Hebu nii'pasue taratiiibuSURA YA KUMI NA SABA
Wakati ule tulipokuwa tukitazama kila kitu katika Mahali pa Mauti. Gagula alikuwa akifanya kazi yake. Alipanda mezani akaenda karibu na maiti ya Twala, na tena akampitia kila maiti akafanya kama anaongea na maiti.
Alipokwisha fanya hivyo akakaa kitambo kidogo chini ya ile sanamu kubwa akaanza kusema maneno mengi kama anasali.
Basi nikasema, ‘Haya Gagula, tuongoze katika chumba.’ Yule kizee akaondoka, akanitazama usoni, akasema, ‘Mabwana zangu hamuogopi?’
Nikajibu, ‘Tuongoze.’
Akasema, ‘Vema, mabwana zangu.’ Akazunguka nyuma ya ile sanamu ya Mauti, akasema, ‘Chumba kiko hapa. Afadhali uwashe taa kwanza.’
Akasimama ukutani. Basi nikawasha taa nikatazama nione mlango uko wapi, nisiuone; niliona ukuta tu. Gagula akacheka sana akasema, ‘Njia ni ile, mabwana zangu. Ha!Ha!Ha!’ nikasema, ‘Usifanye udamisi.’
Akajibu, ‘Mimi sifanyi udamisi, mabwana zangu, tazameni!’
Akatuonyesha ukuta. Tuliinua taa na alipokuwa akituonyesha, ukuta, kumbe ule mkubwa ulianza kupanda juu na kuingia katika sehemu ya juu ya pango.
Namna alivyo fyatua mtambo ulioinua ukuta ule, sisi hatukuona, maana alifanya hila za kutuficha.
Vile ukuta ulipanda pole pole mpaka ukaingia kabisa, tukaona mlango wa kuingilia katika pango la ndani. Sasa hatukuweza kusubiri tena, maana tupo hapo kwenye hazina, lakini mimi nilianza kuogopa na kutetemeka, sijui wenzangu walikuwaje.
Je, itakuwa ni hila tu, au yale maneno ya Da Silvestre yatatokea kuwa ya kweli? Kweli katika pango zimo hazina nyingi sana hata kutufanya kuwa matajiri kupita wote duniani? Punde tutajua.
Gagula akasema, ‘Haya ingieni nyinyi watu weupe mliotoka katika nyota, lakini kwanza msikilizeni mtumishi wenu, kizee Gagula.
Mawe yanayong’aa mtakayoyaona yalichimbuliwa katika shimo lile kubwa lililo chini ya Watatu Walio Kimya, nayo yaliwekwa hapa sijui na nani.
Mahali hapa pameingiliwa mara moja tu tangu wakati ule walipotoka kwa haraka sana wale walioyaweka mawe haya wakayaacha.
Habari za hazina zilijulikana na watu, maana zimekuwa zikipokezana kizazi baada ya kizazi, lakini hapana aliyejua chumba kiko wapi wala siri ya mlango wa chumba hicho.
Lakini mtu mweupe alitokea, akafika nchi hii kwa kuvuka milima ile, sina habari kama yeye alitoka katika nyota, akapokewa vizuri na mfalme wa wakati ule. Ilisadikika kuwa mwanamke mmoja wa nchi hii alisafiri pamoja naye, na Yule mwanamke akapata kujua siri ya ule mlango.
Basi Yule mtu mweupe aliingia pamoja na Yule mwanamke, wakaona mawe, akajaza mawe katika kifuko kidogo cha ngozi ya mbuzi alichokichukua Yule mwanamke ili kuwekea chakula chao.
Alipokuwa akitoka chumbani akainama achukue jiwe moja jingine lililokuwa kubwa, akalishika mkononi.’
Hapa Gagula akanyamaza . nikamuuliza, ‘Yapi yaliyompata Da Silvestre?’
Yule kizee akashtuka mno, akaniuliza, ‘Umejuaje jina la mtu huyo aliyekufa?
Hapana mtu anayejua yaliyotokea; lakini ilikuwa dhahiri kuwa Yule mtu mweupe aliogopa sana, akatupa kifuko kile cha mawe akatoka chumbani mbio huku kachukua jiwe moja tu.’
Jiwe lenyewe ni lile ulilolifungua wewe Makumazahn, katika paji la uso wa Twala.’ Nikamuuliza, ‘Je, hapana aliyepata kuingia tokea wakati huo?’
Akajibu, ‘Hapana, mabwana zangu. Lakini siri ya mlango ilisitirika na kila mfalme amefungua mlango, lakini hapana aliyethubutu kuingia.
Imesemwa kuwa atakayeingia katika chumba hiki atakufa katika muda wa mwezi mmoja, kama mtu Yule mweupe alivyokufa katika pango mlimani pale ulipomwona wewe Makumazahn, na kwa hivyo wafalme hawaingii.
Ha!Ha! maneno yangu ni ya kweli kabisa.’
Basi kusikia maneno hayo, tukatazamana, ghafula nikaona baridi na kuchafukwa na moyo. Kizee huyu alijuaje habari hizi zote?
Basi akasema, ‘Haya ingieni, mabwana zangu. Ikiwa nimesema kweli mtaona kifuko kile cha ngozi ya mbuzi kilichojaa mawe kimetupwa chini, na ikiwa ni kweli kuwa wale watakaoingia watakufa, basi haya mtapata kuyajua halafu!Ha!Ha!Ha!’
AiseeAkaingia mlangoni huku kachukua ile taa lakini lazima nikiri kuwa nilisita tena.
Bwana Good akasema, ‘Mimi nitaingia, hiki kishetani hakiwezi kunitisha mimi, ‘Akaingia na Foulata akamfuata na sisi tuliwafuata upesi.
Gagula alisimama mbele kidogo anatungoja, akasema, ‘Tazameni, mabwana zangu, wale walioweka hazina hapa walikimbia kwa haraka, wakafikiri kulinda siri, isijulikane na watu wengine lakini hawakupata nafasi.’
Akatuonyesha mawe makubwa yaliyoletwa tayari kusudi kuziba ile njia.
Basi tulikwenda mbele na Foulata akazidi kuogopa akasema kuwa hawezi kuendelea, basi tukamwambia akae atungojee, tukaweka kikapu karibu naye, tukaendelea.
Tulipokwisha kwenda kadiri ya hatua kumi na tano, tuliona mlango wa mbao umekaa wazi.
Yule aliyekuwa wa mwisho kutoka alikuwa amesahau kuufunga au labda alitishwa na kitu. Na pale mlangoni tuliona kifuko cha ngozi ya mbuzi kimejaa mawe! Gagula alicheka akasema, ‘Hee!Hee!
Watu weupe, niliwaambia nini? Sikusema kuwa Yule mtu weupe alifika hapa, akakimbia kwa haraka, akatupa kile kifuko cha mwanamke? Kitazameni!’
Bwana Good akainama akakiokota, akakiona kizito na akasema, ‘Lo! Kimejaa almasi.’
Bwana Henry akasema, ‘Haya twendeni mbele; nipe taa wewe kizee.’
Akatwaa ile taa akaingia chumbani, na sisi tulimfuata karibu na mara tukajiona katika chumba cha hazina za Sulemani.
Tulipozoea giza tuliona chumba kimechimbwa katika mlima. Tukaona pembe za ndovu nyingi sana, yapata mia nne au mia tano. Pembe hizi peke yake zilikuwa zinatosha kumfanya mtu kuwa tajiri maisha yake yote.
Katika upande mwingine wa chumba tuliona masanduku madogo yaliyo pakwa rangi nyekundu, nikasema, ‘Hizi ni almasi, lete taa.’
Bwana Henry akaleta taa akaiweka karibu na sanduku ambalo mbao zake za juu zilikuwa zimevunjika ; nikaingiza mikono yangu na kuitoa imejaa, si almasi bali sarafu za dhahabu. Basi nilirudisha dhahabu ile nikasema, ‘Hatutarudi mikono mitupu.’
Basi Gagula alitwambia, ‘Mabwana zangu mkitaka almasi na muende pale pembeni mtaona makasha matatu, mawili yametiwa muhuri na moja tayari limefunguliwa.’
Kabla sijatafsiri maneno haya kuwaambia Bwana Henry na Bwana Good, nilifikiri moyoni jinsi alivyopata kujua habari hizo huyu Gagula, yaani ikiwa hapana aliyeingia humu tangu Yule mtu mweupe alipoingia zamani, vizazi vingi nyuma.
Gagula alitambua mawazo yangu, akasema kwa maneno ya kunidharau, ‘Ah! Makumazahn, wewe unayekesha usiku, nyinyi mkaao katika nyota, hamjui kuwa wapo wanaoweza kuona hata ndani ya majabali? Ha!Ha!Ha!’
Lakini Bwana Good alikuwa amekwisha ona zile almasi, akasema, ‘Haya jamani, njooni mtazame.’ Tukaenda kwa haraka, tukaona pembeni makasha matatu, mawili yametiwa muhuri na moja limefunguliwa.
Tukatazama tukaona kuwa zimejaa almasi, nikasema kwa sauti ndogo, ‘Sisi ni matajiri kupita watu wote duniani.’
Bwana Henry akasema, ‘Ndiyo, lakini lazima tuzichukue kwetu kwanza!’ Tukasimama tunatazamana, na mara tukamsikia Gagula anacheka tena; Hee!Hee!Hee! Hayo ndiyo mawe meupe mnayopenda; yachukueni, myale, na myanywe, ha!ha!h!’
Basi hapo nilipomsikia akisema maneno hayo, nikaona ni maneno ya kuchekesha tu! Maana nani aliyesikia mtu akila na akinywa almasi! Nikaanza kucheka, na wenzangu nao wakaanza kucheka vile vile; tukacheka sana.
Gagula akasema, ‘Haya, mabwana zangu, chukueni kadiri mnavyotaka.’
Basi tukazidi kutazama almasi zile huku tumefurahi lakini hatukuona jinsi Gagula alivyotoka pole pole katika kile chumba na sasa anakaribia ule ukuta mkubwa wa jabali.
Mara tukashtuka sana kwa kusikia sauti ya Foulata.’Lo!Lo!Lo! Mwamba unaanguka!’
Dah, foulata aisee dahTukasikia sauti ya Gagula, ‘Niachilie wewe! Niachilie. Na tena sauti ya Foulata, ‘Aa!Aa! Amenichoma kisu!’ lakini sasa tulikuwa tunakwenda mbio na tulipofika karibu, mwangaza wa taa ulituonyesha hivi:
Ukuta ule ukirudi pole pole katika mahali pake, na sasa nafasi iliyobaki kwa chini ni kadiri ya futi tatu tu.
Pale karibu na mwamba Foulata na Gagula wamekamatana wa kiviringishana. Damu ilikuwa ikimtoka Foulata, lakini hakukubali kumwacha kile kichawi kilichokuwa kikipigana kama paka wa mwituni.
Ah! Amemtoka! Foulata ameanguka chini na Gagula anatambaa chini ya ukuta wa jabali kama nyoka. Yupo chini sasa! Lo! Amechelewa! Amechelewa! Ukuta unamponda naye analia kwa maumivu. Chini, chini, ule ukuta mzito unazidi kumponda.
Analia vilio tusivyosikia maishani mwetu, kisha, tulisikia namna ukuta ule ulivyombinya mifupa yake, na mara tukafika kwenye ukuta, tumekwisha chelewa, tumekwisha fungiwa ndani!
Sasa tulimtazama Foulata, tukaona kuwa amechomwa kisu maungoni, naye yumo katika kukata roho.
Akasema, ‘Ah! Bwana wangu, nakufa! Gagula alikuwa akinyatia; sikumwona kwanza maana hakukuwa na mwangaza wa kutosha, na ukuta ukaanza kurudi chini; alirudi nyuma ili atazame mara ya pili, nikamwona, nikamshika, akanichoma kisu, na sasa nakufa!’
Basi akafa, na Bwana Good akasimama na machozi yakimtiririka, akasema, ‘Amekufa! Amekufa!’
Bwana Henry akasema, ‘Basi nawe usijisumbue rafiki, maana karibu utaweza kumfuata alipo. Maana huoni kuwa sisi tumezikwa tungali hai?’
Nadhani mpaka Bwana Henry aliposema maneno hayo, hatukutambua kwa hakika hatari itakayo tupata. Lakini sasa tulifahamu.
Jabali lile lililoshuka chini limekwisha kutufungia ndani ya chumba, na aliyejua siri ya kulifungua amekwisha kufa! Amepondeka chini yake! Kwa muda tulipigwa na mshangao, ikawa kama nguvu zimetuisha, na Bwana Henry akasema, ‘ Haya, tutafute siri ya mtambo unaoendesha huu ukuta, upesi.’
Tukapapasa papasa kila mahali tukijaribu kutafuta huo mtambo hatukuona hata alama. Nikasema, ‘Mimi naona kuwa mtambo haupo upande huu; kama ungekwepo kwa nini Gagula alijitia katika hatari ya kutambaa chini apate kutoka kabla ukuta haujashuka?
Alijaribu kutambaa chini kwa sababu alijua kuwa hapana njia nyingine ya kutoka katika chumba.’
Bwana Henry akasema, ‘Lakini Mungu amemlipa upesi, maana kufa kwake kulikuwa kubaya sana. Hatuwezi kuinua ukuta. Basi naturudi katika chumba cha hazina.’
Tukarudi na tulipokuwa tukimpita Foulata niliona kapu lile lenye chakula na vibuyu vya maji, nikalichukua katika chumba. Tukakaa juu ya makasha yale ya hazina, na Bwana Henry akasema, ‘Tugawanye hicho chakula tukitunze kadiri tunavyoweza.’
Tukakigawanya. Chakula kilikuwa cha kutosha kadiri ya siku mbili tu. Tulipokwisha kula kidogo tukaondoka tukatazama kila mahali kutafuta njia ya kutokea tusiione.
Taa ikaanza kuzimika, na mafuta yalikuwa karibu kwisha. Bwana Henry akauliza, ‘Je, Quatermain, sasa saa ngapi?’ Nikatazama saa yangu nikamwambia kuwa ni saa kumi na mbili, nasi tuliingia pangoni saa tano, nikasema, ‘Infadus atatukumbuka, na kama hatatutafuta leo, basi kesho ni lazima atatutafuta.’
Bwana Henry akajibu, ‘Ndiyo, lakini anaweza kututafuta bure. Yeye hajui siri ya kuinua ukuta huu, wala hana habari ya mlango ulipo.
Ni mtu mmoja tu alijua, naye ni Gagula, na hapana mtu mwingine anayejua. Hata akiuona, yeye hawezi kuvunja jabali lile, hata akileta jeshi zima la Wakukuana.
Rafiki zangu, mimi naona hatuna la kufanya ila kujiweka katika mikono ya Mungu. Kutafuta utajiri kumewaangamiza wengi; nasi tutazidisha hesabu yao.’
Hapo taa ikazidi kuzimika. Na mara moja ilipanda juu tena na tukaona pembe zote na makasha ya almasi naya dhahabu, na kifuko kile cha ngozi, na tukamwona maiti Foulata. Kisha taa ikazimika kabisa.
Bwana Henry alikuwa mtu mwema sana! Hata tungalikuwa watoto wawili naye ni mlezi wetu, nadhani asingaliweza kutufanyia wema zaidi.SURA YA KUMI NA NANE
Siwezi kabisa kueleza vitisho na taabu za usiku uliofuata. Zilipunguzwa kidogo kwa usingizi, maana hata katika hatari kama ile tuliyokuwa nayo, usingizi ulitujia kwa jinsi tulivyochoka.
Lakini sikuweza kulala sana, maana niliona mauti yananikaribia, kimya kikawa kingi hata sikuweza kupata usingizi. Tumezikwa ndani ya mlima wa theluji, na hata vishindo vya mizinga yote ya dunia haviwezi kutufikia.
Tumetengwa kabisa na kila sauti ya duniani, tumekuwa kama watu waliokwisha kufa. Ndipo nilipokumbuka mambo yote yaliyotupata. Hapo karibu nasi ziko fedha za kutosha kulipia madeni ya watu wote duniani, na kuunda meli zilizo bora, lakini hazitufai kabisa. Kweli, mali ambayo watu wengi huitafuta maisha yao yote, mwisho wake haina thamani hata kidogo.
Usiku ulipita. Baadaye, Bwana Henry akauliza, ‘Je, Bwana Good, unazo chembe ngapi za kibiriti?’ Akajibu, ‘Vijiti vinane tu.’
Akasema, ‘Vema, afadhali washa kimoja sasa tupate kujua ni saa ngapi.’
Akawasha kimoja, na kulikuwa giza totoro, hata alipokiwasha macho yaliingiwa na kiwi. Ilikuwa saa kumi na moja.
Akasema, ‘Afadhali na tule kidogo sasa tupate nguvu kidogo.’ Na Bwana Good akauliza, ‘Ya nini kula, si afadhali tukihimize kifo?’
Bwana Henry akajibu, ‘Kama maisha yapo, basi na tamaa ipo.’ Basi tukala, tukanywa maji kidogo; tukangoja. Kisha Bwana Good akasema, ‘Afadhali na tukae karibu na mlango tupate kumsikia atakayekaribia.’
Basi akakaribia mlangoni akaanza kupiga kelele, lakini wapi! Alifanya kelele nyingi sana, lakini zilitufaa nini? Baadaye akaacha kupiga kelele, maana tuliona kuwa zinatuzidishia kiu tu.
Basi tulikaa tena juu ya makasha yale ya almasi yaliyokuwa na hazina za thamani nyingi, na mimi nilikata tamaa nikaweka kichwa changu kwenye bega la Bwana Henry nikalia na kutokwa na machozi; na nadhani nilimsikia Bwana Good akilia vile vile.
Bwana Henry alikuwa mtu mwema sana! Hata tungalikuwa watoto wawili naye ni mlezi wetu, nadhani asingaliweza kutufanyia wema zaidi.
Alisahau sehemu yake ya taabu akajaribu kutuliwaza kwa kutusimuliwa hadithi za watu waliopatwa na mambo kama haya yaliyotupata sisi, na namna walivyookoka mwishoni.
Na alipoona hadithi zile haziwezi kutuliwaza akatwambia kuwa ni lazima watu wote wafe siku moja, basi sisi tumepungukiwa siku zetu kidogo tu. Alijaribu kwa kila namna kutuliwaza.
Alikuwa mtu mpole na mtaratibu wala hana makuu, lakini alikuwa mtu imara.
Basi mchana nao ulipita kama ulivyopita usiku, tukatazama saa tena tukaona kuwa ni saa moja, na tena tukala kidogo tukanywa, na tulipokuwa tunakula nikapata wazo nikasema, ‘Je, imekuwaje kuwa hewa iliyomo katika chumba hiki ni nzuri? Kweli ni nzito kidogo, lakini ni safi kabisa.’
Bwana Good akashtuka akasema, ‘Kweli! Sikufikiri hivyo. Hewa haiweze kuingia kwa mlangoni, maana pamezibwa kabisa,. Ingelikuwa hewa haingii siku zote, tulipoingia tungalihisi hewa mbaya. Tutazame.’
Basi ikawa ajabu namna tulivyochangamka kwa kupata cheche hizo za tamaa. Na mara sote watatu tulianza kutambaa chini na kupapasa kila mahali tupate kutafuta hata dalili ya hewa.
Kwa muda wa saa nzima na zaidi tulifanya hivi mpaka Bwana Henry na mimi tulikata tamaa tena, maana tuliumia mara nyingi kwa kujigonga na zile pembe na yale makasha, lakini Bwana Good hakukubali kushindwa, akasema afadhali kufanya hivi kuliko kukaa bure.
Baadaye kidogo akatuita, na mara tukamwendea, akasema, ‘Haya, Quatermain, weka mkono wako ulipowangu. Je, unaona kitu?’
Nikajibu, ‘Nadhani nasikia kitu. Nadhani nasikia kama baridi inaingia.’
Akasema, ‘Basi, sasa sikiliza.’ Akasimama akakanyaga chini kwa mguu mmoja, na mara ile tamaa yetu ndogo ikageuka na kuwa tamaa nyingi zilizotujaa maana palilia wazi.
Mambo ni moto chief nakuelewaga sanaaa... MzeeBabaaAkajibu, ‘Ndiyo, nilitamani sana, Makumazahn.’ Nikasema, ‘Ndivyo, Ignosi, mioyo yetu inavyotamani kwetu, nchi yetu.’
Basi, akakaa kimya kwa muda, kisha akasema, ‘Sasa nimefahamu kuwa maneno yako yana maana, nayo ni ya busara kama yalivyo siku zote.
Wale warukao hewani hawapendi kutambaa chini; watu weupe hawapendi kukaa wanavyokaa watu weusi.
Haya, kama lazima mwende, nendeni, mniache na moyo mnyonge, kwa sababu mkisha kwenda mtakuwa kwangu kama mliokufa, maana sipati habari zenu tena.
Infadus, mjomba wangu, atawachukueni na yeye mwenyewe pamoja na jeshi lake atawaongozeni. Nimesikia kuwa ipo njia nyingine ya kuvukia milima, naye atawaonyesheni.
Kwa herini, ndugu zangu, watu weupe mashujaa. Msinitazame tena, maana sina moyo tena.
Tazameni, natoa amri nayo itatangazwa kutoka milima mpaka milima, majina yenu, Ndovu, na Makumazahn, na Bougwan yatakuwa mwiko kutajwa tokea hivi leo, kama yanavyokuwa majina ya wafalme wanaokufa.
Atakayeyataja, atakufa, hivyo ndivyo majina yenu yatakavyo kumbukwa daima katika nchi hii.
‘Nendeni sasa machozi yasije yakanimiminika kama mwanamke.
Kila mkikumbuka mambo yaliyopita kumbukeni namna tulivyopigana bega kwa bega katika vita vikubwa ulivyoviongoza wewe, Makumazahn, au namna wewe ulivyokuwa mwisho wa askari wale waliozunguka upande wakalishinda jeshi la Twala, wewe Bougwan, au namna ulivyokaa katikati ya Wajivu na watu wakaanguka kama mavuno mbele ya shoka lako, wewe Ndovu; na namna ulivyozivunja nguvu za fahali Twala, ukakivunja na kukizika kiburi chake.
Kwaaherini, kwa heri milele, Ndovu na Makumazahn na Bougwan, rafiki zangu.’
Basi Ignosi akatutazama kimya kwa muda kidogo. Kisha akavuta ngezi ile aliyovaa akajifunika kichwa kujificha uso, Tukatoka kimya.
Kulipopambazuka tulitoka mji wa Loo, na rafiki yetu Infadus, naye vile vile moyo wake ulikuwa na huzuni kwa kuagana nasi.
Ingawa tuliondoka mapema sana, njia zote zilijaa watu, wakituamkia kwa maamkio ya kifalme tulipokuwa tukipita, na wanawake wakatushukuru kwa sababu tulimwondoa Twala, wakatutupia maua.
Tulipokuwa tukisafiri, Infadus alitwambia kuwa ipo njia nyingine ya kuvukia milima. Baada ya kusafiri kwa muda wa siku nne mwendo wa taratibu tulifika tena kwenye milima inayopakana na nchi ya Wakukuana na lile jangwa.
Hapa tuliagana na Infadus, askari shujaa, akatutakia mema katika safari yetu, na akawa karibu ya kulia kwa huzuni; akasema, ‘Mabwana zangu, macho yangu hayataona tena watu kama nyinyi.’
Nasi tuliona huzuni kuagana naye. Basi, baada ya kutazama kuwa chakula na maji na kila kitu cha safari yetu kiko sawa, tulipeana mikono na kuagana na Infadus, nasi tukaanza kushuka mlima. Ilikuwa kazi ngumu, lakini tulifika chini salama.
Asubuhi tulianza safari yetu ya taabu ya kuvuka lile jangwa, lakini tulikuwa na maji ya kutosha yaliyochukuliwa na wapagazi watano.
Saa sita, siku ya tatu tulifika kwenye mahali penye majani na miti.
Pamoja mkuuMambo ni moto chief nakuelewaga sanaaa... MzeeBabaa
Asante mkuuSURA YA ISHIRINI
Na sasa nitasimulia habari zilizo za ajabu kupita zote za safari yetu, nazo labda zitaonyesha namna mambo yanavyotokea kwa ajali. (mambo yote hutokea kwa sababu)
Nilikuwa nikitembea pale tulipofika penye majani na miti, na mara niliona mambo ya kustajabisha. Mbele yangu, kadiri ya hatua ishirini, niliona banda limejengwa chini ya mti.
Nikasema kimoyomoyo, ‘Je, banda hili limekujaje hapa?’ Na mara niliona mtu mweupe anachechemea akitoka bandani amevaa ngozi, naye ana ndevu nyeusi ndefu.
Kwanza nilifikiri kuwa labda nimeshikwa na homa na nimo njozini. Maana, ilikuwa haimkiniki.
Hapana mwindaji aliyepata kufika hapa na hakika hapana mtu aliyepata kujenga nyumba hapa na kupafanya kwake.
Nikatazama tazama, na hapo Bwana Henry na Bwana Good wakaja, nikawaambia, ‘Haya jamani, huyu ni mtu mweupe au labda nimeshikwa na wazimu?’
Bwana Henry akatazama, na Bwana Good akatazama, ndipo Yule mtu mweupe alipotuona akatupigia kelelena akaanza kutujia anachechemea. Alipofika karibu, akaanguka kama kwamba amezimia.
Mara Bwana Henry upesi akamwinamia, akasema, ‘Alhamdulilahi! Ni ndugu yangu George!’
Kusikia kelele, mara mtu mwingine amevaa ngozi vile vile akatoka bandani kachukua bunduki, akatujia mbio.
Aliponiona, akasema, ‘Makumazahn, hunijui, bwana? Mimi ni Jim, mwindaji. Barua ile uliyonipa nimpe bwana wangu ilinipotea nasi tumekaa hapa hapa kwa muda wa miaka miwili.’
Na pale pale akaanguka penye miguu yangu akagaagaa na kupiga kelele kwa furaha. Nikasema, ‘Ee wewe, mzembe! Unastahili kupigwa sana.’
Huku nyuma Yule mtu mweupe akazinduka tena, akasimama, na yeye na Bwana Henry wakashikana mikono kwa nguvu kimya! Hawakuweza kusema hata neno. Ule ugomvi wa zamani ulisahauli kabisa.
Baadaye Bwana Henry akapata kauli akasema, ‘Mpenzi ndugu yangu, nilifikiri kuwa umekwisha kufa. Nimevuka milima ya Sulemani ili kukutafuta, na sasa ninakuona unakaa jangwani kama kunguru!’
Yule mtu akajibu, ‘Mimi nilijaribu kuvuka milima miaka miwili nyuma, lakini nilipofika hapa jabali liliniangukia likanivunja mguu, nami nikakaa hapa, sikuweza kwenda mbele wala kuru nyuma .’
Ndipo nilipokaribia mimi, nikasema, ‘Hujambo, bwana Neville? Unaweza kunikumbuka?’
Akanitazama akasema ‘Kumbe, Quatermain, na wewe Bwana Good vile vile. Ngojeni, rafiki zangu, naona kizunguzungu tena. Mambo haya ni ya ajabu na ya furaha tupu na hasa kwa mtu aliyekwisha kata tamaa.