Hadithi ya umslopagaas

Huko alipokewa kwa ukarimu akakaa kwa muda, mpaka makuhani wa nchi ile walipo chochea habari ya kuwa yeye ni shetani, basi watu wakamfukuza, akasafiri muda wa miezi minane hata akafika mahali alipomkuta Bwana Meckenzie anakufa.
Inaendelea tulipo ishia..

Basi, hivyo ndivyo nilivyosikia, na hizo ndizo habari ninazozijua. Mimi nasadiki ya kuwa ni uwongo mtupu lakini ukitaka kujua habari zaidi, afadhali uufuate mto Tana mpaka mahali hapo anapokaa Bwana Mackenzie, ukamuulize yeye habari hizo.’’

Sir Henry na mimi tulitazamana, maana sasa tumekwisha pata habari za kuzithibitisha zile tulizokwishazisikia. Nikasema, ‘’Nadhani tutakwenda kwa Bwana Mackenzie.’’

Bwana Balozi akasema, ‘’Vyema, ni shauri linalowafaa zaidi, lakini nawaonya ya kuwa labda safari yenu itakuwa ya matata, maana nimesikia kuwa Wajivuni wanatembeatembea huko, nao kama mjuavyo si watu wapole.


Shauri litakalofaa zaidi ni kuchagua watu wachache wenye sifa nzuri wawe watumishi na wawindaji wenu na kuajiri wapagazi kuichukua mizigo yenu toka mji mpaka mji.

Jambo hli litawasumbua, lakini nadhani litakuwa shauri jema na rahisi kuliko kuajiri wapagazi kufuatana nanyi safari nzima, tena udhia wa wapagazi kutoroka utapungua.’’

Kwa bahati yetu, walikuwapo Lamu askari wa Kikazi wachache. Wakazi wamefanana na Wajivuni ni watu hodari wenye nguvu, wenye tabia nyingi njema kama zile za Wazulu, tena ni wawindaji hodari.

Watu hawa walikuwa wamekwenda safari ndefu pamoja na Mwingereza aliyetoka Mombasa akasafiri kuuzunguka mlima Kilimanjaro.


Mwingereza huyo maskini alikufa kwa ugonjwa wa homa wakati alipokuwa akirudi. Alikuwa amekwisha fika karibu na Mombasa ; ilibaki Safari ya siku moja tu.

Basi, wawindaji wake walimzika, kisha wakaja mpaka Lamu katika jahazi.
Rafiki yetu Bwana Balozi alitushauri afadhali tujaribu kuwaajiri watu hao, na kwa hivi asubuhi yake tulifuatana na mkalimani wetu tukaenda ili tujaribu kupatana nao.


Tuliwakuta katika nyumba mwisho wa mji. Watatu walikuwa wamekaa nje ya nyumba, nao walikuwa watu wazuri wanaonekana kama kwamba wanaweza kutumainiwa.


Tuliwaambia sababu tuliyowaendea, na kwanza hawakukubali hata kidogo. Walisema ya kuwa hawawezi kabisa kwenda pamoja nasi, ya kuwa wamechoka kabisa kwa safari ndefu, tena mioyo yao ni mizito kwa kufiwa na bwana wao. Walikusudia kurudi makwao wakapumzike kwa muda.


Nikawauliza wenzao wako wapi, maana niliambiwa ya kuwa wako sita, nahapo niwatatu tu. Mmoja wao akasema, ‘’Wamo ndani ya nyumba wamepumzika baada ya taabu waliyopata. Usingizi unawaelemea machoni ni bora walale usingizi, maana usingizi huleta usahaulifu.’’ Lakini walikubali kuwaamsha.


Baadaye kidogo wale watatu wengine walitoka nyumbani, wanapiga miayo watu wawili wa kwanza walikuwa wa kabila lile lile na namna ile ile ya wale tuliowakuta wamekaa nje ya nyumba, lakini Yule watatu alinifanya nishtuke mno.


Alikuwa mtu mrefu sana, nakisia urefu wake ulikuwa kadiri ya futi sita na inchi tatu, lakini mwembamba, na viungo vyake vilikuwa na nguvu kama nyuzi za chuma.

Mara nilipomtazama nilitambua ya kuwa huyu si Mkazi ni Mzulu halisi. Alitoka, na huku ameuweka mkono wake mwembamba mbele ya uso wake kukiziba kinywa chake alipokuwa akipiga miayo, nikaona ya kuwa ni mtu mzima, naye ana shimo lenye pembe tatu katika paji la uso wake.

Kisha, aliuondoa mkono wake, nikaona uso wa nguvu wa Kizulu, na kinywa cha ucheshi, na ndevu fupi zenye mvi kidogo, macho ya kahawia makali kama ya mwewe.


Nikamtambua mara ile, ingawa nilikuwa sijamwona kwa muda wa miaka kumi na miwili. Nikasema kwa sauti ndogo kwa lugha ya Kizulu, ‘Hujambo Umslopogaas?’’

Mtu huyo mrefu, ambaye hadithi zake nyingi zilisimuliwa katika nchi ya Wazulu, na ambaye katika watu wake huitwa ‘’Gogota,’’ na ‘’Mchinjaji’’ alishtuka, na shoka lake la vita lenye kipini kirefu lilikuwa karibu kumponyoka kwa mshangao.
Aisee, hii kitu ni murua sana
 
Basi nilikaa nikivuta tumbako na kuwaza juu ya mambo mengi na hatari ipo ya kupatwa na homa kwa kulala mahali kama hapa, tena mguu wangu wa kuume umekufa ganzi kwa kukaa hali umekunjwa katika mtumbwi, lakini nilianza kuufurahia uzuri wa usiku.

Miali ya mbalamwezi ilichezacheza juu ya uso wa maji yanayopita kasi kuendea baharini, kama maisha ya wanadamu yapitavyo kuendea kaburini, mpaka yakang’aa kama utando mpana wa fedha, yaani mahali pa wazi pasipo fikiwa na vivuli vya miti.

Lakini karibu na kando ya mto palikuwa giza sana na upepo ulivuma katika matete, ukafanya sauti ya kuhuzunisha.


Upande wa kushoto, ng’ambo ya mto, palikuwapo namna ya ghuba ndogo yenye mchanga pasipo na miti, na hapo niliweza kuona vivuli vya wanyama wengi waliokuja kunywa maji, mpaka kwa ghafla nilisikia ngurumo ya kutisha sana, na mara ile wote wakatimka.

Baadaye kidogo, niliona umbo kubwa la simba akija kunywa maji baada ya kula kwake.

Halafu aliondoka, ndipo niliposikia kishindo katika matete kadiri ya yadi hamsini kutoka hapo tulipokuwapo, na baada ya dakika chache kitu kikubwa cheusi kiliibuka katika maji.

Kumbe, ni kichwa cha kiboko. Kikazama tena bila kufanya sauti, kikaibuka tena karibu, yaani kadiri ya yadi tano tu kutoka mahali tulipo.

Hapo niliona ya kuwa yupo karibu sana, na kwa hivi sikuona raha, na hasa kwa kuwa alionekana kama atakaye kujua mitumbwi yetu ni kitu gani.

Alikifunua kinywa chake kipana, labda apige miayo tu, nikayaona meno yake, nikafikiri jinsi anavyoweza kuusagilia mbali mtumbwi wetu mdogo kwa dhoruba moja.

Nilianza kufikiri labda itafaa nimpige risasi, lakini nilipofikiri zaidi, niliazimu kumwacha kama asipojaribu kuushambulia mtumbwi. Halafu alizama tena bila kufanya sauti hata kidogo, wala sikumwona tena.

Papo hapo nilitupa macho ng’ambo ya kuume, nikawa kama ninaweza kuona kitu cheusi kinapita katika mashina ya miti.

