Hamad rashidi kutangaza chama kipya leo wawi

Hamad rashidi kutangaza chama kipya leo wawi

Kalunguine

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2010
Posts
2,543
Reaction score
134
Wanajamvi,aliyekuwa kaimu mwenyekiti wa wilaya ya ilemela wa CUF Hapa Mwanza,ambaye yuko kambi moja na HR na ambae mwishoni alhamisi ya wiki iliyopita amaetangaza kujiondoa CUF na wanachama zaidi ya 1222,amenidokeza muda sio mrefu kuwa wako pemba na wamepata mapokezi makubwa na kuwa katika mkutano wao na wananchi wa jimbo la wawi wanakusudia kutangaza rasmi chama chao kipya cha ADP ( hajaniambia kirefu chake,nikipata mawasiliano nae nitawafahamisheni)
 
kwa hiyo Hamad ameamua kuachia ule ubunge wa mahakamani
 
all the best waje tu kuonyesha demcrasia ya ukweli labda kitakuwa chama cha upinzani cha ukweli
 
hamad anahangaika, hajui wenzao wabara hamtaki? hakuona magazeti yalivyomchafua baada ya kuisema cdm vibaya?
 
kwa mujibu wa shabani itutu aliekuwa kaimu mwenyekiti wa ilemela si tetesi,ni ukweli wanatangaza chama leo hii
 
Kwani si anasema yeye bado ni mbunge halali wa Wawi kwa ticketi ya CUF! Ama kweli huyu 'mshkaji' amesharogwa!
 
haya kipya chama au chama kipya.,
Hapo kuna jina jipya tu wengne wale wale.
 
HONGERA HAMAD RASHID kwa ujasiri wako wa kutumia uhuru wako wa kujitamka,na kuchaguwa.
Uliyoyataja katika "Yaliyojiri " yameamsha wengi.
HAPANA UTUME WALA UMILIKI WA CHAMA NA SIASA ZA ZANZIBAR.WEWE MZANZIBARI-MTANZANIA UNA UHURU
WA KUJICHAGULIA .
Fuguwa chama na hilo litakuwa ni pigo kubwa la ile porojo za kutaka kukutia dosari kuwa unatumiliwa
na CCM au CHADEMA .
Wapo wengi watakao kuunga mkono .
 
Ngoja msambaratike, ccm ipate nafasi ya kuwatawala milele kiulaiiiini.
 
huyu nae anatangatanbga utadhani muuza karanga ....kwani lazima uwe mwanasiasa bana...aghhhh
 
Wanajamvi,aliyekuwa kaimu mwenyekiti wa wilaya ya ilemela wa CUF Hapa Mwanza,ambaye yuko kambi moja na HR na ambae mwishoni alhamisi ya wiki iliyopita amaetangaza kujiondoa CUF na wanachama zaidi ya 1222,amenidokeza muda sio mrefu kuwa wako pemba na wamepata mapokezi makubwa na kuwa katika mkutano wao na wananchi wa jimbo la wawi wanakusudia kutangaza rasmi chama chao kipya cha ADP ( hajaniambia kirefu chake,nikipata mawasiliano nae nitawafahamisheni)

mwambie asimsahau kafulira kwenye utukufu wake,ubunge wa mahakama ni kashfa kwa mtu mwenye akili timamu!!
 
Hamad kumbe alikuwa na mpango wa kuanzisha chama ila lengo lake ni kutaka kuwa mwenyekiti au katibu mkuu. Akikosa hizo nafasi hicho chama kinakufa
 
Back
Top Bottom