IsayaMwita
JF-Expert Member
- Mar 9, 2008
- 1,127
- 140
- Thread starter
- #21
Dark City kama huelewi tofauti ya success na failures sana itakuwa jambo lingine hlo.
Pia Msanii aliahidi kupitia na kurekebisha mikataba ya sekta ya madini. Kwa kweli mpaka leo mimi sijaelewa kabisa deliverables muhimu katika hili?
Suala la mpasuko wa kisiasa Zanzibar alilojifanya kuongea kwa hisia kali sana, mpaka leo ni kitendawili.
Suala la nyumba za serikali walizoziuza wakati wa Mkapa aliloahidi kulipitia mpaka leo anasuasua tu.
Hoja:
Kama ameshindwa kuyafanya yote hayo na mengineyo kipindi cha kwanza cha miaka mitaka (hadi mwakani) ikiwa ingekuwa ni vyema kwa ajili ya kugombea kipindi cha pili, sidhani kama kipindi cha atakuwa na changamoto yoyote muhimu kwani anajua hataweza kugombea kwa mujibu wa kikatiba.
Kumbukeni hata Chinga Mkapa alifanya madudu sana kipindi chake cha pili.
Kazi kwetu.
La muhimu ni wa Tanzania ni kuchagua wabunge wengi wa upinzani ili kuweza kulipa bunge guvu ya kuidhibiti serikali.
Nsololi;
Ndugu yangu jina lako ni jema sama kule kwetu jina lako lina maana kuwa mtoto aliyezaliwa pekee,
Ila nataka nikuamshe usingizini, najua wewe haujui mchezo mchafu wa CCM, wao ccm kwa sasa hawalali wanatafakari 2010 ila kwa sisi wapinzani hatujipangi tunaishia kupiga kelele huku tukuwapa mwanya ccm kujikosoa.