Hakuna Mwisho wa Dunia

Hakuna Mwisho wa Dunia

Throne Heir

Member
Joined
May 17, 2018
Posts
63
Reaction score
109
Kwa Kipindi Kirefu binadamu wameishi kwenye Uelewa hafifu wa Kuhusu mwisho wa Dunia, hii inaweza kuwa ni kwa makusudi au kwa bahati mbaya.

Kuhusu mwanzo na mwisho wa DUnia asilimia kubwa ya wanadamu uelewa wao kuhusu chanzo cha na asili ya Dunia ni kutokana na vitabu vitakatifu kama Quran na Biblia ambavyo vinawafuasi wengi.

Sina shaka juu ya maneno yake ila shaka yangu ni tafsiri wanadamu waliyoitoa kuhusu Mwisho wa Dunia. Vitabu vyote hivi vinasema kuwa kutakuwa na mwisho wa Uhai au uwepo wa mwanadamu na viumbe wengine hapa Duniani.

Vitabu hivi hakuna sehemu vinasema Kuwa Dunia Kama Sayari (Earth) ambayo ndio tunaishi sisi kwa sasa itafikia mwisho wake yaani mwisho wake eidha kwa kuyeyuka au kupukutika au kupotea hakuna kitabu Kinachosema Dunia itafikia Mwisho wake.

Binadamu sijui walitoa wapi matumizi ya Neno "Mwisho wa Dunia" badala ya Kusema mwisho wa Uhai wa viumbe waliopo kwenye sayari ijulikanayo kama Dunia au Earth. Dunia hii na Sayari zingine kuanzia leo elewa ni za milele kisicho milelel ni viumbe vilivyopo. Don't Get Twisted.. Emancipation.
 
Jua likizima ndo mwisho wa dunia yako

Kwenye huu ulimwengu wewe ni km haupo tu!
 
Cha kuzingatia ni kwamba tangu Yesu azaliwe hadi sasa ni siku 2 tu zimepita maana miaka elfu moja ya duniani ni siku moja ya Mungu. Kwahiyo usidhani binadamu anaishi muda mrefu saaana hapa duniani.
 
Kila lenye halikosi kua na mwisho
Ni wapi kuna uthibitisho kuwa hizi sayari zitafikia mwisho wake..Maandiko yote yanazungumzia uhai ndio utakao kuwa na Mwisho. Kwa Mfano Uislamu unasema "Kila Nafsi itaonja Umauti". Hapa Kinachotajwa ni nafsi ambayo ina uhai na Dunia na Sayari zingine si sehemu ya vitu au viumbe vyenye nafsi. Kwa taafsiri ya Kawaida ni kwamba Dunia (Earth) na Sayari zingine ni za Milele.
 
Ni wapi kuna uthibitisho kuwa hizi sayari zitafikia mwisho wake..Maandiko yote yanazungumzia uhai ndio utakao kuwa na Mwisho. Kwa Mfano Uislamu unasema "Kila Nafsi itaonja Umauti". Hapa Kinachotajwa ni nafsi ambayo ina uhai na Dunia na Sayari zingine si sehemu ya vitu au viumbe vyenye nafsi. Kwa taafsiri ya Kawaida ni kwamba Dunia (Earth) na Sayari zingine ni za Milele.
Na mm nakufundisha kupitia hio hio Qur'an kua dunia na vilivyomo vina mwisho wake

{ إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ }
[Surah Al-Infiṭār: 1]


Mbingu itapo chanika,
{ وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ }
[Surah Al-Infiṭār: 2]

Na nyota zitapo tawanyika,

{ وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ }
[Surah Al-Infiṭār:
Na bahari zitakapo pasuliwa,

{ وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ }
[Surah Al-Infiṭār: 4]
Na makaburi yatapo fukuliwa,

{ عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ }
[Surah Al-Infiṭār: 5]

Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.

Hizi ni baadhi ya aya tu zinazoonyesha mwisho wa dunia
 
Back
Top Bottom