CHA The GREAT
JF-Expert Member
- Nov 11, 2010
- 651
- 854
Nimekuwa napata shida kidogo kutokana na maoni ya watu kuhusu hotuba ya Rais alipokutana na wadau wa mifuko ya hifadhi ya jamii, vyama vya wafanyakazi na wengineo. Katika hotuba hiyo, Rais alinukuliwa akisema kwamba, utaratibu wa zamani katika kikokotoo na kabla mifuko haijaungwa urudi kwa kipindi hiki cha mpito ambacho kitakwenda hadi mwaka 2023.
Kutokana na kauli hiyo ya Rais, kumekuwepo maoni tofauti tofauti kuhusu sheria mpya iliyosainiwa na Rais. Wapo watu wanasema kwa kauli ya Rais, basi hata sheria iliyosainiwa na yeye imekuwa nullified, na kama imekuwa nullified, basi utaratibu wa zamani ndiyo utatakiwa kutumika mpaka hapo kutakapokuwa na utaratibu mwingine ambao utashirikisha wadau wa pande zote.
Ningependa kufahamu haya: Je, lile Fao pendwa maarufu kama FAO LA KUJITOA pia litatolewa kwa kipindi hiki cha mpito? Pamoja na hilo, pia ningependa kujua kuhusu mengineyo ya sheria hiyo. Je, wale ambao walikuwa wakiacha kazi kwa hiyari (resignation) sasa watapata fao hilo? Je, wale waliopunguzwa kazi watapewa pia mafao yao kwa asilimia mia moja? Je, lile fao la upotevu wa ajira ambalo kimsingi utaratibu wake ni wa kinyonyaji na kandamizi, ndiyo kusema limesitishwa?
Nawasilisha.
Kutokana na kauli hiyo ya Rais, kumekuwepo maoni tofauti tofauti kuhusu sheria mpya iliyosainiwa na Rais. Wapo watu wanasema kwa kauli ya Rais, basi hata sheria iliyosainiwa na yeye imekuwa nullified, na kama imekuwa nullified, basi utaratibu wa zamani ndiyo utatakiwa kutumika mpaka hapo kutakapokuwa na utaratibu mwingine ambao utashirikisha wadau wa pande zote.
Ningependa kufahamu haya: Je, lile Fao pendwa maarufu kama FAO LA KUJITOA pia litatolewa kwa kipindi hiki cha mpito? Pamoja na hilo, pia ningependa kujua kuhusu mengineyo ya sheria hiyo. Je, wale ambao walikuwa wakiacha kazi kwa hiyari (resignation) sasa watapata fao hilo? Je, wale waliopunguzwa kazi watapewa pia mafao yao kwa asilimia mia moja? Je, lile fao la upotevu wa ajira ambalo kimsingi utaratibu wake ni wa kinyonyaji na kandamizi, ndiyo kusema limesitishwa?
Nawasilisha.