Macho yangu ni makali sana, nami nadhani niliona kitu kwa hakika, lakini kama ni ndege, au mnyama, au mtu sikuwa na hakika.

Lakini papo hapo wingu jeusi lilipita mbele ya mwezi, kwa hiyo sikukiona kilekitu tena. Tena, papo hapo nilisikia mlio kama wa bundi akilia mfulilizo, baadaye kukawa kimya kabisa isipokuwa sauti za kuchakacha katika miti na matete, wakati upepo ulipoyatikisa.

Lakini kwa jinsi isiyoelekezeka, sasa nilianza kushuku hatari za kuona hofu,hapakuwapo wala sababu ya dhahiri ya kunitia hofu hivyo zaidi ya zile zinazomzunguka msafiri yeyote katika nchi ya Afrika, lakini hata hivyo, bila shaka niliona hofu.

Lakini nilikaza nia nisishindwe na hofu, ingawa jasho baridi lilinitoka pajini mwa uso. Wala sikukubali kuwaamsha wenzangu.

Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, na moyo wangu ulinipigapiga kama moyo wa mtu anayekaribia kufa. Na mishipa yangu ilinichezacheza kana kwamba kitisho kiovu kiko karibu. Watu waliopata kuota jinamizi, watafahamunamna hali yangu ilivyokuwa.
Daaah, hatari
 
Lakini hata hivyo nilijikaza nikakaa kimya, nikageuza uso wangu tu kumtazama Umslopogaas na Wakazi wale wawili waliokuwa wamelala kando yake.

Nilisikia kishindo kidogo cha kiboko mbali, na Yule bundi alilia tena, na upepo ulianza kuvuma katika miti na kufanya sauti ya kuhuzunisha iliyopoozesha moyo. Baadaye nilipata kujua kuwa Wajivuni huitana kwa kuiga sauti ya bundi.

Juu niliona wingu jeusi, na chini maji meusi yalikuwa yakipita kasi, nikaona kama kwamba mimi na mauti tupo katika yake. Niliona ukiwa kabisa.


Mara damu yangu ilikuwa kama imevia katika mishipa yangu, na moyo wangu kusimama kimya. Je, ni ndoto tu ama ndio mwendo?

Niliyageuza macho yangu kuutazama mtumbwi wa pili uliokuwa ukielea kando yetu, nisiuone, ila badala yake niliona mkono mweusi mwembamba umeinuliwa juu ya ubavu mwa mtumbwi.

Hakika ni jinamizi! Lakini mara ile uso mwovu ulitokea juu kama kwamba umetoka majini, ndipo mtumbwi ulipoinama, kisu kikang’aa ghafla, na Mkazi mmoja aliyekuwa amelala kando yangu akapiga ukelele na kitu cha moto kilichuzurika usoni pangu.

Mara ile kuduwaa kwangu kukakoma, nikatambua kwamba si jinamizi, ila tumeshambuliwa na Wajivuni wanaogelea majini.

Nikashika silaha ya kwanza niliyoweza kuipata ikatokea kuwa ni shoka la vita la Umslopogaas, nikapiga kwa nguvu zangu zote pale nilipokuwa nimekiona kisu kinang’aa .
Pigo liliangukia juu ya mkono wa mtu likaugandamiza juu ya ubavu mnene wa mtumbwi, na kuukata kisiginoni.

Yule mtu asifanye sauti hata kidogo akatoweka kama kivuli, alikuja kama kivuli na akaondoka kama kivuli. Ameacha nyuma yake ule mkono wake wenye damu ungali umeshika sime ile iliyokuwa imechomwa katika moyo wa mtumishi wetu msikini.


Mara kulikuwa ghasia na fujo, nikadhani, sijui ni kweli au je, nikaona vichwa vyeusi vingine vikielea majini kuendea ng’ambo ya kuume, ambako mtumbwi wetu uliendea kasi kwa sababu kamba ile iliyokuwa na nanga ya jiwe imekatwa kwa kisu.


Mara nilipotambua hivyo, nilifahamu pia ya kuwa shauri lao ni kuikata kamba ili mtumbwi uchukuliwe na maji ili kuiendea ile ng’ambo ya kuume; na huko bila shaka Wajivuni wanangojea kutuchoma kwa mikuki yao.

Basi, nilishika kafi moja mwenyewe, nikamwambia Umslopogaas aishike nyingine, maana wale Wakazi walikuwa wameduwaa kwa hofu hata kushindwa kuhema, tukapiga kafi kwa nguvu kurejea tena katikati ya mto.

Wala hatukufanya hivyo kwa haraka zaidi kuliko ilivyopasa, maana katika dakika nyingine tungali kwamba na bila shaka ingalikuwa ndiyo mwisho wetu.

Mara tulipofika katikati ya mto tena, tulianza kupiga kafi kupaendea pale ulipokuwapo ule mtumbwi mwingine umetiwa nanga nayo ilikuwa kazi ngumu na hatari pia, kwa sababu hakuna la kutuongoza ila sauti ya Good, maana alipiga kelele mara kwa mara.

Mwishowe tuliufikia mtumbwi, tukashukuru tulipoona ya kuwa hawakushambuliwa.

Haikosi ule mkono ulioikata kamba ya mtumbwi wetu ungaliikata yao, na Yule mtu asingalivutwa na tamaa ya kuua na jambo hilo, ingawa lilitupotezea maisha ya mtu mmoja na Yule Mjivuni mkono wake, lakini pia lilituokoa sote wengine tusiangamizwe.

Kukosa kukiona kile kitisho kiovu kikitokea juu ya ubavu wa mtumbwi, kitisho ambacho sitakisahau mpaka siku ya kufa kwangu. Mtumbwi wetu ungalichukuliwa kando ya mto kabla sijatambua umepatwa na nini, na habari hizi hazingaliandikwa nami.
Ahsante sana mkuu blackstarline
 
SURA YA TATU

Tulifunga mtumbwi wetu pamoja na mtumbwi ule mwingine kwa kipande cha kamba kilichobaki, tukakaa tukingojea mapambazuko, na kufurahi kwa vile tulivyookoka.


Baada ya kukesha sana, kukapambazuka, nami sijapata kupendezwa kuuona mwangaza kama nilivyopendezwa kuuona siku ile, ingawa uliangaza juu ya kitu cha kutisha ndani ya mtumbwi wangu.

Maana, pale chini katika mtumbwi Yule maskini askari alikuwa amelala na sime imesimama kifuani mwake, na ule mkono uliokatwa ungali umeishika sime.


Sikuweza kuvumilia kumtazama zaidi, basi, nililivuta ndani lile jiwe lililokuwa nanga yetu, nikamfungia Yule askari aliyeuawa, nikamtumbukiza majini, akazama mpaka chini.


Kisha, tulitoa mtu mmoja katika mtumbwi mwingine tukamweka katika mtumbwi wangu, tukaendelea tena katika safari yetu, wote tumeshikwa na majonzi, wala hatukuweza kuona raha kwa kufikiri juu ya mambo ya mbele yetu, ila tulitumaini kufika misioni kabla ya kuingia usiku.


Hapo mambo yalizidi kuwa mabaya, maana jioni ilipokaribia, ilianza kunyesha mvua tukalowa kabisa, tena ikawa lazima pengine kukumba maji katika mitumbwi, na kwa kuwa upepo ulitulizwa na mvua, matanga hayakufaa kitu, ikawa lazima tupige kafi kadiri tulivyoweza.


Saa tano tulishuka mahali pa wazi kando ya mto kwa upande wa kushoto, na kwa kuwa mvua ilipungua kidogo, tulivua samaki tukazibanika motoni. Hatukuthubutu kwenda kutafuta wanyama.

Saa nane tuliondoka tena, tukachukua akiba ya samaki wa kuchoma na baada ya kitambo ilianza kunyesha tena mvua nyingi kuliko kwanza.


Tena, tulianza kuona shida zaidi kwenda mbele mtoni kwa sababu ya miamba mingi, na mafungu ya mchanga, na nguvu ya mkondo wa maji ilizidi, basi, ilikuwa dhahiri ya kuwa hatutawahi kuifikia nyumba ya Bwana Mackenzie kabla usiku haujaingia na habari hizi zilizidi kutusumbua.


Ingawa tulivuta kafi kadiri tulivyoweza, lakini hata hivyo hatukuweza kwenda mbele zaidi ya maili moja kwa saa moja, na ilipofika saa kumi na moja jioni, tulikuwa tumechoka taabani, na kwa kadiri tulivyoweza kukisia, nyumba ya misioni ipo mbali mwendo wa maili kumi.


Basi, tulianza kutengeneza mambo kadiri tulivyoweza tayari kwa usiku.

Baada ya mambo yaliotokea jana, hatukuthubutu kufanya kambi nchi kavu, na hasa kwakuwa kingo za mto Tana zimefunikwa na vichaka vinene vya kutosha Wajivuni elfu tano kujificha humo wasionekane, na kwanza tulifikiri tutakuwa hatuna budi kukaa tena katika mitumbwi.

Lakini kwa bahati, tuliona kisiwa kidogo, kadiri ya upana na urefu wa yadi kumi na tano, katikati ya mto. Basi, tulipiga kafi mpaka kufikia, tukaiegesha mitumbwi yetu, tukashuka na kutengeneza mambo kadiri tulivyoweza.


Mvua ilizidi kunyesha, tukaona baridi hata ndani ya mifupa yetu, wala hatukuweza kukoka moto.

Lakini mvua ilitufariji kwa neno moja, yaani Wakazi walituambia kuwa Wajivuni hawata tushambulia wakati wa mvua kwa sababu inawasumbua sana. Tulikula kipande cha samaki kilicholowa maji, isipokuwa Umslopogaas, maana yeye kama Wazulu wote, hali samaki.

Ndipo ulipoanza usiku wa taabu kupita zote ninazozikumbuka, isipokuwa taabu ya usiku ule ambao sisi watu weupe watatu tulivumilia pamoja tulipokuwa karibu kuangamia kwa baridi na theluji juu ya Ziwa la Sheba katika safari yetu ya kuiendea nchi ya Wakukuana.

Usiku ulikuwa kama hauna mwisho, na mara mbili tatu nilifikiri labda askari wetu wawili watakufa kwa maji na baridi na taabu. Bila shaka wangalikufa kama tusingaliwapa divai mara kwa mara.


Niliweza kuona ya kuwa hata Yule mzee shupavu Umslopogaas naye pia anaona maumivu, ingawa alikaa kimya tu, wala si kama wale Wakazi waliolalamikia hali zao bila kunyamaza. Mambo yalizidi kuwa mabaya kwenye saa saba ya usiku tuliposikia tena mlio wa bundi.

Basi, tukajifanya tayari kujitetea kama tukishambuliwa, lakini nadhani tungalishambuliwa wakati huo, tungalishindwa upesi.

Lakini labda mlio ulikuwa wa bundi hasa, au labda Wajivuni nao waliona taabu hata hawana moyo kutushambulia. Kwa vyo vyote hatukuwaona kabisa.

Hatimaye kulipapazuka na ukungu ukatambaa juu ya uso wa maji, na kulipokuwa kweupe, kukatakata, na mvua iliacha kunyesha, ndipo jua tukufu lilipochomoza, tukajivuta miguu, tukaenda tukasimama katika joto la jua, tukashukuru.
 
Naweza kufahamu kwa nini watu wengine wasiostarabika huliabudu jua, na hasa kama hali ya maisha yao huwalazimisha pengine kuvumilia mvua na baridi kali.


Baada ya kupita nusu saa, tulikuwa tukiendelea tena vizuri kwa msaada wa upepo mzuri. Mioyo yetu ilichangamka kwa kuuona tena mwanga wa jua, tukawa tayari kuzicheka shida na hatari zilizotuelemea jana.


Basi, hivyo tuliendelea kwa furaha mpaka kadiri ya saa tano, na hapo tulipoanza kufikiri kushuka kama ilivyokuwa desturi yetu ili tujaribu kuwinda wanyama tupate kula, mara mto ulipinda, tukaona nyumba imara ya Kizungu iliyozungukwa na baraza imesimama vizuri juu ya mwinuko.

Nyumba ilikuwa imezungukwa na boma la mawe, na handaki nje ya boma.
Karibu na nyumba palikuwa na mti mrefu sana, namna ya msunobari.

Mimi nilikuwa wa kwanza kuiona ile nyumba, nami sikuweza kujizuia nisipige ukelele wa furaha, na wenzangu nao na watumishi wetu pia wakapiga ukelele kadhalika.


Sasa hatukuwa na nia ya kusimama tena. Tukasukuma mbele kwa nguvu, lakini ingawa nyumba ilionekana kama I karibu, ilikuwa mbali kwa kuufuata mwendo wa mto, wala hatukuifikia mpaka saa saba.

Ndipo tulipojiona chini ya mwinuko iliposimama ile nyumba.

Tuliisogeza mitumbwi, yetu mpaka kando ya mto, tukashuka, tukawa katika kuikweza nchi kavu ndipo tulipoona watu watatu waliovaa mavazi ya Kizungu wanatujia kwa haraka wakipita katikati ya miti.

Bwana Good aliwachungulia kwa rodi yake, akasema, ‘’Bwana mmoja, na Bibi mmoja na mtoto mwanamke mmoja, wanakuja kistaarabu karibu na bustani ya kistaarabu kutulaki katika mahali kama hapa kweli hili ni jambo la ajabu kupita yote!’’


Basi, walitukaribia. Yule Bwana Mckenzie alikuwa mtu mwembamba, mwenye mvi, na uso wake ulikuwa wa kupendeza, akasema, ‘’Mhali gani mabwana, natumaini hamjambo?

Watu wangu waliniambia tangu saa moja ya kuwa waliona mitumbwi miwili inakuja mtoni, basi, tumekuja kuwalaki.’’ Na Yule bibi, akasema, ‘’Tumefurahi sana kuonana tena na watu weupe.’’

Tukavua kofia zetu kuwaamkia, tukawajulisha tu nani. Kisha, Bwana Mackenzie akasema, tumefurahi sana kuwaona. Mwaka mzima umepita tangu alipofika hapa mtu mweupe wa mwisho aliyetujia.’’


Huku nyuma tulikuwa tukiupanda ule mwinuko ambao sehemu ya chini yake ni mashamba ya mahindi na maboga na viazi, na vyakula vinginevyo.

Wenyeji wengine, watu wa misioni walikuwa wamejenga nyumba zao katika mashamba hayo.

Katikati ya mashamba palikuwa na barabara, na kando yake ilikuwapo michungwa mingi iliyojaa machungwa.

Tokea hapo nimependa sana bustani, na nilipoiona ile ya Bwana Mackenzie nilifurahi sana, nikasema, ‘’Lo, bwana, tazama jinsi ilivyo nzuri bustani yako’’.

Akajibu, ‘’Kweli, ni bustani nzuri sana, wala si ajabu kwa sababu nimefanya kazi nyingi humo, lakini pamoja na hivyo tabia ya nchi hii ni nzuri, na miti huota vizuri sana.’’

Basi, tukaendelea, tukafika kwenye ile handaki ambayo upana wake ulikuwa futi kumi, imejaa maji, na ng’ambo yake palikuwa na boma la mawe urefu wa kwenda juu futi nane, lina vitundu huko na huko vya kupitishia bunduki.

Na juu yake pametapakaa mawe makali na vigae vilivyosakafiwa katika mgongo wa ukuta.

Bwana Mackenzieakalielekezea kidole chake, akasema, ‘’Hii ndiyo kazi yangu iliyo kubwa, au tuseme hii pamoja na kanisa lililojegwa nyuma ya nyumba.

