papason
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 5,119
- 5,683
Mshambuliaji aliyetupiwa virago na klabu ya Simba, Hamisi Kiiza amesema timu hiyo ya Simba haiwezi kupata mafanikio hata kama itawasajili wachezaji wote wanaofanya vizuri Tanzania, na kumrudisha Mbwana Samatta, kwani tatizo kubwa lililopo Simba ni baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakianzisha na kuendekeza na chuki na wachezaji hasa wanaposema ukweli na kudai haki zao stahiki,”alisema Kiiza.
Nyota huyo raia wa Uganda, amekwenda mbali zaidi akisema timu ya Simba haitakuwa na mafanikio hadi baadhi ya viongozi wanaoendekeza chuki, fitna na migogoro isiyokuwa na tija kwa timu waondoke madarakani.
Kiiza alisema Simba ilikuwa na nafasi kubwa ya kubeba ubingwa msimu uliopita, lakini fitna za baadhi ya viongozi hao ndiyo ziliwaumiza sana wachezaji na kuwatoa kabisa kwenye ramani ingawa walikuwa na nafasi kubwa ya kufanya vizuri tangu wakiwa na kocha Dylan Kerr na Jackson Mayanja
Kiiza aliye enguliwa kwenye kikosi cha msimu ujao wa Ligi Kuu na uongozi wa timu hiyo, licha ya kushika nafasi ya pili kwa ufungaji bora kwa kufunga mabao 19, kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita alisema tatizo kubwa la Simba ni uongozi na siyo wachezaji wala makocha ambao wamekuwa wakibadilishwa kila msimu,
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, alisema ameshindwa kumalizia mkataba wake wa mwaka mmoja uliobaki Simba kwa sababu ya tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikimkabili ndani ya timu hiyo, kubwa ikiwa ni kuambiwa anaigawa timu na kwamba ana mapenzi na Yanga, alisema kama angekuwa anaihujumu timu hiyo asingefunga mabao 19 ambayo ndiyo yaliipa ushindi timu hiyo, hadi kuna wakati ikawa inaongoza ligi na kuziacha mbali Yanga na Azam.
Source: Gazeti la HabariLeo!
Nyota huyo raia wa Uganda, amekwenda mbali zaidi akisema timu ya Simba haitakuwa na mafanikio hadi baadhi ya viongozi wanaoendekeza chuki, fitna na migogoro isiyokuwa na tija kwa timu waondoke madarakani.
Kiiza alisema Simba ilikuwa na nafasi kubwa ya kubeba ubingwa msimu uliopita, lakini fitna za baadhi ya viongozi hao ndiyo ziliwaumiza sana wachezaji na kuwatoa kabisa kwenye ramani ingawa walikuwa na nafasi kubwa ya kufanya vizuri tangu wakiwa na kocha Dylan Kerr na Jackson Mayanja
Kiiza aliye enguliwa kwenye kikosi cha msimu ujao wa Ligi Kuu na uongozi wa timu hiyo, licha ya kushika nafasi ya pili kwa ufungaji bora kwa kufunga mabao 19, kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita alisema tatizo kubwa la Simba ni uongozi na siyo wachezaji wala makocha ambao wamekuwa wakibadilishwa kila msimu,
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, alisema ameshindwa kumalizia mkataba wake wa mwaka mmoja uliobaki Simba kwa sababu ya tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikimkabili ndani ya timu hiyo, kubwa ikiwa ni kuambiwa anaigawa timu na kwamba ana mapenzi na Yanga, alisema kama angekuwa anaihujumu timu hiyo asingefunga mabao 19 ambayo ndiyo yaliipa ushindi timu hiyo, hadi kuna wakati ikawa inaongoza ligi na kuziacha mbali Yanga na Azam.
Source: Gazeti la HabariLeo!