hahah Vibuti vyengine bana!! (Single mwaka mzima)

buzzfeed

Senior Member
Jan 4, 2018
145
107
Habari zenu wanaJamii.. Nina imani mko Salama kabisa..

Kwa mara nyengine tena nimekuja na story hii.. inayohusu, ni namna gani nilivyouanza na kuumaliza mwaka wa 2018.

Nirudishe Historia nyuma kidogo mpaka mwaka 2017, ambapo kuanzia mwezi wa 9 mpaka wa 11, niliachana na mabinti wanne ambao nilikuwa nao kwenye mahusiano.. Na mwezi wa 12 nikapata binti mwengine.. ambaye huyu mahusiano yake kidogo yalikuwa serious, kwa maana pia alisisitiza kunipeleka mpaka kwao na alinitambulisha.

Maisha yakaenda na Mwezi ukafika Mwishoni.. Yaani kuukaribisha mwaka 2018 sasa.

Kama ishara ya shukrani na Upendo nikaamua kujitutumua nikamnunulia yule binti simu flani kali ili akaribishie mwaka.. ingawa sikuwa nimemkabidhi

Usiku wake nikaenda mpaka Chuo alichokuwa anasoma.. Nikapaki ndinga nikawa nimekaa naye hapo huku tukisubiri mwaka mpya uingie.. Sasa ile saa tano na nusu inafika.. kidogo wakaja jamaa wawili waliovalia nguo za kiaskari na wakapiga lock Gari yangu, na kuanza kunizingua vibaya, hadi yule binti akaanza kupata wasiwasi.. ila mimi nikawa nawajibu kawaida tuu, na nikafunga gari ..nikasepa zangu kwenye kituo chao kidogo cha polisi ili niepushe utata nikiwa na yule Binti wa watu..

Tuliyazungumza yakaisha na hapo ndipo nilipopata nafasi ya kwenda kutoa gari yangu na kuagana na yule binti mida ya saa 6 na nusu.. yaani mwaka mpya 2018.

Ule mwaka ukawa umeingia kwa style hiyo ya shari.. na yule binti kiukweli alionekana amechukizwa, hivyo hakutaka kuzungumzia jambo lolote na hata zawadi yake hakutaka kuipokea.. basi nikaamua kumpeleka hadi kwenye malazi yake na kumwacha hapo nikiwa bado nambembeleza..

Cha kushangaza kesho yake naamka asubuhi mida ya saa 3 napokea Text inasema ..PLEASE CAN WE END THIS AND JUST BE FRIENDS.. nilishangaa sana na kuishia kucheka tuu.. na nilishukuru kwa upande mwengine kwa maana Simu yangu aina ya iPhone 6s ilipona.. maana sikutaka kubembelezana naye..

Ila nahisi lilikuwa Gundu, kwa maana tangu pale.. sikupata binti hadi mwaka huu tarehe 2 mwezi wa 1..

Karibuni.





Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom