Hali ya Umeme nchini yazidi kuimarika
Shirika la Umeme TANESCO limesema kuwa Uhakika wa umeme unaonekana sasa kwa mikoa iliyoungwa kwenye grid ya taifa unatokana na kuendelea kuwashwa kwa mitambo ya kufua umeme kwa kutumia gesi.
Mitambo hiyo ni ya Kinyerezi 150 MW, Ubungo 2 (105MW) na Symbion 112 MW. Mvua zilizoanza kunyesha bado hazinyeshi kwenye mikoa yenye mita inayoweza kujaza Bwawa la Mtera, Kidatu na Kihansi ambayo ndio vyanzo vikubwa vya kufua umeme wa maji.
Hayo yalisemwa leo na Meneja Uhusiano TANESCO Adrian Severin wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Ubungo jijini Dar es salaam
Shirika la Umeme TANESCO limesema kuwa Uhakika wa umeme unaonekana sasa kwa mikoa iliyoungwa kwenye grid ya taifa unatokana na kuendelea kuwashwa kwa mitambo ya kufua umeme kwa kutumia gesi.
Mitambo hiyo ni ya Kinyerezi 150 MW, Ubungo 2 (105MW) na Symbion 112 MW. Mvua zilizoanza kunyesha bado hazinyeshi kwenye mikoa yenye mita inayoweza kujaza Bwawa la Mtera, Kidatu na Kihansi ambayo ndio vyanzo vikubwa vya kufua umeme wa maji.
Hayo yalisemwa leo na Meneja Uhusiano TANESCO Adrian Severin wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Ubungo jijini Dar es salaam