Hadithi: Uchawi wa bilionea Bazoka

Hadithi: Uchawi wa bilionea Bazoka

Chilojnr

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2012
Posts
308
Reaction score
1,354
NYEMO CHILONGANI.
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA.
0718069269


Ndiyo kwanza mwanga wa asubuhi ulikuwa ukitokeza, watu waliokuwa wakifanya kazi sehemu za mbali, wakaamka na kuanza kujiandaa kwenda makazini, kwa wale waliokuwa njiani kuelekea makazini kwao, wakaongeza kasi ili kuwahi na kuanza kazi.

Wabeba mizigo waliokuwa wakifanya kazi katika masoko makubwa kama Kariakoo, Tandale na Buguruni tayari walianza kazi zao mapema kabisa, siku hiyo ilionekana kama siku nyingine na hivyo walitakiwa kufanya kazi kwa bidii.

Katika muda huohuo, kijana aliyekuwa akiishi maisha ya chini katika Mtaa wa Kwa Ally Maua, Emmanuel Bazoka ndiyo kwanza alikuwa akiamka katika usingizi mzito. Alionekana kuchoka mno, pale kitandani alipokuwa, hakutaka kuteremka, aliyafumbua macho yake na kuangalia huku na kule kama mtu aliyekuwa akimtafuta mtu fulani ndani ya chumba hicho.

Joto likaanza kumsumbua, jua lililokuwa limechomoza liliambatana na joto kali. Akashuka kutoka kitandani na kukaa sakafuni, kichwa chake kikaanza kufikiria mambo mengi, maisha aliyokuwa akipitia ambayo yalimfanya kuwa hapo siku hiyo.
Alikuwa kijana msomi kidogo aliyeishia kidato cha nne, alikuwa na cheti chake ambacho kwa kipindi hicho hakuona kama kilikuwa na kazi yoyote ile. Maisha aliyokuwa akiishi, yalikuwa ya kimasikini mno.
Hakuwa mtu wa kula milo mitatu kwa siku, kila siku alikuwa akila asubuhi na usiku kisha kulala. Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, yalimuumiza lakini hakuwa na jinsi, ili aendelee kuishi ilikuwa ni lazima afanye kazi ndogondogo alizokuwa akizifanya.
Maisha yake yalichakaa, kila siku alimuomba Mungu kuondoka katika maisha aliyokuwa akiishi lakini ilishindikana kabisa. Aliendelea kuishi hivyohivyo na kila siku asubuhi aliondoka nyumbani kwake kuelekea katika Soko Kuu la Tandale na kubeba mizigo.
Siku hiyo hakujisikia kwenda kufanya kazi, alitamani kuendelea kulala lakini alipokumbuka kwamba kama asingetoka basi asingeweza kula, hakuwa na jinsi, akainuka na kuelekea nje, akachukua maji, akaenda kuoga na kujiandaa kwenda kazini kwake.
Maisha yake yalikuwa ya mateso sana, hakuwa na mke, hakuwa na mchumba wala mtu yeyote yule. Wazazi wake walikuwa masikini kama yeye, hawakuwepo tena duniani, walifariki miaka miwili iliyopita, katika mwaka ambao alikuwa akimaliza kidato cha nne.
Alifeli. Kufeli kwake hakukumaanisha kwamba hakuwa na akili, hapana, alikuwa na uwezo mkubwa ila msongo wa mawazo juu ya vifo vya wazazi wake vilimfanya kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yake.
Aliuchukia umasikini, katika maisha yake alipanga kuwa tajiri mkubwa hapo baadaye. Hakujua angeanza vipi, hakujua ni sehemu gani ambayo angeanzia kuupata utajiri ambao kila siku alikuwa akiufikiria kichwani mwake.
Hakutaka kuiba, aliamini kwamba kama angeendelea kupambana basi kuna siku angekuwa tajiri mkubwa na kufanikiwa kuiteka Tanzania kwa kuwa na mali nyingi.
“Kuna siku nitakuwa tajiri! Labda tajiri mkubwa kama Bakhresa,” alijisemea huku akivaa nguo zake na kuondoka.
Ni kama aliishi ndani ya ndoto kubwa iliyomfanya kuona kuna siku angekuwa tajiri mkubwa, hakujua kama ndoto hiyo aliyokuwa akiiota kila siku ingekuja kuwa kweli au alikuwa akipoteza muda wake.
Siku hiyo, akaelekea kazini kama kawaida, aliungana na wenzake na kuanza kubeba mizigo kama siku nyingine. Sokoni huko, alikuwa na rafiki yake aliyekuwa akipenda sana kufanya naye kazi, huyo aliitwa Hamisi Kibwila.
Huyo ndiye aliyekuwa akishirikiana naye kwenye kila kitu, ndiye ambaye alimwambia mambo mengi kuhusu maisha yake, ndiye ambaye alizijua siri za Bazoka kwamba leo alikula au alilala bila kula.
“Kuna siku naamini nitakuwa tajiri mkubwa,” alisema Bazoka huku akimwangalia rafiki yake huyo ambaye kabla ya kusema kitu chochote, akamwangalia, tabasamu la mbali likautawala uso wake.
Si kwamba alipingana na alichokuwa akikizungumza rafiki yake, alikubaliana nacho ila kilichokuwa kikimuumiza ni aina ya maisha waliyokuwa wakiishi.
Waliishi kwa shida, ili wale, walitakiwa kufanya kazi kwa nguvu sana, hawakuona dalili zozote za kuweza kufanikiwa kutoka katika maisha waliyokuwanayo, kwao, walijiona kuwa masikini milele, walijiona kufanya kazi ya kubeba mizigo milele, ilikuwaje Bazoka aseme kwamba kuna siku angekuwa tajiri? Jambo hilo halikuweza kukubalika kichwani mwa Hamisi hata kidogo.
“Wewe uwe tajiri?” aliuliza Hamisi huku akimwangalia rafiki yake huyo.
“Ndiyo! Unadhani inashindikana?” aliuliza Bazoka huku akimwangalia Hamisi.
“Si kwamba inashikana!”
“Kumbe?”
“Kwa Maisha haya ya kubeba mizigo unataka kuniaminisha kwamba kuna siku utakuwa bilionea! Utaanzia wapi Bazoka? Kuna wengine kama sisi, Mungu aliandika kwamba tutakuwa wabeba mizigo mpaka vifo vyetu, na hivi ndivyo inavyotokea,” alisema Hamisi, tabasamu lile likapotea, akaamua kulikalia gunia lililokuwa na mchele.
Bazoka alimwangalia kwa macho yaliyoonekana kutokukubaliana na kile alichokisema, kwake, alitamani kuwa bilionea mkubwa, alijua kabisa kwamba kuna siku maisha yangebadilika na kuendesha magari, kumiliki majumba ya kifahari na hata kusafiri huku na kule kama bilionea.
Walizungumza mambo mengi mpaka baadaye alipoamua kuendelea kufanya kazi zake. Kila siku ilikuwa ni mawazo tu, aliupenda utajiri, alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile lakini mwisho wa siku awe tajiri mkubwa.
Katika nyumba aliyokuwa akiishi, aliishi na wapangaji wengine na mwenye nyumba aliyeitwa mzee Ramadhani Kibidu ambaye alikuwa na watoto wawili wa kike, Asha na Amina.
Asha ndiye alikuwa binti mkubwa wa mzee huyo. Alikuwa msichana mweupe, mrefu, mwembamba ambaye uso wake ulipendezeshwa na vishimo viwili maishavuni mwake.
Japokuwa alikuwa na uzuri wa ajabu na kupendwa na wanaume wengi, kwa Asha hakuwa akijali kuhusu mahusiano ya kimapenzi. Moyo wake ulikuwa umejeruhiwa baada ya kuacha na mwanaume aliyekuwa akimpenda sana.
Baada ya kuachana naye kwa takribani miaka miwili iliyopita, hakutaka kuwa na mwanaume mwingine yeyote yule. Aliamua kubaki peke yake mpaka kipindi ambacho Bazoka alihamia ndani ya nyumba hiyo.
Alikuwa kijana masikini ambaye katika kipindi cha kodi ilikuwa ni lazima kugombana na baba yake lakini huyohuyo masikini Asha alikuwa akimpenda kweli. Kila alipomwangalia Bazoka, moyo wake ulifarijika na kuona kabisa kwamba huyo ndiye mwanaume ambaye alitakiwa kuwa naye katika kipndi chote cha maisha yake.
Wakati akimpenda Bazoka, mwenzake hakuwa na habari naye, alikuwa bize na mambo yake, alikuwa akiyaangalia maisha yake yaliyokuwa yakimuendesha mno. Hakuwa na pesa, wakati mwingine Asha ndiye aliyekuwa akimpelekea chakula na kula.
Kwa Bazoka, alikuwa akijishtukia lakini hakuwa na jinsi, alichukulia kama urafiki tu kwa kuwa alikuwa mpangaji kumbe mwenzake kichwani alikuwa akifikiria mambo mengne kabisa.
Asha aliogopa kumwambia Bazoka ukweli, aliona kabisa kwamba asingekuja kukubaliwa kwa kuwa tu kijana huyo alikuwa masikini na hakuona kama angeweza kuishi na msichana huyo.
Ila hakuacha, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu katika maisha yake. Wakati mwingine alikuwa akitoka chumbani kwake usiku na kwenda katika chumba cha Bazoka na kuangalia televisheni ndogo iliyokuwa humo ndani. Bazoka hakuwa na mawazo na Asha, alimchukulia kama dada yake kitu ambacho hakikukubalika kichwani mwa msichana huyo.
Kila alipokuwa akikaa chumbani kwa Bazoka, hakuonyesha kitu chochote kile, alionekana kama gogo ambalo halikuwa na hisia zozote zile. Hilo lilimuumiza sana Asha kiasi kwamba akafikia hatua ya kumwambia ukweli.
“Bazoka..” alimuita kijana huyo.
“Naam.”
“Mbona unanitesa hivyo?” aliuliza msichana huyo kwa sauti ya chini huku uso wake ukianza kuingiwa na aibu.
“Nakutesa? Unamaanisha nini?” aliuliza Bazoka.
“Huoni kama unanitesa? Ninakupenda sana, nimejaribu kukuonyeshea kila kitu lakini naona mwenzangu huelekei kabisa,” alisema Asha kwa sauti ile ile ya chini.
Bazoka hakuzungumza kitu, alibaki akimwangalia Asha. Msichana huyo aliona haitoshi, akasimama na kumsogelea Bazoka pale alipokaa na kukaa karibu naye.
Huo ulikuwa wakati wake wa kulalamika, alimwambia jinsi alivyokuwa akijisikia kwamba kwake hakuwa akipindua, wakati akilalamika hayo yote Bazoka alikuwa kimya tu akimsikiliza.
Kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, alishangaa, hakujua sababu iliyomfanya msichana huyo kumpenda namna hiyo na wakati hakuwa na kitu chochote kile, hakuwa na maisha mazuri, aliishi kwa kuungaunga kama masikini wengine, kama angeamua kuwa na Asha, angempa nini?
“Asha! Hivi upo siriazi kweli au unanitania?” alimuuliza msichana huyo.
“Bazoka! Ninakupenda kwa moyo wa dhati.”
“Na maisha haya?”
“Ndiyo! Ninakupenda, naomba unikubalie, naomba uupoze moyo wangu, unateseka na hakuna mtu ambaye atanipa tulizo la moyo zaidi yako,” alisema Asha huku akimwangalia Bazoka kwa macho yaliyoonyesha kumaanisha kile alichokizungumza.

Je, nini kitaendelea?
IMG_20201111_020334_172.jpg
 
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA.
MSIMULIAJI: Hussein
IMEANDIKWA: MWANDISHI MAALUMU.
0756362035

Sehemu ya 02.

“Bazoka! Ninakupenda kwa moyo wa dhati.”
“Na maisha haya?”
“Ndiyo! Ninakupenda, naomba unikubalie, naomba uupoze moyo wangu, unateseka na hakuna mtu ambaye atanipa tulizo la moyo zaidi yako,” alisema Asha huku akimwangalia Bazoka kwa macho yaliyoonyesha kumaanisha kile alichokizungumza.
Bazoka akashusha pumzi ndefu, akatulia na kuyapelekea macho yake chini, alifikiria mambo mengi, bado moyo wake haukukubaliana na kile alichokizungumza msichana huyo. Baada ya muda, akauinua uso wake.
“Mimi ni masikini!” alisema Bazoka.
“Najua! Nimekupenda hivyojivyo, naomba uwe wangu,” alisema Asha kwa sauti ya kulalamika.
Ni kama alilazimishwa sana, hatimaye Bazoka akakubaliana na msichana huyo na hatimaye mapenzi yakaanza. Hakujisikia raha kama aliyotakiwa kujisikia, muda mwingi kichwa chake kilifikiria zaidi maisha kuliko mapenzi.
Asha alikuwa msumbufu, alitamani kuona akiwa karibu na kijana huyo, kwenye simu, alisumbua sana, muda mwingi alimpigia kumsalimia au hata kumtumia ujumbe mfupi.
Mapenzi yao yalikuwa siri kubwa, hakukuwa na mtu aliyefahamu kitu kilichokuwa kikiendelea. Kila siku usiku Asha alitoka chumbani kwake na kwenda chumbani kwa Bazoka kisiri na kulala huko huku akitoka alfajiri kabisa.
Wazazi wake hawakujua kilichokuwa kikiendelea, kwao, Bazoka alionekana kuwa kijana mpole, asiyekuwa na majivuno ambaye hawezi kutembea na binti yao kwani tangu alipofika hapo, hakuwahi hata kuingiza msichana chumbani kwake.
Bado aliendelea na kazi ya kubeba mizigo kama kawaida. Hakuacha kumwambia rafiki yake, Hamisi kwamba kuna siku angekuwa bilionea mkubwa mno nchini Tanzania.
Aliendelea kupambana huku ndoto zake za kuwa tajiri zikiendelea kuchipua moyoni mwake. Baada ya kukaa hapo kwa miezi kadhaa, akatokea kufahamiana na mwanaume mmoja aliyekuwa akija sana kununua nafaka mahali hapo.
Mwanaume huyo alikuwa akifika na gari lake, anapaki pembeni na watu ambao aliwazoea kumbebea nafaka walikuwa Bazoka na Hamisi.
Kila siku Bazoka alipoyaangalia maisha ya mwanaume huyo aliyeitwa Sultani, aliyapenda. Alikuwa akimiliki simu ya gharama, mavazi aliyokuwa akivaa yalionyesha kabisa kwamba alikuwa na pesa.
Gari aliyokuwa akija nayo mahali hapo ilikuwa ni ya kifahari sana. Hakuwa na maringo, kwake, kila mtu alionekana kuwa sawa na hata alipokuwa akizungumza nao, alizungumza kwa upole na unyenyekevu mkubwa.
Watu wengi walimshangaa Sultani, alionekana tajiri wa aina yake kwani matajiri wengi walikuwa na kujiona, waliringa lakini ilikuwa tofauti na tajiri huyo, maisha aliyokuwa akiishi, wabeba mizigo wengi walikuwa wakimpenda.
“Mmekula?” aliuliza Sultani baada ya kufika mahali hapo kununua mahindi kama kawaida yake.
“Hatujala bosi,” alijibu Bazoka harakahara. Alichokifanya Sultani ni kutoa pochi yake, akatoa noti nne za elfu kumi na kuwapa Bazoka na Hamisi.
Kwao ilionekana kama ndoto, hawakuamini kama Sultani angeweza kuwapa kiasi kikubwa cha pesa kama hicho. Hawakuwahi kukishika tangu walipoanza kufanya kazi ya kubeba mizigo katika soko hilo.
Jamaa huyo hakuishia hapo tu, akawapa kazi ya kumbebea magunia ya nafaka, na walipomaliza tu, akawalipa kama kawaida.
Walimshukuru sana, kwao, mwanaume huyo alionekana kuwa muhimu sana. Wakakaa na kuzungumza naye na baada ya nusu saa, akaondoka zake.
Huo haukuwa mwisho wa kukutana naye, mara kwa mara alikuwa akifika mahali hapo. Walizoeana sana na walikuwa wakizungumza mambo mengi kuhusu maisha.
Bazoka kila alipomwangalia Sultani, moyo wake ulikuwa na maswali mengi, ni kwa jinsi gani mwanaume huyo alifanikiwa na kuwa na maisha hayo? Aliendesha magari ya kifahari na kuvaa vizuri, ni kweli alizaliwa katika maisha ya kimasikini kama yake au alizaliwa katika familia ya mtu mwenye pesa?
Hayo yalikuwa maswali yaliyokisumbua sana kichwa chake, kila siku alikuwa akimfikiria Sultani na kujiuliza mambo mengi mno, nyumbani, hakuwa akilala vizuri, alihitaji kuwa na pesa, inawezekana ziwe kama Sultani au zaidi ya mwanaume huyo.
Alivumilia na kuvumilia lakini uvumilivu wake ukafika mwisho na hivyo kuamua kumuuliza ili kama ikiwezekana na yeye awe tajiri kama alivyokuwa.
“Kwani mimi tajiri?” aliuliza Sultani huku akitabasamu.
“Daah! Bro unajua una hela sana, unataka kukataa kama wewe siyo tajiri! Hebu angalia magari yako, nguo zako, simu, kweli unakataa pia?” aliuliza Bazoka, maswali yake yalikuwa siriazi sana lakini kwa Sultani na Hamisi, wakaanza kucheka.
“Mimi siyo tajiri!”
“Basi sawa wewe siyo tajiri, sasa kama mimi nikitaka kuwa na pesa kama zako, nafanyaje?” aliuliza Bazoka.
“Unapambana tu. Hakikisha unakuwa na kiu ya kuwa na hela ya kila mtu atakayepita mbele yako,” alisema Sultani, akatoa tabasamu tena.
“Kwa hiyo na wewe ulikuwa masikini?” aliuliza Bazoka.
“Tena zaidi yako! Kuna wakati nilikuwa sili kabisa chakula kwa kuwa siku na pesa, na kazi hazikuwepo, ila mwisho wa siku nikafanikiwa,” alisema Sultani.
“Kweli?”
“Siwezi kukudanganya. Cha msingi pambana, kuna siku utafanikiwa tu,” alisema mwanaume huyo.
“Kingine?”
“Weka akiba, jifunze kuweka akiba, jinyime, kuwa na akiba ni kitu muhimu sana,” aliongezea.
Kidogo maneno hayo yakamtia nguvu na kuona kwamba kila kitu kilikuwa kinawezekana, alichokifanya ni kuendelea kupambana tu.
Kila siku alifanya kazi kwa bidii, aliamka asubuhi na mapema kabla ya siku nyingine na kuanza kujishughulisha kupita kawaida.
Kwa kuwa aliambiwa kwamba ilikuwa ni kitu muhimu kuweka akiba, akaanza kufanya hivyo. Alijitesa, alijinyima lakini ndoto yake ya kuwa bilionea bado iliendelea kuishi kichwani mwake.
Siku ziliendelea kwenda mbele, hakuacha kumwambia Hamisi kwamba alihitaji sana kuwa bilionea na aliamini kwamba kuna siku angekuwa kama alivyotaka kuwa.
Kwa kuwa Asha alikuwa mpenzi wake alichokifanya ni kumshirikisha kile kilichokuwa kikiendelea na msichana huyo kumuunga mkono kwa kila kitu alichokifanya.
Siku zikakatika na baada ya miezi sita ya kupambana, Asha akampa taarifa ambayo kwake hakuona kama ilikuwa nzuri, msichana huyo alimwambia kwamba alikuwa na mimba ya wiki mbili.
“Unasemaje?” alimuuliza Bazoka huku akionekana kushtuka.
“Nina mimba mpenzi!”
Bazoka akakaa kimya kwa muda, kichwa chake kikawa na mawazo mengi, maisha yake yalikuwa magumu na aliona kabisa kulikuwa na tatizo kubwa mbele yake.
Alimwangalia Asha, hakutaka msichana huyo agundue kwamba hakuipenda taarifa ile, akamuonyeshea tabasamu na kumkumbatia huku akimwambia kwamba alifurahi kusikia hivyo.
Hilo ndilo lililomfanya Bazoka kupambana zaidi, hakutaka kubaki kama alivyokuwa, alijua kuwa mtoto alikuwa njiani na hivyo ilimbidi kupambana mpaka kuhakikisha kwamba anapata pesa kwa ajili ya kumlisha Asha ambaye kwa kipindi cha ujauzito kama huo alitakiwa kula vizuri kuliko kipindi kingine.
“Sultani anaweza kunisaidia zaidi, ngoja nimtafute,” alijisemea.
Hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kuanza kumtafuta Sultani. Hakujua mahali alipokuwa akiishi, hakujua kitu chochote kile kuhusu mwanaume huyo zaidi ya kuonana naye sokoni alipokuwa akienda kununua nafaka.
Alimsubiri kwa siku kadhaa, hakuja mara kwa mara kama ilivyokuwa zamani, hiyo ikamfanya kuhisi kwamba kulikuwa na jambo baya lililokuwa limempata mwanaume huyo na ndiyo maana mpaka kipindi hicho hakuwa amefika sokoni hapo kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
“Sultani vipi?” aliuliza Bazoka huku akimwangalia Hamisi.
“Sijajua kapatwa na ninI! Hajaja kitambo sana,” alijibu Hamisi.
“Ninataka sana nionane naye, najua anaweza kunisaidia,” alisema Bazoka.
“Kukusaidia nini?”
“Kuwa bilionea. Natumaini kwamba kuna kazi nyingine anaifanya ambayo inamuingizia sana pesa. Ngoja nionane naye,” alisema Bazoka huku hata uso wake tu ukionyesha kwamba kweli alikuwa na hamu ya kuwa bilionea mkubwa Tanzania.

Je, nini kitaendelea?
 
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA.
MSIMULIAJI: Hussein
IMEANDIKWA: MWANDISHI MAALUMU.
0756362035

Sehemu ya 02.

“Bazoka! Ninakupenda kwa moyo wa dhati.”
“Na maisha haya?”
“Ndiyo! Ninakupenda, naomba unikubalie, naomba uupoze moyo wangu, unateseka na hakuna mtu ambaye atanipa tulizo la moyo zaidi yako,” alisema Asha huku akimwangalia Bazoka kwa macho yaliyoonyesha kumaanisha kile alichokizungumza.
Bazoka akashusha pumzi ndefu, akatulia na kuyapelekea macho yake chini, alifikiria mambo mengi, bado moyo wake haukukubaliana na kile alichokizungumza msichana huyo. Baada ya muda, akauinua uso wake.
“Mimi ni masikini!” alisema Bazoka.
“Najua! Nimekupenda hivyojivyo, naomba uwe wangu,” alisema Asha kwa sauti ya kulalamika.
Ni kama alilazimishwa sana, hatimaye Bazoka akakubaliana na msichana huyo na hatimaye mapenzi yakaanza. Hakujisikia raha kama aliyotakiwa kujisikia, muda mwingi kichwa chake kilifikiria zaidi maisha kuliko mapenzi.
Asha alikuwa msumbufu, alitamani kuona akiwa karibu na kijana huyo, kwenye simu, alisumbua sana, muda mwingi alimpigia kumsalimia au hata kumtumia ujumbe mfupi.
Mapenzi yao yalikuwa siri kubwa, hakukuwa na mtu aliyefahamu kitu kilichokuwa kikiendelea. Kila siku usiku Asha alitoka chumbani kwake na kwenda chumbani kwa Bazoka kisiri na kulala huko huku akitoka alfajiri kabisa.
Wazazi wake hawakujua kilichokuwa kikiendelea, kwao, Bazoka alionekana kuwa kijana mpole, asiyekuwa na majivuno ambaye hawezi kutembea na binti yao kwani tangu alipofika hapo, hakuwahi hata kuingiza msichana chumbani kwake.
Bado aliendelea na kazi ya kubeba mizigo kama kawaida. Hakuacha kumwambia rafiki yake, Hamisi kwamba kuna siku angekuwa bilionea mkubwa mno nchini Tanzania.
Aliendelea kupambana huku ndoto zake za kuwa tajiri zikiendelea kuchipua moyoni mwake. Baada ya kukaa hapo kwa miezi kadhaa, akatokea kufahamiana na mwanaume mmoja aliyekuwa akija sana kununua nafaka mahali hapo.
Mwanaume huyo alikuwa akifika na gari lake, anapaki pembeni na watu ambao aliwazoea kumbebea nafaka walikuwa Bazoka na Hamisi.
Kila siku Bazoka alipoyaangalia maisha ya mwanaume huyo aliyeitwa Sultani, aliyapenda. Alikuwa akimiliki simu ya gharama, mavazi aliyokuwa akivaa yalionyesha kabisa kwamba alikuwa na pesa.
Gari aliyokuwa akija nayo mahali hapo ilikuwa ni ya kifahari sana. Hakuwa na maringo, kwake, kila mtu alionekana kuwa sawa na hata alipokuwa akizungumza nao, alizungumza kwa upole na unyenyekevu mkubwa.
Watu wengi walimshangaa Sultani, alionekana tajiri wa aina yake kwani matajiri wengi walikuwa na kujiona, waliringa lakini ilikuwa tofauti na tajiri huyo, maisha aliyokuwa akiishi, wabeba mizigo wengi walikuwa wakimpenda.
“Mmekula?” aliuliza Sultani baada ya kufika mahali hapo kununua mahindi kama kawaida yake.
“Hatujala bosi,” alijibu Bazoka harakahara. Alichokifanya Sultani ni kutoa pochi yake, akatoa noti nne za elfu kumi na kuwapa Bazoka na Hamisi.
Kwao ilionekana kama ndoto, hawakuamini kama Sultani angeweza kuwapa kiasi kikubwa cha pesa kama hicho. Hawakuwahi kukishika tangu walipoanza kufanya kazi ya kubeba mizigo katika soko hilo.
Jamaa huyo hakuishia hapo tu, akawapa kazi ya kumbebea magunia ya nafaka, na walipomaliza tu, akawalipa kama kawaida.
Walimshukuru sana, kwao, mwanaume huyo alionekana kuwa muhimu sana. Wakakaa na kuzungumza naye na baada ya nusu saa, akaondoka zake.
Huo haukuwa mwisho wa kukutana naye, mara kwa mara alikuwa akifika mahali hapo. Walizoeana sana na walikuwa wakizungumza mambo mengi kuhusu maisha.
Bazoka kila alipomwangalia Sultani, moyo wake ulikuwa na maswali mengi, ni kwa jinsi gani mwanaume huyo alifanikiwa na kuwa na maisha hayo? Aliendesha magari ya kifahari na kuvaa vizuri, ni kweli alizaliwa katika maisha ya kimasikini kama yake au alizaliwa katika familia ya mtu mwenye pesa?
Hayo yalikuwa maswali yaliyokisumbua sana kichwa chake, kila siku alikuwa akimfikiria Sultani na kujiuliza mambo mengi mno, nyumbani, hakuwa akilala vizuri, alihitaji kuwa na pesa, inawezekana ziwe kama Sultani au zaidi ya mwanaume huyo.
Alivumilia na kuvumilia lakini uvumilivu wake ukafika mwisho na hivyo kuamua kumuuliza ili kama ikiwezekana na yeye awe tajiri kama alivyokuwa.
“Kwani mimi tajiri?” aliuliza Sultani huku akitabasamu.
“Daah! Bro unajua una hela sana, unataka kukataa kama wewe siyo tajiri! Hebu angalia magari yako, nguo zako, simu, kweli unakataa pia?” aliuliza Bazoka, maswali yake yalikuwa siriazi sana lakini kwa Sultani na Hamisi, wakaanza kucheka.
“Mimi siyo tajiri!”
“Basi sawa wewe siyo tajiri, sasa kama mimi nikitaka kuwa na pesa kama zako, nafanyaje?” aliuliza Bazoka.
“Unapambana tu. Hakikisha unakuwa na kiu ya kuwa na hela ya kila mtu atakayepita mbele yako,” alisema Sultani, akatoa tabasamu tena.
“Kwa hiyo na wewe ulikuwa masikini?” aliuliza Bazoka.
“Tena zaidi yako! Kuna wakati nilikuwa sili kabisa chakula kwa kuwa siku na pesa, na kazi hazikuwepo, ila mwisho wa siku nikafanikiwa,” alisema Sultani.
“Kweli?”
“Siwezi kukudanganya. Cha msingi pambana, kuna siku utafanikiwa tu,” alisema mwanaume huyo.
“Kingine?”
“Weka akiba, jifunze kuweka akiba, jinyime, kuwa na akiba ni kitu muhimu sana,” aliongezea.
Kidogo maneno hayo yakamtia nguvu na kuona kwamba kila kitu kilikuwa kinawezekana, alichokifanya ni kuendelea kupambana tu.
Kila siku alifanya kazi kwa bidii, aliamka asubuhi na mapema kabla ya siku nyingine na kuanza kujishughulisha kupita kawaida.
Kwa kuwa aliambiwa kwamba ilikuwa ni kitu muhimu kuweka akiba, akaanza kufanya hivyo. Alijitesa, alijinyima lakini ndoto yake ya kuwa bilionea bado iliendelea kuishi kichwani mwake.
Siku ziliendelea kwenda mbele, hakuacha kumwambia Hamisi kwamba alihitaji sana kuwa bilionea na aliamini kwamba kuna siku angekuwa kama alivyotaka kuwa.
Kwa kuwa Asha alikuwa mpenzi wake alichokifanya ni kumshirikisha kile kilichokuwa kikiendelea na msichana huyo kumuunga mkono kwa kila kitu alichokifanya.
Siku zikakatika na baada ya miezi sita ya kupambana, Asha akampa taarifa ambayo kwake hakuona kama ilikuwa nzuri, msichana huyo alimwambia kwamba alikuwa na mimba ya wiki mbili.
“Unasemaje?” alimuuliza Bazoka huku akionekana kushtuka.
“Nina mimba mpenzi!”
Bazoka akakaa kimya kwa muda, kichwa chake kikawa na mawazo mengi, maisha yake yalikuwa magumu na aliona kabisa kulikuwa na tatizo kubwa mbele yake.
Alimwangalia Asha, hakutaka msichana huyo agundue kwamba hakuipenda taarifa ile, akamuonyeshea tabasamu na kumkumbatia huku akimwambia kwamba alifurahi kusikia hivyo.
Hilo ndilo lililomfanya Bazoka kupambana zaidi, hakutaka kubaki kama alivyokuwa, alijua kuwa mtoto alikuwa njiani na hivyo ilimbidi kupambana mpaka kuhakikisha kwamba anapata pesa kwa ajili ya kumlisha Asha ambaye kwa kipindi cha ujauzito kama huo alitakiwa kula vizuri kuliko kipindi kingine.
“Sultani anaweza kunisaidia zaidi, ngoja nimtafute,” alijisemea.
Hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kuanza kumtafuta Sultani. Hakujua mahali alipokuwa akiishi, hakujua kitu chochote kile kuhusu mwanaume huyo zaidi ya kuonana naye sokoni alipokuwa akienda kununua nafaka.
Alimsubiri kwa siku kadhaa, hakuja mara kwa mara kama ilivyokuwa zamani, hiyo ikamfanya kuhisi kwamba kulikuwa na jambo baya lililokuwa limempata mwanaume huyo na ndiyo maana mpaka kipindi hicho hakuwa amefika sokoni hapo kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
“Sultani vipi?” aliuliza Bazoka huku akimwangalia Hamisi.
“Sijajua kapatwa na ninI! Hajaja kitambo sana,” alijibu Hamisi.
“Ninataka sana nionane naye, najua anaweza kunisaidia,” alisema Bazoka.
“Kukusaidia nini?”
“Kuwa bilionea. Natumaini kwamba kuna kazi nyingine anaifanya ambayo inamuingizia sana pesa. Ngoja nionane naye,” alisema Bazoka huku hata uso wake tu ukionyesha kwamba kweli alikuwa na hamu ya kuwa bilionea mkubwa Tanzania.

Je, nini kitaendelea?
tunasubiri mwendelezo
 
NYEMO CHILONGANI
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA
0756362035

Sehemu ya 03.

“Kukusaidia nini?”
“Kuwa bilionea. Natumaini kwamba kuna kazi nyingine anaifanya ambayo inamuingizia sana pesa. Ngoja nionane naye,” alisema Bazoka huku hata uso wake tu ukionyesha kwamba kweli alikuwa na hamu ya kuwa bilionea mkubwa Tanzania.
Baada ya wiki moja ndipo Sultani akarudi tena sokoni hapo kununua nafaka kama zamani. Bazoka alipomuona tu,akahisi moyo wake ukiwa na shauku kubwa ya kumwambia kile alichopanga kumwambia kwa kipindi kirefu.
Akamfuata, akamuonyeshea tabasamu, akamsalimia na kuzungumza mambo mengine kuhusu kazi ya kubebewa nafaka zake mpaka katika gari lake. Muda wote huo Bazoka alikuwa na presha kubwa, alitamani kumwambia Sultani kile kilichokuwa kikiutesa moyo wake kwa kipindi kirefu.
Baada ya kumaliza, akamuomba muda wa kuzungumza naye, hilo halikuwa tatizo, Sultani akamwambia wakae pembeni na kuzungumza kuhusu hilo alilotaka kumwambia, wakaenda pembeni.
“Nina shida kubwa,” alianza Bazoka.
“Shida gani?” aliuliza Sultani.
Bazoka hakutaka kuchelewa, alichokifanya ni kuanza kumsimulia Sultani kila kitu kilichokuwa kimetokea katika kipindi ambacho hakuwa ameonana na mwanaume huyo. Alimwambia ukweli kuhusu hali ya mpenzi wake, Asha, alimwambia ukweli kuhusu mzigo mzito aliokuwanao kwa msichana huyo.
“Nitakusaidia kiasi cha pesa kwa ajili yake,” alisema Sultani huku akionyesha huruma usoni mwake.
“Sultani! Sihitaji msaada wako wa pesa.”
“Sasa unahitaji nini?”
“Njia za kupata pesa. Ninataka kupata pesa kama wewe,” alisema Bazoka.
“Si nilikwambia ni kwa jinsi gani unaweza kupata pesa?”
”Ndiyo! Ila njia zile naona hazitoshi. Naomba unisaidie, ninahitaji kupata pesa kwa nguvu zote,” alisema Bazoka huku akimwangalia mwanaume huyo kwa macho yaliyoonyesha kwamba kweli alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile lakini mwisho wa siku apate utajiri ambao kila siku alikuwa akiuhitaji maishani mwake.
Sultani hakutaka kumwambia kitu chochote kuhusu utajiri aliokuwanao bali alichokifanya ni kurudia maneno yaleyale kwamba alitakiwa kupambana sana. Hilo lilimuumiza mno Bazoka, moyo wake ukanyong’onyea na kuona kabisa kwamba alikuwa akienda kufeli maishani mwake.
“Sultani! Nimepambana sana, yaani nimepambana vya kutosha,” alisema Bazoka huku akimwangalia mwanaume huyo.
“Na bado hujafanikiwa?”
“Ndiyo!”
“Basi bado hujapambana vya kutosha. Nenda kapambane, mafanikio yatakuja tu, nakuhakikishia hilo,” alisema mwanaume huyo ambaye hakutaka kubaki mahali hapo, akasimama, akaingia ndani ya gari lake na kuondoka huku akimpa kiasi cha shilingi elfu hamsini kwa ajili ya kumsaidia katika matatizo aliyokuwanayo.
“Natakiwa kupambana zaidi ya hapa! Napambanaje sasa?” alijiuliza.
Kila alipomuona Asha, moyo wake uliishiwa nguvu, alihuzunika, hakutaka kumuona msichana huyo akipata tatizo lolote lile, alitamani kumuona akiishi vizuri na hata kujifungua salama hapo baadaye.
Mara baada ya mzee Kibidu kugundua kwamba binti yake alikuwa na ujauzito wa Bazoka, moyo wake ulimuuma mno, alikasirika sana kwani aliona kabisa kwamba binti yake alikuwa akienda kupata shida maisha yake yote.
Ila pamoja na hasira zake, hakutaka kumuonyeshea Bazoka hasira zozote zile, alihisi kwamba kama angefanya hivyo lisingekuwa jambo la busara, alichokifanya ni kuzungumza naye sana kuhusu maisha yake.
“Unatakiwa kupambana sana, unakwenda kuwa na familia yako, pambana sana Bazoka,” alisema mzee huyo maneno ambayo kila siku yalijirudia kichwani mwake.
Baada ya miezi miwili, Sultani akarudi sokoni pale na kitu pekee alichokuwa amekifuata kilikuwa ni kuongea na Bazoka. Aliacha ujumbe kwamba alikuwa akimtafuta hivyo akaacha namba yake ya simu na kuwaambia vijana waliokuwa mahali hapo wampe taarifa kijana huyo amtafute.
Hilo halikuwa tatizo, baada ya Bazoka kwenda sokoni, akapewa taarifa, haraka sana akatafuta simu na kumpigia Sultani ambaye alimwambia kwamba alitaka kuonana naye.
“Wapi bosi?” aliuliza Bazoka.
“Njoo hapa Golden Tulip, unapajua?”
”Ndiyo bosi.”
“Basi nakusubiri!”
Hakutaka kusubiri mahali hapo, alichokifanya, haraka sana akaondoka sokoni na kuelekea Golden Tulip. Njiani mawazo yake yalikuwa kwa Sultani tu, hakuamini, siku hiyo alijiona kuwa bilionea mkubwa, humo ndani ya daladala akaanza kupanga mipango yake kwamba ni kwa namna gani angezitumia pesa ambazo angezipata katika maisha yake.
Alijiona kama tayari alikuwa bilionea, akisafiri kwa ndege kuelekea nje ya nchi na kufanya mambo mengi mno. Hakuchukua muda mwingi, akafika na kuelekea Golden Tulip.
Alipofika, macho yake yakatua kwa Sultan, alikuwa mahali hapo huku akiwa na mwanaume mmoja pembeni yake. Mwanaume huyo alikuwa mnene, ndevu nyingi na kichwani alinyoa kwa staili ya kiduku.
Shingoni alikuwa na cheki kubwa za dhahabu, katika vidole vyake alikuwa na pete kubwa, kwa kumwangalia harakaharaka haikuwa vigumu kugundua kama mwanaume huyo naye alikuwa na pesa kama Sultani. Akawasogelea mahali pale na kuwasalimia, akakaribishwa kiti na kutulia.
“Huyu ni rafiki yangu anaitwa Christopher ila anapenda zaidi kuitwa Bonge,” alimtambulisha rafiki yake kwa Bazoka, wawili hao wakapeana mikono.
“Na huyu anaitwa Bazoka!” alisema Sultani.
Kitu cha kwanza kabisa ni Bazoka kutakiwa kuwaambia kila kitu alichokuwa akikihitaji, wanaume hao walikaa kimya wakimsikiliza. Alielezea kwa hisia kali, alionekana dhahiri kuhitaji utajiri kwa nguvu zote.
Muda wote wanaume hao walikuwa wakimsikiliza huku wakiwa na tabasamu pana katika nyuso zao. Hilo lilimshangaza Bazoka, hakutegemea kuona akisimulia kuhusu shida alizokuwa akizipata maishani mwake halafu watu hao wakabaki wakitabasamu badala ya kumuonea huruma.
Hakuwa na jinsi, hakutakiwa kukasirika, kwa kuwa alihitaji msaada ilimbidi aelezee mpaka pale alipomaliza ambapo Bonge akachukua glasi ya pombe iliyokuwa mezani na kupiga funda moja.
“Kwa hiyo unahitaji utajiri?” aliuliza Bonge huku akimwangalia Bazoka.
“Ndiyo! Ninahitaji kwa nguvu zote!” alijibu Bazoka.
“Kwa hiyo unahitaji utajiri?” alilirudia swali hilo.
“Kwa nguvu zote bosi, ninahitaji kuwa tajiri!”
“Kwa hiyo unahitaji utajiri?”
“Ndiyo bosi! Ninauhitaji kwa nguvu zote.”
“Kweli?” aliuliza Bonge.
“Kweli! Ninahitaji bosi!”
“Basi sawa! Kama kweli unahitaji utajiri, chukua hii pete, ivae, usiku wa saa saba kuna gari litakufuata nyumbani, usishtuke, ukisikia honi, wewe toka, ingia na hiyo gari itaupeleka mahali fulani, utatukuta huko,” alisema Bonge huku akimpa Bazoka pete ile.
Hilo lilimchanganya Bazoka, hakujua ni kitu gani alikuwa akiambiwa. Ni kweli alihitaji utajiri, sasa ile pete ilihusika nini na utajiri aliokuwa akiutaka? Aliambiwa kwamba kuna gari lingefika nyumbani alipokuwa akiishi usiku wa siku hiyo, kilichomshangaza, aliamini kwamba si Bonge wala Sultani ambaye alikuwa akipafahamu alipokuwa akiishi, sasa hilo gari lingekuja na nani aliyekuwa akipafahamu?
Akaambiwa aivae pete ile, akafanya hivyo. Pete ilipokuwa kidoleni, akashangaa kuona akishikwa na kiu kubwa ya kutaka utajiri zaidi ya ile aliyokuwanayo kabla.
Alishangaa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea. Aliwaangalia watu hao, akatokea kuwaamini kuliko kipindi kilichopita, akaamini kila kitu alichoambiwa kwamba angekuwa tajiri mkubwa hapo baadaye kama tu angefanya kile walichokuwa wamemwambia.
Walipozungumza naye, walipomaliza, akaondoka huku akipewa kiasi cha shilingi milioni moja kama pesa ya matumizi. Hakuamini, kwake, yale yaliyokuwa yakitokea yalionekana kama ndoto moja ya kusisimua maisani mwake.
Akaelekea nyumbani, alipofika, akaingia chumbani kwake na kupumzika ambapo baada ya dakika kadhaa, Asha akaingia humo na kuanza kuzungumza naye. Alitamani kumwambia kile kilichotokea, kila alipotaka kufumbua mdomo wake kumwambia, alihisi kabisa mdomo ukiwa mzito kufunguka.
Alishangaa, hakuwahi kupatwa na hali hiyo kabla, alipojaribu kumwambia mambo mengine, mdomo wake ulifunguka lakini kila alipotaka kuzungumzia suala la kukutana na wanaume wale ambao walimwambia kwamba wangemsaidia katika kuutafuta utajiri kwani na usiku huo kuna gari lingefika mahali hapo, alishangaa mdomo kuwa mzito kufumbuka.
Alibaki na jambo hilo moyoni mwake, hakuwa na jinsi, alitulia mpaka usiku ulipoingia ambapo akajilaza kitandani huku Asha akiwa amekwenda chumbani kwake kulala.
Bado kulikuwa na swali moja lililokuwa likikisumbua kichwa chake, lilikuwa ni juu ya gari aliloambiwa kwamba lingefika usiku wa siku hiyo na kumchukua, hakujua ni nani aliyekuwa akiendesha gari hilo na mtu huyo angepafahamu vipi mahali hapo pasipo kumuelekeza.
Akapuuzia na kulala. Ilipofika majira ya saa saba, akasikia honi ikipigwa kutoka nje, akaamka kutoka usingizini. Kwa jinsi honi ilivyokuwa ikipigwa kwa fujo alihisi watu wengine wangeamka na kumwambia dereva aache lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeamka hali iliyoonyesha kwamba ile honi pamoja na kuwa na sauti kubwa, hakukuwa na mtu yeyote aliyesikia zaidi yake.

Je, nini kitaendelea?
 
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA.
IMEANDIKWA: NYEMO CHILONGANI.
0756362035

Sehemu ya 04.

Akapuuzia na kulala. Ilipofika majira ya saa saba usiku, akasikia honi ikipigwa kutoka nje, akaamka kutoka usingizini. Kwa jinsi honi ilivyokuwa ikipigwa kwa fujo alihisi watu wengine wangeamka na kumwambia dereva aache lakini hapakuwa na mtu yeyote aliyeamka hali iliyoonyesha ile honi pamoja na kuwa na sauti kubwa, hapakuwa na mtu yeyote aliyesikia zaidi yake.
Akatoka ndani na kuelekea nje, akakutana na gari aina ya Verrosa ikimsubiri. Aliishangaa gari ile, ilikuwa nzuri mno na rangi yake haikuweza kuelekezeka mara moja na inawezekana kabisa tangu alipozaliwa hakuwahi kukutana na rangi hiyo.
Akaifuata kwa lengo la kumuuliza dereva lakini kitu cha ajabu akaisikia sauti ya dereva ikimwambia alitakiwa kuingia ndani. Alishangaa, kilichomshangaza ni kwamba vioo vyote vya dirisha vilikuwa vimefungwa, ilikuwa vigumu kwa sauti kutoka nje lakini yeye alisikia vizuri kabisa akiambiwa aingie.
“Wewe nani?” aliuliza Bazoka.
“Bazoka! Ingia, tutachelewa,” aliisikia sauti ya dereva.
Alishangaa, ilikuwa dereva wa gari hilo amfahamu kwa jina? Wakati anajiuliza, akakumbuka hiyo ndiyo ile gari aliyoambiwa ingekuja kumchukua, alipokumbuka hivyo tu, akaingia ndani.
Aliingia na kukaa kiti cha nyuma, ndani ya gari hilo walikuwa wawili tu, yeye na dereva aliyekuwa akiendesha ambaye hakutaka hata kuonekana sura yake.
Alikuwa na maswali mengi kwa dereva huyo lakini wakati mwingine alikuwa na hofu nzito kwani hakujua mahali alipokuwa akipelekwa na mbaya zaidi wakati mwingine alijiona mjinga sana, alikubalije kuingia ndani ya gari pasipo kumfahamu dereva wala kujua mahali alipokuwa akipelekwa?
Ikambidi atulie na kushuhudia ni kitu gani kingetokea mbele ya safari. Safari iliendelea mpaka baada ya dakika kadhaa ambapo gari lile likasimama nje ya jumba moja kubwa na la kifahari. Dereva akapiga honi, geti likajifungua na kuanza kuliingiza gari hilo ndani ya jumba hilo kubwa.
Bazoka alibaki akilishangaa, kila kitu kilichokuwa kikionekana mbele yake kilimshangaza sana. Alitembea sana jijini Dar es Salaam lakini hakuwahi kuona jumba la kifahari kama lililokuwa hilo.
Kwenye eneo ya kuegesha magari kulikuwa na magari mengi ya kifahari, bwawa la kuogelea, bustani kubwa iliyokuwa na wanyama wadogo kama sungura, kulikuwa na sehemu iliyokuwa na bembea, yaani kila kitu alichokuwa akikiona mahali pale kilimshangaza kupita kawaida.
Gari likasimamishwa na kufunguliwa mlango kama bosi. Akateremka na dereva yule kumwambia amfuate mpaka kule alipokuwa akielekea ndani ya jumba lile. Mwili wake ulimsisimka mno, hakuamini kama masikini yeye alikuwa akiingia ndani ya jumba hilo la kifahari.
Walipofika mlangoni, mlango ukafunguliwa, akaingia ndani. Macho yake yakatua kwa Sultani na Bonge waliokuwa sebuleni hapo. Walipomuona, wakaonyesha tabasamu pana, wakamsogelea na kumsalimia huku wakimkumbatia.
Walifurahishwa na kumuona mahali hapo, walimpongeza kwa uamuzi wake wa kukubaliana nao kwenda nyumbani pale. Wakazungumza mambo mengi kuhusu utajiri, aliambiwa hakutakiwa kuogopa kwa kuwa kitu alichokuwa akikitafuta kilikuwa ni heshima.
“Unapokuwa na pesa unakuwa na heshima, hata kama hukuwahi kusoma hata darasa moja, wenye digrii watakuheshimu tu,” alisema Bonge huku akimwangalia Bazoka.
“Kweli kabisa,” alisema Bazoka na kutingisha kichwa kuonyesha alikubaliana naye.
“Tunapoamua kutafuta pesa, hatutakiwi kuangalia ni njia gani tunatumia. Pesa ni tamu, mtu akiua, haimaanishi pesa yake inakuwa chungu, hapana, utamu wa pesa bado unabaki palepale, si tunakubaliana Bazoka?” alisema Bonge na kuuliza.
“Ndiyo! Kweli kabisa.”
“Una uhakika unahitaji utajiri?”
“Ndiyo! Ninahitaji kwa nguvu zote.”
“Unaposema kwa nguvu zote unamaanisha nini? Yaani hata kuua?” aliuliza Bonge, Bazoka alipoulizwa hivyo, hakuwa na haraka ya kujibu, kwanza akanyamaza.
“Usiogope Bazoka,” aliingilia Sultan.
“Bazoka. Nakuhakikishia utakapotoka hapa, utakuwa na utajiri mkubwa sana, watu watakuheshimu, utakuwa na uwezo wa kununua kitu chochote unachokitaka, utakuwa na jumba la kifahari, yaani utatisha kwa utajiri, swali ni moja tu, utakuwa tayari?” alisema Bonge na kuuliza.
“Mimi? Nipo tayari bosi.”
“Basi nyanyuka utufuate,” alisema.
Hapohapo wakasimama na kuelekea katika chumba kingine kilichokuwa ghorofani. Walipofika mlangoni, akaambiwa asimame kwanza, akaambiwa avue nguo alizovaa na kuvaa nguo nyingine maalumu ambazo alipewa mahali hapo.
Alifanya hivyo harakaharaka, pete aliyokuwa ameivaa ilimuondolea woga wote na hata kujiuliza kwamba alifanya hayo kwa sababu ya utajiri tu, alishindwa.
Alipozivaa nguo hizo, wakaingia ndani ya chumba hicho. Macho yake yakatua katika katika kiti kimoja kilichokuwa katikakati ya chumba, mwanga wa taa mweupe uliokuwa ukiwaka ukabadilika na kuwa rangi nyekundu. Bazoka akaanza kujisikia hali ya tofauti moyoni mwake, ilikuwa ni kama kulikuwa na nguvu mbili zilizokuwa zikivutana.
Alitulia, akaambiwa avae na kilemba cheusi kilichokuwa katika mfuko wa nguo ile aliyokuwanayo. Akakitoa na kukivaa kisha kuambiwa kusimama huku akitakiwa kufumba macho yake, akafanya kama alivyoambiwa.
Baada ya dakika moja akaambiwa afumbue, kilichomshangaza, mahali alipokuwa hamukuwa mule chumbani, kulikuwa ni sehemu nyingine kabisa ambayo hakuifahamu.
Sehemu hiyo kulikuwa na watu zaidi ya hamsini, walikuwa wamesimama huku wakiwa wameinamisha sura zao na mbele kabisa kulikuwa na mwanaume mwenye umbo la ajabu akiwa amekalia kiti.
Kwa kumwangalia mwanaume yule, aligundua hakuwa mtu wa kawaida hata kidogo. Alikuwa na kwato za ng’ombe, kifua chake kilikuwa kipana, uso wa kawaida lakini kichwani alikuwa na mapembe huku mdomo wake ukiwa mwekundu kupita kawaida.
Alishangaa, hakujua ni mahali gani alipokuwa. Mwanaume yule ambaye alikuwa ni kiumbe cha ajabu akaliita jina lake, haraka sana akapiga hatua kumfuata mpaka kule mbele. Kucha za jitu hilo zilikuwa ndefu kupita kawaida. Alimwangalia Bazoka kwa macho ambayo yalimfanya mwanaume huyo kuogopa na kutamani kukimbia.
“Unahitaji utajiri?” liliuliza jitu hilo huku likimwangalia Bazoka.
“Ndiyo!” alijibu Bazoka.
“Mimi ni mungu wako! Ninapokuuliza sema ndiyo mungu wangu,” alilisema jitu lile.
“Ndiyo mungu wangu!’
Kila mtu mahali hapo alikuwa kimya, ni jitu lile tu ndilo lililokuwa likiongea, liliongea mfululizo pasipo kupumzika, lilimwambia Bazoka alikuwa tayari kumpa utajiri, tena mkubwa lakini alitakiwa kumwabudu.
Kwake, hilo halikuwa na tatizo, alichokihitaji kilikuwa ni utajiri tu. Hakutaka kulala na njaa, hakutaka kudharaulika, hakutaka kuona akinyanyasika kisa hana pesa, hivyo alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile lakini mwisho wa siku kuwa bilionea mkubwa.
“Hutotakiwa kuingia kanisani wala msikitini katika maisha yako yote,” lilisema jitu lile.
“Ndiyo mungu wangu!”
“Hutotakiwa kushika Biblia wala Koraan.”
“Ndiyo mungu wangu!”
“Ila utajiri huu utaambatana na maumivu, upo tayari kuyapokea?” liliuliza jitu lile.
“Ndiyo!” alijibu Bazoka.
“Sawa. Unaruhusiwa kuondoka, kuanzia leo utaitwa bilionea mkubwa, maelekezo mengine watakupa wenzako,” lilisema.
“Ahsante mungu wangu!”
Waliendelea kuliabudu jitu lile mahali pale walipokuwa mpaka waliporuhusiwa kuondoka. Hapakuwa na kutumia usafiri wowote ule, ni kitendo cha kufumba na kufumbua tayari walikuwa katika chumba kile walichoondokea katika lile jumba kubwa na la kifahari.
Kila mmoja alionekana kuwa na furaha, kwa Bazoka alihisi angekuta mifuko iliyojaa pesa lakini akaambiwa utajiri haukuwa ukipatikana hivyo, ilikuwa ni lazima kufanya biashara yoyote ile na angekuwa tajiri mkubwa kupitia hiyo biashara.
Wakazungumza mambo mengi huku wakimwambia maisha yake yalikuwa yamebadilika na yeye angeshika pesa kama walivyokuwa watu wengine. Hakuamini lakini akaambiwa hakuwa amebakiza siku nyingi naye angeitwa bilionea mkubwa.
Ikambidi akubaliane nao na hivyo kutaka kurudi nyumbani ambapo akachukuliwa na gari lilelile kurudishwa. Njiani, alikuwa na mawazo tele, aliyafikiria maisha yake, hayakuwa yale aliyokuwa akiyatamani hata kidogo, aliambiwa angekuwa tajiri, utajiri angeupataje na wakati hakuwa na pesa hata kidogo?
Hawakuchukua muda mwingi wakafika nyumbani na kuelekea chumbani. Hamukuwa na mtu aliyeshtuka, alielekea mpaka chumbani kwake na kutulia. Maneno ya Sultani na Bonge yakaanza kujirudia kichwani mwake kwamba alitakiwa kufanya biashara yoyote ile na hatimaye angekuwa tajiri mkubwa sana.
“Ila sina pesa! Ngoja nikakope kesho,” alijisemea Bazoka.
Akalala. Asubuhi ilipofika kabla ya kuelekea kwenye kazi zake akamuita Asha na kuanza kuongea naye, alimwambia kuwa alihitaji kuanzisha biashara ndogondogo kwani bado kiu yake ya kuwa bilionea iliendelea kuusumbua moyo wake.
Msichana huyo akatulia, alimpenda sana Bazoka, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu. Alipoambiwa alihitaji kufanya biashara tayari kichwa chake kilimwambia kuwa hakuwa na pesa hivyo alihitaji msaada wa pesa ili kufanya hiyo biashara.
Asha akatoka chumbani humo na kuelekea kwa baba yake, alimwambia kile alichokuwa amekisema Bazoka, alihitaji kufanya biashara ila hakuwa na pesa. Kwa kuwa mzee huyo alimpenda Bazoka kwa kuwa alimpa mimba binti yake, akamkopesha kiasi cha shilingi laki moja na kumwambia alitakiwa kukirudisha baada ya kuingiza pesa.
“Nashukuru sana Asha! Sasa ninakwenda kuwa bilionea,” alisema Bazoka.
Aliongea kama utani lakini moyo wake ulimaanisha kile alichokisema. Aliondoka na kuelekea Tandale Sokoni, alipofika huko, akanunua mchele kutoka katika gari moja lililofika hapo ambalo lilitoa mchele kutoka mkoani Mbeya.
Kwa laki moja aliyokuwanayo, alinunua kilo mia moja na kuanza kuuza sokoni hapo. Alichukulia kawaida, alihisi utajiri ungemfikia hata baada ya mwaka mzima lakini cha kushangaza wakati akianza kuuweka mchele kwenye meza aliyokodi, tayari kulikuwa na watu ishirini walikuwa wamesimama mbele yake.
“Kuna nini?” aliuliza huku akiwaangalia.
“Tunataka mchele!”
“Mchele?” aliuliza kwa mshangao.
“Ndiyo! Tupimie, nataka kilo kumi,” alisema mteja mmoja huku akitoa pesa na kumpatia.
Alishangazwa kwa kile kilichotokea, ilikuwaje awe amefika tu na ghafla wateja kumiminika kwake na kuanza kununua mchele, tena walikuwa wakichukua kilo nyingi?
Ni ndani ya nusu saa tu, kilo mia moja zilikuwa zimekwisha na kupata zaidi ya laki mbili. Hakutaka kuishia hapo, akaenda kununua mwingine kwenye lilelile gari na kwenda kuuza.
Kilichokuwa kikimshangaza, siku hiyo lile gari la mchele lilifika na tani moja lakini hapakuwa na muuzaji yeyote aliyekwenda kununua zaidi yake.
Si yeye tu aliyeshangaa bali hata wenye gari wenyewe walishangaa, walikaa na mchele tu na mteja aliyekuwa akija kununua alikuwa Bazoka peke yake.
Ilikuwa kazi ngumu, kila aliponunua kilo mia moja, alipoondoka, alikaa nusu saa, mchele ulikwisha na kurudia kilo mia moja.
Ni ndani ya saa tatu tu, zile tani moja za mchele kwenye gari lile zilimalizika, zote aliuza Bazoka kitu kilichokuwa kimemshangaza sana.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom