Uchaguzi 2020 Haileti mantiki

hippocratessocrates

JF-Expert Member
Jul 1, 2012
3,598
1,539
Katika uchaguzi huru na wa haki, kila mpiga kura huwa na uhuru wa kuchagua mgombea yeyote anayeona anafaa lakini pia huwa huru kwa lolote ikiwa kura yake ameiharibu, amechagua kiongozi ambaye hatafaa au yule anayefaa.

Katika uchaguzi wa mwaka 2020 Tanzania, inaweza kuonekana ulipagwa kwa ubora (ubora wa siku zaidi ya moja) za upigaji kura, ikipendekezwa kwa makundi maalumu mfano wanausalama kama vile Jeshi la polisi,ulinzi,wanajeshi n.k

Tukumbuke Jeshi lolote humtii Amiri Jeshi mkuu na halipaswi kuenenda kinyume na matakwa ya amiri jeshi mkuu. Na hivyo katika uchaguzi wa mwaka huu 2020 Tanzania, "uhuru" wa wanausalama n.k kwenda kupiga kura siku tofauti na "raia" wengine ni kuondolewa uhuru wao.

Ni nani asiyejua kura zinahesabiwa?
Katika heshima ya watumishi wa umma, jeshi n.k kuwa mkubwa yuko sahihi siku zote. Ni mwana jeshi gani -anga,ardhini,majini n.k atakayekuwa na uhuru wa kupiga kura kinyume na chama tawala cha amiri jeshi mkuu na awe salama?

Makundi ya wahitaji maalumu mfano walemavu, wazee sana, wajawazito n.k kwanini hawa hawakuwa na siku yao pekee? Ikiwa walipishwa na mahali pengine kuwekewa msururu/ mstari/ foleni yao pekee kwanini ishindikane kwa wanaulinzi na usalama?

Ni dhahiri ni njia ya utisho usioonekana kwa macho na kwa urahisi kwa wanausalama, jeshi, watumishi wa umma n.k ili kujihakikishia kura kwa kiongozi mkuu wa umma na jeshi.
 
Inaonekana Tanzania chama kisafi kuliko vyote ni ccm ndio maana wamechukua majimbo yote.japo sio sawa hata kidogo hakuna aliyekamilika kiasi hicho chini ya hili jua. Ni wazi hata mumngu mwenyewe pamoja na ukamilifu wake lakini bado ana mpinzani wake ambaye ni lucifer hata mwanaye yesu kristo pamoja na ukamilifu wake wote bado alipata mpinzani Yuda eskarioti ccm ni nani mpaka wakubalike kiasi hicho, ngekewa hii!!! 😎
 
Inaonekana Tanzania chama kisafi kuliko vyote ni ccm ndio maana wamechukua majimbo yote.japo sio sawa hata kidogo hakuna aliyekamilika kiasi hicho chini ya hili jua. Ni wazi hata mumngu mwenyewe pamoja na ukamilifu wake lakini bado ana mpinzani wake ambaye ni lucifer hata mwanaye yesu kristo pamoja na ukamilifu wake wote bado alipata mpinzani Yuda eskarioti ccm ni nani mpaka wakubalike kiasi hicho, ngekewa hii!!! 😎
Kura ndo zmeongea sasa ulitaka wafanye nn
 
Mmeweka mawakala hamjaweka?
Hao mawakala watabadili nini ikiwa nyinyi hamkutaka kwenda katika haki. Acheni kuhalalisha wizi wenu wa fedha za watanzania bila aibu tena mchana kweupe.

Kulikuwa na haja gani kusema tutakuwa na uchaguzi mkuu tena kwa kutenga mabilioni ya pesa kwaajili ya kuukamiilisha mchakato wa uchaguzi ili hali mwajua hatutokuwa na uchaguzi bali uteuzi.

Tena bila aibu eti unasingizia mawakala!!! Kwamba wao ndio walikuwa wasimamizi wa Uchaguzi ama!!! Shame on you 😑😑
 
Hao mawakala watabadili nini ikiwa nyinyi hamkutaka kwenda katika haki...
Acheni kuhalalisha wizi wenu wa fedha za watanzania bila aibu tena mchana kweupe....
Kulikuwa na haja gani kusema tutakuwa na uchaguzi mkuu tena kwa kutenga mabilioni ya pesa kwaajili ya kuukamiilisha mchakato wa uchaguzi ili hali mwajua hatutokuwa na uchaguzi bali uteuzi..
tena bila aibu eti unasingizia mawakala!!! Kwamba wao ndio walikuwa wasimamizi wa Uchaguzi ama!!! Shame on you 😑😑


Uchaguzi ulikua mweupe, wakala wenu walikuepo, kura zmehesabiwa, matokeo yametoka sasa unataka kujitetea nn? We we ndo umeona zaidi ya mawakala?
 
