Hali ni tete huku kwetu, Serikali iko wapi?

Hali ni tete huku kwetu, Serikali iko wapi?

Tanki

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2013
Posts
538
Reaction score
248
Amakweli vita vya panzi furaha kwa kunguru.

Hivi serikali inajua kuwa huku kwetu ( Kivule - Gongo la mboto ) kuanzia juzi yani baada ya mafuriko na kuvunjika daraja lililo karibu na Kivule Shule nauli ya mwanafunzi imekuwa shilingi 500 badala ya shilingi 200. Wakati watu wazima wakilipa shilingi 1000 badala ya 500.

Tena hapo kwakuwa daraja halipitishi gari isipokuwa watembea kwa miguu tu. Hivyo inatubidi tutembee kutoka kivule mwisho hadi tuje kuvuka daraja kwa juu kuna kituo kinaitwa Muembeni hapo ndo unakuta gari. Lakini licha kutembea umbali mrefu hadi kufika hapo lakini bado tu tunalipishwa 1000 na wanafunzi wanalipishwa 500. Hiyo hata ukiwa Banana unataka kuja Kivule bado tena nauli ni 1000 na mwanafunzi 500. Hali ni tete sana. Cha ajabu hadi magari ya UDA nayo yanafanya hivyo hivyo 1000 kwa 500.

Wito wangu : Serikali tunaomba mtutupie jicho la huruma. Watu mnaohusika na maswala ya usafiri mje huku Kivule - Gongo la mboto msaidie wananchi dhidi ya huu uhalamia.
 
Serikali iko busy wanabishana kuhusu Serikali moja,mbili au Tatu.Wakimaliza watakuja kuwaona.
 
Wakitoka bungeni watakuja kuwaoneni, poleni sana
 
Nilikwambia jirani yangu umechagua CCM subiri!
 
Acha mpate adabu, hayo maeneo ndio huwa mnaongoza kwa kuichagua ccm
 
Pole mwenzangu wa kivule, mie ni mwenzio wa Ulongoni B ambapo tangu daraja limekatika kutokana na mvua ni majanga matupu...kwanza wakajitokeza vijana wakaweka magogo na nguzo za tanesco na kuanza kutoza kila apitae..kwakweli tunateseka mno na hatujaona cha jerry slaa wala kiongozi yeyote kutembelea maeneo yalioathirika...yani jamaa wakishachaguliwa wanapotea mazima! Wananchi tuamke, uchaguzi 2015 unakuja tusichague viongozi wasiotujali..
 
Pole mwenzangu wa kivule, mie ni mwenzio wa Ulongoni B ambapo tangu daraja limekatika kutokana na mvua ni majanga matupu...kwanza wakajitokeza vijana wakaweka magogo na nguzo za tanesco na kuanza kutoza kila apitae..kwakweli tunateseka mno na hatujaona cha jerry slaa wala kiongozi yeyote kutembelea maeneo yalioathirika...yani jamaa wakishachaguliwa wanapotea mazima! Wananchi tuamke, uchaguzi 2015 unakuja tusichague viongozi wasiotujali..
Jerry Silaa yupo Mwanza anaponda raha, na alipoambiwa kuhusu maafa ya mvua akasema kwani akiwa Dar ndiyo atazuia mvua iache kunyesha....huyo ndiyo diwani na Meya wenu, nawapa pole sana wadau

 
Amakweli vita vya panzi furaha kwa kunguru.

Hivi serikali inajua kuwa huku kwetu ( Kivule - Gongo la mboto ) kuanzia juzi yani baada ya mafuriko na kuvunjika daraja lililo karibu na Kivule Shule nauli ya mwanafunzi imekuwa shilingi 500 badala ya shilingi 200. Wakati watu wazima wakilipa shilingi 1000 badala ya 500.

Tena hapo kwakuwa daraja halipitishi gari isipokuwa watembea kwa miguu tu. Hivyo inatubidi tutembee kutoka kivule mwisho hadi tuje kuvuka daraja kwa juu kuna kituo kinaitwa Muembeni hapo ndo unakuta gari. Lakini licha kutembea umbali mrefu hadi kufika hapo lakini bado tu tunalipishwa 1000 na wanafunzi wanalipishwa 500. Hiyo hata ukiwa Banana unataka kuja Kivule bado tena nauli ni 1000 na mwanafunzi 500. Hali ni tete sana. Cha ajabu hadi magari ya UDA nayo yanafanya hivyo hivyo 1000 kwa 500.

Wito wangu : Serikali tunaomba mtutupie jicho la huruma. Watu mnaohusika na maswala ya usafiri mje huku Kivule - Gongo la mboto msaidie wananchi dhidi ya huu uhalamia.
Kwani Tanzania ina serikali?
 
Na tena huku Ulongoni ni kama tupo nje ya dar, hakuna mwamko wa maendeleo kabisa umeme shida nguzo hazilwetwi huu mwaka wa 5 ni ahadi tu, maji tunatumia ya visima hakuna dawasco huku, usafiri ni wa shida, hakuna daladala na hizo barabara utadhani za kupitishwa ngo'mbe, na mbaya zaidi hata wahalifu nao wameona ni sehemu salama kwao...kwakweli tunaishi kinyonge sana.
 
Acha mpate adabu, hayo maeneo ndio huwa mnaongoza kwa kuichagua ccm.
sio wote mkuu kama usemavyo..ujue mwamko wa wananchi ni mdogo, ila natamani sasa wananchi waamke, wajitambue na watambue kura zao zinaweza leta maendelo ama kudidimiza maendeleo...
 
Amakweli vita vya panzi furaha kwa kunguru.

Hivi serikali inajua kuwa huku kwetu ( Kivule - Gongo la mboto ) kuanzia juzi yani baada ya mafuriko na kuvunjika daraja lililo karibu na Kivule Shule nauli ya mwanafunzi imekuwa shilingi 500 badala ya shilingi 200. Wakati watu wazima wakilipa shilingi 1000 badala ya 500.

Tena hapo kwakuwa daraja halipitishi gari isipokuwa watembea kwa miguu tu. Hivyo inatubidi tutembee kutoka kivule mwisho hadi tuje kuvuka daraja kwa juu kuna kituo kinaitwa Muembeni hapo ndo unakuta gari. Lakini licha kutembea umbali mrefu hadi kufika hapo lakini bado tu tunalipishwa 1000 na wanafunzi wanalipishwa 500. Hiyo hata ukiwa Banana unataka kuja Kivule bado tena nauli ni 1000 na mwanafunzi 500. Hali ni tete sana. Cha ajabu hadi magari ya UDA nayo yanafanya hivyo hivyo 1000 kwa 500.

Wito wangu : Serikali tunaomba mtutupie jicho la huruma. Watu mnaohusika na maswala ya usafiri mje huku Kivule - Gongo la mboto msaidie wananchi dhidi ya huu uhalamia.

kuweni na umoja....pandeni halafu basi zima mnalipa nauli halali muone kama konda atawashusha....
 
Na tena huku Ulongoni ni kama tupo nje ya dar, hakuna mwamko wa maendeleo kabisa umeme shida nguzo hazilwetwi huu mwaka wa 5 ni ahadi tu, maji tunatumia ya visima hakuna dawasco huku, usafiri ni wa shida, hakuna daladala na hizo barabara utadhani za kupitishwa ngo'mbe, na mbaya zaidi hata wahalifu nao wameona ni sehemu salama kwao...kwakweli tunaishi kinyonge sana.

Aseee poleni sana, ila mkate rufaa mrudishwe Mkoa wa pwani
 
Heri yenu nyie ni daraja na nauri kupanda Je, wale wa Tarime waliokuwa wakiuwawa na mtu kwa kupigwa risasi kila leo hadi watu 10 kufa na serikali ilitulia tu ama wale wa Butiama ambao wanawake wanauwawa kila siku serikali iko kimya tu. Tuko kama hatuna haki ktk nchi hii.
 
Back
Top Bottom