Halima Mdee amsambaratisha Magufuli

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa Halima Mdee jana alitikisa Jimboni Chato kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara kuwahi kuhutubiwa jimboni hapo miaka ya karibuni.

Awali Mdee alilakiwa na umati mkubwa wa watu wakiwa na msururu mrefu wa magari,pikipiki,baiskeli huku akina mama wakiwa kandokando ya barabara wakipunga matawi ya miti.

Ujumbe mkubwa wa Halima Mdee kwa wanaChato ni kuikataa Katiba Haramu ya CCM na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.

Halima Mdee maarufu kama Tanzanian Iron Lady alipokea kadi 200 za watu walioamua kujitoa CCM na kujiunga Chadema.Huku mamia ya wananchi wengine ambao hawakuwa na chama wakijiunga pia Chadema.

Ikumbukwe jimbo la Chato linaongozwa na mbunge wa CCM John Pombe Magufuli ambaye ni waziri wa Ujenzi.

Ni simulizi hapa Chato kuanzia jana mpaka asubuhi hii kumzungumzia Halima Mdee na Chadema!




 
Mkuu Molemo tupia basi picha za watu hao walihudhuria mkutano pamoja na akina mama ambao walikuwa wakipunga matawi njiani.

Picha huongea zaidi kuliko maneno.
 
Last edited by a moderator:
Magufuli atakumbwa na aibu kubwa kama hataondoka mwenyewe
 
We masauti nadhani akili zako ziko matakoni kwanini asitoke yeye ninani,
hakuna utawala wa milele kwanini mnakuwa na akili mgando tena za kipumbafu.watanzania tumeamka haki kwa wote.
 
ndo maaana yaling'ang'ania ubunge usiwe na kikomo.
 
Kwa Chato siwezi kushangaa kwani jamaa hakubaliki na hana ushawishi tena kutokana na mabavu yake ktk kila kitu.
 
Mkuu Molemo tupia basi picha za watu hao walihudhuria mkutano pamoja na akina mama ambao walikuwa wakipunga matawi njiani.

Picha huongea zaidi kuliko maneno.

Mkuu Kimbunga vaa miwani uone vizuri
 
Last edited by a moderator:
Kati ya hao walioshiriki mkutano ni wangapi wapo tayari kupiga kura? Bado na sisitiza kinachowafanya watu wajae kwenye mikutano hii ni ukosefu wa ajira. Watu wangekuwa na kazi usingewaona wakijaa kwenye viwanja hivi kusikiliza watu waliopo kwenye kazi zao.
 
....ninachoweza kusema ni uwezo wa chadema kuandaa wanasiasa vijana,wenye elimu nzuri,wanaojiamini,naona kwa mbele ccm itabaki bagamoyo tu.......
 
....ninachoweza kusema ni uwezo wa chadema kuandaa wanasiasa vijana,wenye elimu nzuri,wanaojiamini,naona kwa mbele ccm itabaki bagamoyo tu.......

umeona mbali sana
 

Nakushauri na wewe ukafanye mkutano wako huko Chato alafu tuwaone hao wasiokuwa na ajira wakijitokeza.
 
jipe moyo, nmeshuhudia kwa macho yangu watu wanafunga maduka wanawah kucklza mkutano wa chadema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…