Hapa Dodoma: Mambo ni moto!

Hapa Dodoma: Mambo ni moto!

Tunawajua wale wabunge wa CCM ambao hata kuchangia hawawezi hadi wakayatwike maji ya Pansiasi au Ilala. Wakijua tu wamo kwenye list ya wachangiaji wanakimbilia baa kwanza. Mbona wanajulikana hapa Dom. Ndiyo maana huwa wanaitikia ndiyoooo hata kwa vitu wasivyovijua. Mambo mengi huchangia.

Na bunge likiisha tu wabunge wa CCM mikono yao(viganja) hua inasugu itokanayo na kupiga meza kwa msukumo wa kilevi na umbumbu wa kuaina mambo,maana hawa hawana tofauti na mwanafunzi anaeimba ana ana anado....wakati akijibu maswai ya kuchagua,tehtehtehteh!! ccm oyeeeeeee
 
VUTA-NKUVUTE

Tunashukuru sana kwa taarifa hii yenye mvuto ya kwamba kabisa serikali legele ya ccm inahanya kwa hilo!
Mambo ya kulewa kwa vijana wabunge wa vyama pinzani isikupe tabu kamanda wangu kwani hakika wako makini zaidi ya uwatazamavyo!

Usisite ku2pa newz zaidi mara upatapo!

Sasa niko Dodoma 'kikazi' kwa shughuli za chama yaani CCM. Hapa Dodoma,pamoja na kufuatilia nyendo za Wabunge wa CCM,lakini pia tunazifuatilia nyendo za Wabunge wa upinzani hasa wa CHADEMA. Tumearifiwa hapa kuwa Wakili Msomi Tundu Antipas Mughway Lissu(Mbunge) ametua Dodoma na nyaraka mbalimbali zinazogusa 'skendo' za wenye nchi.

Katika pitapita zetu na kupitia taarifa na nyaraka,tumegundua kuwa Ofisi ya Spika wa Bunge haina amani na Wabunge wa CHADEMA. Hivyobasi,Ofisi ya Spika imeomba msaada wa Serikali-hasa wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali-Jaji na Wakili Msomi Fredrick Mwita Werema na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Uratibu na Bunge)-Ndugu William Lukuvi kudhibiti kombora lolote la CHADEMA. Pia,wabunge wengine wa upinzani wasiotokana na CHADEMA wanaandaliwa zawadi kama wakitoa msaada wa kiudhibiti.

Hapa Dodoma,habari kuu ni kuwafunga midomo Wabunge wa CHADEMA na wanaofanana nao,ili kulinda taswira ya Serikali ya CCM. Sifa kemkem zinamwagwa kwa Spika Anne Makinda na uongozi wa Bunge kwa ujumla kwa kupitisha kanuni mpya zitakazopunguza presha kwa kiti cha Spika na Serikali wakati wa kujadilina kupitisha Bajeti ya Serikali.Kimsingi,wapinzani wamejipanga na kupangika.Vivyo hivyo kwa Serikali na Wabunge wa chama tawala. Patakuwa padogo hapa Dodoma.Stay tuned!

Crazy observation: Wabunge wengi vijana hasa wa upinzani wanakunywa sana pombe jamani.Wajirekebishe.Wasipofanya hivyo,nitawaweka hapa majina na picha zao wakiwa chakari. Niko hapa karibu yao wakiwa wamelewa sana. Not good at all!

Kila kitu kitakachojiri hapa ambacho watanzania watapaswa kukijua,watakijua tena kwa haraka sana. Usiku mwema!

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam(sasa Dodoma)
 
Last edited by a moderator:
tunasubiri kwa hamu makombora ya Lissu na fichua fichua maouvu serikalini.
suala la kuuzwa kwa liliondo kwa waaarabu nalo nadhani lipo ndani.
Mze tupa tupa ubarikiwe kwa kukataa kwako kuwa mnafiki kama hao wengine.
 
Mkuu Rweye,tuko pamoja.Kufichaficha ni sawa na kuua

mmh navutiwa na hoja zako lakini hofu yangu haifichiki ukichukulia kwamba na wewe ni wa lumumba je huwezi kuwa sawa na maccm wengine?usijetuvika vilemba vya ukoka plse!
 
Last edited by a moderator:
Mchungeni Lem,a asije rudia aliyofanya UK

Hapa tupo tz na si uk.hayo hayatatusaidia kwa lolote sisi walalahoi.kama unachuki binafsi na lema uwe unampigia simu na kumwambia live na si kujakusemea humu jamvini.
 
Crazy observation: Wabunge wengi vijana hasa wa upinzani wanakunywa sana pombe jamani.Wajirekebishe.Wasipofanya hivyo,nitawaweka hapa majina na picha zao wakiwa chakari. Niko hapa karibu yao wakiwa wamelewa sana. Not good at all!

Kila kitu kitakachojiri hapa ambacho watanzania watapaswa kukijua,watakijua tena kwa haraka sana. Usiku mwema!

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam(sasa Dodoma)
thanks for updates (najua kabisa kuna kamba umeongezea hapo pia)

ila hapo kwenye red hapo ndio bbbaaaaaaaaaaaaaaaaasssssssssssssss!!!!

Niliwahi kumpigia simu marehemu Regia one day nikamwambia kwamba wenzake wameptiliza, wanajidhalilisha aisee,

i do drink lakini kuna vijana wanakunywa mno hadi wanakera, ni kama malimbukeni fulani
 
Tunawajua wale wabunge wa CCM ambao hata kuchangia hawawezi hadi wakayatwike maji ya Pansiasi au Ilala. Wakijua tu wamo kwenye list ya wachangiaji wanakimbilia baa kwanza. Mbona wanajulikana hapa Dom. Ndiyo maana huwa wanaitikia ndiyoooo hata kwa vitu wasivyovijua. Mambo mengi huchangia.
wewe watetee hao wa chama chenu, tumeanza kuelewa siri ya zomea zomea ya ccm,ccm bungeni, ulevi nooma!
 
wapo wabunge wanavuta bangi pia wasiira alishatoa ushuhuda
 
tunasubiri kwa hamu makombora ya Lissu na fichua fichua maouvu serikalini.
suala la kuuzwa kwa liliondo kwa waaarabu nalo nadhani lipo ndani.
Mze tupa tupa ubarikiwe kwa kukataa kwako kuwa mnafiki kama hao wengine.
lissu dawa yake ni werema na lukuvi, werema akizidiwa anaanza kufanya personal attack, chezea werema wewe!
 
Wanakunywa SAAANA Pombe. Kuna kifungu cha sheria za Bunge kinakataza wabunge kunywa Pombe nje ya ukumbi wa bunge na wakati usio wa vikao?
 
Watu wanaongelea pombe jamani kila mtu anastarehe yake, jambo la msingi ni hoja wanazowasilisha kwa niaba ya wananchi. Tukisema kila mtu aseme starehe yake kiukweli tutakimbiana hapa. Watanzania tusiwe personal, maslahi ya taifa mbele kwanza.
 
Makinda na mumewe Ndugai hawana jipya, Lisu mashine nyingine.
 
sasa mtu anaefanya personal attack bila kujenga hoja huyo ndio dawa au tatizo serikalini?
Lukuvi tunamjua taaluma yake na upeo wake kisiasa yeye atasema chochote kudhoofisha hoja
kwa kuleta hoja dhaifu
kwa werevu tunamwona kama msema chochote ili kulinda tumbo lake na sio maslahi ya taifa.
lissu dawa yake ni werema na lukuvi, werema akizidiwa anaanza kufanya personal attack, chezea werema wewe!
 
Kunywa pombe wanakunywa kipindi cha kazi bungeni au baada ya kazi? Kama huo ulevi unaingilia masaa ya kazi ni vema kuwalipua tu. Lakini kama ni baada ya masaa ya kazi.....mmmh bado wanahitaji ku-protect ethical behavior wakati waki-enjoy.
 
Sasa niko Dodoma 'kikazi' kwa shughuli za chama yaani CCM. Hapa Dodoma,pamoja na kufuatilia nyendo za Wabunge wa CCM,lakini pia tunazifuatilia nyendo za Wabunge wa upinzani hasa wa CHADEMA. Tumearifiwa hapa kuwa Wakili Msomi Tundu Antipas Mughway Lissu(Mbunge) ametua Dodoma na nyaraka mbalimbali zinazogusa 'skendo' za wenye nchi.

Katika pitapita zetu na kupitia taarifa na nyaraka,tumegundua kuwa Ofisi ya Spika wa Bunge haina amani na Wabunge wa CHADEMA. Hivyobasi,Ofisi ya Spika imeomba msaada wa Serikali-hasa wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali-Jaji na Wakili Msomi Fredrick Mwita Werema na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Uratibu na Bunge)-Ndugu William Lukuvi kudhibiti kombora lolote la CHADEMA. Pia,wabunge wengine wa upinzani wasiotokana na CHADEMA wanaandaliwa zawadi kama wakitoa msaada wa kiudhibiti.

Hapa Dodoma,habari kuu ni kuwafunga midomo Wabunge wa CHADEMA na wanaofanana nao,ili kulinda taswira ya Serikali ya CCM. Sifa kemkem zinamwagwa kwa Spika Anne Makinda na uongozi wa Bunge kwa ujumla kwa kupitisha kanuni mpya zitakazopunguza presha kwa kiti cha Spika na Serikali wakati wa kujadilina kupitisha Bajeti ya Serikali.Kimsingi,wapinzani wamejipanga na kupangika.Vivyo hivyo kwa Serikali na Wabunge wa chama tawala. Patakuwa padogo hapa Dodoma.Stay tuned!

Crazy observation: Wabunge wengi vijana hasa wa upinzani wanakunywa sana pombe jamani.Wajirekebishe.Wasipofanya hivyo,nitawaweka hapa majina na picha zao wakiwa chakari. Niko hapa karibu yao wakiwa wamelewa sana. Not good at all!

Kila kitu kitakachojiri hapa ambacho watanzania watapaswa kukijua,watakijua tena kwa haraka sana. Usiku mwema!

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam(sasa Dodoma)
wewe endelea kuficha uchi uone kama utazaa
 
Walevi sugu wanajulikana: Kigwangala, Sendeka, Maji marefu, Airo, Komba, Zungu, Kilango, Pinda, Lameck, Tyson, Ngeleja, werema, Maige, Majimarefu na yule shoga wa kigoma mjini...
 
Crazy observation: Wabunge wengi vijana hasa wa upinzani wanakunywa sana pombe jamani.Wajirekebishe.Wasipofanya hivyo,nitawaweka hapa majina na picha zao wakiwa chakari. Niko hapa karibu yao wakiwa wamelewa sana.

Vipi kwani tayari wameshachukua posho mapema hivi?

Hii ngoma Asprin hataiweza. Hakyanani tena!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom