Hadithi : Singidani (A Story From My Heart)

Hadithi : Singidani (A Story From My Heart)

SEHEMU YA 17


ILIPOISHIA..
“Ndiyo maana nakuambia unataka kunichezea mchezo... mbona mimi nilikuja kutafutwa na maaskari wakisema nimetembea na mke wa mtu... tena mke wa mkuu wa kituo?”
SASA ENDELEA...

LAURA alihisi kizunguzungu kikali. Yeye awe mke wa mtu? Tangu lini ameolewa? Alihisi kichwa chake kikigonga kwa kasi sana. Ukweli alioujua yeye ni kwamba hakuwahi kuolewa achilia mbali mchumba wa uhakika.
Hakuposwa!

Hakuwa na pete ya uchumba. Hata mwanaume wa uhakika pia hakuwa naye. Ni kweli hakuwa ameolewa. Ilikuwa ni yeye na masomo na starehe tu. Mara chache kuna wakati alikuwa akitoka na wanaume tofauti kwa ajili ya liwazo la moyo wake. Hivyo tu!
Laura alishtuka si mchezo!!!

“Aaaaah! Sasa naanza kupata picha. Hata mimi pia nilifuatwa nikaambiwa kwamba, wewe ni mume wa mtu na mkeo yupo palepale Singida. Nilikwenda hadi kituoni kutafuta ukweli, lakini cha kushangaza, wakasema hakuna kitu kama hicho na wala hakuna maaskari waliotumwa kunitafuta mimi kwa madai ya kutembea na mume wa mtu!” akasema Laura kwa sauti tulivu akionekana dhahiri kuwa na uhakika na alichokuwa akikizungumza...

Chris alibaki mdomo wazi. Hata hivyo, bado hakumwamini Laura hata kidogo.
“Nitaaminije?” akauliza Chris akimkazia macho Laura.
“Subiri,” Laura akasema kwa sauti ya chini.

Alichokifanya ilikuwa ni kufungua pochi yake, kisha akatoa kitambulisho chake cha chuo na kumkabidhi. Baada ya hapo alitoa kitambulisho cha kupigia kura nacho akamkabidhi. Chris akaonekana akivitazama vile vitambulisho kwa makini sana.
“Kwahiyo sasa hii inathibitisha nini?”

“Kwamba mimi ni mwanafunzi wa chuo.”
“Kwani mwanachuo hawezi kuolewa?”
“Anaweza, lakini uliambiwa mimi siyo mwanachuo ni mke wa mtu tu.”
Chris akatulia kwa muda.

“Na hiki kitambulisho cha kura?”
“Angalia nimejiandikishia wapi? Nilishakuambia mimi kwetu siyo Singida, natokea Mwanza. Naona hata kitambulisho changu kimekuthibitishia hilo sasa.”
“Siyo kigezo sana Laura, lakini naomba nikuulize kitu.”
“Uliza tu.”

“Kwanini umekuja Dar?”
“Nimekuja kwa ajili yako Chris. Nakupenda sana, huwezi kuamini jambo hili hasa kutokana na mwanzo wetu ulivyokuwa, lakini nataka uamini kuwa umeingia moyoni mwangu kama cheche za umeme. Unaniumiza baba. Mapenzi yako yananitesa sana ndiyo maana nikaamua kuja hadi huku kwa ajili yako.

“Usinione tapeli au mwenye nia mbaya na wewe, amini moyo wangu baba. Nakupenda sana. Nahitaji kutengeneza familia na wewe. Najua ni kiasi gani una wasiwasi na mimi. Ni haki yako kuwa na mashaka kutokana na mazingira yenyewe na hata mimi niliingiwa na wasiwasi kidogo baada ya kufuatwa na maaskari eti natembea na mume wa mtu.

“Najua ni jambo gumu kidogo kupenya kichwani mwako mpenzi lakini nakuomba sana utambue kuwa moyoni mwangu, mwanaume pekee aliyejaa ni wewe. Niamini na unipe pumziko tafadhali,” Laura alizungumza kwa dakika tatu peke yake bila kupumzika.
Kwa kiasi kikubwa, maneno ya Laura yalimwingia Chris taratibu ubongoni mwake. Alianza kumwamini taratibu kabisa...

“Una uhakika na unayozungumza Laura?”
“Zaidi ya uhakika.”
“Kweli?”
“Niamini.”

Chris alitulia kwa muda tena. Akamwangalia Laura sasa kwa macho ya kawaida yasiyo na hasira. Moyo wake ulilipuka. Laura alikuwa mwanamke mrembo kuliko kawaida. Alihisi mpangilio wa mapigo ya moyo wake ukibadilika kabisa.

Alijilamba midomo yake, akamwangalia kwa makini Laura ambaye sasa macho yake yalishaanza kuchuruzisha machozi mepesi. Chris akasimama na kumshika mikono Laura kisha akamwonyesha ishara asimame. Laura akasimama. Chris kama aliyechanganyikiwa, alimvutia kwake, Laura akaenda mzima-mzima.
Wakakumbatiana!

“Nakupenda sana Laura, nakupenda mama.”
“Nakupenda pia Chris.”
“Tafadhali usiniumize moyo wangu mama, usiniingize kwenye matatizo mama. Isije kuwa unatumiwa na watu ili uniharibie. Tafadhali sana mpenzi wangu, naomba unipende kwa moyo wako.”

“Sijui niseme nini ili uelewe hili ninalosema lakini itoshe tu kukuambia kuwa, linatokea ndani ya moyo wangu!”
Waliangaliana kwa muda mrefu, macho ya wote yakapoteza uwezo wa kutazama vyema, wakakutanisha midomo yao kisha wakaanza kubadilishana mate.

Walidumu katika zoezi hilo kwa dakika mbili nzima, kila mmoja akionyesha hisia kali kwa mwenzake.
“Pwaaaa! Pwaaaa! Pwaaaa! Pwaaaaaaa....” makofi yasikika yakipigwa!

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 18



ILIPOISHIA..
Walidumu katika zoezi hilo kwa dakika mbili nzima, kila mmoja akionyesha hisia kali kwa mwenzake.
“Pwaaaa! Pwaaaa! Pwaaaa! Pwaaaaaaa....” makofi yasikika yakipigwa!
SASA ENDELEA...

MSHTUKO wa ghafla ukawapata Laura na Chris waliokuwa wamezama kabisa kwenye ulimwengu wa mapenzi. Walikuwa kwenye dunia ya peke yao kabisa, wakiwa hawana habari na watu walikuwa eneo lile.
Makofi yaliyopigwa kama vile watu walikuwa wakishangilia tukio fulani muhimu yaliwachanganya kwa hakika. Haraka wakaachiana. Walishangaa kuona kundi zima la Bongo Film Club likiwa limewazunguka wakiwapigia makofi.

Chris akatabasamu.
“Naomba mnisamehe sana rafiki zangu kwa yote yaliyotokea. Laura, pia naomba unisamehe mama. Ndugu zangu, naomba sasa niwatangazie rasmi kuwa huyu ndiye mama watoto wangu mtarajiwa!” akasema Chris akiachia tabasamu!
Mlipuko wa shangwe ukaendelea.

“Kikao cha kwanza ni wiki ijayo hapa hapa Leaders. Mimi ndiye mwenyekiti na mchango wangu ni milioni tatu,” akasema Jaybee, wenzake wakimshangilia.
“Hayo ndiyo maneno sasa ya kuzungumza... kuhusu usafiri wa maharusi, wazazi na wahudhuriaji wengine kutoka kanisani hadi ukumbini, itakuwa juu yangu,” akasema Chika, wote wakicheka na kuachia shangwe.

Lilikuwa tukio la kufurahisha sana. Jaybee akajitolea ofa ya vinywaji kwa wenzake wote, kisha wakamimina kwenye glasi na kugongesha kwa furaha. Kikao cha kikazi kikabadilika, hawakujadiliana tena kuhusu filamu, walizungumzia ujio wa shemeji yao mpya; Laura.
***
Giza jepesi lilichukua nafasi katika chumba hicho kikubwa chenye hewa safi iliyotoka moja kwa moja kutokea nje kupitia madirisha makubwa mawili kila upande. Pamoja na hewa hiyo nzuri iliyopenya kwenye mapazia mepesi, feni ilisaidia kupooza joto na kuwafanya viumbe hawa kusahau kabisa kama Dar es Salaam ni mji wenye joto kali.

