Me370
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 985
- 293
- Thread starter
- #21
23
SASA ENDELEA...
"Tumekuwa watu wa kipigo kila kukicha ili turudishe mali zako."
"Kipigo! Toka kwa nani?"
"Mumeo, tena amekuwa akitufuata ndotoni na kutusumbua turudishe mali zako zote bila kuacha kitu chochote."
"Ina maana bila kupata kipigo msingenirudishia mali yangu?"
"Hapana Jeska...ooh samahani Lakashina tulikutafuta muda mrefu bila mafanikio, lakini sasa hivi mali zote zimekatika, sasa hivi maisha yetu yamekuwa ya kubahatisha."
"Sasa mimi niwafanyeje?"
"Muombe mumeo atusamehe au atupe muda tuitafute."
"Mmh, mimi sina neno labda mwenyewe."
"Basi mwambie umetusamehe ili atuache."
"Nitamwambia akirudi."
"Amekwenda wapi?"
"Sijui."
"Atarudi lini?"
"Sijui."
"Lakashina mtumie ujumbe hata kwa njia ya simu kumueleza umetusamehe ili kutupunguzia mateso."
"Mume wangu sijawahi kumuona na simu hata siku moja, na muda huu hayupo."
"Basi akija nitamueleza kuwa umetusamehe."
"Mmh! Sawa."
Baada ya simu kukatwa Lakashina alijikuta akijawa na mawazo juu ya kauli za baba zake wadogo waliomdhulumu mali yake. Moyoni alikuwa radhi kuwasamehe, aliamini mali ile isingewafikisha popote. Lakini alikumbuka kauli ambayo hakujua ni ya nani iliyomuelekeza awashe simu na kuikubali mali yake yote na asiwaonee huruma hata kidogo.
Lakashina aliamini kama ni mali yake, alikuwa na uwezo wa kusamehe hata kuigawa kwa mtu aliyempenda. Hakuona umuhimu wa kung'ang'ania kulipwa mali asiyokuwepo. Akiwa katika lindi la mawazo simu yake iliita, aliipokea.
"Asalamu aleykum," Lakashina alisalimia.
"Waleyku musalam," sauti nzito ilijibu upande wa pili na kumfanya Lakashina ashtuke na simu kumponyoka, lakini sauti ilisikika kama ameweka ‘loud speaker'.
"A..a..abee."
"Lakashina nani kakuita, acha kujitia hofu usipokuwa na kosa."
"Sa...sa...wa," alijibu kwa kutetemeka.
"Lakashina."
"Abee."
"Tuliza moyo wako kabla hatujazungumza lolote."
"Nimetuliza," Lakashina alisema huku akijiweka vizuri kwenye kochi na kufuta mikono usoni kujipa ujasiri.
"Lakashina," Sauti ile nzito ilimwita tena.
"Abee."
"Umetulia?"
"Ndiyo."
"Vizuri, umewasikia baba zako wadogo?"
"Ndiyo."
"Wamesema wataleta lini mali yako yote?"
"Mmh, wameomba niwaombee msamaha kwa vile mali yote hawana kwa sasa."
"Lakashina hakuna kitakachobadilika mali yako inatakiwa mara moja."
"Wamesema tuwape muda."
"Ha...ha...ha...he...he...he...ee," sauti ilicheka sana mpaka ikamkera Lakashina.
"Lakashina," sauti ilimwita baada ya kicheko.
"Abee."
"Unataka tugombane?"
"Hapana."
"Sasa nisikilize, nakuomba hiyo mali iletwe mara moja, mbona wao hawakukusubiri mpaka upate akili ndipo wakudhurumu...Lakashina," sauti ilijirudia kama mwangwi.
"Hii ni amri na siyo ombi, nataka uwakaripie wakuletee mali yako mara moja, kila kitu walichochukua warudishe. Hawakukuonea huruma wakati unamatatizo kwa nini unawasamehe. Kilio chako ndicho kilichofanya niitafute mali yako na kukupa maisha mazuri. Kama hutafanya hivyo adhabu yao itakurudia wewe."
Sauti ile ilinyamaza ghafla na kumfanya Lakashina azidi kuchanganyikiwa, sauti ya adhana ndiyo iliyoufanya moyo wake utulie. Alinyanyuka na kwenda kutia udhu kwa ajili ya swala ya adhuhuri. Alipomaliza kuswali alirudi sebuleni kujipumzisha simu iliita tena moyo ulimpasuka, aliichukua na kuzungumza.
"Asalamu aleykum."
"Lakashina, mama wewe pekee wa kuiokoa familia yako, bila huruma yako tunateketea wote," sauti ya upande wa pili iliyoambatana na kilio pili ilikuwa ya baba yake mdogo.
Lakashina alishindwa awajibu nini, huruma ilimjaa moyoni lakini onyo alilopewa muda mfupi lilimtisha kwa kuhofia maisha yake. Alijikuta akiporomokwa na machozi na kukosa la kuwaeleza baba zake wadogo.
