Haina maana yoyote -- siyo katika zile kamati tatu nyeti zilizogombewa last week.
Hamadi Rashidi mtu mnafiki wa kupindukia. Kwanza nadhani wengi wenu hamna habari kwamba Makinda alimtosa huyu Hamadi Rashidi ambaye ukweli ni kwamba harakati zake zote za hujuma dhidi ya Chadema kumbe alikuwa anaimezea ile kamati ya Mashirika ya Umma -- POC, ile aliyopata Zitto.
Alikuwa amepeleka maombi kwa Spika kuwamo katika kamati hiyo ili baadaye agombee uenyekiti. Badala yake Makinda akampeleka katika ile nyingine aliyopata.
Hamadi Rashidi ni mtu mwenye uchu sana wa madaraka!
Kwa hilo nampongeza Spika.
Kwa watakaouliza source yangu ni swahiba wangu aliyepo katika ofisi ya Spika ambaye alinihakikishia aliiona Fomu ya Hamadi kuomba kuwa katika POC. Na hili sasa hivi litalipuka katika magazeti.
Nyani haoni kundule