jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
Wakati jana Mheshimiwa Sabaya akielezea ugumu wa Wilaya ya Hai kiuhalifu leo Gazeti la Mwananchi mtandaoni linatuambia kisa hiki cha kusikitisha.
"Mwili wa mhasibu wa Shule ya Sekondari Nronga inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Helga Lema umekutwa kichakani.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumanne Mei 12, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Amon Kakwale amethibitisha kifo hicho akibainisha kuwa kimetokea jana asubuhi katika kijiji cha Nronga wilayani Hai.
"Ni kweli kuna mwili wa mwanamke mmoja, mhasibu wa Shule ya Sekondari Nronga umekutwa pembeni mwa barabara,” amesema akibainisha kuwa uchunguzi wa kifo hicho unaendelea na kwamba mwili umehifadhiwa katika hospitali ya Machame wilayani Hai."
Chanzo: Mwananchi
"Mwili wa mhasibu wa Shule ya Sekondari Nronga inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Helga Lema umekutwa kichakani.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumanne Mei 12, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Amon Kakwale amethibitisha kifo hicho akibainisha kuwa kimetokea jana asubuhi katika kijiji cha Nronga wilayani Hai.
"Ni kweli kuna mwili wa mwanamke mmoja, mhasibu wa Shule ya Sekondari Nronga umekutwa pembeni mwa barabara,” amesema akibainisha kuwa uchunguzi wa kifo hicho unaendelea na kwamba mwili umehifadhiwa katika hospitali ya Machame wilayani Hai."
Chanzo: Mwananchi