Hali ya hatari itangazwe kuhusiana na mapenzi!

Hali ya hatari itangazwe kuhusiana na mapenzi!

M4CODES

Member
Joined
Jul 10, 2013
Posts
19
Reaction score
4
Wasalaam,

Naona hali ya mapenzi si sawa kabisa, kuna maumivu makubwa makubwa sana kuliko inavyoripotiwa humu jf! kwa kifupi hali ni mbaya sana, hk ndicho unachowezasema kwa kifupi kuhusiana na mapenzi! kuna wengine wanagugumia kimya kimya hawana la kufanya, kuna wengine hadi kwa waganga wa kienyeji, kuna wengine kila leo wanasaka ushauri, wanawake kwa wanaume wanajitahidi kubadilisha wapenzi katika nia ya kusaka suluhu la maumivu ya kimapenzi! alieolewa analia, alieoa analia, mwanafunzi analia, housegirl analia hadi kujinyonga, kondakta na dreva wake wanalia, mwalimu analia, ........... . . .. . .. . . . . .hali ni mbaya sana kwa kifupi!

hv kuna dawa ya kuzuia maumivu ya mapenzi?, maana kuna kilio nchi nzima kuhusu mapenzi!
huyu analia hv, yule analia vile ili mradi hali ya mapenzi si sawa kabisaaa!

Wanaume kwa wanawake itangazeni hali ya hatari kwenye dimbwi hili la mapenzi, labda itasaidia!
 
Kwa taarifa yako Ufukara wa Fikra na Mali unawatafuna Watanzania wengi kuliko hayo mapenzi...

Wengi unaoona walia lia hapa ni vijana wadogo walioparamia mti wa mchongoma na sasa kimbembe cha kushuka kimewakuta...
 
dawa nikujiamin! usijipe stress...focus on ur ambitions.... dem atakae jleta mpe ukwel(si kumgonga) km vp peaaace m2 wng
 
We hu mugeni katika mambo hayo? Mimi nimeoa lakini kwa sababu nilijua nini maana ya ndoa nimekomaa na nimekuwa sugu ya hayo matatizo bila stress bila chuki bila ugomvi tunasonga mbele kwa speed. Ukichukulia ndoa kama safari ambayo njiani gari inapata pacha na kuziba, inaisha mafuta na kuongeza inachemsha na kuweka maji then safari kuendelea. ukichukulia ndoa hivyo maisha yatakuwa murua na ndoa itadumu
 
Una akili sana mheshimiwa,hili suala la mapenzi linaonekana ni dogo kwa sababu tu ni siri binafsi ila ni tatizo sana, na linaingilia hadi ujenzi wa kawaida wa kijamii na kitaifa
 
hii kitu mapenzi..ngumu kwa kila mtu...
 
Kuwa mkweli tangu mwanzo kwa kuonyesha misimamo yako sio unajifanya baby wangu sijui nini kumbe moyoni unajua unalolitaka akiingia kwenye line na ndoa ikafungwa unambadilikia. Kama wewe ni mtu wa daladala panda/mpandishe daladala siku moja moja ukiwa vizuri unamchukulia taxi hali ikiwa tata unarudi kwenye utaratibu wako uliouzoea. Tatizo letu ni pale tunapojitutumua kupita maelezo hasa wanaume na kinadada nao bila ajizi anakuchukulia poa kama wewe unavyojifanyisha na mwisho wa siku kunapokuwa na mabadiliko makubwa / huduma zinashuka kwa kasi kama binadamu na yeye anakuwa na wasiwasi na wewe huenda ulikuwa tapeli hasa kama umejiajiri na hukumwonyesha kabisa deal zako ndio itakuwa balaa kubwa. Ni kuwa real tu hakuna cha zaidi

Otherwise naunga mkono hoja iliyotolewa na lito jiniaz na MVUMBUZI
 
Last edited by a moderator:
Mambo yanayohusu usalama wa nchi rais ndo mwenye mamlaka ya kutangaza hali ya hatari,sasa hili la mapenzi nani atatangaza hali ya hatari na kwa kutumia sheria ipi kikatiba?
 
Back
Top Bottom