Kama ilivyotarajiwa na Watanzania wengi ile safari iliyianzishwa na vyama vinne vya siasa nchini Tanzania yaani CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI na NLD inaelekea ukingoni kutokana na mambo kadhaa wa kadhaa ambayo yameendelea kufukuta ndani ya UKAWA kwa wiki kadhaa sasa. Chanzo cha mgogoro unao endelea kukua siku hadi siku unatokana na baadhi ya vigogo ndani ya UKAWA kuanzisha tuhuma nzito juu ya Freeman Mbowe wakimtaka ajiuzuru katika nafasi yake kwa kutumia mabavu kumkaribisha ndani ya chama aliyekua Waziri Mkuu wa Tanzania ndg. Edward N. Suala hili limeendelea kuwagawa Viongozi kadhaa wa ngazi za juu wa UKAWA huku ikipelekea kuitishwa vikao vya kila mara baada ya Kampeni.
Suala la Mgawanyo wa majimbo nalo limeendelea kujenga chuki miongoni mwa Viongozi wanaounda UKAWA hali inayohatarisha uwepo wa UKAWA. Taarifa toka katika kikao cha juzi kilichivunjika baada ya Viongozi wa CUF na NCCR MAGEUZI kutishia kujitoa katika UKAWA kulingana na majimbo yao kivamiwa na wagombea wa CHADEMA. Hali hii ilimfanya Mh. James Mbatia kung'aka na kusema CHADEMA inawachezea akili kwa kuwa mda wa kusimamisha Mgombea urais umepita. Kikao hicho kilivunjika baada ya Viongozi hao wa UKAWA kushambuliana kwa maneno makali sana na kulushiana matusi huku Viongozi wa CHADEMA wakiwataka vyama vinavyohisi vimeonewa wajitoe UKAWA.
Suala la afya ya Mh. Lowasa NI wazi sasa limezidi kuleta mpasuko wa dhahiri ndani ya UKAWA hali iliyofanya kila baada ya Kampeni kikao cha tathimini kutawaliwa na agenda hiyo huku Mbowe akiwekwa lawamani kwa kuwapotosha Viongozi wa UKAWA. Katika kikao cha juzi ilimradhimu Mchungaji Gwajima kuingilia kati kusuruhisha mgogoro ulio ibuka baada ya team nzima ya Kampeni kumjia juu Mwenyekiti wa chadema ndg. Freeman Mbowe. Hii ilikua baada ya kuonekana wazi afya ya ndg. Lowasa kudhoofu siku hadi siku. Moja ya watu alisikika akisema " wakati ameshinda kushika mic pale Dodoma tulikua kimya japo tuliaibika lakini KWA hali aliyo nayo na hili LA kupanda jukwaani akiwa ameshikiliwa itatugjarimu na Mimi sitaki niwe sehemu ya suala hilo"
Kutokana na matukio haya ni wazi kabisa kuw ndani ya wiki mbili zijazo kuna matukio makubwa ya kuhama baadhi ya vigogo ndani ya UKAWA na wakati mwingine baadhi wakitangaza kustaafu siasa ili kujiepusha na aibu na fedheha baada ya Uchaguzi.