Halmshauri ya Jiji la Dar toeni risiti za TRA

Halmshauri ya Jiji la Dar toeni risiti za TRA

MWALLA

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2006
Posts
16,952
Reaction score
10,510
Hawa jamaa wa jiji haswa wa halmashauri ya jiji Dar kwanini hawatoi risiti za tra?

Juzi nimelipia vibali vya pikipiki 4 wamenipa risiti kama zile za cash sale ila wao wameziremba ili kupoteza lengo ukiwauliza wanasema hizo ndio risiti zao.

Nimewauliza kwanini hamtoi risiti za tra? Jibu hizo ndio risiti zao wao hawatumii risiti za tra.

Wizi huu halamshauri ya jiji Dar inaiibia serikali, Mamlaka fuatilia utumbue na huku.

Nikawaambia Magufuli kasema ukiuza toa risiti (tra) ukinunua dai risiti. Hawana risiti za tra tunaibiwa.
 
Kweli Mkuu, hawa jamaa hawashirikishi wananchi vizuri kuna maeneo mengi sana hawatoi hizo risiti. Ule mpango wao wa 3% naona kama haupo tena maana kuna mtu aliwasaidia kupata kodi ya mabilioni lakini hakumpa, wakasema mwisho Mil 20 tu na hata hiyo hakupewa alivyodai akakamtwa na polisi. Kuna clinic moja ya macho city centre kabisa na wala hawatoi risiti za EFD, nina ushahidi mtu kalipa jumla ya laki na elfu 85, wakati kuna sehemu sh 200 ya kujisaidia inatolewa EFD. Elimu zaidi na ushirikishwaji wa wananchi unahitajika, kwa mfano wewe ilitakiwa uwe na namna ya kuwasiliana na TRA , wangekuwa wametoa mawasiliano. T
 
Kituo cha mabasi Msamvu Morogoro nao hivyohivyo. Hawatoi risiti za tra wao wanatoa zile kama za Daladala maarufu kama vishina. Rais aliamrisha wafanyabiashara watumie efd lakini Msamvu wanafanya biashara wamegoma
 
Back
Top Bottom