Alafu MBNA wachangiaji hakuna Leo, wamepata pressure nn
Swali lako amelijibu vizuri kabisa huyu mtumishi Bagonza WOTE HAWAAMINI...



Na Askofu Benson Bagonza, KKKT Dayosisi ya Karagwe



Waliopiga kura hawaamini,

Waliogoma kupiga kura hawaamini,

"Walioshinda" hawaamini,

"Walioshindwa" hawaamini,

Walioshuhudia hawaamini,

Waliohesabu kura hawaamini,

Wasimamizi hawaamini,

Waangalizi wa ndani na nje hawaamini,

Walinzi wa amani hawaamini,



KWA nini lakini?



KWA sababu mwaka 2019 baada ya Uchaguzi wa serikali za mitaa,



"Walioshinda" hawakuwa na furaha,

"Walioshindwa" hawakuwa na furaha,

Waliopiga kura, ambao hawakupiga kura, waliohesabu, waliotangaza na waliosikia, WOTE hawakuwa na furaha. FURAHA alipotea, hajarudi. Sasa na IMANI ametoweka.



Usinibishie kwa sababu ubishi ni hulka ya watu waliopoteza furaha na Imani.



Nani anafuata kuwafuata FURAHA na IMANI?
 
Inaonekana Tanzania chama kisafi kuliko vyote ni ccm ndio maana wamechukua majimbo yote.japo sio sawa hata kidogo hakuna aliyekamilika kiasi hicho chini ya hili jua. Ni wazi hata mumngu mwenyewe pamoja na ukamilifu wake lakini bado ana mpinzani wake ambaye ni lucifer hata mwanaye yesu kristo pamoja na ukamilifu wake wote bado alipata mpinzani Yuda eskarioti ccm ni nani mpaka wakubalike kiasi hicho, ngekewa hii!!! 😎
Watz wanaipenda sana ccm ndio maana wapo majumbani wanafurahia ushindi wa ccm kwa amani. Kinyume na hapo wangekuwa mabarabarani wanaandamana.
 
Watz wanaipenda sana ccm ndio maana wapo majumbani wanafurahia ushindi wa ccm kwa amani. Kinyume na hapo wangekuwa mabarabarani wanaandamana.
waandamane nini wakati iko wazi uchaguzi haukwepo Tanzania bali Kulikuwa na igizo la uchaguzi ⚠
 
Uchaguzi ulikua mweupe, wakala wenu walikuepo, kura zmehesabiwa, matokeo yametoka sasa unataka kujitetea nn? We we ndo umeona zaidi ya mawakala?
Ni kweli kabisa uchaguzi ulikua mweupe, ila vipi hizo kura fake zmetokea wap!?
Ukinijibu hili ntakuunga mkono kabisa kua CCM inastahili hayo majimbo yote.
 
Ni kweli kabisa uchaguzi ulikua mweupe, ila vipi hizo kura fake zmetokea wap!?
Ukinijibu hili ntakuunga mkono kabisa kua CCM inastahili hayo majimbo yote.

Wakala wenu wanafanya nn sasa? Hakuna kura yoyote fake, si hata lissu alipiga kura akasema uchaguzi unaenda vizuri, sasa .mdomo wa nn
 
Swali lako amelijibu vizuri kabisa huyu mtumishi Bagonza WOTE HAWAAMINI...



Na Askofu Benson Bagonza, KKKT Dayosisi ya Karagwe



Waliopiga kura hawaamini,

Waliogoma kupiga kura hawaamini,

"Walioshinda" hawaamini,

"Walioshindwa" hawaamini,

Walioshuhudia hawaamini,

Waliohesabu kura hawaamini,

Wasimamizi hawaamini,

Waangalizi wa ndani na nje hawaamini,

Walinzi wa amani hawaamini,



KWA nini lakini?



KWA sababu mwaka 2019 baada ya Uchaguzi wa serikali za mitaa,



"Walioshinda" hawakuwa na furaha,

"Walioshindwa" hawakuwa na furaha,

Waliopiga kura, ambao hawakupiga kura, waliohesabu, waliotangaza na waliosikia, WOTE hawakuwa na furaha. FURAHA alipotea, hajarudi. Sasa na IMANI ametoweka.



Usinibishie kwa sababu ubishi ni hulka ya watu waliopoteza furaha na Imani.



Nani anafuata kuwafuata FURAHA na IMANI?

Dogo, tuliwaaambia APA APA jf mwenendo wenu sio mzuri mkipata hata mbunge mmoja mshukuru Mungu , nyie mnajikuta wajuaji kuliko wanaowapigia kura? Yametoka kama tulivowaambia hapa
 
Wakala wenu wanafanya nn sasa? Hakuna kura yoyote fake, si hata lissu alipiga kura akasema uchaguzi unaenda vizuri, sasa .mdomo wa nn
 

Attachments

  • Screenshot_20201029-151932.png
    Screenshot_20201029-151932.png
    162 KB · Views: 1
Back
Top Bottom