Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

UTANGULIZI
Hadithi hii ilipigwa chapa kwa lugha ya Kiingereza katika mwaka 1885. Katika mwaka 1905 Bwana H. Rider Haggard aliandika maneno haya: 'Sasa katika mwaka 1905 naweza kuzidisha maneno yangu kwa kusema ya kuwa nimefurahishwa sana kuona hadithi yangu inadumu kuwapendeza wasomaji wengi. Hayo yaliyobuniwa yamedhibitishwa kuwa ni kweli: Mashimo ya Malme Sulemani niliyokuwa nikiyafikiri sasa yamegunduliwa nayo sasa yanatoa dhahabu tena, na kwa habari zilizotoka hivi karibuni hata almasi pia hutoka.'

MASHIMO YA MFALME SULEIMAN​

SURA YA KWANZA​

Kukutana na Bwana Henry Curtis​

Ni ajabu sana kwa mtu aliyefika umri wangu, yaani miaka hamsini na tano, kushika kalamu na kuanza kuandika kitabu, kama hivi ‘nifanyavyo mimi sasa. Sijui habari hizi zitakuwaje nikiisha kuzitunga, yaani nikijaliwa kufika mwisho wa safari yangu salama, maana ingawa nimefanya mambo mengi katika maisha yangu, lakini sijawahi kujaribu kuandika kitabu. Tokea utoto wangu nimeshughulika na kazi ya biashara na kuwinda, kupigana na kuchimba dhahabu, na tangu kupata utajiri huu nilionao ni miezi minane tu.



Sasa nina mali nyingi sana, hata jumla yake siijui, lakini nadhani nisingekubali kuvumilia tena hayo yote niliyoyavumilia katika miezi kumi na tano iliyopita hata kama ningejua kwa hakika kuwa nitatoka salama pamoja na mali nyingi pia. Mimi ni mtu mtaratibu, sipendi ghasia, na tena nimechoka kabisa kusafirisafiri na kupambana na mambo ya ajabu. Sijui kwa nini naandika kitabu hiki, maana uandishi si kazi yangu. Mimi si mwana chuoni ingawa napenda sana kusoma vitabu. Hebu kwanza nijaribu kuandika sababu zangu za kutunga kitabu hiki, ili muone kama kweli ninazo sababu.

Sababu ya kwanza ni kuwa Bwana Henry Curtis na Bwana Good wameniomba nikitunge. Sababu ya pili ni kuwa nimebaki hapa Durban kwa kuwa mguu wangu wa kushoto waniuma sana. Tangu nilipoumwa na simba ninapata maumivu, na hasa siku hizi yanazidi, hata siwezi kwenda vizuri. Nadhani haikosi meno ya simba yana sumu na kama sivyo majeraha yangeisha pona kabisa na yasinge rudi tena, na hasa ajabu ni kuwa yanarejea mwezi ule ule niliyong’atwa. Ni ajabu sana kuwa baada ya kuua simba sitini na tano na labda zaidi, Yule wa sitini na sita aliniuma mguu. Jambo hili limeharibu mipango yangu ya desturi yote, na kwa kuwa mimi ni mtu wa kufuata taratibu na mipango naona dhiki kabisa. Lakini hayo hayamo katika habari za kitabu hiki.

Sababu ya tatu ni kuwa nataka mwanangu Harry anaesoma katika chuo cha utabibu, awe na mazungumzo ya kumfurahisha na kumpendeza. Asifanye upumbavu. Kusomea utabibu si kazi rahisi, na kazi ya kuvumbua habari za mwili vile vile inachosha. Habari zilizomo katika kitabu hiki si kama zile zinazotokea kila siku, kwa hivyo labda zitamfurahisha kwa muda kidogo.

Sababu ya nne na ilivyo ya mwisho ni kuwa nataka kusimulia hadithi ya ajabu kupita zote ninazozijua. Labda itakuwa ajabu kweli kwa kuwa hapana mwanamke aliyetajwa katika hadithi hii, ila Foulata. Lakini ngoja kwanza! Nilitaka kumsahau Gagula, lakini sina hakika kama alikuwa mwanamke au shetani. Lakini kwa umri wake ulizidi miaka mia moja na kwa kuwa: haoleki, basi simhesabu kuwa mwanamke. Basi afadhali nijifunge kibwebwe. Kazi ni ngumu nami naona kama nimekwisha yavulia nguo maji. Lakini kama wasemavyo wajuzi, ‘Pole pole ndio mwendo,’ Basi sasa naanza.

‘Mimi Alan Quatermain, mzaliwa wa Durban, Natal, naapa na kusema …’Hii ndiyo namna nilivyoanza kusema mbele ya kadhi nilipokuwa natoa habari za kufa kwa Khiva na Ventvogel, lakini naona kuwa hii siyo namna ya kuanza kutunga kitabu. Basi, je, mimi ni muungwana? Muungwana ni nini? Sijui hakika. Maisha yangu yote nilikuwa nikifanya kazi ya biashara na kuwinda tu. Nimejaribu daima kuwa muungwana, basi wewe usomaye utanihukumu. Mungu ajua kuwa nimejaribu. Ama kweli katika maisha yangu nimeua watu wengi, lakini sikuu mtu bure wala sikuua mtu asiye na hatia, ila kwa kujilinda mwenyewe tu. Mwenyezi Mungu alitupa maisha, nadhani nia yake ni kwamba tujilinde, nami siku zote nimeshikilia hivyo ; natumaini kwamba hayo hayatanitia hatiani siku ya kuhukumiwa itakapowadia.

Lakini dunia ina ukali na maovu, na ingawa mimi ni mtu taratibu na mwoga kidogo nimeona mauaji mengi. Lakini naweza kusema kuwa sijaiba, ingawa mara moja nilimdanganya mtu mmoja nikachukua kundi la ng’ombe wake. Lakini yeye alikuwa amenifanyia mambo mabaya kabisa na hata hivyo, tangu siku ile ninajuta kwa vitendo vyangu nilivyovifanya.

Toka nilipokutana na Bwana Henry Curtis na Bwana Good mara ya kwanza, imepita miezi kumi na nane, na namna tulivyokutana ilikuwa hivi: Nilikwenda kupita Bamangwato ili kuwinda ndovu. Nikawa na bahati mbaya sana katika safari hiyo, na juu ya hayo nilishikwa na homa kali. Nilipopona nikasafiri mpaka kunakochimbwa almasi, nikauza pembe zangu zote nilizokuwa nazo pamoja na gari la ng’ombe, nikawapa ruhusa wawindaji wangu, na mimi mwenyewe nikapanda gari niende Captown. Baada ya kukaa Captown kwa muda wa jumaa moja niliona kuwa gharama za hoteli zinazidi sana, tena nilikuwa nimekwisha ona yote niliyoyataka kuyaona, basi nikanuia kurudi Natal kwa meli iitwayo Edinburg Castle inayotoka Ulaya.

Basi nikaenda kukata tiketi nikaingia melini, na jioni ile ile meli ikang’oa nanga tukasafiri. Katika abiria walioingia melini niliona wawili niliowatazama sana. Mmoja alikuwa mtu mwenye umri kadiri ya miaka thelathini, kifua kipana na mikono mirefu kushinda watu wote niliowahi kuwaona. Nywele zake zilikuwa za rangi ya kimanjano na alikuwa na ndevu nyingi za rangi ile ile, na macho yake yalikuwa ya rangi ya kijivujivu tena yameingia ndani. Wala nilikuwa sikupata kuona mtu mzuri kumpita yeye. Halafu nikajua kuwa huyu ni Bwana Henry Curtis. Yule mtu mwingine aliyekuwa akiongea na Bwana Henry alikuwa mfupi tena mnene, kisha mweusi kidogo, na sura yake ilikuwa haikufanana hata kidogo na ile ya Bwana Henry. Halafu nikajua kuwa anaitwa Bwana Good.

Basi jioni nilipokuwako sitahani nilisikia sauti, mara nikageuka kuangalia, nikaona kuwa ni Yule Bwana Good. Hata tulipokwenda chini kula chakula tulimkuta Bwana Henry amekwisha kaa mezani, na mara tukaanza kuongea habari za kuwinda na mambo mengineyo. Akaniuliza maswali mengineyo. Akaniuliza maswali mengi sana, nami nikamjibu kadiri nilivyoweza. Halafu yake tukaanza kuongea habari za ndovu, na mtu mmoja aliyekuwa karibu yetu akasema, ‘Ee bwana, kama ukitaka mtu hasa anayeweza kukwambia kweli habari za ndovu, ni mwindaji Quatermain.’ Bwana Henry Curtis aliposikia hivi, akashtuka na akasema kwa sauti ya upole, ‘Niwie radhi bwana, jina lako wewe ni Allan Quatermain?’ Nikamwambia, ‘Ndiye mimi.’

Tulipokwisha kula, tukawa tunatoka mezani, na Bwana Henry akanijia kunikaribisha niende chumbani kwake tukavute tumbako, nami nikakubali. Mradi tulikuwa watu watatu, na mara Bwana Henry Curtis akasema, ‘Bwana Quatermain, nadhani miaka miwili iliyopita ulipata kuwako mahali panapoitwa Bamangwato katika nchi ya Transvaal,sivyo? Kusikia hivyo nikaona ajabu sana yeye kujua habari za safari zangu. Nikamwambia, ‘Ndiyo nilikuwako’, Bwana Good akauliza, ‘Ulikuwa ukifanya biashara sivyo?’ Nikajibu, ‘Ndiyo, nilichukua gari la bidhaa nikapiga kambi nje ya mji, nikakaa huko mpaka nilipokwisha kuuza zote .’ Bwana Henry aliyekuwa amekaa katika kiti kukabili kiti changu, akaniuliza, ‘Ulipata kukutana na mtu mmoja jina lake Neville?’ Nikajibu, ‘Ndiyo, tulipiga kambi zetu karibu kwa muda wa siku kumi na nne, na baada ya miezi michache nikapokea barua kutoka kwa Mwana Sheria ya kuniuliza habari zake kama namjua alipo, nami nikapeleka majibu kueleza habari zake kama nilivyoweza.’

Bwana Henry akasema, ‘Najua, maana barua yako ililetwa kwangu. Ulisema kwamba mtu aitwaye Neville alitoka Bamangwato mwanzo wa mwezi wa Mei akasafiri kwa gari pamoja na watu wake na mwindaji mtu mweusi mmoja jina lake Jim, naye alisema kuwa anakwenda mpaka Inyati ambao ndio mji wa mwisho katika nchi ya Mtabele ; akifika hapo atauza gari lake aende kwa miguu. Kisha ulisema kuwa kweli aliuza gari lake kwa sababu uliliona tena baada ya miezi sita, na mtu uliyemwona nalo alikuwa ni Mreno mfanya biashara aliyekwambia kuwa amelinunua Inyati kwa mtu mweupe mmoja, ambaye jina lake amelisahau ila anafikiri kuwa yeye pamoja na boi wake amekwenda mwituni kuwinda.’ Nikajibu, ‘Hayo ni kweli.’ Basi tukanyamaza kidogo, kisha, Bwana Henry Curtis akasema, ‘Naona ya kuwa hujui vema habari hizo. Huwezi kukisia sababu zake za kusafiri kwenda kaskazini na mahali gani alipokwenda?’ Nikamjibu, ‘Nilisikia kidogo.’

Na kwa kuwa sikutaka kusema naye zaidi juu ya habari hizi nikanyamaza kimya. Bwana Henry na Bwana Good wakatazamana, kisha Bwana Good akatikisa kichwa kwa kumfanyia ishara Bwana Henry, akasema, ‘Bwana Quatermain nitakusimulia hadithi yangu, halafu unipe shauri na msaada wako. Yule wakili wangu aliyeniletea barua yako aliniambia kuwa wewe ni mtu wa heshima sana na watu wote wanakustahi, na kwa hiyo naweza kukuamini. Basi nikainamisha kichwa kwa haya kwa vile nilivyosifiwa na Bwana Henry akaendelea kusema, ‘Huyo Bwana Neville ni ndugu yangu.’ Niliposikia hivi nikastuka sana, maana sasa nalifahamu sababu ya kumtazama sana nilimwona mara ya kwanza, kwa kuwa wamefanana sana.

Basi Bwana Henry akaendelea kusema, ‘Yeye ni mdogo wangu, na mpaka miaka mitano iliopita nadhani hatukupata kuachana hata kwamuda wa mwezi mmoja. Lakini katika mwaka ule wa mwisho tulioonana tulipatwa na msiba kama wanavyopatwa watu wote mara kwa mara. Maana tuligombana sana hata nilimtenda mambo yasiyo ya haki kwa ajili ya hasira zangu. Haikosi unajua kuwa mtu akifa na kama mali yake ni mashamba tu, wala naye hakuacha wosia wowote, kwa sheria ya Uingereza mrithi huwa ni Yule mtoto mwanaume mkubwa, yaani aliyezaliwa kwanza, ndiye anayechukua mali yote. Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa. Na wakati ule tulipokuwa tukigombana baba yetu alifariki naye hakuwahi kuandika wosia. Basi kwa hivyo ilionekana kuwa mdogo wangu hakuwa na urithi.

Kusema kweli ilikuwa ni wajibu wangu kumsaidia na kumtunza, lakini kwa ule uchungu wa ugomvi jinsi ulivyokuwa mwingi sana, hata sasa naona aibu kukiri kuwa sikufanya jambo. Sikuwa na nia ya kumnyima haki yake, ila nilitaka yeye aje kwangu’ kuomba suluhu, naye hakuja. Nasikitika sana kukuudhi kwa habari hizi zangu, lakini naona sina budi kukueleza waziwazi mambo yote, sivyo Bwana Good?’ Bwana Good akajibu, ‘Ndivyo, nami najua kwa hakika kuwa Bwana Quatermain atayasitiri yote moyoni mwake.’ Nikajibu, ‘Vema,’ Maana mimi natafakari sana kuwa si mtu wa kupayuka.

Halafu Bwana Henry akasema, ‘Mdogo wangu alikuwa na fedha kidogo na bila kunishauri alitoa fedha zote alizokuwa nazo katika banki, na kuchukua jina lingine la Neville, akafunga safari kwenda kuchuma Afrika ya Kusini. Nikakaa kwa muda wa miaka mitatu bila kupata habari zake wala salamu zake, ingawa mimi nilimwandikia barua nyingi. Labda zilikuwa hazimfikii. Lakini baadaye nikaanza kuwa na wasiwasi, maana mtu haachi kumpenda ndugu yake.’
Nikasema, ‘Hayo ni ya kweli. ‘Maana nilikuwa nikimkumbuka mtoto wangu. Bwana Henry akawa anaendelea kusema, ‘Nikahisi kuwa hata nusu ya mali yangu yote nitatoa ili nipate kujua yaliyompata mdogo wangu, maana ni mmoja tu aliyebaki katika ukoo wangu. Basi siku zilipozidi kupita nami nikazidi kuwa na wasiwasi, nikatamani sana kupata habari zake. Ndipo nikaanza kuulizauliza, hata nikapata ile barua. Basi mpaka sasa habari ni nzuri, maana zaonyesha kuwa yu hai mpaka sasa. Na nilitia nia kwenda mwenyewe kumtafuta, na Bwana Good amenifurahisha sana kwa kufuatana nami.’ Basi Bwana Good akasema, ‘Ndiyo na sasa Bwana, labda utatwambia habari zote ujuazo za Yule mtu aitwaye Neville.’

SURA YA PILI

Basi kabla sijaanza kumjibu Bwana Good, nilitia tumbako katika kiko changu, na Bwana Henry akauliza, ‘ Ulisikia habari gani juu ya safari ya ndugu yangu ulipokuwako Bamangwato?’ Nikamjibu, ‘Nalisikia hivi, ya kuwa anakwenda kutafuta Mashimo ya Sulemani. Na tangu siku hiyo hata hivi leo, sijamwambia mtu habari hizo.’ Wote wawili wakauliza pamoja, ‘Mashimo ya Sulemani! Yapo wapi?’ Nikajibu, ‘Mimi sijui, lakini najua mahali ambapo watu husema kuwa yapo. Siku moja niliona vilele vya milima inayopakana nayo, lakini baina ya mahali hapo nilipokuwa mimi na milima hiyo palikuwa na jangwa la upana wa maili mia moja na thelathini, nami sijapata kusikia kuwa Mzungu yeyote amepata kuvuka jangwa hilo, isipokuwa mtu mmoja tu.



Lakini nadhani itakuwa vizuri zaidi nikisimulia habari hizo, yaani kama nilivyopokea kutoka kwa wenyeji, za Mashimo ya Sulemani kwa kadiri ninavyojua, ikiwa mtaahidi kuwa mtazisitiri mioyoni mwenu na kutomwambia mtu yeyote bila ya idhini yangu. Je, mtakubali sharti hilo?’ Bwana Henry akainamisha kichwa, na Bwana Good akaitikia, ‘Naam, naam.’ Basi, nikaanza kutoa hadithi yangu: ‘Kwa kawaida mwajua kuwa wawindaji wa ndovu ni watu wasiotamani anasa za dunia, wala hawashughuliki na mambo ila ya kweli ya dunia. Lakini pengine mwaweza kumkuta mtu mmoja mmoja anajitia katika mambo ya kuandika hadithi na kujaribu kutunga habari za zamani za watu wa kale. aliyeniambia maneno haya alikuwa ni mtu wa namna hiyo, na tangu aliponiambia maneno haya umepita muda wa miaka thelathini. Ilikuwa hivi: katika safari yangu ya kwanza nilikwenda kuwinda ndovukatika nchi ya Matabele. Mtu mmoja aliyeitwa Evans ndiye aliyeniambia maneno hayo, naye masikini aliuawana nyati mwaka wa pili yake, akazikwa mahali palipokuwa karibu na maporomoko ya maji yam to wa Zambezi. Nami nakumbuka sana kuwa siku moja nilikuwa nikizungumzia habari za kulungu na pofu katika mtaa mmoja wa Transvaal.’

Evans akasema, ‘Ndiyo, lakini mimi nitakutolea hadithi iliyo ya ajabu zaidi kupita habari za wanyama.’ Akaendelea kuhadithia jinsi alivyopata kuvumbua magofu ya mji wa zamani sana ambao aliamini kuwa ni mji ule uliokuwa ukiitwa Ophir uliotajwa katika Agano la Kale,na tangu siku hizo, watu wengi wenye maarifa kuliko yeye marehemu Evans wamesema hivyohivyo. Mimi nikakaa kusikiliza sana, maana wakati ule mimi nilikuwa bado kijana, na hadithi zile za kale zilinipendeza sana, na mara akasema, ‘je, mwanangu, umepata kusikia habari za milima ya Sulemani iliyo upande wa kaskazini wa nchi ya Mashukulumbwe?’’ , Nikamwambia, ‘Sijapata kusikia .’Akasema, ‘Basi, haidhuru, hapo ndipo mashimo ya Sulemani yalipo, yaani mashimo ya almasi.’ Nikamuuliza, ‘Je, wewe umejuaje?’ Akajibu, ‘Najuaje! Najua kwa jina lake lilivyo, na tena niliambiwa na mwanamke mmoja mchawi wa kabila la Isanusi katika nchi ya Manika. Alisema kwamba watu wanaokaa upande wa pili wa milima ile ni wa ukoo wa Amazulu, wanasema lugha inayofanana na Kizulu, ila wao ni wakubwa, tena wazuri zaidi ya Amazulu. Lakini kuna wachawi wenye nguvu nyingi wanaokaa humo na walikuwa na siri ya shimo la ajabu lenye mawe yale yanayong’aa.’ Nilicheka sana niliposikia hadithi hii, nikaipuuza, lakini ilinipendeza sana, maana wakati ule mashimo ya almasi yalikuwa bado hayajavumbuliwa. Lakini Yule marehemu Evans aliuawa, nami nikakaa muda wa miaka ishirini bila kufikiri tena jambo hili.

Baada ya miaka ishirini, na huo ni muda mrefu sana, maana mwindaji wa ndovu ana shida kuishi miaka ishirini katika kazi yake, nikasikia habari zaidi juu ya milima ya Sulemani na nchi iliyo upande wa pili yake. Hapo mimi nilikuwa katika nchi ya Manika, mahali paitwapo KwaSitanda, napo ni mahali pabaya sana, maana sikuweza kupata chakula wala wanyama hakuna. Nilishikwa na homa kali mno hata hali yangu ikawa dhaifu sana, na siku moja akafika Mreno mmoja pamoja na mwenziwe mmoja suriama. Tukaongea kidogo pamoja, maana yeye aliweza kusema Kiingereza kidogo, nami pia nilijua kusema Kireno kidogo, akaniambia kuwa jina lake ni Jose Silvestre, na tena ana shamba karibu na Delagoa Bay. Lakini siku ya pili yake aliondoka pamoja na mwenziwe. Katika kuniaga akasema ‘Bwana, tukionana tena natumai mimi nitakuwa tajiri kuliko watu wote duniani, nami nitakukumbuka.’ Nikacheka kidogo, maana nilikuwa mnyonge kwa homa na kwa hivyo sikuweza kucheka sana; nikamwona akienda kuvuka lile jangwa kwenda upande wa magharibi. Nikadhani kuwa ana wazimu, kwani anakwenda kutafuta nini huko? Baada ya juma moja, nikapona, na jioni nilipokuwa nimekaa nje ya hema langu dogo, nikitafuna paja la kuku wa mwisho niliyemnunua kwa mtu mmoja kwa bei ya kitambaa kimoja kilichonipatia kuku ishirini, nikitazama jua jinsi lilivyokuwa jekundu linavyoshuka nyuma ya jangwa hilo, mara nikaona kitu kama mzungu amevaa koti akiteremka mteremko uliokuwako kiasi hatua mia sita, mbele yangu.

Kwanza mtu huyo alitambaa kwa magoti na mikono, kisha akasimama na kupepesuka hatua chache mbele, tena akaanguka na kutambaa. Mradi nikaona kuwa ni mtu aliye taabani. Nikapeleka mmoja wa wawindaji wangu kwenda kumsaidia, na baadae kidogo akaja nae. Je, wadhani alikuwa ni nani? Alikuwa ni Yule Jose Silvetre, kwa kweli, mifupa yake ilikuwa dhaifu, tena alikuwa amekonda kabisa. Uso wake ulikuwa manjano, uking’aa kwa homa aliyokuwa nayo, nayale macho yake meusi makubwa yalionekana kama yaliyotokeza nje, maana alikuwa hana nyama kabisa .. Ngozi yake ilikuwa imekauka, na nywele zake zilikuwa zimegeuka rangi zikawa nyeupe, na mifupa imemtoka. Akawa anaugua huku akisema, ‘Nipeni maji! Jamani.

Nikaona kuwa midomo yake imepasuka na ulimi ulikuwa mweusi tena umevimba. Nikampa maji yaliyochanganyika na maziwa kidogo, akayabugia. Nikamzuia kusudi asinywe zaidi. Na mara homa ilimshika tena na kuanza kupayuka na kusema habari za milima ya Sulemani, na almasi na jangwa. Nikamchukua na kumweka hemani mwangu nikamtunza kama nilivyoweza; lakini nilijua kuwa atakufa. Kama saa tano ya usiku akatulia kidogo, nami ndipo nilipopata usingizi kidogo, nikalala. Kulipopambazuka nikaamka, nikamwona namna alivyokuwa amekonda sana amekaa na kulikodolea jangwa macho. Baadae kile kianga cha kwanza chajua kilionekana mawinguni, kikaangaza jangwa mpaka kufika kilele kirefu katika milima ya Sulemani, masafa ya maili mia moja na zaidi. Mara Yule mgonjwa akanyosha mkono wake mwembamba kuelekeza kileleni na huku akisema kwa Kireno, ‘Ndipo, ndipo papo hapo, lakini mimi sitawahi kupafikia kamwe. Wala hapana atakayepafikia kwamwe!’ Mara akakaa kimya kidogo kama mtu anayewaza jambo moyoni, halafu akanigeukia akasema, ‘Rafiki bado ungalipo? Ama sasa naona macho yangu yanaingia giza,’ Nikajibu, ‘Ndiyo, nipo hapa hapa.

Lakini sasa afadhali ulale upumzike.’ Akasema, ‘Ndiyo nitapumzika sasa hivi; tena nitakuwa na wasaa mwingi wa kupumzika, hata milele. Nisikilize, ninakufa! Wewe umenitendea mema. Nitakupa hati. Labda utaweza kupafikia ikiwa utaishi na kuvuka jangwa ambalo limemuua mtumishi wangu na mimi!’

Akapapasapapasa katika mfuko wake akatoa kitu nilichokidhania kuwa kikoba cha kuwekea tumbako kilichofanywa kwa ngozi ya mnyama. Kikoba hicho kilifungwa kwa uzi wa ngozi naye alijaribu kukifungua asiweze. Akanipa akisema, ‘Fungua.’Nikakifungua nikatoa kipande cha kitambaa kikuukuu cha katani kilichokuwa kimeandikwa maneno, na ndani ya kitambaa hicho mlikuwamo karatasi. Kisha akasema kwa sauti ya kufifia, maana alizidi kudhofu, akanena, ‘Juu ya hiyo karatasi kumeandikwa yote yaliyoshindikwa juu ya kitambaa na hivyo ilinibidi kufanya kazi miaka hata kuweza kuisoma. Sikiliza: Babu yangu ambaye ilimlazimu kuutoka mji wa Lisbon alikuwa katika Wareno hao wa kwanza waliofika katika nchi hii.

Aliandika maneno hayo wakati alipokuwa akifa katika milima ile ambayo hapana hata Mzungu mmoja aliyepata kuikanyaga kwa miguu yake mpaka hivi leo. Jina lake lilikuwa Jose da Silvestre, naye aliishi miaka mia tatu, nyuma. Mtumishi wake aliyekuwa akimngojea upande huu wa milima aliona kuwa amekwisha kufa, nae ndiye aliyeleta maandishi haya mpaka Delagoa. Na tokea wakati huo yametunzwa na warithi wake, lakini hapana aliyetaka kuyasoma, mpaka mimi nilipofaulu. Nami nimepoteza maisha yangu kwa ajili yake, lakini labda mtu mwingine ataweza kufaulu na kuwa tajiri kupita watu wote duniani. Lakini usimpe mtu mwingine bwana, wewe nenda mwenyewe!’ Akaanza kuugua tena, na baada ya saa moja akafa. Mungu amrehemu. Nilimzika katika kaburi la kwenda chini sana, nikaweka na mawe makubwa juu ili kusudi asifukuliwe na fisi. Kisha nikaondoka pale.

Bwana Henry akauliza, na sauti yake ilionyesha jinsi alivyokuwa akisikiliza maneno yangu, ‘Ehe, lakini hiyo hati iko wapi? Naye Bwana Good akaongeza, ‘Hati hiyo iko wapi sasa, iliandikwa habari gani?’ Nikasema, ‘Mkitaka nitawasimulia habari zake. Nami sijamwonyesha hata mtu mmoja ila Mreno mmoja mfanya biashara aliyekuwa amelewa wakati alipoitafsiri, tena hakosi’ kuwa alikuwa amekwisha sahau habari zake ulevi ulipomtoka. Hicho kitambaa chenyewe nimekiweka kwangu Durban pamoja na hiyo karatasi aliyoifasiri marehemu Jose, lakini hapa ninayo tafsiri ya Kiingereza na nakala ya ramani iliyokuwamo, nayo ni hii:’

Mimi Jose da Silvestre nipo hapa ninakufa kwa njaa ndani, ya pango dogo katika upande wa kaskazini mwa titi la mlima ulio upande wa kusini wa milima miwili ambayo nimeipa jina la Maziwa ya Sheba. Naandika haya kwa kipande cha mfupa na wino wa damu yangu mwenyewe katika mwaka 1590. Ikiwa mtumishi wangu atakuja na kuiona na kuichukua mpaka Delagoa, nataka rafiki yangu (Na hapo katika hati, jina lake limefutika.) ampashe habari mfalme ili alete jeshi la askari watakaoweza kuvuka jangwa hili na kuwashinda hawa Wakukuana walio majabali sana na wenye uchawi mwingi. Lakini kwa sababu ya hila na udanganyifu wa Mchawi Gagula sikuweza kuleta kitu cha ushahidi, tena hata maisha yangu nayo nimeyaokoa kwa shida nyingi. Na huyu atakayekuja na afuate ramani, apande theluji ya ziwa la kushoto la Sheba mpaka afike penye titi, ambapo kwa upande huo wa kaskazini pana njia kuu iliyotengenezwa na Sulemani. Kutoka hapo ni mwendo wa siku tatu kufikia jumba la Mlalme. Basi na amwue Gagula. Nawe niombe dua.

Kwaheri. Jose da Silvestre.

Nilipokwisha soma barua na kuonyesha ile nakala ya ramani iliyoandikwa na Yule mzee kwa damu ya mkono wake, wakanyamaza kimya kwa ajili ya kustaajabu kwao. Baadae Bwana Good akasema, ‘Lo! Nimezunguka dunia mara mbili, tena nimefika bandari nyingi lakini sijapata kusikia hadithi kama hii hata vitabuni.’ Bwana Henry akasema, ‘Ni hadithi ya ajabu Bwana Quatermain. Natumai unajaribu kutuhadaa! Najua kwamba watu hudhani kuwa si vibaya kumhadaa mjinga.’ Niliposikia hivi nikaudhika, nikatwaa karatasi nikaiweka mfukoni, maana sikupenda kudhaniwa kuwa ni mmoja wa wale wapendao kusimulia uwongo na kuwahadithia wageni habari za kuwinda na mambo mengine ambayo hayakutokea kamwe. Basi nikajibu, ‘Kama unafikiri hivyo basi mambo yaishe hapa hapa. Nikasimama nikataka kwenda zangu. Bwana Henry akaniwekea mkono wake begani pangu akasema, ‘ Kaa, Bwana Quatermain, niwie radhi, usiudhike; kwani naona kuwa hupendi kutuhadaa, lakini hadithi yenyewe ni ya ajabu mno hata kwanza niliona vigumu kuisadiki.’

Basi ndipo nilipoanza kutulia kidogo, maana nilipofikiri niliona kuwa si ajabu kuwa yeye hawezi kusadiki hadithi, nikamwambia, Tutakapojaliwa kufika Durban utaona ramani ya asili na maandishi yake. Lakini bado sijakwambia habari za ndugu yako. Nilimjua Yule Jim aliyekuwa pamoja naye. Yeye ni Mbechuana, mwindaji hodari, tena na mtu mwenye busara. Siku hiyo Bwana Neville alipoanza safari yake nilimwona Jim amesimama karibu na gari langu akisokota tumbako yake, nikasema, ‘Jim, safari hii unakwenda wapi? Kuwinda ndovu?’ Akajibu ‘La! Tunakwenda kutafuta kitu kinachotafutwa sana zaidi ya pembe za ndovu.’ Mimi nikazidi kumdadisi, nikamuuliza, ‘Je, kitu hicho chaweza kuwa nini? Ni dhahabu? Akacheka akajibu, ‘siyo Bwana, ni kitu kinachotakiwa zaidi ya dhahabu.’

Basi sikumuuliza neno tena, maana sikupenda kuonekana kuwa ni mdaku. Baada ya Jim kuisha kusokota tumbako yake, akasema ‘Bwana, sisi tunakwenda kutafuta almasi.’ Nikasema, ‘Almasi! Lakini mbona unafuata njia ambayo si njia ya kwendea huko; kwa nini hufuati njia inayoendelea kwenye mashimo?’ Akajibu, ‘ Bwana, umepata kusikia habari za mlima wa Sulemani?’ Nikamjibu, ‘Ndiyo.’ Akaniuliza, ‘Umesikia habari za almasi zilizoko huko?’ Nikwamwambia, ‘Ni upuuzi tu.’ Akanena, ‘Si upuuzi,? Wana maana, namjua mwanamke aliyetoka huko, naye alifika Natal pamoja na mtoto wake, akaniambia; lakiniamekufa sasa.’

Nikamjibu, ‘Wewe na bwana wako mkijaribu kufika nchi ya Sulemani, hamkosi mtaliwa na tai.’ Akacheka, akasema, ‘Labda, bwana . Mtu amezaliwa naye atakufa; nami ningependa kutembea katika nchi ngeni; maana ndovu wanakwisha katika nchi hii.’ Nikasema, ‘Haya, tutaona.’ Baada ya nusu saa nikaona gari la Neville likitoka. Na baadae kidogo Jim akarudi mbio akasema, ‘Kwaheri bwana, kwani sikupenda kuanza safari bila kuagana nawe. Ninaona labda umesema kweli ya kuwa hatutasafiri kwenda kusini tena.’ Nikamuuliza, ‘Je, Jim, wasema kweli? Bwana wako amesema kuwa anakwenda mlima wa Sulemani, au sivyo?’ Akasema, ‘Ni kweli bwana maana aliniambia kuwa imempasa ajaribu kuchuma mali kwa njia yoyote; basi ni afadhali ajaribu kutafuta hiyo almasi.’ Nikasema, ‘Vema Jim, lakini ngoja kwanza, nataka uchukue barua hii, lakini lazima uahidi kuwa hutampa mpaka nifike Inyati.’ Kufika Inyati ilikuwa ni mwendo wa maili kama mia. Basi akaahidi. Nami nikachukua karatasi nikaandika maneno haya: ‘Kwa huyo atakayekuja ..apande theluji ya ziwa la kushoto la Sheba mpaka afike penye titi, ambapo kwa upande huo wa kaskazini pana njia kuu iliyotengenezwa na Sulemani.’

Basi nikampa, kisha nikamwambia, ‘Sasa utakapompa bwana wako barua hii, mwambie afuate sana shauri lililomo. Wala usimpe sasa barua hii kwa sababu sipendi arudi kuja kuniuliza maswali mengi ambayo sitaweza kuyajibu. Haya nenda.’ Basi Jim akaitwaa barua akaenda zake. Na hayo ndiyo yote ninayoyajua juu ya ndugu yako, Bwana Henry; lakini nachelea sana ya kuwa.. ‘Bwana Henry akasema, ‘Tazama, Bwana Quatermain, mimi ninakwenda kumtafuta ndugu yangu; nitamtafuta hata mlima wa Sulemani, hata nitaupita ikiwa ni lazima, mpaka hapo nitakapomwona au mpaka hapo nitakapo hakikisha ya kuwa amekufa; je, utafuatana nami?’

Nimekwisha sema kuwa mimi ni mtu wa taratibu , kweli na pengine ni mwoga kidogo, na haya yalinitia hofu. Maana safari kama hiyo iliyokusudiwa nilibaini kuwa ni kufa tu. Na tena juu ya hivyo nina mtoto anaenitegemea mimi kwa hivi sipendi nife. Basi nilijibu, ‘Hapana bwana, ahsante sana lakini naona ni afadhali nisiende. Sasa mimi ni mzee siwezi kusafiri safari ya kubahatisha hivyo, na tena naona mwisho wetu utakuwa kama ule wa rafiki yetu Silvestre. Mtoto wangu ananitegemea mimi, basi kwa hivyo sina haki ya kujitia katika hatari.’

Basi hapo wote wawili, yaani Bwana Henry na Bwana Good wakahuzunika sana, na Bwana Henry alisema, ‘Bwana Quatermain, mimi ni tajiri sana, nami nimenuia kusafiri ili nimtafute ndugu yangu, na kadhalika waweza kutaja mshahara wowote uutakao nami nitakupa kabla ya kuanza safari. Tena nitausia kuwa tukipatikana na ajali, mtoto wako atazamwe. Mradi sasa naona kwa maneno hayo utaweza kutambua jinsi tunavyo kuhitaji wewe ufuatane pamoja nasi. Tena ikiwa kwa bahati tutavumbua mahali pale palipo na almasi, basi hizo zitakuwa shirika wewe na Bwana Good, mimi sizitaki. Vile vile ikiwa tutapata pembe za ndovu. Waweza kutoa shauri na kufanya mapatano yoyote yanayokupendeza, na tena gharama zote za safari ni juu yangu mwenyewe.’ Nikajibu, ‘Bwana Henry, maneno yako ni mema kweli kweli, lakini lazima niyafikiri kwanza, maana mimi sina mali nyingi, pili kwa sababu najua kuwa ni kazi kubwa sana, basi nipe nafasi nipate kuyafikiri zaidi. Nitakupa jibu kabla hatujafika Durban.’ Bwana Henry akasema, ‘Vema.’ Nikamwambia kwa heri, nikaenda kulala, na nilipolala nilimwota Yule marehemu Silvestre na almasi!

Itaendelea...
Nice

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SURA YA TANO
SAFARI YETU YA JANGWANI
Tulikuwa tumeua ndovu tisa, ikachukua kazi ya siku mbili kutoa pembe zao. Tulipokwisha kuzitoa tulizileta kambini tukachimba shimo chini ya mti mkubwa tukaziweka humo tukafukia shimo. Pembe zilikuwa nzuri kabisa, nadhani sijaona namna yake, maana zile za Yule mkubwa aliyemuua Khiva zilikuwa yapata ratili mia na sabini, kadiri tulivyoweza kukisia. Na marehemu Khiva tulimzika katika kaburi pamoja na sagai lake kama ilivyo desturi, yaani apate kujitetea katika safari yake ndefu kwenda ahera. Siku ya tatu tuliondoka tukafunga safari yetu tukitumaini kuwa tutarudi salama na kuchimbua pembe zetu. Baada ya safari ndefu ya kuchosha tulifika mji wa Sitanda karibu na mto wa Lukanga, na hapo kwa kweli ni mwanzo wa safari yetu. Nakumbuka sana siku ile tuliyofika huko.

Kwa upande wa kulia zilikuwa nyumba chache zimetawanyika pamoja na mazizi ya ng’ombe, na karibu na mto yalikuwapo mashamba ya wenyeji. Kupita mashamba hayo ni mwitu wenye majani marefu umejaa wanyama wa porini. Upande wa kushoto palikuwa jangwa lile kubwa. Hapo paonekana kwamba ni mwisho wa ardhi inayofaa kuoteshwa vitu, siwezi kujua kwa sababu gani, lakini ndivyo ilivyo.

Upande wa chini ya kambi yetu maji yalitiririka katika mto mdogo, na ng’ambo yamto palikuwa mteremko wenye mawe mengi. Huu ndio ulikuwa mteremko ule ule nilipomwona Yule Silvestre akitambaa kwa mikono na magoti miaka ishirini nyuma, yaani aliporudi katika safari yake ya kutafuta Mashimo ya Sulemani. Na kupita mteremko huo ni jangwa lile lisilo na maji, jangwa la ukiwa kabisa.

Tulipo piga kambi yetu ilikuwa ni jioni, na jua lilikuwa likizama, mfano wa mpira mkubwa mwekundu. Mishale ya nuru ya rangi mbali mbali ilitoka ikaenea jangwani. Bwana Henry na mimi tulimwacha Bwana Good atengeneze kambi, nasi tulipanda mteremko ule tukasimama tukitazama jangwa.

Mbingu zilikuwa nyeupe kabisa, na mbali sana tuliweza kuona milima ya Sulemani kama vivuli vikubwa, na wakati mwingine kuona theluji juu ya vilele vyake. Basi nikasema, ‘Kule ndipo upo ukuta unaozunguka Mashimo ya Sulemani, lakini anaejua kama tutaweza kuupita ni Mungu tu.’ Bwana Henry akasema, ‘Nadhani ndugu yangu yupo, na ikiwa yupo basi tutaonana, lazima.’ Nikasema, ‘InshaIlah.’

Tukageuka turudi kambini, nikaona kuwa sisi hatupo pekee yetu, maana nilimwona Umbopa amesimama nyuma yetu na macho yake ameyakodolea milima ile ya mbali. Umbopa alipoona tumemwona, akamwambia Bwana Henry, ‘Je, Inkubu, ile ndiyo nchi unayotaka kufika?’ (na jina la Inkubu ndilo jina walilomwita wenyeji, nadhani maana yake ni ‘ndovu’).

Basi Bwana Henry, akajibu, ‘Ndiyo ile nchi ninayokwenda.’ Umbopa akasema , ‘Inkubu, jangwa ni pan asana, tena hapana maji kabisa, milima ni mirefu sana na vilele vyake vimefunikwa na theluji, na mwanadamu hawezi kukisia kuna nini pale nyuma pale linaposhukia jua; utafika huko kwa njia gani, na kwa nini unataka kwenda?’

Basi nilimtafsiria maneno yale yote, na Bwana Henry akasema, Mwambie ya kuwa na kwenda kumtafuta ndugu yangu aliyenitangulia.’ Umbopa akasema, ‘Inkubu, ni kweli: maana njiani nilikutana na mtu mmoja kabila lake Hottentot akaniambia kuwa miaka miwili nyuma Mzungu mmoja alianza kuvuka jangwa amefuatana na mtumishi mmoja, nao hawakurudi.’ Bwana Henry akamuuliza, ‘Je, waona ya kuwa huyo ni ndugu yangu?’
Umbopa akajibu, ‘La, bwana sijui, ila nilipomuuliza Yule mtu yu wanamna gani, akajibu kuwa ana macho kama yako, lakini ndevu zake ni nyeusi, na tena amefuatana na mtumishi mmoja Mbechuana jina lake Jim.’

Basi nilipotafsiri maneno haya nikasema, ‘ Ndhani ‘ndiye bila shaka, maana mimi namjua Jim tangu zamani.’ Basi Bwana Henry akatikisa kichwa akasema, ‘Mimi nilijua hakika, maana ndugu yangu akitia nia yake kutenda jambo atalitenda. Ikiwa alitaka kuvuka milima ya Sulemani basi amekwisha kuivuka isipokuwa amezuiwa na jambo.

Na kwa hivi lazima tumtafute upande wa pili.’ Umbopa alifahamu Kiingereza ingawa hakukisema ila mara chache, akasema, ‘Inkubu, ni safari ndefu.’ Bwana Henry akajibu, ‘Ndiyo ni mbali, lakini hakuna jambo duniani asiloweza kufanya ‘mwanadamu ikiwa amedhamiria kulifanya.

Umbopa, ikiwa mapenzi yanamvuta mtu naye yu tayari kukosa maisha yake kama kwamba si kitu, hakuna jambo asiloweza kulitenda, hakuna milima asiyoweza kuipanda, hakuna jangwa asiloweza kulivuka, ila mlima mmoja na jangwa moja ambalo wewe hulijui.’ Nilipoyatafsiri maneno hayo , Umbopa alijibu, ‘Maneno makubwa, baba yangu, maneno yanapovuma kweli yanayostahili kusemwa na mwanaume. Umesema kweli, Inkubu baba yangu.

Sikiliza! Maisha ni kitu gani? Ni unyoya, ni mbegu ya majani, ikipeperushwa huko na huko, pengine huzaa na kujizidisha na ikisha kufanya hivyo hufa, pengine huchukuliwa mawinguni. Lakini ikiwa mbegu ni njema na nzito, huenda itasafiri kidogo katika njia ambayo inataka. Ni vizuri kujaribu kusafiri katika njia yako na kushindana na ajali. Kila mtu ameandikiwa kufa. Kama mambo yamezidi, basi hufa upesi kidogo zaidi tu. Baba yangu, nitafuatana nawe kuvuka jangwa na milima mpaka nitakapozuiwa na ajali njiani.’
 
Hapo alinyamaza kimya kidogo, na baadae akaendelea kutoa hotuba yake kama ilivyo desturi ya Wazulu. ‘Maisha ni kitu gani? Niambieni, Ee Wazungu, nyinyi wenye busara, nyinyi mjuao siri za dunia, na dunia ya nyota, na dunia iliyo juu na kuzunguka nyota; nyinyi mpelekao maneno yenu mbali bila kutumia sauti; niambieni, Ee nyinyi Wazungu, siri ya maisha yetu ni nini huenda wapi, hutoka wapi? Hamwezi kunipa jawabu; hamjui! Sikilizeni, nitawaambia. Maisha ni mkono tunaotumia kukinga mauti.

Ni kimulimuli kinachong’aa wakati wa usiku; ni kama pumzi nyeupe za ng’ombe zinazoonekana wakati wa baridi; ni kivuli kidogo kile kinachokimbia katika majani na kupotea katika jua hapo linaposhuka.’

Bwana Henry akasema, ‘Wewe Umbopa ni mtu wa ajabu.’ Umbopa akacheka kidogo akasema, ‘Huoni kuwa wewe na mimi tumefanana sana. Huenda hata na mimi nakwenda kuvuka milima ile ili kumtafuta ndugu yangu!; Nikamtazama sana nikamuuliza, ‘Je, maneno gani hayo, maana yake ni nini? Wewe unajua habari gani ya ile milima? Akajibu, ‘Kidogotu, kidogo sana.

Ni nchi ngeni kabisa, nchi ya uchawi na vitu vizuri; nchi ya watu hodari na miti na vilele vya theluji na njia nyeupe kubwa. Nimesikia habari zake, lakini iko faida gani kusema.? Sasa giza linashuka. Wale watakaoishi kuona wataiona.’ Nikamtazama tena, maana ilinibainika kuwa anajua habari zaidi. Alifahamu ninayoyafikiri, akasema, ‘Usiniogope, Makumazahn, mimi sitegi mitego upate kutegwa.

Mimi sifanyi hila. Ikiwa tutajaaliwa kuvuka milima ile iliyo nyuma ya jua, nitakwambia yote ninayoyajua. Lakini mauti yamekaa juu ya milima ile. Uwe na busara, urudi nyuma, nendeni mkawinde ndovu, mabwana. Nimesema.’

Na bila kusema neon jingine, aliinua sagai lake kutuaga akageuka akarudi kambini, na baadaye tulimkuta huko anasafisha bunduki kama wale watu wengine, Bwana Henry akasema, ‘Mtu huyu wa ajabu sana.’ Nikasema, ‘Ndiyo, nampenda kama simpendi.

Ajua neno lakini hataki kulisema. Lakini ya nini kugombana naye! Safari yetu ni ya ajabu na Mzulu wa ajabu hawezi kuzidisha ajabu yake.’ Siku ya pili tulifanya vitu vyote tayari kuanza safari yetu. Hatukuweza kuchukua bunduki nzito tukaziacha pamoja na vitu vingine kwa wapagazi wetu, tukafanya shauri kuwaacha katika nyumba ya mtu mmoja aliyekaa karibu.

Sikupenda kabisa kuviacha vitu hivyo, maana Yule mtu alivitazama kwa macho ya uroho sana, lakini nilifanya hila. Kwanza nilishindilia bunduki zote, nikaziweka tayari kupigwa, nikamwambia kuwa akizigusa hata kidogo, basi zitalia.

Yeye hakusadiki, na mara ile akashika moja, na kama nilivyomwonya, ikalia, na risasi ikampiga ng’ombe wake mmoja, na vile vile kishindo chake kikamwangusha chini. Akainuka upesi ameshtuka kabisa tena anaona uchungu kwa kupata hasara ya ng’ombe wake, akataka nimlipe, lakini hakutaka kabisa kugusa tena bunduki.

Akasema, ‘Weka shetani wale katika majani ya paa la nyumba au zitatuua sote.’ Nikamwambia kuwa tutakaporudi nikiona kuwa moja imepotea nitamuua yeye na watu wake wote kwa uchawi; na ikiwa haturudi naye akijaribu kuiba bunduki, basi vivuli vyetu vitakuja kumfuata na kuwatia wazimu ng’ombe wake, na kuharibu maziwa yao kabisa, mpaka maisha yake yatakuwa na udhia mtupu! baada ya hayo, akaapa kuwa atazitunza awezavyo.

Basi tukisha kuweka vitu vyetu salama, tulifunga mizigo midogo, tukawachagua Umbopa na Ventvogel wafuatane nasi, tukawa watano, yaani, Bwana Henry, Bwana Good, mimi na Umbopa na Ventvogel. Hatukuchukua vitu vingi, tulipunguza mzigo kadiri tulivyoweza. Tulichukua bunduki tano na bastola tatu, na viriba vya maji vitano, na mablanketi matano, na nyama kavu na shanga za kutoa zawadi, na dawa.

Tena tukachukua visu vyetu na vitu vidogo vidogo kama vile dira na vibiriti na tumbako. Basi vitu hivyo pamoja na nguo tulizokuwa tukivaa ndivyo tulivyo chukua, basi, Siku ya pili hatukufanya kitu, tulipumzika tu, na jua liliposhuka tuliamka tukala, tukafunga vitu vyote tayari, tukalala tena kungojea mbalamwezi.

Yapata saa tatu mwezi ukatoka ukaangaza nchi nzima na mbele yetu tukaona lile jangwa kubwa la kutisha sana. Tukaondoka, na baada ya dakika chache tukawa tayari, lakini hata sasa tulisita kidogo kama ilivyo desturi, ya kibinadamu ikiwa anaanza safari ya hatari. Sisi watu watatu tulisimama pamoja.

Umbopa akasimama mbele kidogo ameshika sagai lake mkononi na bunduki ameweka begani analitazama sana jangwa; na Ventvogel na watu watatu waliokubali kufuatana nasi kuchukua vibuyu vya maji kwa safari ya siku ya kwanza wakasimama pamoja nyuma yetu.

Basi Bwana Henry akasema, ‘Rafiki zangu, sasa tu tayari kuanza safari yetu ya ajabu. Labda hatutafaulu. Lakini sisi ni watu watatu, nasi tutashirikiana katika mambo mema na maovu mpaka mwisho, Na sasa kabla hatujaanza, na tumwombe Mungu anayeumba na kuandika ajali za wanadamu, ambaye tangu zamani amekwisha amuru njia zetu, atuongoze miguu yetu kama apendavyo.’

Akavua kofia yake na Bwana Good pia akavua yake, wakasimama kimya kwa muda. Mimi si mtu wa kuomba, nadhani wawindaji wachache sana huwa wa namna hiyo; wala sijamsikia Bwana Henry akisema namna hiyo lakini nadhani katika moyo wake ni mtu wa dini. Bwana Good vile vile ni mtu wa dini. Lakini siwezi kukumbuka hata siku moja niliyoomba kama nilivyoomba siku ile. Na lazima nikiri kuwa niliona faraja kwa kuomba hivyo.

Maana yaliyo mbele yetu hatukuyajua, na siku zote mambo yanayotisha na yasiyojulikana huvuta wanadamu wamkaribie Muumba wao. Kisha Bwana Henry akasema, ‘ Haya twendeni!’ Tukaanza safari yetu.

Hatukuwa na kiongozi ila milima ya mbali na ile ramani aliyoandika mzee Jose da Silvestre, na kwa kuwa iliandikwa na mtu aliyekuwa akifa juu ya kipande cha kitambaa miaka mia tatu iliyopita, haikuwa kiongozi cha kutia moyo sana.

Lakini hii ndiyo iliyokuwa tama yetu kufaulu. Tukikosa kuliona ziwa lile la maji machafu ambayo alama yake ilionyesha kuwa ni katikati ya jangwa, basi haikosi tutakufa kwa kiu.
Na nilifikiri kuwa bahati ya kuliona haiwezi kutumainiwa sana.

Na hata ikiwa Yule mzee da Silvestre alipima sawasawa na kufanya alama barabara katika ramani, je, baada ya miaka hii yote iliyopita sip engine limekauka,au labda wanyama wa porini wamekwisha kuyakanyaga maji mpaka yamekwisha, au labda yamekwisha kufunikwa na mchanga uliyopeperushwa na upepo? Basi tukaenda, tukaenda, usiku tukikanyaga mchanga na majani yale yaliyosokotana sokotana yalitunasa miguuni, na mchanga uliingia katika viatu vyetu ikawa mara kwa mara kusimama tupate kuutoa.

Basi hivi hivi tulisafiri, na Bwana Good alijaribu kututia moyo kwa kupiga mbinja, lakini sauti yake ilizidi kututia huzuni tu, akaacha. Baadae kidogo jambo lilitokea lililotushtua sana kwanza, lakini kisha lilituchekesha mno. Tulikuwa tukifuatana mmoja mmoja na Bwana Good ametangulia, mara nilisikia sauti yake inafifia kabisa, na tena tukasikia kelele na ghasia, na mkoromo na mguno na vishindo vya miguu. Katika giza tuliweza kuona kama vivuli vinakimbia vimefichwa kidogo kwa mavumbi ya mchanga.


Bwana Henry na mimi tulisimama tumeshangaa; na mshangao wetu ulizidi tulipoona Bwana Good anakwenda mbio kuelekea milima, juu ya kitu tulichodhani kuwa ni kama farasi, akipiga makelele moja kwa moja. Mara tulimwona ametupa mikono juu, tukamsikia akianguka chini kwa kishindo. Ndipo nilipotambua kuna nini; tulikuwa tumetokea kwenye kundi la punda milia waliokuwa wamelala, na Bwana Good alianguka juu ya mgongo wa mmoja ambaye aliamka akamchukua mgongoni mwake.


Nikawaambia watu wetu wasiogope, nikamkimbilia Bwana Good nikichelea kuwa labda ameumia, lakini nilifurahi nilipoona kuwa amekaa kitako juu, ya mchanga ameshangaa na kuogopa sana. Lakini hakuumia, Baada ya hayo tulikwenda bila ya kupatwa na jambo jingine mpaka saa saba hivi, tukapumzika kidogo tukanywa maji kidogo na baada ya kupumzika kwa muda wa nusu, ambaye mpaka sasa alikuwa akituchekesha mara kwa mara alinyamaza tu.


Basi ilipopata saa nane, tukafika kwenye kile kilima kidogo, tumechoka kabisa, na hapo tulikaa na kwa sababu kiu kilituzidi, tulimaliza maji yote. Tena hayakutosha . Basi tukalala, Nilipokuwa katika kusinzia, nilisikia Umbopa akisema peke yake, ‘Kama hatupati maji kesho kabla mwezi haujapanda mawinguni, basi tutakuwa maiti.’ Joto lilikuwa jingi sana, lakini hata hivyo nilitetemeka kama mtu aliyeshikwa na baridi. Maana kutarajia mauti si vizuri, na hasa mauti ya namna ile. Lakini hata fikira za mauti hazikuweza kunizuia nisipatwe na usingizi, nikalala.
 
Hapo alinyamaza kimya kidogo, na baadae akaendelea kutoa hotuba yake kama ilivyo desturi ya Wazulu. ‘Maisha ni kitu gani? Niambieni, Ee Wazungu, nyinyi wenye busara, nyinyi mjuao siri za dunia, na dunia ya nyota, na dunia iliyo juu na kuzunguka nyota; nyinyi mpelekao maneno yenu mbali bila kutumia sauti; niambieni, Ee nyinyi Wazungu, siri ya maisha yetu ni nini huenda wapi, hutoka wapi? Hamwezi kunipa jawabu; hamjui! Sikilizeni, nitawaambia. Maisha ni mkono tunaotumia kukinga mauti.

Ni kimulimuli kinachong’aa wakati wa usiku; ni kama pumzi nyeupe za ng’ombe zinazoonekana wakati wa baridi; ni kivuli kidogo kile kinachokimbia katika majani na kupotea katika jua hapo linaposhuka.’

Bwana Henry akasema, ‘Wewe Umbopa ni mtu wa ajabu.’ Umbopa akacheka kidogo akasema, ‘Huoni kuwa wewe na mimi tumefanana sana. Huenda hata na mimi nakwenda kuvuka milima ile ili kumtafuta ndugu yangu!; Nikamtazama sana nikamuuliza, ‘Je, maneno gani hayo, maana yake ni nini? Wewe unajua habari gani ya ile milima? Akajibu, ‘Kidogotu, kidogo sana.

Ni nchi ngeni kabisa, nchi ya uchawi na vitu vizuri; nchi ya watu hodari na miti na vilele vya theluji na njia nyeupe kubwa. Nimesikia habari zake, lakini iko faida gani kusema.? Sasa giza linashuka. Wale watakaoishi kuona wataiona.’ Nikamtazama tena, maana ilinibainika kuwa anajua habari zaidi. Alifahamu ninayoyafikiri, akasema, ‘Usiniogope, Makumazahn, mimi sitegi mitego upate kutegwa.

Mimi sifanyi hila. Ikiwa tutajaaliwa kuvuka milima ile iliyo nyuma ya jua, nitakwambia yote ninayoyajua. Lakini mauti yamekaa juu ya milima ile. Uwe na busara, urudi nyuma, nendeni mkawinde ndovu, mabwana. Nimesema.’

Na bila kusema neon jingine, aliinua sagai lake kutuaga akageuka akarudi kambini, na baadaye tulimkuta huko anasafisha bunduki kama wale watu wengine, Bwana Henry akasema, ‘Mtu huyu wa ajabu sana.’ Nikasema, ‘Ndiyo, nampenda kama simpendi.

Ajua neno lakini hataki kulisema. Lakini ya nini kugombana naye! Safari yetu ni ya ajabu na Mzulu wa ajabu hawezi kuzidisha ajabu yake.’ Siku ya pili tulifanya vitu vyote tayari kuanza safari yetu. Hatukuweza kuchukua bunduki nzito tukaziacha pamoja na vitu vingine kwa wapagazi wetu, tukafanya shauri kuwaacha katika nyumba ya mtu mmoja aliyekaa karibu.

Sikupenda kabisa kuviacha vitu hivyo, maana Yule mtu alivitazama kwa macho ya uroho sana, lakini nilifanya hila. Kwanza nilishindilia bunduki zote, nikaziweka tayari kupigwa, nikamwambia kuwa akizigusa hata kidogo, basi zitalia.

Yeye hakusadiki, na mara ile akashika moja, na kama nilivyomwonya, ikalia, na risasi ikampiga ng’ombe wake mmoja, na vile vile kishindo chake kikamwangusha chini. Akainuka upesi ameshtuka kabisa tena anaona uchungu kwa kupata hasara ya ng’ombe wake, akataka nimlipe, lakini hakutaka kabisa kugusa tena bunduki.

Akasema, ‘Weka shetani wale katika majani ya paa la nyumba au zitatuua sote.’ Nikamwambia kuwa tutakaporudi nikiona kuwa moja imepotea nitamuua yeye na watu wake wote kwa uchawi; na ikiwa haturudi naye akijaribu kuiba bunduki, basi vivuli vyetu vitakuja kumfuata na kuwatia wazimu ng’ombe wake, na kuharibu maziwa yao kabisa, mpaka maisha yake yatakuwa na udhia mtupu! baada ya hayo, akaapa kuwa atazitunza awezavyo.

Basi tukisha kuweka vitu vyetu salama, tulifunga mizigo midogo, tukawachagua Umbopa na Ventvogel wafuatane nasi, tukawa watano, yaani, Bwana Henry, Bwana Good, mimi na Umbopa na Ventvogel. Hatukuchukua vitu vingi, tulipunguza mzigo kadiri tulivyoweza. Tulichukua bunduki tano na bastola tatu, na viriba vya maji vitano, na mablanketi matano, na nyama kavu na shanga za kutoa zawadi, na dawa.

Tena tukachukua visu vyetu na vitu vidogo vidogo kama vile dira na vibiriti na tumbako. Basi vitu hivyo pamoja na nguo tulizokuwa tukivaa ndivyo tulivyo chukua, basi, Siku ya pili hatukufanya kitu, tulipumzika tu, na jua liliposhuka tuliamka tukala, tukafunga vitu vyote tayari, tukalala tena kungojea mbalamwezi.

Yapata saa tatu mwezi ukatoka ukaangaza nchi nzima na mbele yetu tukaona lile jangwa kubwa la kutisha sana. Tukaondoka, na baada ya dakika chache tukawa tayari, lakini hata sasa tulisita kidogo kama ilivyo desturi, ya kibinadamu ikiwa anaanza safari ya hatari. Sisi watu watatu tulisimama pamoja.

Umbopa akasimama mbele kidogo ameshika sagai lake mkononi na bunduki ameweka begani analitazama sana jangwa; na Ventvogel na watu watatu waliokubali kufuatana nasi kuchukua vibuyu vya maji kwa safari ya siku ya kwanza wakasimama pamoja nyuma yetu.

Basi Bwana Henry akasema, ‘Rafiki zangu, sasa tu tayari kuanza safari yetu ya ajabu. Labda hatutafaulu. Lakini sisi ni watu watatu, nasi tutashirikiana katika mambo mema na maovu mpaka mwisho, Na sasa kabla hatujaanza, na tumwombe Mungu anayeumba na kuandika ajali za wanadamu, ambaye tangu zamani amekwisha amuru njia zetu, atuongoze miguu yetu kama apendavyo.’

Akavua kofia yake na Bwana Good pia akavua yake, wakasimama kimya kwa muda. Mimi si mtu wa kuomba, nadhani wawindaji wachache sana huwa wa namna hiyo; wala sijamsikia Bwana Henry akisema namna hiyo lakini nadhani katika moyo wake ni mtu wa dini. Bwana Good vile vile ni mtu wa dini. Lakini siwezi kukumbuka hata siku moja niliyoomba kama nilivyoomba siku ile. Na lazima nikiri kuwa niliona faraja kwa kuomba hivyo.

Maana yaliyo mbele yetu hatukuyajua, na siku zote mambo yanayotisha na yasiyojulikana huvuta wanadamu wamkaribie Muumba wao. Kisha Bwana Henry akasema, ‘ Haya twendeni!’ Tukaanza safari yetu.

Hatukuwa na kiongozi ila milima ya mbali na ile ramani aliyoandika mzee Jose da Silvestre, na kwa kuwa iliandikwa na mtu aliyekuwa akifa juu ya kipande cha kitambaa miaka mia tatu iliyopita, haikuwa kiongozi cha kutia moyo sana.

Lakini hii ndiyo iliyokuwa tama yetu kufaulu. Tukikosa kuliona ziwa lile la maji machafu ambayo alama yake ilionyesha kuwa ni katikati ya jangwa, basi haikosi tutakufa kwa kiu.
Na nilifikiri kuwa bahati ya kuliona haiwezi kutumainiwa sana.

Na hata ikiwa Yule mzee da Silvestre alipima sawasawa na kufanya alama barabara katika ramani, je, baada ya miaka hii yote iliyopita sip engine limekauka,au labda wanyama wa porini wamekwisha kuyakanyaga maji mpaka yamekwisha, au labda yamekwisha kufunikwa na mchanga uliyopeperushwa na upepo? Basi tukaenda, tukaenda, usiku tukikanyaga mchanga na majani yale yaliyosokotana sokotana yalitunasa miguuni, na mchanga uliingia katika viatu vyetu ikawa mara kwa mara kusimama tupate kuutoa.

Basi hivi hivi tulisafiri, na Bwana Good alijaribu kututia moyo kwa kupiga mbinja, lakini sauti yake ilizidi kututia huzuni tu, akaacha. Baadae kidogo jambo lilitokea lililotushtua sana kwanza, lakini kisha lilituchekesha mno. Tulikuwa tukifuatana mmoja mmoja na Bwana Good ametangulia, mara nilisikia sauti yake inafifia kabisa, na tena tukasikia kelele na ghasia, na mkoromo na mguno na vishindo vya miguu. Katika giza tuliweza kuona kama vivuli vinakimbia vimefichwa kidogo kwa mavumbi ya mchanga.


Bwana Henry na mimi tulisimama tumeshangaa; na mshangao wetu ulizidi tulipoona Bwana Good anakwenda mbio kuelekea milima, juu ya kitu tulichodhani kuwa ni kama farasi, akipiga makelele moja kwa moja. Mara tulimwona ametupa mikono juu, tukamsikia akianguka chini kwa kishindo. Ndipo nilipotambua kuna nini; tulikuwa tumetokea kwenye kundi la punda milia waliokuwa wamelala, na Bwana Good alianguka juu ya mgongo wa mmoja ambaye aliamka akamchukua mgongoni mwake.


Nikawaambia watu wetu wasiogope, nikamkimbilia Bwana Good nikichelea kuwa labda ameumia, lakini nilifurahi nilipoona kuwa amekaa kitako juu, ya mchanga ameshangaa na kuogopa sana. Lakini hakuumia, Baada ya hayo tulikwenda bila ya kupatwa na jambo jingine mpaka saa saba hivi, tukapumzika kidogo tukanywa maji kidogo na baada ya kupumzika kwa muda wa nusu, ambaye mpaka sasa alikuwa akituchekesha mara kwa mara alinyamaza tu.


Basi ilipopata saa nane, tukafika kwenye kile kilima kidogo, tumechoka kabisa, na hapo tulikaa na kwa sababu kiu kilituzidi, tulimaliza maji yote. Tena hayakutosha . Basi tukalala, Nilipokuwa katika kusinzia, nilisikia Umbopa akisema peke yake, ‘Kama hatupati maji kesho kabla mwezi haujapanda mawinguni, basi tutakuwa maiti.’ Joto lilikuwa jingi sana, lakini hata hivyo nilitetemeka kama mtu aliyeshikwa na baridi. Maana kutarajia mauti si vizuri, na hasa mauti ya namna ile. Lakini hata fikira za mauti hazikuweza kunizuia nisipatwe na usingizi, nikalala.
Safiii. Ngoja niitafune taratibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SURA YA TANO
SAFARI YETU YA JANGWANI
Tulikuwa tumeua ndovu tisa, ikachukua kazi ya siku mbili kutoa pembe zao. Tulipokwisha kuzitoa tulizileta kambini tukachimba shimo chini ya mti mkubwa tukaziweka humo tukafukia shimo. Pembe zilikuwa nzuri kabisa, nadhani sijaona namna yake, maana zile za Yule mkubwa aliyemuua Khiva zilikuwa yapata ratili mia na sabini, kadiri tulivyoweza kukisia. Na marehemu Khiva tulimzika katika kaburi pamoja na sagai lake kama ilivyo desturi, yaani apate kujitetea katika safari yake ndefu kwenda ahera. Siku ya tatu tuliondoka tukafunga safari yetu tukitumaini kuwa tutarudi salama na kuchimbua pembe zetu. Baada ya safari ndefu ya kuchosha tulifika mji wa Sitanda karibu na mto wa Lukanga, na hapo kwa kweli ni mwanzo wa safari yetu. Nakumbuka sana siku ile tuliyofika huko.

Kwa upande wa kulia zilikuwa nyumba chache zimetawanyika pamoja na mazizi ya ng’ombe, na karibu na mto yalikuwapo mashamba ya wenyeji. Kupita mashamba hayo ni mwitu wenye majani marefu umejaa wanyama wa porini. Upande wa kushoto palikuwa jangwa lile kubwa. Hapo paonekana kwamba ni mwisho wa ardhi inayofaa kuoteshwa vitu, siwezi kujua kwa sababu gani, lakini ndivyo ilivyo.

Upande wa chini ya kambi yetu maji yalitiririka katika mto mdogo, na ng’ambo yamto palikuwa mteremko wenye mawe mengi. Huu ndio ulikuwa mteremko ule ule nilipomwona Yule Silvestre akitambaa kwa mikono na magoti miaka ishirini nyuma, yaani aliporudi katika safari yake ya kutafuta Mashimo ya Sulemani. Na kupita mteremko huo ni jangwa lile lisilo na maji, jangwa la ukiwa kabisa.

Tulipo piga kambi yetu ilikuwa ni jioni, na jua lilikuwa likizama, mfano wa mpira mkubwa mwekundu. Mishale ya nuru ya rangi mbali mbali ilitoka ikaenea jangwani. Bwana Henry na mimi tulimwacha Bwana Good atengeneze kambi, nasi tulipanda mteremko ule tukasimama tukitazama jangwa.

Mbingu zilikuwa nyeupe kabisa, na mbali sana tuliweza kuona milima ya Sulemani kama vivuli vikubwa, na wakati mwingine kuona theluji juu ya vilele vyake. Basi nikasema, ‘Kule ndipo upo ukuta unaozunguka Mashimo ya Sulemani, lakini anaejua kama tutaweza kuupita ni Mungu tu.’ Bwana Henry akasema, ‘Nadhani ndugu yangu yupo, na ikiwa yupo basi tutaonana, lazima.’ Nikasema, ‘InshaIlah.’

Tukageuka turudi kambini, nikaona kuwa sisi hatupo pekee yetu, maana nilimwona Umbopa amesimama nyuma yetu na macho yake ameyakodolea milima ile ya mbali. Umbopa alipoona tumemwona, akamwambia Bwana Henry, ‘Je, Inkubu, ile ndiyo nchi unayotaka kufika?’ (na jina la Inkubu ndilo jina walilomwita wenyeji, nadhani maana yake ni ‘ndovu’).

Basi Bwana Henry, akajibu, ‘Ndiyo ile nchi ninayokwenda.’ Umbopa akasema , ‘Inkubu, jangwa ni pan asana, tena hapana maji kabisa, milima ni mirefu sana na vilele vyake vimefunikwa na theluji, na mwanadamu hawezi kukisia kuna nini pale nyuma pale linaposhukia jua; utafika huko kwa njia gani, na kwa nini unataka kwenda?’

Basi nilimtafsiria maneno yale yote, na Bwana Henry akasema, Mwambie ya kuwa na kwenda kumtafuta ndugu yangu aliyenitangulia.’ Umbopa akasema, ‘Inkubu, ni kweli: maana njiani nilikutana na mtu mmoja kabila lake Hottentot akaniambia kuwa miaka miwili nyuma Mzungu mmoja alianza kuvuka jangwa amefuatana na mtumishi mmoja, nao hawakurudi.’ Bwana Henry akamuuliza, ‘Je, waona ya kuwa huyo ni ndugu yangu?’
Umbopa akajibu, ‘La, bwana sijui, ila nilipomuuliza Yule mtu yu wanamna gani, akajibu kuwa ana macho kama yako, lakini ndevu zake ni nyeusi, na tena amefuatana na mtumishi mmoja Mbechuana jina lake Jim.’

Basi nilipotafsiri maneno haya nikasema, ‘ Ndhani ‘ndiye bila shaka, maana mimi namjua Jim tangu zamani.’ Basi Bwana Henry akatikisa kichwa akasema, ‘Mimi nilijua hakika, maana ndugu yangu akitia nia yake kutenda jambo atalitenda. Ikiwa alitaka kuvuka milima ya Sulemani basi amekwisha kuivuka isipokuwa amezuiwa na jambo.

Na kwa hivi lazima tumtafute upande wa pili.’ Umbopa alifahamu Kiingereza ingawa hakukisema ila mara chache, akasema, ‘Inkubu, ni safari ndefu.’ Bwana Henry akajibu, ‘Ndiyo ni mbali, lakini hakuna jambo duniani asiloweza kufanya ‘mwanadamu ikiwa amedhamiria kulifanya.

Umbopa, ikiwa mapenzi yanamvuta mtu naye yu tayari kukosa maisha yake kama kwamba si kitu, hakuna jambo asiloweza kulitenda, hakuna milima asiyoweza kuipanda, hakuna jangwa asiloweza kulivuka, ila mlima mmoja na jangwa moja ambalo wewe hulijui.’ Nilipoyatafsiri maneno hayo , Umbopa alijibu, ‘Maneno makubwa, baba yangu, maneno yanapovuma kweli yanayostahili kusemwa na mwanaume. Umesema kweli, Inkubu baba yangu.

Sikiliza! Maisha ni kitu gani? Ni unyoya, ni mbegu ya majani, ikipeperushwa huko na huko, pengine huzaa na kujizidisha na ikisha kufanya hivyo hufa, pengine huchukuliwa mawinguni. Lakini ikiwa mbegu ni njema na nzito, huenda itasafiri kidogo katika njia ambayo inataka. Ni vizuri kujaribu kusafiri katika njia yako na kushindana na ajali. Kila mtu ameandikiwa kufa. Kama mambo yamezidi, basi hufa upesi kidogo zaidi tu. Baba yangu, nitafuatana nawe kuvuka jangwa na milima mpaka nitakapozuiwa na ajali njiani.’
 
Hapo alinyamaza kimya kidogo, na baadae akaendelea kutoa hotuba yake kama ilivyo desturi ya Wazulu. ‘Maisha ni kitu gani? Niambieni, Ee Wazungu, nyinyi wenye busara, nyinyi mjuao siri za dunia, na dunia ya nyota, na dunia iliyo juu na kuzunguka nyota; nyinyi mpelekao maneno yenu mbali bila kutumia sauti; niambieni, Ee nyinyi Wazungu, siri ya maisha yetu ni nini huenda wapi, hutoka wapi? Hamwezi kunipa jawabu; hamjui! Sikilizeni, nitawaambia. Maisha ni mkono tunaotumia kukinga mauti.

