Haki na maendeleo havichangamani


Magufuli angekuwa na sifa ya kupenda maendeleo a singetumia mabilioni ya walipa kodi kujenga kijiji chake alichozaliwa na kuwaacha mamilioni ya waTanzania katika hali mbaya kiuchumi,kijamii,afya na elimu.
 
Magufuli angekuwa na sifa ya kupenda maendeleo a singetumia mabilioni ya walipa kodi kujenga kijiji chake alichozaliwa na kuwaacha mamilioni ya waTanzania katika hali mbaya kiuchumi,kijamii,afya na elimu.
Huo ni mtizamo tu, kwani wakati chato, shinyanga na mikoa mingine ikiwa kwenye giza totoro kwenye awamu ya kwanza, pili, tatu na ya nne ilikuwepo mikoa ambayo umeme ulikuwa umawaka hata kwenye mashamba ya migomba na kahawa vijijini, ilikuwepo mikoa ambayo barabara zake za kuunganisha kata na kata zilijengwa kwa kiwango cha lami. Ilikuwepo mikoa ambayo ilikuwa na usafiri mzuri wa barabara, reli, ndege na majini wakati mikoa mingine ilikuwa na baranara za vumbi tu. Alichofanya JPM ni kuwakumbuka wale waliokuwa wamesahauliwa kabisa kwenye awamu zikizopita, bahati ambaya na kwao chato kulisahauliwa pia.

Elimu hii ya Haki na maemdeleo haviendi pamoja haikiwekwa kwenye mitaala yetu na wakoloni kwa makusudi kabisa. Wakoloni walilifahamu hili kwa miaka mingi sana na ndio maana walitafuta makoloni ya kunyonya na mpaka sasa bado wanaendelea kuzikandamiza nchi nyingine ili kuendeleza nchi zao.

Hata familia haiwezi kutajirika kama haitapata watu wa kuwanyonya. Ili upate maendeleo kwa kupitia kilimo lazima upate vibarua wa bei nafuu au wa bure wa kukufanyia kazi shambani (cheap labour) vinginevyo huwezi kupata maendeleo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…