Hapa January Makamba alimlenga nani hasa ndani ya CCM?

Hapa January Makamba alimlenga nani hasa ndani ya CCM?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,147
Reaction score
48,389
Kuna maneno aliyachapisha January Makamba kuelekea uchaguzi wa kumpata mgombea Urais wa chama chake CCM kwa mwaka 2015 yamenitafakarisha Sana.

IMG-20251210-WA0032.jpg

Hivi haya maneno ya Makamba yalikuwa yamelilenga kundi lipi ndani ya chama chake?

Jee CCM kuna kundi ilikuwa likishinda uchaguzi wa mgombea Urais wa Chama hicho mwaka 2015 nchi yetu ingeendeshwa na walafi?

Hao walafi kwa Sasa bado wamo ndani ya CCM ama hawapo. Na kama wapo wana nafasi gani kwenye chama Chao au serikalini?

Jee hao walafi ndiyo walimfanya Makamba asiwe mgombea Ubunge kwa Jimbo la Bumbuli?
 
Watabiri wengine wanajua mfano wale mashaikh kusema mbona fulani sio wao ni ujumbe tosha kuwa ndani ya CCM kuna magenge na mengine uvujisha siri ili kutendeka.
 
Watabiri wengine wanajua mfano wale mashaikh kusema mbona fulani sio wao ni ujumbe tosha kuwa ndani ya CCM kuna magenge na mengine uvujisha siri ili kutendeka.
Hao "walafi" ni kina nani?
 
Kipindi hicho mzigo wa ufisadi alibebeshwa ENL pekee, CCM wote hadi January walikuwa wasafi.
 
Hao "walafi" ni kina nani?
Hapa alikuwa anamsema Lowassa. Unakumbuka kwenye uchaguzi wa 2015 alikuwa mtu muhimu kwenye kampeni za Magufuli? Halafu Magufuli hakumpa cheo alichokuwa anakitaka hivyo akaamua ku-post vile vikatuni vya nguruwe! Tangu hapo yeye na Magufuli zikawa haziiviani na baadae ndiyo wakaandika ile barua.
 
Tafuta clip za polepole.
Alianika kila kitu.

Unajua watu wanamlaumi Mange kimambi.
But trust me speech za polepole ndo zimewafumbua watz wengi kuhusu uhuni ulioko serikalini na CCM
Kimsingi polepole ndo amewafanya watu wengi wasiamini CCM.
CCM walipaswa wamsikilize.
Wao wakaamua kumteka.

Sasa oná. CCM kinaonekana Chama cha wahuni
 
Kuna maneno aliyachapisha January Makamba kuelekea uchaguzi wa kumpata mgombea Urais wa chama chake CCM kwa mwaka 2015 yamenitafakarisha Sana.

View attachment 3514031
Hivi haya maneno ya Makamba yalikuwa yamelilenga kundi lipi ndani ya chama chake?

Jee CCM kuna kundi ilikuwa likishinda uchaguzi wa mgombea Urais wa Chama hicho mwaka 2015 nchi yetu ingeendeshwa na walafi?

Hao walafi kwa Sasa bado wamo ndani ya CCM ama hawapo. Na kama wapo wana nafasi gani kwenye chama Chao au serikalini?

Jee hao walafi ndiyo walimfanya Makamba asiwe mgombea Ubunge kwa Jimbo la Bumbuli?

Makamba yupo USA kabla hata ya uchaguzi
 
Alikua anamlenga Lowassa, ila jamani EL sijui alikosea wapii? Sio kwa zigo lile la misumari,
Ilifikia hatua, CCM wote ni wasafi, mchafu pekee yake.
Niliumia sana, na nilikua nampenda yule mzee jamani.
Apumzike salama huko, ila wee kingmaker?? Mmmh sio kwa kumgeuka mwenzio, hadi uzao wake unaufutilia mbali, alikukosea nn yule mmsai?? Rostam alisema wazi siku ya msiba wa EL.

UWIIIIIII!! Urafiki wa kinafiki ni mbayaaa.
 
Hapa alikuwa anamsema Lowassa. Unakumbuka kwenye uchaguzi wa 2015 alikuwa mtu muhimu kwenye kampeni za Magufuli? Halafu Magufuli hakumpa cheo alichokuwa anakitaka hivyo akaamua ku-post vile vikatuni vya nguruwe! Tangu hapo yeye na Magufuli zikawa haziiviani na baadae ndiyo wakaandika ile barua.
Makamba alitaka awe PM? au.
 
Tafuta clip za polepole.
Alianika kila kitu.

Unajua watu wanamlaumi Mange kimambi.
But trust me speech za polepole ndo zimewafumbua watz wengi kuhusu uhuni ulioko serikalini na CCM
Kimsingi polepole ndo amewafanya watu wengi wasiamini CCM.
CCM walipaswa wamsikilize.
Wao wakaamua kumteka.

Sasa oná. CCM kinaonekana Chama cha wahuni
Ukweli huu.
Mange na vyama vya siasa vya upinzani vimehamasisha maandamo mara nyingi kwa miaka mingi havikupata muitikio wa MO29.
Polepole ndiyo alipandikiza ule moyo wa kijasiri na kizalendo wa GenZ.
Hii siyo kudogosha mchango wa Lissu, Heche, Mange , Maria Sarungi na Sativa. NRNE imesaidia pakubwa.
 
Pia kushindwa kwa CCM ya Sasa kuendana na hoja za zama hizi. Polepole mchango wake ni mkubwa sana kwenye harakati hizi za Gen Z.

Titicomb
 
Back
Top Bottom