Macho ya Chris yalikuwa yamemwelekea Laura aliyekuwa kitandani na gauni jepesi la kulalia. Chris alikuwa amevaa bukta pekee. Alimwangalia sana kama anayemfananisha na mtu anayemfahamu! Laura alikuwa kimya akijilamba midomo yake.

Hapo sasa, Chris aliamini kweli Laura alikuwa mwanamke mrembo. Macho yake yalizidi kumchanganya Laura na hivyo kushindwa kuvumilia na kumwangushia Chris swali: “Vipi dear, mbona unaniangalia hivyo?”
“Siamini tu kama nipo na wewe.”
“Kwanini mpenzi wangu?”

“Basi tu... sikia darling, kama kuna wanaume wenye bahati duniani, mimi ni mmoja wao. Ni vigumu sana kumpata mwanamke wa ndoto zako katika mazingira kama tuliyokutana mimi na wewe. Kiukweli najisikia faraja sana.”
“Usijali baba, wewe ni wangu, imeshapangwa iwe hivyo.”
“Ahsante mama.”

Chris alivuta shuka, akalitupa juu ya mwili wa Laura, naye akaingia ndani yake. Akamvutia Laura karibu yake, akamkumbatia. Hakuwa na haja ya kuzima, chumba kilikuwa na giza jepesi, mwanga hafifu kutoka taa iliyokuwa nje, ukisaidia kukifanya chumba kiwe katika mwonekano wa kimahaba.

Chris aliuchoropoa ulimi wake kinywani, akausogeza jirani na mdomo wa Laura, kwa fujo akaanza kulambalamba midomo yake. Zoezi hilo halikudumu kwa muda mrefu sana, Chris akaupeleka ulimi wake kinywani mwa Laura, akaupokea!
Hawakuwa na sababu za kuzima taa, mwanga mwepesi kutoka taa iliyokuwa nje ya chumba kile uliwatosha kabisa... wakaamua kuendelea na mambo yao wenyewe!
***
Alihisi mwili wake ukiguswa lakini alifikiri alikuwa ndotoni. Mwili uliendelea kutingishwa kwa kasi, mwisho akaamua kufumbua macho. Alikutanisha macho na uso wa mwanamke mrembo sana; Laura. Kwa mara nyingine aliushangaa uzuri wa Laura.

Laura alikuwa amevaa kanga moja tu kifuani, akionekana alikuwa kwenye pilikapilika za usafi wa asubuhi. Chris alitabasamu, akamwambia: “Vipi dear, umeamkaje?”
“Salama baba, nilikuwa nafanya usafi... nimeshakuandalia kifungua kinywa. Mbona unachelewa sana kuamka? Unatakiwa kwenda kazini.”

“Najua darling, ngoja niingie bafuni nikajimwagie maji kwanza, ahsante sana mpenzi wangu,” akasema Chir.
Haraka akainuka na kwenda bafuni, aliporejea alikwenda moja kwa moja kwenye meza ya chakula.

Wote kwa pamoja wakaanza kupata kifungua kinywa! Uzuri mwingine wa Laura ukaonekana! Alikuwa mtaalamu sana jikoni.
“Mh! Kweli hapa nimepata mke,” akajisemea moyoni mwake Chris.

Itaendelea
 
SEHEMU YA 19



ILIPOISHIA...
“Mh! Kweli hapa nimepata mke,” akajisemea moyoni mwake Chris.
SASA ENDELEA...
HISIA za kuwa ndani ya ndoa zilimvamia Chris kwa kasi sana, ni kweli alikuwa anakimbia kuoa muda mrefu kwa sababu hakupata mwanamke ambaye amempenda kwa dhati ya moyo wake, lakini safari hii alikiri kuwa kweli Laura alikidhi vigezo vyote.
“Kama sijawahi kukuambia, naomba nikuambie leo kutoka moyoni mwangu, nakupenda sana Laura,” akasema Chris.
Laura akacheka sana!
“Mbona unacheka?”
“Ni mara ngapi baby umeniambia kuwa unanipenda? Mara nyingi tu... hata jana usiku uliniambia neno hilo.”
“Basi kama ndivyo, naomba nibadilishe maneno, leo utambue kuwa ninasema kwa kumaanisha kuliko siku zote; nakupenda sana Laura, sijajuta kuwa na wewe na kamwe sitajuta mpenzi wangu.”
“Ahsante sana mpenzi wangu kwa maneno yako mazuri.”
Kimya kifupi kilipita, wote wakiendelea kula. Kila mmoja kichwani mwake alikuwa na mawazo yake. Laura alikuwa akiota ndoa na Chris. Kijana mtanashati kama yule, maarufu anayejulikana ndani na nje ya Tanzania kwa kazi yake ya sanaa lakini zaidi ya yote daktari!
Chris yeye alikuwa akifikiria zaidi kuhusu baba yake, ni kweli amempenda sana Laura, lakini maelekezo ya baba yake ilikuwa lazima mkewe atokee kijijini kwao. Tayari alimshamdanganya kuwa mchumba amepatikana kijijini.
“Itakuwaje? Mbona naanza kuona dalili mbaya za kumkosa Laura?” akawaza Chris.
“Lakini nitajua cha kufanya, hawezi kunisumbua. Kichwa changu kinafanya kazi sawasawa,” akajiliwaza kwa maneno hayo.
Ukimya huo wa mawazo ya ndani kwa ndani huku kila mmoja akiwaza lake, ulivunjwa na Laura: “Halafu dear, kuna jambo nataka kukuuliza.”
“Uliza tu mama.”
“Imekuwaje wewe daktari mzima, ukaingia kwenye mambo ya filamu?”
“Kwanza kwa nini umesema daktari mzima? Inamaana hupendi mimi kuwa msanii?”
“Sina maana hiyo mpenzi wangu. Ninavyojua mimi, wengi wanaoingia kwenye sanaa huwa hawana elimu ya kutosha lakini wewe kitaaluma uko vizuri kabisa. Kwa nini sasa ukaingia kwenye filamu?”
“Ni habari ndefu Laura lakini jambo kubwa ambalo nataka kukuambia ujue, napenda sana sanaa na siku zote ndiyo imekuwa chanzo cha ugomvi kati yangu na mzee wangu. Baba alitaka sana niwe daktari, ndiyo maana alinilazimilisha nikazanie masomo ya Sayansi.
“Alijua kunishawishi, kweli nikajikuta taratibu nimeanza kupenda masomo ya Sayansi na nikayamudu vizuri. Baada ya kumaliza kidato cha sita, mzee alinipeleka Uingereza kusomea udaktari. Nimeishi huko kwa miaka saba.
“Pamoja na hayo, bado ndani yangu kulikuwa na chembechembe za sanaa, ndiyo maana nikaamua kurudi nchini kwa lengo hilo, lakini kwa sababu kiu ya mzee ni kutaka kusikia nikiitwa daktari tena nikiwatibu watu, nikaamua kuomba kazi Hospitali ya Kinondoni.
“Mpaka sasa nafanya kazi hapo, lakini nikiendelea na sanaa kama kawaida. Bosi wangu hana tatizo na hilo, maana nilimweleza hali halisi kabla ya kuanza kazi. Naijua vizuri taaluma yangu lakini napenda sana sanaa, vyote vinanipa fedha na ninafanya vyote kwa wakati mmoja,” alisema Chris.
“Hongera yako.”
“Ahsante.”
Walipomaliza kula, wote walitoka kwa pamoja na kuingia kwenye gari la Chris, wakaenda moja kwa moja kazini kwa Chris, akamtambulisha kwa baadhi ya wafanyakazi wenzake kisha akamruhusu aendelee na mizunguko yake mingine.
Laura hakuwa na mambo mengi sana siku hiyo, kikubwa hasa ilikuwa ni kwenda Kariakoo kufanya manunuzi ya mavazi na vitu vingine vya kwenda navyo Singida.
***
Laura alikaa Dar kwa wiki nzima akipoteza vipindi vyote kwa muda huo. Siku ya kurejea Singida ilikuwa ya huzuni sana kwake. Chris alimsindikiza mpaka kituoni, Ubungo ambapo alikuwa ameshamkatia tiketi kwenye basi la ABC.
Laura aliagana na Chris wakiwa wamekumbatiana kwa muda mrefu sana. Ilikuwa ni kama hawakuwa na mpango wa kuachiana. Mwili wa Laura ulisisimka sana, alitamani kuendelea kubaki Dar lakini haikuwezekana, alipaswa awahi masomo Singida.
Muda wa safari ulipowadia, hakuwa na jinsi – aliingia garini na kumwacha Chris akiwa anamtazama kupitia dirishani. Saa 12:00 asubuhi, gari lilianza kuondoka. Laura akampungia Chris mkono huku akitoa machozi, ni kama walikuwa wanarekodi filamu lakini ilikuwa kweli.
Waliendelea kupungiana mikono mpaka gari lilipofika mbali. Chris akaenda kwenye maegesho, akaingia kwenye gari lake, akaondoka. Ilikuwa safari ya kuelekea kazini kwake. Saa 3:00 asubuhi hiyo alikuwa na kazi ngumu sana ya kumfanyia mtu upasuaji mkubwa!
 