Ni kimulimuli kinachong’aa wakati wa usiku; ni kama pumzi nyeupe za ng’ombe zinazoonekana wakati wa baridi; ni kivuli kidogo kile kinachokimbia katika majani na kupotea katika jua hapo linaposhuka.’

Bwana Henry akasema, ‘Wewe Umbopa ni mtu wa ajabu.’ Umbopa akacheka kidogo akasema, ‘Huoni kuwa wewe na mimi tumefanana sana. Huenda hata na mimi nakwenda kuvuka milima ile ili kumtafuta ndugu yangu!; Nikamtazama sana nikamuuliza, ‘Je, maneno gani hayo, maana yake ni nini? Wewe unajua habari gani ya ile milima? Akajibu, ‘Kidogotu, kidogo sana.

Ni nchi ngeni kabisa, nchi ya uchawi na vitu vizuri; nchi ya watu hodari na miti na vilele vya theluji na njia nyeupe kubwa. Nimesikia habari zake, lakini iko faida gani kusema.? Sasa giza linashuka. Wale watakaoishi kuona wataiona.’ Nikamtazama tena, maana ilinibainika kuwa anajua habari zaidi. Alifahamu ninayoyafikiri, akasema, ‘Usiniogope, Makumazahn, mimi sitegi mitego upate kutegwa.

Mimi sifanyi hila. Ikiwa tutajaaliwa kuvuka milima ile iliyo nyuma ya jua, nitakwambia yote ninayoyajua. Lakini mauti yamekaa juu ya milima ile. Uwe na busara, urudi nyuma, nendeni mkawinde ndovu, mabwana. Nimesema.’

Na bila kusema neon jingine, aliinua sagai lake kutuaga akageuka akarudi kambini, na baadaye tulimkuta huko anasafisha bunduki kama wale watu wengine, Bwana Henry akasema, ‘Mtu huyu wa ajabu sana.’ Nikasema, ‘Ndiyo, nampenda kama simpendi.

Ajua neno lakini hataki kulisema. Lakini ya nini kugombana naye! Safari yetu ni ya ajabu na Mzulu wa ajabu hawezi kuzidisha ajabu yake.’ Siku ya pili tulifanya vitu vyote tayari kuanza safari yetu. Hatukuweza kuchukua bunduki nzito tukaziacha pamoja na vitu vingine kwa wapagazi wetu, tukafanya shauri kuwaacha katika nyumba ya mtu mmoja aliyekaa karibu.

Sikupenda kabisa kuviacha vitu hivyo, maana Yule mtu alivitazama kwa macho ya uroho sana, lakini nilifanya hila. Kwanza nilishindilia bunduki zote, nikaziweka tayari kupigwa, nikamwambia kuwa akizigusa hata kidogo, basi zitalia.

Yeye hakusadiki, na mara ile akashika moja, na kama nilivyomwonya, ikalia, na risasi ikampiga ng’ombe wake mmoja, na vile vile kishindo chake kikamwangusha chini. Akainuka upesi ameshtuka kabisa tena anaona uchungu kwa kupata hasara ya ng’ombe wake, akataka nimlipe, lakini hakutaka kabisa kugusa tena bunduki.

Akasema, ‘Weka shetani wale katika majani ya paa la nyumba au zitatuua sote.’ Nikamwambia kuwa tutakaporudi nikiona kuwa moja imepotea nitamuua yeye na watu wake wote kwa uchawi; na ikiwa haturudi naye akijaribu kuiba bunduki, basi vivuli vyetu vitakuja kumfuata na kuwatia wazimu ng’ombe wake, na kuharibu maziwa yao kabisa, mpaka maisha yake yatakuwa na udhia mtupu! baada ya hayo, akaapa kuwa atazitunza awezavyo.

Basi tukisha kuweka vitu vyetu salama, tulifunga mizigo midogo, tukawachagua Umbopa na Ventvogel wafuatane nasi, tukawa watano, yaani, Bwana Henry, Bwana Good, mimi na Umbopa na Ventvogel. Hatukuchukua vitu vingi, tulipunguza mzigo kadiri tulivyoweza. Tulichukua bunduki tano na bastola tatu, na viriba vya maji vitano, na mablanketi matano, na nyama kavu na shanga za kutoa zawadi, na dawa.

Tena tukachukua visu vyetu na vitu vidogo vidogo kama vile dira na vibiriti na tumbako. Basi vitu hivyo pamoja na nguo tulizokuwa tukivaa ndivyo tulivyo chukua, basi, Siku ya pili hatukufanya kitu, tulipumzika tu, na jua liliposhuka tuliamka tukala, tukafunga vitu vyote tayari, tukalala tena kungojea mbalamwezi.

Yapata saa tatu mwezi ukatoka ukaangaza nchi nzima na mbele yetu tukaona lile jangwa kubwa la kutisha sana. Tukaondoka, na baada ya dakika chache tukawa tayari, lakini hata sasa tulisita kidogo kama ilivyo desturi, ya kibinadamu ikiwa anaanza safari ya hatari. Sisi watu watatu tulisimama pamoja.

Umbopa akasimama mbele kidogo ameshika sagai lake mkononi na bunduki ameweka begani analitazama sana jangwa; na Ventvogel na watu watatu waliokubali kufuatana nasi kuchukua vibuyu vya maji kwa safari ya siku ya kwanza wakasimama pamoja nyuma yetu.

Basi Bwana Henry akasema, ‘Rafiki zangu, sasa tu tayari kuanza safari yetu ya ajabu. Labda hatutafaulu. Lakini sisi ni watu watatu, nasi tutashirikiana katika mambo mema na maovu mpaka mwisho, Na sasa kabla hatujaanza, na tumwombe Mungu anayeumba na kuandika ajali za wanadamu, ambaye tangu zamani amekwisha amuru njia zetu, atuongoze miguu yetu kama apendavyo.’

Akavua kofia yake na Bwana Good pia akavua yake, wakasimama kimya kwa muda. Mimi si mtu wa kuomba, nadhani wawindaji wachache sana huwa wa namna hiyo; wala sijamsikia Bwana Henry akisema namna hiyo lakini nadhani katika moyo wake ni mtu wa dini. Bwana Good vile vile ni mtu wa dini. Lakini siwezi kukumbuka hata siku moja niliyoomba kama nilivyoomba siku ile. Na lazima nikiri kuwa niliona faraja kwa kuomba hivyo.

Maana yaliyo mbele yetu hatukuyajua, na siku zote mambo yanayotisha na yasiyojulikana huvuta wanadamu wamkaribie Muumba wao. Kisha Bwana Henry akasema, ‘ Haya twendeni!’ Tukaanza safari yetu.

Hatukuwa na kiongozi ila milima ya mbali na ile ramani aliyoandika mzee Jose da Silvestre, na kwa kuwa iliandikwa na mtu aliyekuwa akifa juu ya kipande cha kitambaa miaka mia tatu iliyopita, haikuwa kiongozi cha kutia moyo sana.

Lakini hii ndiyo iliyokuwa tama yetu kufaulu. Tukikosa kuliona ziwa lile la maji machafu ambayo alama yake ilionyesha kuwa ni katikati ya jangwa, basi haikosi tutakufa kwa kiu.
Na nilifikiri kuwa bahati ya kuliona haiwezi kutumainiwa sana.

Na hata ikiwa Yule mzee da Silvestre alipima sawasawa na kufanya alama barabara katika ramani, je, baada ya miaka hii yote iliyopita sip engine limekauka,au labda wanyama wa porini wamekwisha kuyakanyaga maji mpaka yamekwisha, au labda yamekwisha kufunikwa na mchanga uliyopeperushwa na upepo? Basi tukaenda, tukaenda, usiku tukikanyaga mchanga na majani yale yaliyosokotana sokotana yalitunasa miguuni, na mchanga uliingia katika viatu vyetu ikawa mara kwa mara kusimama tupate kuutoa.

Basi hivi hivi tulisafiri, na Bwana Good alijaribu kututia moyo kwa kupiga mbinja, lakini sauti yake ilizidi kututia huzuni tu, akaacha. Baadae kidogo jambo lilitokea lililotushtua sana kwanza, lakini kisha lilituchekesha mno. Tulikuwa tukifuatana mmoja mmoja na Bwana Good ametangulia, mara nilisikia sauti yake inafifia kabisa, na tena tukasikia kelele na ghasia, na mkoromo na mguno na vishindo vya miguu. Katika giza tuliweza kuona kama vivuli vinakimbia vimefichwa kidogo kwa mavumbi ya mchanga.


Bwana Henry na mimi tulisimama tumeshangaa; na mshangao wetu ulizidi tulipoona Bwana Good anakwenda mbio kuelekea milima, juu ya kitu tulichodhani kuwa ni kama farasi, akipiga makelele moja kwa moja. Mara tulimwona ametupa mikono juu, tukamsikia akianguka chini kwa kishindo. Ndipo nilipotambua kuna nini; tulikuwa tumetokea kwenye kundi la punda milia waliokuwa wamelala, na Bwana Good alianguka juu ya mgongo wa mmoja ambaye aliamka akamchukua mgongoni mwake.


Nikawaambia watu wetu wasiogope, nikamkimbilia Bwana Good nikichelea kuwa labda ameumia, lakini nilifurahi nilipoona kuwa amekaa kitako juu, ya mchanga ameshangaa na kuogopa sana. Lakini hakuumia, Baada ya hayo tulikwenda bila ya kupatwa na jambo jingine mpaka saa saba hivi, tukapumzika kidogo tukanywa maji kidogo na baada ya kupumzika kwa muda wa nusu, ambaye mpaka sasa alikuwa akituchekesha mara kwa mara alinyamaza tu.


Basi ilipopata saa nane, tukafika kwenye kile kilima kidogo, tumechoka kabisa, na hapo tulikaa na kwa sababu kiu kilituzidi, tulimaliza maji yote. Tena hayakutosha . Basi tukalala, Nilipokuwa katika kusinzia, nilisikia Umbopa akisema peke yake, ‘Kama hatupati maji kesho kabla mwezi haujapanda mawinguni, basi tutakuwa maiti.’ Joto lilikuwa jingi sana, lakini hata hivyo nilitetemeka kama mtu aliyeshikwa na baridi. Maana kutarajia mauti si vizuri, na hasa mauti ya namna ile. Lakini hata fikira za mauti hazikuweza kunizuia nisipatwe na usingizi, nikalala.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom