Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,660
- 46,350
Hamas wametoboa mtumbiwi wa mabadiliko na kufunguliwa kwa mashariki ya kati. Mahusiano ambayo yalikuwa yameimarika na kufikia kukomaa kati ya Israel na mataifa ya Kiarabu kama Saudi Arabia sasa yametumbukia nyongo.
Mataifa ya mashariki ya kati ambayo yalikuwa yanaenda kwa kasi kukumbatia mahusiano imara zaidi na mabadiliko ya j
kimagharibi sasa watapunguza spidi na kuwa na kisirani wakiamini ndugu zao wanadhulimiwa vibaya sana na marafiki zao ambao siku zote wamejisema na kujitambulisha kama waliostaarabika zaidi.
Utawala wa Biden na Netanyahu haziivi sana kwa sababu japo hawakubaliani kabisa na kile walichokifanya Hamas bado wanamuona Netanyahu kama mtu aliyechanganyikwa asiyejua anafanya nini au anaelekea wapi. Wao wenyewe wana somo zuri jinsi walivyochanganyikwa baada ya September 11 na kufanya mambo mengine hovyo kwa kuwehuka na papara.
Upande mwingine wanamgambo magaidi kama Houthi wa Yemen na huko Syria wakichagizwa na Iran wamepata moto na wanachezea sharubu za Simba.
Hali si hali.
Mataifa ya mashariki ya kati ambayo yalikuwa yanaenda kwa kasi kukumbatia mahusiano imara zaidi na mabadiliko ya j
kimagharibi sasa watapunguza spidi na kuwa na kisirani wakiamini ndugu zao wanadhulimiwa vibaya sana na marafiki zao ambao siku zote wamejisema na kujitambulisha kama waliostaarabika zaidi.
Utawala wa Biden na Netanyahu haziivi sana kwa sababu japo hawakubaliani kabisa na kile walichokifanya Hamas bado wanamuona Netanyahu kama mtu aliyechanganyikwa asiyejua anafanya nini au anaelekea wapi. Wao wenyewe wana somo zuri jinsi walivyochanganyikwa baada ya September 11 na kufanya mambo mengine hovyo kwa kuwehuka na papara.
Upande mwingine wanamgambo magaidi kama Houthi wa Yemen na huko Syria wakichagizwa na Iran wamepata moto na wanachezea sharubu za Simba.
Hali si hali.