Hakuna Mbunge Mteule, bali Rais Mteule

Hakuna Mbunge Mteule, bali Rais Mteule

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,461
JF ni Jukwaa la maarifa,

Kwa muda sasa naona kuna kosa tunalifanya, ama kwa kujua, au kwa kutojua. Naomba niwashirikishe jambo.

Mwaka 2000, Spika wa Bunge wa wakati huo, Mzee Pius Msekwa, alitukosoa kwa kosa la kuandika "Mbunge Mteule". Hoja yake ilikuwa kwamba hakuna mbunge mteule. Akasema mbunge akishatangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi, basi moja kwa moja huyo ni Mbunge tayari, na si Mbunge Mteule. Hivyo hivyo kwa Diwani.

Mzee Msekwa, katika kuipa nguvu hoja hiyo, akasema ndiyo maana Wabunge wanapokutana katika Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge, kazi yao kwanza ni kumchagua Spika wa Bunge. Kama si wabunge, hawawezi kumchagua Spika. Wanamchagua Spika kwa sababu tayari ni wabunge, na kwamba kiapo wanachoapa ni kwa ajili ya kutekeleza dhima zao.

Mambo ni tofauti kwa Rais. Mshindi wa kiti cha urais, kabla hajaapishwa, huyo ni Rais Mteule.

Nimeona nilete hili jambo nikiamini kuwa humu wamo wanafunzi ambao haya mambo wanapaswa wayatambue.

Nawasilisha.
 
Labda ungefafanua watu wakishafahamu maana na matumizi ya hilo neno kuna faida gani kwa mtu binafsi na taifa taifa kwa ujumla.
 
Labda ungefafanua watu wakishafahamu maana na matumizi ya hilo neno kuna faida gani kwa mtu binafsi na taifa taifa kwa ujumla.
Rejea kwenye uzi utaona kuna mahali nimesema "wanafunzi". Maswali kama haya huwaangusha wanafunzi hata walio vyuo vikuu.
 
Rejea kwenye uzi utaona kuna mahali nimesema "wanafunzi". Maswali kama haya huwaangusha wanafunzi hata walio vyuo vikuu.

Pole mkuu! it needs heart to deal with people! naona comment ya kwanza tu majungu! as if umeleta utumbo hapa!

Thanks mkuu!
 
hii aina umuhimu wowote kwa sababu aina madhara yoyote ikitamkwa tofauti
 
Rejea kwenye uzi utaona kuna mahali nimesema "wanafunzi". Maswali kama haya huwaangusha wanafunzi hata walio vyuo vikuu.

Pole mkuu! it needs heart to deal with people! naona comment ya kwanza tu majungu! as if umeleta utumbo hapa!

Thanks mkuu!
Nyie ndo mnasababisha wanafunzi wafeli mitihani, tangu lini JF ikawa Mamlaka ya kutoa Rejea mashuleni ? Kama ni tafsiri ya maneo ya Kiswahili sitarajii kama JF ni Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Je, mwanafunzi akifanya rejea ya neno kutoka Jf kwenye majibu ya mtihani ataandika kuwa source ni JF ? Aidha, hao wana JF watakakaotoa maana ya hilo neno, una uhakika gani ni ni sawa ? Acheni kuchangia kushusha kiwango cha elimu ya Tanzania.
 
Nyie ndo mnasababisha wanafunzi wafeli mitihani, tangu lini JF ikawa Mamlaka ya kutoa Rejea mashuleni ? Kama ni tafsiri ya maneo ya Kiswahili sitarajii kama JF ni Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Je, mwanafunzi akifanya rejea ya neno kutoka Jf kwenye majibu ya mtihani ataandika kuwa source ni JF ? Aidha, hao wana JF watakakaotoa maana ya hilo neno, una uhakika gani ni ni sawa ? Acheni kuchangia kushusha kiwango cha elimu ya Tanzania.
Wenye akili wamekuelewa.
 
[QUOTEsawabhoE=;145428mm59]Lamkbda ungefafanua watu wakishafahamu maana na matumizi ya hilo neno kuna faida gani kwa mtu binafsi na taifa taifa kwa ujumla.[/QUOTE]
 
wenye akili tumekuelewa.

malofa watakupuuza.

hata magazeti nao wanaandika mbunge mteule.
 
wenye akili tumekuelewa.

malofa watakupuuza.

hata magazeti nao wanaandika mbunge mteule.
Mnadanganya na kupongeza baada ya kudanganyana. Tume inakasimu madaraka yake kwa Watendaji wa Kata na Mkrugezi wa Halmashauri kutangaza washindi wa nafasi za Udiwani na Ubunge katika ngazi hiyo. Hivyo katika ngazi hizo, hao wanaotangaza matokeo hayo ndio "Tume". Katika ngazi ya Urais matokeo yanatangazwa na Mwenyekti wa Tume ambaye pia katika ngazi hii ni "Tume". Sasa inakuwaje Diwani na Mbunge wasiwe "wateule" kabla ya kuapishwa ? Rais kabla ya kuapishwa awe Mteule ilhali hawa wawe ni Wabunge na Madiwani kabla ya kuapishwa ilihali wote wametoka kwenye chungu kimoja. Jaribuni kuchmbua mambo sio kila kichosemwa na Kiongozi mnaona sawa tu hata kama ni kwa manufa yake binafsi.
 
Labda ungefafanua watu wakishafahamu maana na matumizi ya hilo neno kuna faida gani kwa mtu binafsi na taifa taifa kwa ujumla.
Muone juha huyu!! Ukishafahamu maana yake umeelimika na ukielimika huwezi kuendelea kufanya makosa au kurudia kosa!! Voda fasta buanaaa!!!
 
Inakuwa kama hadithi ya kuku na yai. Wabunge ndio wanachagua spika. Iweje wamchague kama sio wabunge ni wateule tu? Maana katiba inasema wazi spika anachuguliwa na wabunge. Baada ya kumchagua, spika huyo huyo ndiyo anawaapisha tena!
 
Nyie ndo mnasababisha wanafunzi wafeli mitihani, tangu lini JF ikawa Mamlaka ya kutoa Rejea mashuleni ? Kama ni tafsiri ya maneo ya Kiswahili sitarajii kama JF ni Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Je, mwanafunzi akifanya rejea ya neno kutoka Jf kwenye majibu ya mtihani ataandika kuwa source ni JF ? Aidha, hao wana JF watakakaotoa maana ya hilo neno, una uhakika gani ni ni sawa ? Acheni kuchangia kushusha kiwango cha elimu ya Tanzania.

Hujui hili ni jukwaa la kuelimishana pia?!!!!
 
umesomeka mkuu Manyerere...nadhani wabunge wateule ni wale ambao wapo bado chamani/wanaoshinda katika vyama vyao ili kwenda kupambana na wenzao wa vyama tofauti katika tarehe tajwa ya uchaguzi.
Au kwa yule atakaechaguliwa na chama husika na kukosa mpinzani kama Nanyumbu(naweza sahihishwa hapa) anasubiri mpaka tarehe ya uchaguzi tajwa na kuweza kutangazwa mbunge
 
Mnadanganya na kupongeza baada ya kudanganyana. Tume inakasimu madaraka yake kwa Watendaji wa Kata na Mkrugezi wa Halmashauri kutangaza washindi wa nafasi za Udiwani na Ubunge katika ngazi hiyo. Hivyo katika ngazi hizo, hao wanaotangaza matokeo hayo ndio "Tume". Katika ngazi ya Urais matokeo yanatangazwa na Mwenyekti wa Tume ambaye pia katika ngazi hii ni "Tume". Sasa inakuwaje Diwani na Mbunge wasiwe "wateule" kabla ya kuapishwa ? Rais kabla ya kuapishwa awe Mteule ilhali hawa wawe ni Wabunge na Madiwani kabla ya kuapishwa ilihali wote wametoka kwenye chungu kimoja. Jaribuni kuchmbua mambo sio kila kichosemwa na Kiongozi mnaona sawa tu hata kama ni kwa manufa yake binafsi.

Ukiacha jazba utaelewa tu. Angalia tofauti hizi; Rais Mteule hafanyi chochote-kutoa maagizo, kuteua, kutengua, n.k. Hayo atayafanya baada ya kuapishwa. Kwa Mbunge, yeye tayari ni mbunge akishaapishwa. Kazi moja kubwa anayoifanya ni kumchagua Spika. Spika anachaguliwa na wabunge. Sasa kama ni mbunge mteule, atachaguaje spika? Ndiyo maana sheria ikawa kwamba Msimamizi wa Uchaguzi akishamtangaza mshindi wa ubunge, huyo moja kwa moja keshakuwa mbunge, na si mbunge mteule.
 
Pia mbunge akichaguliwa kuna kuwa hakuna mbunge mwinge aliyeko anatumiakia ubungee Maana binge linakuwa limeshavunjwa. Wakati upande wa uraisi bado raisi anakuwa madarakani kipindi raisi mteule ametangazwa
 
Makosa ya KIMATAMSHI yapo mengi sana ila huwa tunayapotezea kwa vile hayana madhara. Hilo la MBUNGE MTEULE ni mojawapo nalo halina madhara yoyote
 
Back
Top Bottom