Wana JF,
Sioni sababu ya kuchekelea na kufurahia ziara kama hizi za Mkuu wetu wa kaya Bwana Mrisho Kiwete!
Namshangaa hata huyu Kigwangallah anayechekelea kama zuzu kwenye safari hii ya kwenda kujirusha majuu. Kigwangallah ana mgogoro na chama chake cha CCM, hasa kuhusiana na swala la Wachimbaji wadogo kwenye jimbo lake lakini pia kuna mgogoro wa Matumizi ya Fedha zilizotolewa na Mwekezaji wa Mgodi wa Dhahabu jimboni kwake!
Kiukweli ni kwamba kwa Rais yeyote aliye makini na kulingana na hali tete ya Bunge Maalumu la Katiba linaloendelea huko Dodoma, Bwana Kiwete hakupashwa kuwa nje ya nchi kwa sasa. Lakini kwa vile Kiwete ni mwoga na hana maamuzi magumu kwa kutumia akili zake mwenyewe, ameamua kukimbilia nje ya Nchi kuondoa Shinikizo la moyo baada ya kuongea ----- wakti wa kuzindua Bunge Maalumu la Katiba!!!
Sifa zote hizi ni kutaka kujifaragua tu aonekana kuna kitu anachofanya kwa Watanzania ilihali amejaa UNAFIKI MTUPU. Haitasadia lolote hata mkiwaleta WAWEKEZAJI KWA MAMILIONI kama KATIBA(ambayo ndo sheria mama) imekaa kimsegemnege au shagala baghala. Hii yote ni kutumia RASLIMALI ZA WATANGANYIKA VIBAYA lakini pia ni kuwadharau na kuwakebehi kwa kusababisha baadhi ya Wajumbe/Wabunge wa Bunge hilo kukosa VIKAO KWA KUWA KATIKA ZIARA HIYO AMBAYO HAINA UMUHIMU KWA SASA NA INGEWEZA KUSUBIRI BAADA YA KUPATA KATIBA NDIPO IFANYIKE!!!
Mwalimu Nyerere alikuwa kisema KUPANGA NI KUCHAGUA! Kiwete ameamua kupanga haya ili kujinufaisha mwenyewe na hayafanyi haya kwa manufaa ya Watangayika!
Wivu huo ....
anachomaanisha kigwangala ni kuwa kuna cku na yeye anaweza kuwa rais