Hakuna kazi laini kama kilimo

Hakuna kazi laini kama kilimo

Hahahahaha.

Mara ya kwanza kulima matikiti, nililima eka tatu. Yakawa mazuri, makubwa. Siku ya kukaribia mavuno yapo yaliyowahi kukomaa, nikachukuwa moja kwenda kujinafasi. Duh, nakata limetoka tikiti jeupe kabisa ndani, hakuna wekundu hata kidogo. Kulionja, hakuna utamu wala harufu ya tikiti hata chembe.

Ikabidi tuchukuwe lingine, hivyo hivyo. Nikachuma mawili matatu sehemu tofauti ya shamba, hivyo hivyo.

Nikachukua sample nikapeleka kwa bwana shamba Mkuranga wilayani. Akacheka, akanambia mama wamekuuzia mbegu siyo.

Nikawa hoi bin taabani.
🤣🤣🤣Pole sana pembejeo nao wajanja kumbe
 
Kilimo cha korosho ndiyo usiseme. Ni rahisi sana. Hekari moja itoa tani mbili na nusu. Jeahi likizipeleka ghalani wanakwabia wewe ni kangomba, hawakulipi kisha unalima nyingine. Ni rahisi sana
 
Back
Top Bottom