Ilichukua mimi na wenyeji ishirini muda wa miaka miwili kuichimbua ile handaki, na kulijenga boma, lakini kabisa sikuweza kuona ni salama, mpaka kazi zilipokwisha.

Sasa ninaweza kujitetea juu ya watu wakali wote wa katika nchi ya Afrika, maana chemchem inayojaza handaki maji imo ndani ya boma juu ya mwinuko, nayo hububujika siku zote, nami kila mara ninayo akiba ya chakula nyumbani cha kutosha miezi minne.’’
 
Basi, tulivuka daraja dogo, tukapita katika mlango mwembamba katika ukuta wa boma tukaingia katika bustani nzuri sana.

Katikati ya kiwanja mbele ya nyumba, tuliuona ule mti mrefu, na Bwana Mackenzie alituambia kuwa ni mnara wake wa kuangalia nchi yote, kisha, akasema, ‘’Lakini hamkosi mnaona njaa, basi haya twendeni.’’

Tulipokwisha kula, tuliviwasha viko vyetu vya tumbako, na Sir Henry akasimulia habari za safari yetu, na mkarimu wetu alisikiliza kwa fadhaa.

Akasema, ‘’Ni dhahiri ya kuwa wale Wajivuni waovu wanawafuata, nami nashukuru sana kuwa mmefika nyumbani kwangu salama.

Nadhani hawatadhubutu kuwashambuli hapa. Lakini ni bahati mbaya, maana karibu watu wangu wote wamekwenda pwani kupeleka pembe za ndovu na vitu vingine.

Wako watu mia mbili katika msafara huo, na kwa hivi wamebaki watu ishirini tu wanaoweza kulilinda boma letu ikiwa watatushambulia.

Lakini hata hivyo, nitatoa amri kadha wa kadha ili tusije tukatokewa ghafla.’’ Akamwita mtu mmoja aliyekuwa amesimama nje katika bustani, akamwambia maneno kwa Kiswahili. Yule mtu alisikiliza, kisha, alipiga saluti akaondoka.

Bwana Mackenzie alipokaa tena, nilimwambia, ‘’Natumaini sana ya kuwa hatutawaletea misiba, basi ni afadhali twende mbele na kubahatisha ajali yetu, kuliko kuwaletea wale watu waovu hapa.’’

Akajibu, ‘’Hapana kabisa, hamwendi sasa. Wajivuni wakija, basi watakuja, lakini nadhani nitaweza kuwapokea kwa namna itakayofaa. Mimi siwezi kumwondoa mgeni aende zake hata kama Wajivuni wote wa duniani wakija.’’


Nikasema, ‘’Sasa nakumbuka, Bwana Balozi wa Lamu alituambia kuwa alipata barua kutoka kwako, ambayo kwayo ulimpa habari ya kwamba mtu mmoja alifika toka mbali akasema ameona watu weupe mbali sana ndani ya nchi. Je, unasadiki habari alizokuambia?


Nauliza kwa sababu mara mbili tatu katika, maisha yangu nimesikia tetesi ya habari hizo kwa wenyeji waliotoka kaskazini mbali sana, ya kuwa taifa la watu hao lipo.’’

Bwana Mackenzie asijibu kwanza, ila alitoka chumbani, kisha alirudi tena amechukua upanga wa namna.

Ulikuwa mrefu, na bamba lake ambalo lilikuwa nene na zito lilikuwa limetiwa temsi lote hata kufika karibu na makali yake, na kazi yake ilipambwa kwa dhahabu. Akasema, ‘’Je, umepata kuuona upanga kama huu?’’

Sote tuliutazama sana, tukavitikisa vichwa vyetu.
Akaendelea akasema, ‘’Nimeuleta kuwaonyesha kwa sababu Yule mtu aliyesema ameona watu weupe ndiye aliyeuleta pamoja naye tena, kwa sababu unafanya habari alizozisema kuwa kama kwamba ni kweli.

