ha haaaaaaa safi sana
 
Mkuu hata mie hawa viumbe huwa siwaelewi kabisaaaaaa, ila huwa nafurahi sana kuwaona maana ni sinema tosha kwa sababu ya vituko vyao. Kwa hiyo kapigwa miti huko mpaka kazaa afu ndo anataka jamaa amuoe yaani alee damu ya mwanaume aliyemfanya akdharaulika!? ha ha haaaaaaa safi sana
Mimi mwenyewe nashangaa saiz ndo amekuwa wa hadhi yake baada yakuwa na mtoto
 
Wanawake ndiyo watu wanaotumia sana neno "majuto ni mjukuu" mara nyingi wanajifunza baada ya kuumia.

Hongereni sana wanawake wa Duniani.
Kwa kweli hapo majuto ni mjukuu hawachelewi kwenda kuroga ili wapate nafasi
 
Back
Top Bottom