Samson Kwayu
Member
- Jun 9, 2022
- 18
- 90
Hizi ni picha zilizopigwa leo tarehe 4/5/2023 zikiwaonesha vijana manguli wa siasa za Tanzania, Dkt Mwigulu Nchemba, January Makamba na Nape Nnauye wakiwa katika mjadala na tabasamu zito.
Picha hizi zimeibua mijadala mikubwa katika mitandao ya kijamii, baada ya hivi karibu kuiibuka mzozo mkubwa kuwa kuna vita kubwa kati ya Dkt Mwigulu na January Makamba, kuwa hawapikiki chungu kimoja na wanawindana kutoana roho.
Mjadala wa vita ukaanza kuvamiwa na watu mbalimbali wakichagiza yao wa sababu zisizojulikana lakini kubwa zaidi inasemekana kuna kiongozi mkubwa sana ambae anamiliki kundi la waandishi wa habari alichomeka majeshi yake ili kukoleza vita hii kwasababu hii ilikuwa inampatia haueni yeye kuelekea siasa za 2030 na kuendelea kuwa mkuu wao.
Ujio wa picha hizi unaonesha dhahiri shahiri kuwa wanasiasa hawa vijana wanachanga vyema karata zao na walimtega adui yao, na inawezekana tayari wamemwingiza kwenye kumi na nane zao, kinachosubiriwa na kumfyatua tu.
Vijana hawa watakumbukwa kwa mambo makubwa waliyoyafanya miaka 12 iliyopita muda ambao CCM ilikuwa imeelekezwa kibra lakini wao wakaingia na kuinasua, lahaula wakaambulia mabua baada ya waliemwingiza kuwageuka na kuanza kuwamaliza kisiasa kabisa.
Mimi kama mwanasiasa mkongwe nimefurahishwa na picha hizi kwani zinatoa funzo kwa wanasiasa wote nchini kuwa siasa zinahitaji akili tu sio papara.
Rai yangu kwa maadui wa hawa vijana, Rudin nyuma mfanye vyema calculations zenu maana wengi mmeingizwa kwenye siasa juzijuzi tu na mwendazake, hawa wenzenu wamepikwa wakaiva, wameteswa wakajifunza sio rahisi kunasa kwenye mitego ya kitoto.
Wasalaaam.
Picha hizi zimeibua mijadala mikubwa katika mitandao ya kijamii, baada ya hivi karibu kuiibuka mzozo mkubwa kuwa kuna vita kubwa kati ya Dkt Mwigulu na January Makamba, kuwa hawapikiki chungu kimoja na wanawindana kutoana roho.
Mjadala wa vita ukaanza kuvamiwa na watu mbalimbali wakichagiza yao wa sababu zisizojulikana lakini kubwa zaidi inasemekana kuna kiongozi mkubwa sana ambae anamiliki kundi la waandishi wa habari alichomeka majeshi yake ili kukoleza vita hii kwasababu hii ilikuwa inampatia haueni yeye kuelekea siasa za 2030 na kuendelea kuwa mkuu wao.
Ujio wa picha hizi unaonesha dhahiri shahiri kuwa wanasiasa hawa vijana wanachanga vyema karata zao na walimtega adui yao, na inawezekana tayari wamemwingiza kwenye kumi na nane zao, kinachosubiriwa na kumfyatua tu.
Vijana hawa watakumbukwa kwa mambo makubwa waliyoyafanya miaka 12 iliyopita muda ambao CCM ilikuwa imeelekezwa kibra lakini wao wakaingia na kuinasua, lahaula wakaambulia mabua baada ya waliemwingiza kuwageuka na kuanza kuwamaliza kisiasa kabisa.
Mimi kama mwanasiasa mkongwe nimefurahishwa na picha hizi kwani zinatoa funzo kwa wanasiasa wote nchini kuwa siasa zinahitaji akili tu sio papara.
Rai yangu kwa maadui wa hawa vijana, Rudin nyuma mfanye vyema calculations zenu maana wengi mmeingizwa kwenye siasa juzijuzi tu na mwendazake, hawa wenzenu wamepikwa wakaiva, wameteswa wakajifunza sio rahisi kunasa kwenye mitego ya kitoto.
Wasalaaam.