Hakuna kuingia Dodoma bila kitambulisho

Hakuna kuingia Dodoma bila kitambulisho

Apo itafanya wana dodoma wote wakajiandikishe kupata kitambulisho,ata kama agizo lake anajua haitakua hivyo lakini approach anayotumia itasaidia kW kiasi kikubwa ata wale raia wenye kupuuzia kitambulisho vya taifa
Wanajf alikuwa na nia ya kuwatania watani zake . Hakuwaanamainisha kile alichosema.
 
Asitupige mkwara Dodoma nao mji kwamba kwenye maisha yako usipoenda dodoma utakuwa umekosa kitu kikubwa sana duniani. Labda watumishi wa umma ndo awaambie hivyo. Hayo maneno akisema gambo au makonda na pengie mongera yanaweza kunfikirisha mtu kidogo.
 
Tunaelekea kuwa north korea sasa..yaani ktk nchi yenye viongozi wa kibwege nadhani Tanzania yetu ni mijawapo! Hivi kweli watu wa dodoma wakipigwa stop kuingia sehemu yoyote ya tanzania si watakufa na njaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Kenya ambao wamekuwa na vitambulisho vya taifa kwa muda mrefu, hutakiwa kuonyesha kitambulisho hiko wakati wowote wanapotakiwa kufanya hivyo. So sioni ajabu kwa Mtanzania kutohojiwa kitambulisho chake akiwa Dodoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namsikitikia Le Mutuz tu na sijuwi wale nduguze walalao stendi za mabasi na kufanya mapenzi kwenye baraza za watu wata cope vipi na utaratibu huu.
 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 17(1)

17.-(1) Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya
kwenda kokote katika Jamhuri ya Muungano na kuishi katika
sehemu yoyote, kutoka nje ya nchi na kuingia, na pia haki ya
kutoshurutishwa kuhama au kufukuzwa kutoka katika Jamhuri ya Muungano.

________________________________________________________
Tamko la Mkuu wa mkoa wa Dodoma kwa Watanzania wote wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni hivi:-

"Itakua ni marufuku kwa Mtanzania asie na Kitambulisho cha Utaifa, kinacho onyesha uraia wake na mahali anapotokea, kuingia mkoani Dodoma mara baada ya zoezi hilo la utoaji vitambulishi kukamilika nchi nzima" Dk Binilith Mahenge
________________________________________________________
Hapa ndipo CCM MPYA INATUPELEKA, Ikumbukwe pia Nchini North Korea kwa Dogo Kim, ni marufuku kwa Mwananchi kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine bila kua na passport maalumu na barua ya viongozi ya kuidhinisha safari hiyo.


View attachment 844302
Haya si mambo mapya kwa wahenga kama mie!!
Kuna wakati ilikuwa ukifikkiwa na mgeni jambo la kwanza ni kumpeleka kumtambulisha kwa mjumbe wa nyumba kumi,LIKAPITA.
Karibuni hapa aliyekuwa Mkuu wa Polisi Dar aliamrisha mtu asipangishwe nyumba mpaka personal particulars zichukuliwe,IMEPITA.
Haya matamko mengine hayana uhalisia na yasiwasumbue sana.Wa kuteuliwa wanajua nini kinatakiwa kifanyike,amri na matamko!!
Dunia imeendelea sana na huna haja ya kutoa tamko kama hilo.Hata askari weetu wa barabarani,wanasimamisha gari kwa kuhisia ambapo wangetumia elimu ndogo ya kutafuta sampuli wangeweza kusimamisha baadhi ya magari na bado mafanikio yakawa makubwa!!!
 
Back
Top Bottom