SASA ENDELEA...
"Tumekuwa watu wa kipigo kila kukicha ili turudishe mali zako."
"Kipigo! Toka kwa nani?"
"Mumeo, tena amekuwa akitufuata ndotoni na kutusumbua turudishe mali zako zote bila kuacha kitu chochote."
"Ina maana bila kupata kipigo msingenirudishia mali yangu?"
"Hapana Jeska...ooh samahani Lakashina tulikutafuta muda mrefu bila mafanikio, lakini sasa hivi mali zote zimekatika, sasa hivi maisha yetu yamekuwa ya kubahatisha."
"Sasa mimi niwafanyeje?"
"Muombe mumeo atusamehe au atupe muda tuitafute."
"Mmh, mimi sina neno labda mwenyewe."
"Basi mwambie umetusamehe ili atuache."
"Nitamwambia akirudi."
"Amekwenda wapi?"
"Sijui."
"Atarudi lini?"
"Sijui."
"Lakashina mtumie ujumbe hata kwa njia ya simu kumueleza umetusamehe ili kutupunguzia mateso."
"Mume wangu sijawahi kumuona na simu hata siku moja, na muda huu hayupo."
"Basi akija nitamueleza kuwa umetusamehe."
"Mmh! Sawa."
Baada ya simu kukatwa Lakashina alijikuta akijawa na mawazo juu ya kauli za baba zake wadogo waliomdhulumu mali yake. Moyoni alikuwa radhi kuwasamehe, aliamini mali ile isingewafikisha popote. Lakini alikumbuka kauli ambayo hakujua ni ya nani iliyomuelekeza awashe simu na kuikubali mali yake yote na asiwaonee huruma hata kidogo.
Lakashina aliamini kama ni mali yake, alikuwa na uwezo wa kusamehe hata kuigawa kwa mtu aliyempenda. Hakuona umuhimu wa kung'ang'ania kulipwa mali asiyokuwepo. Akiwa katika lindi la mawazo simu yake iliita, aliipokea.
"Asalamu aleykum," Lakashina alisalimia.
"Waleyku musalam," sauti nzito ilijibu upande wa pili na kumfanya Lakashina ashtuke na simu kumponyoka, lakini sauti ilisikika kama ameweka ‘loud speaker'.
"A..a..abee."
"Lakashina nani kakuita, acha kujitia hofu usipokuwa na kosa."
"Sa...sa...wa," alijibu kwa kutetemeka.
"Lakashina."
"Abee."
"Tuliza moyo wako kabla hatujazungumza lolote."
"Nimetuliza," Lakashina alisema huku akijiweka vizuri kwenye kochi na kufuta mikono usoni kujipa ujasiri.
"Lakashina," Sauti ile nzito ilimwita tena.
"Abee."
"Umetulia?"
"Ndiyo."
"Vizuri, umewasikia baba zako wadogo?"
"Ndiyo."
"Wamesema wataleta lini mali yako yote?"
"Mmh, wameomba niwaombee msamaha kwa vile mali yote hawana kwa sasa."
"Lakashina hakuna kitakachobadilika mali yako inatakiwa mara moja."
"Wamesema tuwape muda."
"Ha...ha...ha...he...he...he...ee," sauti ilicheka sana mpaka ikamkera Lakashina.
"Lakashina," sauti ilimwita baada ya kicheko.
"Abee."
"Unataka tugombane?"
"Hapana."
"Sasa nisikilize, nakuomba hiyo mali iletwe mara moja, mbona wao hawakukusubiri mpaka upate akili ndipo wakudhurumu...Lakashina," sauti ilijirudia kama mwangwi.
"Hii ni amri na siyo ombi, nataka uwakaripie wakuletee mali yako mara moja, kila kitu walichochukua warudishe. Hawakukuonea huruma wakati unamatatizo kwa nini unawasamehe. Kilio chako ndicho kilichofanya niitafute mali yako na kukupa maisha mazuri. Kama hutafanya hivyo adhabu yao itakurudia wewe."
Sauti ile ilinyamaza ghafla na kumfanya Lakashina azidi kuchanganyikiwa, sauti ya adhana ndiyo iliyoufanya moyo wake utulie. Alinyanyuka na kwenda kutia udhu kwa ajili ya swala ya adhuhuri. Alipomaliza kuswali alirudi sebuleni kujipumzisha simu iliita tena moyo ulimpasuka, aliichukua na kuzungumza.
"Asalamu aleykum."
"Lakashina, mama wewe pekee wa kuiokoa familia yako, bila huruma yako tunateketea wote," sauti ya upande wa pili iliyoambatana na kilio pili ilikuwa ya baba yake mdogo.
Lakashina alishindwa awajibu nini, huruma ilimjaa moyoni lakini onyo alilopewa muda mfupi lilimtisha kwa kuhofia maisha yake. Alijikuta akiporomokwa na machozi na kukosa la kuwaeleza baba zake wadogo.