Hakatwi mtu hapaaa! Lowassa anaaminika kwa wengi

Hakatwi mtu hapaaa! Lowassa anaaminika kwa wengi

Ndivyo taratibu za uadilifu na sheria za nchi zinavyotaka UWAZI
 
Mama pitia upya kanunu za ccm,wanaotakiwa kudhamini ni 450.usipotoshe,ingekua 45 nani angehangaika kusafir na kupoteza maelf ya fedha
 
Hv huku vichwani tuna ubongo au tuna uji mzito tena yawezekana wa dona!PESA ZOTE ANAZOZITUMIA HATA KM NI WEWE ATAZIRUDISHA VIPI?TUSIWE NA NJAA YA KUFIKIRI HATA KWA JAMBO DOGO KM ILI.
HATA KAMA TUNAPEWA BUKU 5 ZA KUNUNUA 8mb STILL TUSIWE WATUMWA WA KUFIKILI JAPO KWA UPEO MDOGO TU AMBAO MWENYEZI MUNGU AMETUPATIA BURE.
HATA KM NI UHURU WENU WA NANI MTUMIKIE LAKINI MNAKERA SASA
Pamoja na yote huwezi kugombea hata ujumbe wa nyumba kumi bila kutumia hela. Na hakuna mtu anaweza kugombea bila kupata hata msaada wa kupakiwa katika baiskeli. Au watoe pesa kwa kujilipia nauli ili waende kumdhamini. Nadhani tuwe makini maana hata wapigakura wanasubiri hizo fedha. Hivyo mtoa fedha na mpokea fedha wote wana tegemea kupata kitu fulani kwa mtu wao akishinda, hivyo ni mpambano wa mpokeaji kiwaziwazi na mtoaji indirectly maana mtoaji akirelax basi atapata hasara. Kwa mantiki hiyo kama Lowassa kapewa fedha, hao waliompa fedha watacorrupt system ili apite. Hivi umemsikia Makongoro? Kama kiunzi cha kwanza cha Mangula amekipita sijui vingine vitamshinda vipi. Am trying to reason beyond the box
 
Msingi ni ameshawanyia nini Watanzania. Ndoto za aina hiyo hata watoto wanazo
 
Kinachofanyika tupewe jibu kama ndio kupendwa Lowassa. Kama atakuwa baada ya Siku kadhaa ndio Lowassa atafika mahali fulani, hawa Lowassa team wanatangulia pale. Magari yote na mahali pa watu kufikia panalipiwa. Debe linapigwa wilayo zote jirani na hapo kuwa usafiri ni bure, kula ni bure na kulala ni bure. Kila atakaye weka sahihi atalipwa vizuri. Matokeo yake misafara ya watu inaanza kutoka kwingine mbali zaidi ya km 100. Zoezi hili huko mbeya juzi lili sababisha abiria wa kawaida kukosa usafiri kwa kuwa magari yalikuwa yamelipwa vizuri ktk usafirishaji wa watu kumuendea Bopari Lowassa. Huyu banyani ni mbaya ila kiatu chake ni dawa. Watu hawafuati ubora wake wanafuata pesa zake.
Hii pesa iko vipi?
Kwanza wote waliokwapua pesa zetu za umma wapo ktk kampaini kali kuwa kwa uwezo wa pesa lazima Lowassa ndie awe Rais. Kuwa Lowassa ikulu basi ikulu na wao watakuwa ni hao hao. Watakuwa wahindi wote mapapa wakiongozwa na Rostam Aziz na Watu weusi lakini damu zao zimeisha kuwa za kihindi. Utasikia billioni wanasema nivijisenti, nyoka wenye kengeza na million kumi ni pesa ya nyanya chungu.
Kama jina lake litakatwa hawa watu wote watatambua kuwa machimbo ya madini yamefungwa watakimbilia machimbo mengine japo watakuwa hawana ushahidi wakukuta machimbo hayo mengine yatakuwa yanatoa dhahabu kama machimbo ya Lowassa.
Kujua kuwa Lowassa hana la kuwambia wanaomiminika hajawahi kutoa kauli hata moja inayo walenga wao. Hajawahi kuonyesha kama maskini wa Tanzania anawafahamu na kuonyesha kufahamu chanzo cha umaskini wao. Hata wanao mshadidia na wao hawajatuonyesha kama wanaujua umaskini wa watanzania na chanzo chake. 80% ya watanzania ni maskini wanao miliki 20% ya utajiri wa nchi. 80% ya utajiri inamilikiwa na 20% ya watanzania na ktk watanzania hawa 95% yao in watanzania wenye asili ya kihindi na ki Asia. Hao maskini wa Tanzania zaidi ya 80% ni wakulima na chanzo cha umaskini wao ni mfumo wa Kodi unao ruhusu zao Fulani mfn kahawa kutozwa aina za kodi zaidi ya 10. Kila unapolima unapoenda kuuza unapata bila hiari yako malipo chini ya ulivyowekeza ktk hicho kilimo. Lowassa hili analijua na hakuna ambapo aliwahi kulisemea na sio yeye wala ccm. CDM ktk ilani ya 2010 walikuwa wameliweka. Ilikuwa kama wangechukua dola kodi Kwa vifaa vya ujenzi ingetelemshwa Kwa 50% kwa vifaa vya ujenzi ili kila mtanzania ajenge nyumba bora. Hii inatekelezeka na ilieleweka. Sasa Lowassa hata bungeni anasinzia nani atamushabikia kama sio pesa.
 
Hatutamuogopa mtu kutokana na pesa zake au watu wake na wala hatutajifanya kama vile hakuna lolote lililotokea. Jakaya Kikwete Nec Dodoma.
 
Alishavuka hio level hta nanyi mnalijua hilo ndio maana upande wa kambi zenu wooote MATUMBO NI MOTO.

Ukweli ndio huo LOWASSA KAWAZIDI KILA CORNER Mmebakia na ubwatukaji tu.

Nakushangaa sana na ninapata mashaka kuona kijana kama wewe unampigia fisadi chapuo aingie ikulu.Ulishawahi kujiuliza kuwa hiyo buku tano ya MB anayokupa kila siku ili uingie huku kumfagilia atairudisha lini pindi atakapo kuwa Rais? Naomba nikukumbushe tu kuwa hawezi kuwa Rais.Haipo sabuni yoyote ambayo unaweza ukamsafisha nayo ili aonekane msafi,ni mchafu na kila mtu anajua na ndio maana hatuhitaji kuongozwa na mtu mchafu hamna nafasi nyingine ya kutuibia.
 
Nakushangaa sana na ninapata mashaka kuona kijana kama wewe unampigia fisadi chapuo aingie ikulu.Ulishawahi kujiuliza kuwa hiyo buku tano ya MB anayokupa kila siku ili uingie huku kumfagilia atairudisha lini pindi atakapo kuwa Rais? Naomba nikukumbushe tu kuwa hawezi kuwa Rais.Haipo sabuni yoyote ambayo unaweza ukamsafisha nayo ili aonekane msafi,ni mchafu na kila mtu anajua na ndio maana hatuhitaji kuongozwa na mtu mchafu hamna nafasi nyingine ya kutuibia.

UKWELI WATZ mnashangaza sana mimi sikujui na wewe hunijui kwani kusema uongo kiasi hiki?
Sipokei buku za Lowassa mbona mnageuka kuwa waganga wa kienyeji watz wenzangu? maisha ya kubashiri ovyo ovyo hayo sio kabisaaa.
O
Halafu unanikumbusha nini juu ya Lowassa Wenye tuhuma za wazi juu ya Edward Lowassa hakuna hata mmoja wangekuwepo huu ndio wakati wa MAKADA WA CCM kusemana waziwazi ili aliyemchafu atupwe mbali mbona hamsemi kwenye hio Richmond ama ufisadi wa lowassa alitia tshs ngapi mfukoni mwake? ESCROW inajulikana ni akina nani wametafuna fedha na baadhi yao ndio hao wametangaza nia.KWANINI UFISADI WA LOWASA NI FUMBO?

NYAMAZENI KIMYA MAANA MNASUMBULIWA NA UONGO ,UNAFIKI NA CHUKI BINAFSI DHIDI YA LOWASSA.
 
Fisadi Lowassa aliulizwa kuhusu mabilioni aliyokuwa anatoa rushwa kwenye nyumba za ibada kayapata wapi, akadai si pesa zake ni za marafiki zake. Akaambiwa aweke list ya majina ya hao marafiki zake na kiasi alichotoa kila mmoja mpaka kesho kutwa anang'aa macho kuiweka hadharani hiyo list aliyoombwa miezi chungu nzima iliyopita.

alafu huyu fisadi ndio akaja na slogan ELIMU .. ELIMU .. ELIMU kupitia CHADEMA
 
Back
Top Bottom