Kama asingaliuleta nisingalimsadiki. Tazameni; nitawaambieni habari zote kadiri ninavyozijua, lakini si nyingi.

Siku moja jioni nilikuwa nimekaa barazani, na maskini mtu aliyedhoofu sana alikuja akichechemea, akaketi mbele yangu.

Nikamuuliza ana habari gani, akaanza kuniarifu habari kama yeye ni mtu wa kabila linalokaa mbali sana kaskazini.

Na jinsi kabila lake lilivyoangamizwa na watu wa kabila jingine, na yeye pamoja na watu wengine wachache waliosalia, walifukuziwa kaskazini zaidi kupita ziwa liitwalo Laga.

Kutoka huko, alikwenda mpaka ziwa jingine lililoko juu ya mlima, akaliita ‘ziwa lisilo na mwisho kwa kwenda chini.’

Na huko mkewe na ndugu yake wakafa kwa ugonjwa wa kuambukiza labda ndui na kwa hivi watu wa huko walimfukuzia jangwani atoke katika miji yao.

Akatangatanga kupita juu ya milima muda wa siku kumi, kisha, akaingia katika gongo la mwitu wa miti yenye miiba.

Na siku moja akaonekana huko na watu weupe wengine waliokuwa wakiwinda, wakamchukua mahali ambapo watu wote ni weupe, wakaao katika nyumba za mawe.


Alikaa hapo muda wa juma moja amefungiwa katika nyumba, mpaka siku moja mtu mwenye ndevu nyeupe, aliyemtambua kuwa ni mganga, akaja kumtazama, kisha akaongozwa kupita katika mwitu wa miti yenye miiba mpaka jangwani, akapewa chakula na upanga huu, ndivyo alivyosema, akaachwa huru.’’

Sir Henry alikuwa akisikiliza sana habari hizi, akasema, ‘’Ndiyo, halafu alifanya nini?’’
Bwana Mackenzie akasema, ‘’Kadiri alivyosema, alipatikana na taabu na maumivu yasiyo na idadi, akaishi siku nyingi anakula mizizi na matunda ya porini, na vinyama alivyoweza kuvikamata na kuviua.

Mradi aliweza kuishi, na kwa mwendo wa Pole pole alisafiri akijia kusini mpaka akafika hapa.

Sikupata simulizi ya mambo yote ya safari yake, nilimwambia arudi kesho yake, nikamwamuru mmojawapo wa wanyapara amtunze usiku ule.

Yule mnyapara alimchukua, lakini Yule maskini alikuwa na upele mwingi hata mke wake mnyapara asikubali aingie ndani asije naye akapata upele pia. Basi alipewa blanketi akaambiwa alale nje.

Ikatokea ya kuwa wakati huo, simba mmoja alizoea kutembeatembea karibu, na kwa bahati mbaya alisikia harufu ya Yule msafiri maskini, akamrukia, akamuuma kichwa hata karibu kutoka kabisa.

Wale waliokuwamo nyumbani hawakuwa na habari, na huu ulikuwa ndio mwisho wake na wa hadithi yake juu ya watu wale weupe na **** habari hizo ni kweli ama si kweli, siwezi kuwaambia.

Je, wewe Bwana Quatermain waonaje?’’

Nilitikisa kichwa changu, nikajibu, ‘’Mimi sijui.

Yapo mambo mengi ya ajabu yaliyofichika katikati ya kochi hii kubwa, nami sipendi kusema kuwa ni kweli, Ama si kweli.

Lakini liwalo lolote na liwe, tumekaza nia kujaribu kuvumbua habari,. Tumenuia kusafiri mpaka Lekakisera, na kutoka huko tutaenda kule kwenye Ziwa Lagana kama wako watu weupe wanaokaa kupita hapo, basi tutajaribu tuwezavyo kuwagundua.’’

Bwana Mackenzie akasema, ‘’Ninyi watu ni jasiri sana.’’ Akacheka kidogo, tukaziacha habari zile.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom