Kwa kweli hiyo ni strategy nzuri sana, vinginevyo wananchi wanweza kukua kabisa, polisi kama ni mmoja huwa anazidiwa kabisa na wananchi, isitoshe polisi mwenyew hana silaha.......
Hii inanikumbusha enzi zileee za treni ya kati. Tumesafiri na vizee vya kimang'ati tukafika ITIGI, kumbe kulikuwa na kibaka alimchomolea moja wao hela. Kidingi kikamshtukia wakati anashuka....wachaa weee! walianza kumpiga virungu vya kichwa....kibaka anatimua mbio kuelekea kituo cha polisi.....mpaka ndaniiiiii, wazee wanaendelea kumgonga tu na virungu, polisi wakazidiwa nguvu.....kibaka ndani ya meza lakini bado virungu vinamkuta!. Ndipo polisi walipowatishia bunduki hao wazee ndio wakaacha.....ilikuwa "live" burudani aiseee!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.