Halotel huduma zenu mbovu sana

Halotel huduma zenu mbovu sana

tatizo la halotel hawapokei simu.
juzi kati nimekosea kufanya muamala nawapigia simu hawapokei, nikajaribu kurudisha muamala wananiambia muamala haupo, mara wanasema sijafanya muamala wowote, nikawapotezea.
baada ya kama siku tatu hivi jitihada zote nimefeli nikaona sms wameirudisha hela.
Si bora halotel, airtel wana huduma iko kwenye app ya kuhamisha ela kutoka kadi ya visa au mastercard. Nlihamisha pesa ikakatwa kwenye airtel haikufika. Kuwapgia eti wananiambia niwasiliane na kampuni waliyoingia nayo kuhandle hiyo miamala 🤣 sasa nikabaki najiuliza, mimi nachojua natumia huduma yenu, mliyeingia mkataba naye mimi simjui but anyway nikawasiliana nao wakanituma risiti kwa email, nikawatumia airtel wakasema haujafika niendelee kuwasiliana na hao.
Ikabidi niachane nao na ni zaidi ya mwezi haikuwahi kufika
 
Mimi nilinunua umeme hawakuniletea tokens hadi leo
Pambana nao mm ilini tokea ,Kila nikijaribu kuwapigia wanasema wananitumia token mwisho wa siku baada ya siku ya pili nikaona ni ujinga kusubiri token nikawapigia Tena nikawaambia wanitajie izo token wakafanya ivyo .ila walinizungusha sana ,mara ukipiga cmu anapokea mdada yupo usingizini mara mwingine anakukatia cmu ,ila Hawa jamaa niwasumbufu sana kitengo Cha customer care
 
Eeeh kivipi?hebu nihabarishe na Mimi niingie bure na halotel wangu
C unaijua Freebasics.? Hapo kuna web kadhaa za bure ikiwemo JF. Sasa ilikuwa inapatikana kwenye mitandao yote ila wakaitoa ikabaki free kwa halotel.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom