Hali Zanzibar: Ni upi msimamo wa CHADEMA?

Hali Zanzibar: Ni upi msimamo wa CHADEMA?

zanzibar huru

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2012
Posts
218
Reaction score
110
Chama kikubwa na mbadala wa CCM na ambacho kitakuwa na mamlaka ya nchi hii 2015 mbona mpaka sasa hivi kahikatoa tamko au taarifa yoyote kuhusu hali ya kisiasa kule visiwani, vurugu zilizotokea na msimamo wao kuhusu Muungano.

1. Je wanasemaje kuhusu wananchi kuambiwa ni dhambi kujadili kuwepo au kutowepo kwa Muungano?

2. Je wanakubali wananchi waulizwe kama wanautaka muungano au la?

3. Je CHADEMA na CCM na CUF wana sera moja kuhusu Muungano ( kulazimisha wananchi wakubali hii project ya wanasiasa)

4. Je Zitto Kabwe aliposema kuwa Muungano ni "SCARED" je huo ndio msimamo wa CHADEMA?

5. Waziri kivuli wa Muungano ni nani na mbona yuko kimya?

6. JJ Mnyika inabidi am summon Zitto na wanasiasa wengine wa CHADEMA ambao wanatoa matamko ili kupata attention na kuwaambia kuwa CHADEMA si genge la wahuni ambalo kila mmjoja anatoa matamko bila kumhusisha yeye (JJ).

7. Mnyika aki draft hiyo statement nashauri apate input ya Tindu Lissu


Au kama washatoa basi tunaomba bwana Mnyika atuletee hiyo taarifa tuisome
 
MTEGO WA CCM KUTUMIA KARATA YA UDINI VISIWANI WAZANZIBARI WAPENDA MABADILIKO PAMOJA NA CHADEMA WATAUTEGUA TENA KWA AIBU YA MTEGAJI HIVI KARIBUNI

Lengo zima la kufanya shughuli za uchomaji makanisa Zanzibar umefanyika makusudi na CCM ili kutafuta KUKIWEKEA MTEGO CHADEMA ili chama hiki kisije kikaingiza ushawishi wake huko wala kuzoa wanachama kwa kutumia chombo chake cha M4C.

Hata hivyo mtego huu ni lazima CCM ndicho kitakachonasa humo chenyewe maana Wazanzibari na CHADEMA hadi sasa wanazungumza lugha moja kuhusu sera juu ya AINA YA MUUNGANO tutakaoutumia hapo baadaye kidogo.

Laiti CCM wangejua jinsi gani Tanzania Visiwani wanavyosubiri kwa hamu kupokea CHADEMA pamoja na M4C huku Mhe Tundu Lissu akipambanua zaidi mambo hadharani huko ... we acha tu!!!
 
Lakini hotuba ya Mbowe pale Jangwani Jumamosi, alisema wanasimamia serikali tatu, Tanganyika, Zanzibar na Shirikisho Wanajamvi.

Na kuhusu yanayotokea Z'bar, hotuba za Mtwara zimetoa kauli ya chama.
 
MTEGO WA CCM KUTUMIA KARATA YA UDINI VISIWANI WAZANZIBARI WAPENDA MABADILIKO PAMOJA NA CHADEMA WATAUTEGUA TENA KWA AIBU YA MTEGAJI HIVI KARIBUNI

Lengo zima la kufanya shughuli za uchomaji makanisa Zanzibar umefanyika makusudi na CCM ili kutafuta KUKIWEKEA MTEGO CHADEMA ili chama hiki kisije kikaingiza ushawishi wake huko wala kuzoa wanachama kwa kutumia chombo chake cha M4C.

Hata hivyo mtego huu ni lazima CCM ndicho kitakachonasa humo chenyewe maana Wazanzibari na CHADEMA hadi sasa wanazungumza lugha moja kuhusu sera juu ya AINA YA MUUNGANO tutakaoutumia hapo baadaye kidogo.

Laiti CCM wangejua jinsi gani Tanzania Visiwani wanavyosubiri kwa hamu kupokea CHADEMA pamoja na M4C huku Mhe Tundu Lissu akipambanua zaidi mambo hadharani huko ... we acha tu!!!

Tanganyika yetu kwanza. Muungano baadaye
 
Chama kikubwa na mbadala wa CCM na ambacho kitakuwa na mamlaka ya nchi hii 2015 mbona mpaka sasa hivi kahikatoa tamko au taarifa yoyote kuhusu hali ya kisiasa kule visiwani, vurugu zilizotokea na msimamo wao kuhusu Muungano.

Au kama washatoa basi tunaomba bwana Mnyika atuletee hiyo taarifa tuisome
Join Date : 28th May 2012
ID za matukio tuzifuatilie kwa makini zaidi.
 
Wakachome kambi ya jeshi kuna watanganyika kibao tena wakristo..
 
Kumbe mambo mengi huyajui. Tamko mbona lishatoka? au unataka utumiwe kwenye inbox yako!!!
 
mbona mpaka sasa hivi kahikatoa tamko au taarifa yoyote
kuhusu hali ya kisiasa kule visiwani, vurugu zilizotokea na msimamo wao
kuhusu Muungano.

4. Je Zitto Kabwe aliposema kuwa Muungano ni "SCARED" je huo ndio
msimamo wa CHADEMA?

hueleweki una maana SACRED sio SCARED

na KAHIKATOA ndio mdudu gani?
 
kwa nini hampeni watu wawe wanatoa mawazo yao bila kuogopa?

Jadili hoja

unye wewe azoe mwingine. mwaka huu mtajibeba, mumezoea kuona chadema inawatetea mkaendelea kufanya upumbavu mkifikili mtatetewa na chadema?. fanyieni kazi matamko yaliyo tolewa. Nchi haiwezi kuishi kwa matamko.
 
Tuambie chama chenu kimetoa tamko gani

Hakitaki kukurupuka kinataka kikija kije na majibu thabiti na ya kiungwana na siyo ile ya ccm kuzuia wananchi kuongelea muungano kwenye katiba mpya
 
Zanzibar ni Vita daima kati wamiliki wawili Nyerere dhidi ya Sultani
 
YEYOTE ANAYETAKA KUUVUNJA MUUNGANO ATANGULIE KUJIVUNJA KWANZA KWA ULEVI WAKE WOTE HUO!!

Naona kama vile baadhi ya Wazanzibari wachache wenye ulevi kichwani hivi sasa wameamua kugeuza Tanzania maabara yao ya kufanyia majaribio ya MAISHA BILA MUUNGANO.

Watu wenye akili na waona mbali walishayachunguza yote haya na wakajua fika kwamba MAJARIBIO YA KI-MAABARA eti kwa mtu kutaka kujionea mwenyewe MAISHA BILA MUUNGANO yanaweza yakawa vipi ni jambo la hatari mno kwa mustakabali wa umoja wa kitaifa Bara na Visiwani. Hivyo yeyote anyetaka saaana kuuvunja muungano wetu ni vema ulevi wak huo akautumia kwa kujivunja mwenyewe kwanza.

Hatuwezi tukaruhusu walevi wachache kuhamasishana vilabuni kwa misingi ya mawazo ya ki-ayawani na kuuvunja tu chombo kilichotutunza kama taifa kwa zaidi ya miaka 50 wao wakaichezea tu kwa dakika 5 hivi hivi!!

Mawazo, kama ni ya KUBORESHA MUUNGANO hapo nasema serikali imsikilize mtu yeyote yule mchana au usiku, ofisini au nyumbani kwake, kanisani au msikitini; ila kama neno la ufunguzi wa mazungumzo yote ni KITU KUVUNJA MUUNGANO katu siungi mkono kusikilizwa mtu hapa!!!!!!!!!!

WaTanzania tuliowengi hadi hivi sasa tunapigania mabadiliko ya ki-mfumo, katiba na utawala mpya kwa malengo makuu ya KUBORESHA NA KUIMARISHA maendeleo yetu chini ya Umoja wa Kitaifa na mshikamano mara katika kundi letu la watafuta mabadiliko ya KUTUMAINIKA eti tunamsikia mwingine yeye kazi ni kupiga kelele juu ya namna gani TUKAVUNJE KILA KITU na kuanza na utupu kama vile taifa la Tanzania halikuwahi kuwa na watu mawazo mema yaliotufikisha hapa tulipo??

Kwani kujiunga na OIC kuna kitu gani cha ajabu kiasi kuwatieni wehu nyinyi wenzetu kiasi cha kutokuona mema yote ya hapa nyumbani kwetu na badala yake nchi ya ahadi kwenu igeuke ghafla kuwa ni OIC????????

Naam, mimi nasema kwamba walevi hawa wenye ufinyu wa kufikiri na kuona mbali juu ya Muungano ni wakati mwafaka waambiwe TANZANIA NI TAIFA AMBALO LIKO HAPA KUDUMU DAIMA na kamwe halitovunjwa kwa mawazo ya kilevi ila Demokrasia ya kutafuta njia zilizo bora zaidi kuboresha muungano ifunguliwe wazi na bunge letu kule Dodoma ili kuondoa sekeseke.

Lakini kuvunja nasema HAKIVUNJWI KITU HAPA fikra tu za kishetani hizo!! WaTanzania TUNAO UWEZO wakuwazuilia wajukuu wa taifa hili majuto ya hapo baadaye ya kuuvunja Muungano kabla ya Pemba nako hakujafikia kutafuta kuwa Jamhuri ya Chake Chake Kusini na Jamhuri ya Watu wa Pemba Kaskazini.

Nasema kwamjadala kuhusu Muungano kuvunjwa ama kutokuvunjwa; nileteeni hoja nyingine lakini kwa hili katu sisikilizi kitu!!!!
 
Back
Top Bottom