blackstarline
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 3,092
- 7,468
- Thread starter
- #41
Hahaah pole sanaHasha, huyu kizee kichawi simkosi, Foulata pekee ndiye anayefanya moyo wangu kuwa mzito sana, umauti wake ulinitia ufa moyoni, ukaupasua katikati.
Hahaah pole sanaHasha, huyu kizee kichawi simkosi, Foulata pekee ndiye anayefanya moyo wangu kuwa mzito sana, umauti wake ulinitia ufa moyoni, ukaupasua katikati.
Makumazahn ni jina la utani la ALLAN QUATERMAIN Jina hilo analitumia kwenye hadithi ya Mashimo ya Mfalme Sulemani na pia jina hilo lina tumika kwenye hadithi hii.Pia usisahau na ya MAKUMAZANI.
Karibu sanaHodi humu
Asante mkuu. Nilianza kimya kimya mpaka sawa tuko woteKaribu sana
Aisee, hii kitu ni murua sanaHuko alipokewa kwa ukarimu akakaa kwa muda, mpaka makuhani wa nchi ile walipo chochea habari ya kuwa yeye ni shetani, basi watu wakamfukuza, akasafiri muda wa miezi minane hata akafika mahali alipomkuta Bwana Meckenzie anakufa.
Inaendelea tulipo ishia..
Basi, hivyo ndivyo nilivyosikia, na hizo ndizo habari ninazozijua. Mimi nasadiki ya kuwa ni uwongo mtupu lakini ukitaka kujua habari zaidi, afadhali uufuate mto Tana mpaka mahali hapo anapokaa Bwana Mackenzie, ukamuulize yeye habari hizo.’’
Sir Henry na mimi tulitazamana, maana sasa tumekwisha pata habari za kuzithibitisha zile tulizokwishazisikia. Nikasema, ‘’Nadhani tutakwenda kwa Bwana Mackenzie.’’
Bwana Balozi akasema, ‘’Vyema, ni shauri linalowafaa zaidi, lakini nawaonya ya kuwa labda safari yenu itakuwa ya matata, maana nimesikia kuwa Wajivuni wanatembeatembea huko, nao kama mjuavyo si watu wapole.
Shauri litakalofaa zaidi ni kuchagua watu wachache wenye sifa nzuri wawe watumishi na wawindaji wenu na kuajiri wapagazi kuichukua mizigo yenu toka mji mpaka mji.
Jambo hli litawasumbua, lakini nadhani litakuwa shauri jema na rahisi kuliko kuajiri wapagazi kufuatana nanyi safari nzima, tena udhia wa wapagazi kutoroka utapungua.’’
Kwa bahati yetu, walikuwapo Lamu askari wa Kikazi wachache. Wakazi wamefanana na Wajivuni ni watu hodari wenye nguvu, wenye tabia nyingi njema kama zile za Wazulu, tena ni wawindaji hodari.
Watu hawa walikuwa wamekwenda safari ndefu pamoja na Mwingereza aliyetoka Mombasa akasafiri kuuzunguka mlima Kilimanjaro.
Mwingereza huyo maskini alikufa kwa ugonjwa wa homa wakati alipokuwa akirudi. Alikuwa amekwisha fika karibu na Mombasa ; ilibaki Safari ya siku moja tu.
Basi, wawindaji wake walimzika, kisha wakaja mpaka Lamu katika jahazi.
Rafiki yetu Bwana Balozi alitushauri afadhali tujaribu kuwaajiri watu hao, na kwa hivi asubuhi yake tulifuatana na mkalimani wetu tukaenda ili tujaribu kupatana nao.
Tuliwakuta katika nyumba mwisho wa mji. Watatu walikuwa wamekaa nje ya nyumba, nao walikuwa watu wazuri wanaonekana kama kwamba wanaweza kutumainiwa.
Tuliwaambia sababu tuliyowaendea, na kwanza hawakukubali hata kidogo. Walisema ya kuwa hawawezi kabisa kwenda pamoja nasi, ya kuwa wamechoka kabisa kwa safari ndefu, tena mioyo yao ni mizito kwa kufiwa na bwana wao. Walikusudia kurudi makwao wakapumzike kwa muda.
Nikawauliza wenzao wako wapi, maana niliambiwa ya kuwa wako sita, nahapo niwatatu tu. Mmoja wao akasema, ‘’Wamo ndani ya nyumba wamepumzika baada ya taabu waliyopata. Usingizi unawaelemea machoni ni bora walale usingizi, maana usingizi huleta usahaulifu.’’ Lakini walikubali kuwaamsha.
Baadaye kidogo wale watatu wengine walitoka nyumbani, wanapiga miayo watu wawili wa kwanza walikuwa wa kabila lile lile na namna ile ile ya wale tuliowakuta wamekaa nje ya nyumba, lakini Yule watatu alinifanya nishtuke mno.
Alikuwa mtu mrefu sana, nakisia urefu wake ulikuwa kadiri ya futi sita na inchi tatu, lakini mwembamba, na viungo vyake vilikuwa na nguvu kama nyuzi za chuma.
Mara nilipomtazama nilitambua ya kuwa huyu si Mkazi ni Mzulu halisi. Alitoka, na huku ameuweka mkono wake mwembamba mbele ya uso wake kukiziba kinywa chake alipokuwa akipiga miayo, nikaona ya kuwa ni mtu mzima, naye ana shimo lenye pembe tatu katika paji la uso wake.
Kisha, aliuondoa mkono wake, nikaona uso wa nguvu wa Kizulu, na kinywa cha ucheshi, na ndevu fupi zenye mvi kidogo, macho ya kahawia makali kama ya mwewe.
Nikamtambua mara ile, ingawa nilikuwa sijamwona kwa muda wa miaka kumi na miwili. Nikasema kwa sauti ndogo kwa lugha ya Kizulu, ‘Hujambo Umslopogaas?’’
Mtu huyo mrefu, ambaye hadithi zake nyingi zilisimuliwa katika nchi ya Wazulu, na ambaye katika watu wake huitwa ‘’Gogota,’’ na ‘’Mchinjaji’’ alishtuka, na shoka lake la vita lenye kipini kirefu lilikuwa karibu kumponyoka kwa mshangao.
Daaah, hatariBasi nilikaa nikivuta tumbako na kuwaza juu ya mambo mengi na hatari ipo ya kupatwa na homa kwa kulala mahali kama hapa, tena mguu wangu wa kuume umekufa ganzi kwa kukaa hali umekunjwa katika mtumbwi, lakini nilianza kuufurahia uzuri wa usiku.
Miali ya mbalamwezi ilichezacheza juu ya uso wa maji yanayopita kasi kuendea baharini, kama maisha ya wanadamu yapitavyo kuendea kaburini, mpaka yakang’aa kama utando mpana wa fedha, yaani mahali pa wazi pasipo fikiwa na vivuli vya miti.
Lakini karibu na kando ya mto palikuwa giza sana na upepo ulivuma katika matete, ukafanya sauti ya kuhuzunisha.
Upande wa kushoto, ng’ambo ya mto, palikuwapo namna ya ghuba ndogo yenye mchanga pasipo na miti, na hapo niliweza kuona vivuli vya wanyama wengi waliokuja kunywa maji, mpaka kwa ghafla nilisikia ngurumo ya kutisha sana, na mara ile wote wakatimka.
Baadaye kidogo, niliona umbo kubwa la simba akija kunywa maji baada ya kula kwake.
Halafu aliondoka, ndipo niliposikia kishindo katika matete kadiri ya yadi hamsini kutoka hapo tulipokuwapo, na baada ya dakika chache kitu kikubwa cheusi kiliibuka katika maji.
Kumbe, ni kichwa cha kiboko. Kikazama tena bila kufanya sauti, kikaibuka tena karibu, yaani kadiri ya yadi tano tu kutoka mahali tulipo.
Hapo niliona ya kuwa yupo karibu sana, na kwa hivi sikuona raha, na hasa kwa kuwa alionekana kama atakaye kujua mitumbwi yetu ni kitu gani.
Alikifunua kinywa chake kipana, labda apige miayo tu, nikayaona meno yake, nikafikiri jinsi anavyoweza kuusagilia mbali mtumbwi wetu mdogo kwa dhoruba moja.
Nilianza kufikiri labda itafaa nimpige risasi, lakini nilipofikiri zaidi, niliazimu kumwacha kama asipojaribu kuushambulia mtumbwi. Halafu alizama tena bila kufanya sauti hata kidogo, wala sikumwona tena.
Papo hapo nilitupa macho ng’ambo ya kuume, nikawa kama ninaweza kuona kitu cheusi kinapita katika mashina ya miti.
Macho yangu ni makali sana, nami nadhani niliona kitu kwa hakika, lakini kama ni ndege, au mnyama, au mtu sikuwa na hakika.
Lakini papo hapo wingu jeusi lilipita mbele ya mwezi, kwa hiyo sikukiona kilekitu tena. Tena, papo hapo nilisikia mlio kama wa bundi akilia mfulilizo, baadaye kukawa kimya kabisa isipokuwa sauti za kuchakacha katika miti na matete, wakati upepo ulipoyatikisa.
Lakini kwa jinsi isiyoelekezeka, sasa nilianza kushuku hatari za kuona hofu,hapakuwapo wala sababu ya dhahiri ya kunitia hofu hivyo zaidi ya zile zinazomzunguka msafiri yeyote katika nchi ya Afrika, lakini hata hivyo, bila shaka niliona hofu.
Lakini nilikaza nia nisishindwe na hofu, ingawa jasho baridi lilinitoka pajini mwa uso. Wala sikukubali kuwaamsha wenzangu.
Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, na moyo wangu ulinipigapiga kama moyo wa mtu anayekaribia kufa. Na mishipa yangu ilinichezacheza kana kwamba kitisho kiovu kiko karibu. Watu waliopata kuota jinamizi, watafahamunamna hali yangu ilivyokuwa.
Ahsante sana mkuu blackstarlineLakini hata hivyo nilijikaza nikakaa kimya, nikageuza uso wangu tu kumtazama Umslopogaas na Wakazi wale wawili waliokuwa wamelala kando yake.
Nilisikia kishindo kidogo cha kiboko mbali, na Yule bundi alilia tena, na upepo ulianza kuvuma katika miti na kufanya sauti ya kuhuzunisha iliyopoozesha moyo. Baadaye nilipata kujua kuwa Wajivuni huitana kwa kuiga sauti ya bundi.
Juu niliona wingu jeusi, na chini maji meusi yalikuwa yakipita kasi, nikaona kama kwamba mimi na mauti tupo katika yake. Niliona ukiwa kabisa.
Mara damu yangu ilikuwa kama imevia katika mishipa yangu, na moyo wangu kusimama kimya. Je, ni ndoto tu ama ndio mwendo?
Niliyageuza macho yangu kuutazama mtumbwi wa pili uliokuwa ukielea kando yetu, nisiuone, ila badala yake niliona mkono mweusi mwembamba umeinuliwa juu ya ubavu mwa mtumbwi.
Hakika ni jinamizi! Lakini mara ile uso mwovu ulitokea juu kama kwamba umetoka majini, ndipo mtumbwi ulipoinama, kisu kikang’aa ghafla, na Mkazi mmoja aliyekuwa amelala kando yangu akapiga ukelele na kitu cha moto kilichuzurika usoni pangu.
Mara ile kuduwaa kwangu kukakoma, nikatambua kwamba si jinamizi, ila tumeshambuliwa na Wajivuni wanaogelea majini.
Nikashika silaha ya kwanza niliyoweza kuipata ikatokea kuwa ni shoka la vita la Umslopogaas, nikapiga kwa nguvu zangu zote pale nilipokuwa nimekiona kisu kinang’aa .
Pigo liliangukia juu ya mkono wa mtu likaugandamiza juu ya ubavu mnene wa mtumbwi, na kuukata kisiginoni.
Yule mtu asifanye sauti hata kidogo akatoweka kama kivuli, alikuja kama kivuli na akaondoka kama kivuli. Ameacha nyuma yake ule mkono wake wenye damu ungali umeshika sime ile iliyokuwa imechomwa katika moyo wa mtumishi wetu msikini.
Mara kulikuwa ghasia na fujo, nikadhani, sijui ni kweli au je, nikaona vichwa vyeusi vingine vikielea majini kuendea ng’ambo ya kuume, ambako mtumbwi wetu uliendea kasi kwa sababu kamba ile iliyokuwa na nanga ya jiwe imekatwa kwa kisu.
Mara nilipotambua hivyo, nilifahamu pia ya kuwa shauri lao ni kuikata kamba ili mtumbwi uchukuliwe na maji ili kuiendea ile ng’ambo ya kuume; na huko bila shaka Wajivuni wanangojea kutuchoma kwa mikuki yao.
Basi, nilishika kafi moja mwenyewe, nikamwambia Umslopogaas aishike nyingine, maana wale Wakazi walikuwa wameduwaa kwa hofu hata kushindwa kuhema, tukapiga kafi kwa nguvu kurejea tena katikati ya mto.
Wala hatukufanya hivyo kwa haraka zaidi kuliko ilivyopasa, maana katika dakika nyingine tungali kwamba na bila shaka ingalikuwa ndiyo mwisho wetu.
Mara tulipofika katikati ya mto tena, tulianza kupiga kafi kupaendea pale ulipokuwapo ule mtumbwi mwingine umetiwa nanga nayo ilikuwa kazi ngumu na hatari pia, kwa sababu hakuna la kutuongoza ila sauti ya Good, maana alipiga kelele mara kwa mara.
Mwishowe tuliufikia mtumbwi, tukashukuru tulipoona ya kuwa hawakushambuliwa.
Haikosi ule mkono ulioikata kamba ya mtumbwi wetu ungaliikata yao, na Yule mtu asingalivutwa na tamaa ya kuua na jambo hilo, ingawa lilitupotezea maisha ya mtu mmoja na Yule Mjivuni mkono wake, lakini pia lilituokoa sote wengine tusiangamizwe.
Kukosa kukiona kile kitisho kiovu kikitokea juu ya ubavu wa mtumbwi, kitisho ambacho sitakisahau mpaka siku ya kufa kwangu. Mtumbwi wetu ungalichukuliwa kando ya mto kabla sijatambua umepatwa na nini, na habari hizi hazingaliandikwa nami.
Pamoja mkuuAhsante sana mkuu blackstarline
halafu kuna Bougwan (Mr Henry?) na Ndovu (Mr Good?)Makumazahn ni jina la utani la ALLAN QUATERMAIN Jina hilo analitumia kwenye hadithi ya Mashimo ya Mfalme Sulemani na pia jina hilo lina tumika kwenye hadithi hii.
Karibu sanaNipo hapa najisevia
Asante, naKaribu sana
Amina 🙏Asante, na
Ubarikiwe sana
Karibu sana mkuu! Old is goldUnanikumbusha mbali sana, mbele huko malkia wawili ndugu ,Niko sitoki nimeweka kambi