Ndugu zangu huu ni mtandao wa kuandika ukweli hata kama ukweli hautakuwa na ushabiki.
Kitendo cha kuna migomo kila siku kwenye vyuo vya Tanzania ni swala la kisikitisha na tatizo kubwa kwa mawazo yangu ni ukweli kwamba wanafunzi wengi na jamii yetu inafikiria elimu ya juu ni ya bure kama umefanya vizuri form 6 na kuchaguliwa. Ukweli ni kwamba elimu sio bure na nakumbuka miaka michache iliyopita niliambiwa gharama za kusoma Chuo kikuu cha Dar kwa miaka mitatu ni TSH 15,000,000 kwa mwanafunzi kuanzia kulipa walimu, vitabu, posho, nyumba, afya na vyakula. Kabla hatuja kimbilia kuwawekea hawa vijana wa vyuo madeni ni lazima tujiulize je Waliosoma mika ya nyuma kuanzia Kikwete wamelipa madeni? kama hawajalipa na pesa yao imetokana na nchi kuchukua mikopo je ni wakati wa wale waliosoma na wenye uwezo na kazi waanze kulipa madeni yao ili hiyo pesa itumike kwa mikopo ya wanafunzi wengine?. Ninashangaa Watanzania wengi waliosoma kwa mikopo ambayo hawajalipa kuweka ushabiki kwamba chuo ni bure au hawa vijana walipe wakati wenyewe hawajalipa madeni wakati wana uwezo.
Sisi Watanzania wenzenu tuliosoma nje tumesoma kwa mazingira magumu sana na wengi wetu tumekuja nje kwasababu nafasi ya course nzuri za vyuo vikuu zilikuwa chache. Mfano mimi nilipata Div 3 nzuri tu lakini Course niliyopangiwa ya ualimu pale Mlimani sikuipenda nilitaka kusoma Economy au Finance. Nilikuja nje na baada ya miaka mingi nikafanikiwa kupata mkopo wa $20,000 wa kusoma na serikali ya USA inahakikisha mimi nalipa kwani wenyewe ni wa hisani. Sasa mimi ni lazima nilipe kwasababu nisikolipa inachukuliwa kwenye mshahara kama ilivyo kodi vile. Pesa nayolipa inaenda kusaidia wengine na riba yangu ni 3% tu kwa mwaka kwa miaka 20. Lakini elimu ni muhimu kipato cha mtu aliyemaliza chuo ni mara mbili ya mtu aliyemaliza sekondari tu!.
Watu wenye uwezo na waliosomesha vyuo kwa mikopo ya serikali wanatakiwa kulipa lakini ni lazima tuhakikishe hiyo pesa inaenda kwenye mikopo ya vijana wetu wanaomaliza sekondari. Lakini tukikaa hapa tunawadanganya hawa vijana kwamba elimu ni bure na ukimaliza chuo unaingia mitini hatuwezi kusaidia jamii yetu kwani hatutakuwa na middle Class Tanzania.
Kitendo cha kuna migomo kila siku kwenye vyuo vya Tanzania ni swala la kisikitisha na tatizo kubwa kwa mawazo yangu ni ukweli kwamba wanafunzi wengi na jamii yetu inafikiria elimu ya juu ni ya bure kama umefanya vizuri form 6 na kuchaguliwa. Ukweli ni kwamba elimu sio bure na nakumbuka miaka michache iliyopita niliambiwa gharama za kusoma Chuo kikuu cha Dar kwa miaka mitatu ni TSH 15,000,000 kwa mwanafunzi kuanzia kulipa walimu, vitabu, posho, nyumba, afya na vyakula. Kabla hatuja kimbilia kuwawekea hawa vijana wa vyuo madeni ni lazima tujiulize je Waliosoma mika ya nyuma kuanzia Kikwete wamelipa madeni? kama hawajalipa na pesa yao imetokana na nchi kuchukua mikopo je ni wakati wa wale waliosoma na wenye uwezo na kazi waanze kulipa madeni yao ili hiyo pesa itumike kwa mikopo ya wanafunzi wengine?. Ninashangaa Watanzania wengi waliosoma kwa mikopo ambayo hawajalipa kuweka ushabiki kwamba chuo ni bure au hawa vijana walipe wakati wenyewe hawajalipa madeni wakati wana uwezo.
Sisi Watanzania wenzenu tuliosoma nje tumesoma kwa mazingira magumu sana na wengi wetu tumekuja nje kwasababu nafasi ya course nzuri za vyuo vikuu zilikuwa chache. Mfano mimi nilipata Div 3 nzuri tu lakini Course niliyopangiwa ya ualimu pale Mlimani sikuipenda nilitaka kusoma Economy au Finance. Nilikuja nje na baada ya miaka mingi nikafanikiwa kupata mkopo wa $20,000 wa kusoma na serikali ya USA inahakikisha mimi nalipa kwani wenyewe ni wa hisani. Sasa mimi ni lazima nilipe kwasababu nisikolipa inachukuliwa kwenye mshahara kama ilivyo kodi vile. Pesa nayolipa inaenda kusaidia wengine na riba yangu ni 3% tu kwa mwaka kwa miaka 20. Lakini elimu ni muhimu kipato cha mtu aliyemaliza chuo ni mara mbili ya mtu aliyemaliza sekondari tu!.
Watu wenye uwezo na waliosomesha vyuo kwa mikopo ya serikali wanatakiwa kulipa lakini ni lazima tuhakikishe hiyo pesa inaenda kwenye mikopo ya vijana wetu wanaomaliza sekondari. Lakini tukikaa hapa tunawadanganya hawa vijana kwamba elimu ni bure na ukimaliza chuo unaingia mitini hatuwezi kusaidia jamii yetu kwani hatutakuwa na middle Class Tanzania.