Al Sahaf was really a comedian/msanii na ndiyo maana aliajiriwa na Al-jazeera moja kwa moja!
Zanziba hatuna vita kama vya George Bush na Saadam Hussein. Kilichotokea Zanzibar ni ubakaji wa Demokrasia kupitia Sanduku la Kura kwa Mahifidhina wa CCM kutokubali matokeo baada ya kuona wameshindwa.
Tunataka kumwambia Balozi Seif Ali Idd aache usanii wa kuidanganya dunia kama alokuwa akifanya Al-Sahaf wa Iraq.Marekani wameshatoa tamko tayari la kutaka kumalizwa kwa mgogoro Z'bar kwa maana ya kumalizia kutangaza matokeo yaliyokuwa yamebakia kabla ya kufutwa ili kukamilisha Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar 2015 kwa kumtangaza Maalim Seif ambaye ndiyo mshindi.
Uchaguzi ule ulikuwa HURU na HAKI na ulishuhudiwa na watu wote wakiwemo Waangalizi wa Kimataifa wakiwemo Wamerekani ambao ndiyo Wafadhili wakubwa wa nchi yetu. Nje ya hapo Tanzania ijiandae kukosa Tshs. Trilioni 1 za MCC(Millenium Challenge Cooperation).
Tunajua Rais Magufuli kwa sasa anahangaika kukaba mpaka penalti ili apate fueza ya kutimiza ahadi zake kwa Watanzania. Kwanza tutamshanga na kumpunguzia maksi kama kweli yuko tayari kuona hiyo fedha ikizuiliwa na Marekani kwa sababu za mtu mmoja mjinga anayeitwa Jecha Jecha wa CCM.