Halotel ni kiboko kwa internet speed


mkuu, umenishawishi. ngoja niachane na hili livoda nichepukie halotel.
 

pamoja sana mkuu.
 
Hawa jamaa wana customer suport namba ambayo iko reachable kwa mtandao mwengine? Maana nimenunua line yao mpaka leo inasema sijasajiliwa na hapa karibu hakuna duka lao.
 
Hawajafunga 3G minara yao yote.

Kwenye district ambayo ninaisimamia mimi tokea tunaanza kuingia mikataba na wenye maeneo hadi kumaliza ujenzi wa towers, siyo minara yote tuliyofunga 3G japo minara mingi ni ya 3G.

sasa kwanini hamjafunga minara yote mkuu hamuoni kwamba mnatuhujumu wateja wenu watarajiwa?
 

pamoja sana mkuu. endelea kusambaza Sumu ya halotel hadi tigo, voda na mobitel waombe poo!
 
Last edited by a moderator:
asante kwa kutuelimisha hilo maana wao wanajinasibu kuwa wamefunga 3g minara yote.

ila wameanza vizuri...si haba mkuu. ikiwa pamoja na uchanga wao wameweza kutikisa hivyo, wakikomaa watasumbua sana.
 

mkuu, TCRA ni mbwa tena mbwa KOKO...hawana meno ya kung'ata mafisadi wa CCM waliojaa ktk hiyo mitandao.
 
Last edited by a moderator:
ni nouma arifu
 

mkuu meseji huwahi kuingia kwa kuwa speed yao ipo juu. ukitaka kufaidi vzr nunua unlimited bundle.
 
mkuu meseji huwahi kuingia kwa kuwa speed yao ipo juu. ukitaka kufaidi vzr nunua unlimited bundle.
Hamna mtandao wa 3G wenye Unlimited ya Ukweli.
Hiyo meseji nayoisema ni ya Ku Limit Speed!

Sasa Unlimited yenye Limit ya Speed hiyo ni Unlimited au niku Misuse neno
 
Acha kupotosha
Simu za 4G zipo na ili Upate 4G unaitaji Sim card ya 4G na Device ya 4G(simu ya 4G au Modem yenye uwezo wa 4G)

Na wala 64k sio kigezo cha line kuwa na uwezo wa 4G kuna line ni 64K na ni za 3G

oooops! basi tigo ndio walinipotosha...kumbe hawa jamaa ni wezi sasa nimegundua au uwezo wa customer care agents wao uko chini. tigo walinipotosha kwamba ili upate 4g unapaswa kuwa na laini ya 4g au u-upgrade laini ya kawaida hadi 64k. tigo ni mafisadi wa ku2pwa.
 
Labda haukuelewa vizuri
Kama una Line ya 3G unaweza kui Swap ikawa ya 4G au ukasajili line mpya!

Lakini ili utumie Line ya 4G unaitaji Kifaa chako kiwe na Uwezo wa 4G i.e Hauwezi Tumia 4G kwenye simu kama Samsung Galaxy pocket
 
mtu akiisema vibaya halotel ujue ana lake, cc huku kw2
voda E
Airtel G
Tigo E
HALOTEL H+/3G
 
Hamna mtandao wa 3G wenye Unlimited ya Ukweli.
Hiyo meseji nayoisema ni ya Ku Limit Speed!

Sasa Unlimited yenye Limit ya Speed hiyo ni Unlimited au niku Misuse neno

nani anapotosha...mimi au service providers? mkuu UNLIMITED ya kibongo ina maana ya "MUDA wa MATUMIZI" wa bundle uliyojiunga...sio UNLIMITED SPEED! umeelewa? maana yake kama umeambiwa ni kwa matumizi ya saa 24 utatumia ndani ya muda huo. mitandao yote baada ya kutumia kiasi fulani cha bundle hutuma meseji ya kulimit spidi. kibongobongo hiyo ndio maana ya UNLIMITED. haya sasa niambie UNLIMITED ya huko ughaibuni inatafasiriwaje?
 

Duh ama kweli!!!!!!!!
 
Labda haukuelewa vizuri
Kama una Line ya 3G unaweza kui Swap ikawa ya 4G au ukasajili line mpya!

Lakini ili utumie Line ya 4G unaitaji Kifaa chako kiwe na Uwezo wa 4G i.e Hauwezi Tumia 4G kwenye simu kama Samsung Galaxy pocket

du, haya majanga! ina maana hata modem itabidi kumbe ninunue ya 4g? hawa jamaa ni wezi sana na hawaaminiki hata kidogo.
 
Hawa jamaa wana customer suport namba ambayo iko reachable kwa mtandao mwengine? Maana nimenunua line yao mpaka leo inasema sijasajiliwa na hapa karibu hakuna duka lao.

kabla hujaanza kuitumia unatakiwa umpigie mtu yeyote ndo no yako inakua activated
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…