SEHEMU YA 20



ILIPOISHIA...Waliendelea kupungiana mikono mpaka gari lilipofika mbali. Chris akaenda kwenye maegesho, akaingia kwenye gari lake, akaondoka. Ilikuwa safari ya kuelekea kazini kwake. Saa 3:00 asubuhi hiyo alikuwa na kazi ngumu sana ya kumfanyia mtu upasuaji mkubwa!
SASA ENDELEA...
USO wa mzee huyu ulionyesha dhahiri kuwa hauna masihara; alitaka kujua jambo moja tu tena lenye hakika kutoka kwa mwanaye. Alitaka kujua kuhusu ndoa. Chris alitulia akimwangalia baba yake, kichwani akitafakari ni jibu gani lingemfaa baba yake.
“Chris niambie ukweli, umefikia wapi?” baba yake akamwuliza.
“Baba nilishakuambia kuwa lazima nitaoa mwaka huu kwa sababu tayari nimeshapata mchumba.”
“Sasa mbona unachelewesha mambo?”
“Si kuchelewesha baba, ni suala la mipango tu. Nipe muda.”
“Muda gani?”
“Miezi miwili inatosha kabisa, nipatie muda huo baba nitakamilisha hili suala.”
“Nataka iwe hivyo.”
Mzee Shila, baada ya kuzungumza hayo, alitoka haraka na kuelekea chumbani kwake, sebuleni alibaki Chris na mama yake tu. Waliangaliana kwa muda, kisha kila mmoja akajikuta akiinamisha uso wake chini.
“Lakini mwanangu, kwa nini usioe ili kuachana na haya manenomaneno ya baba yako?”
“Mama kwani nimekataa kuoa? Si tayari nimeshasema nimepata mchumba mama, kikubwa hapo ni muda tu.”
“Sawa.”
“Mama ngoja mimi niondoke, nina ratiba nyingi sana kesho asubuhi. Acha tu niende sasa,” akasema Chris akimtulizia macho mama yake.
“Sawa baba, usiku mwema.”
“Nanyi pia.”
***
Kichwa kilitaka kupasuka. Alitulia kitandani mwake akiwaza sana, dalili za kumpoteza mrembo Laura zilianza kuonekana waziwazi. Alitamani sana kumuoa Laura, hakuwa mwanamke wa kucheza naye kwa usiku mmoja tu!
Laura alikuwa mke!
“Lakini itawezekanaje wakati mzee naye analazimisha mke atokee kijijini?” akawaza Chris.
“Kuna kitu natakiwa kufanya hapa, lazima nimpate Laura maishani mwangu, siwezi kukubali akaolewa na mwanaume mwingine, haitawezekana hata kidogo,” akazidi kuwaza Chris.
Akiwa mawazoni, simu yake iliita. Haraka akaichukua na kuangalia kwenye kioo; akakutana na jina la Laura lilitokea. Akapokea haraka sana...
“Haloo mpenzi wangu...” sauti tulivu ya Chris ilitoka.
“Yes darling, za huko?”
“Nzuri tu mama. Unaendeleaje huko?”
“Nipo vizuri tu, nimekukumbuka mpenzi, hata usingizi umekata kabisa.”
“Kweli mpenzi?”
“Kweli kabisa.”
“Nataka kuuliza kitu dear maana naona dalili mbaya.”
“Dalili mbaya za vipi mpenzi?”
“Kuhusu mapenzi yetu.”
“Mh! Mbona sikuelewi? Hebu niulize.”
“Unanipenda kweli mama?”
“Nakupenda sana.”
“Unakumbuka nilikuambia nini kuhusu mzee wangu?”
“Nakumbuka.”
“Sasa hapo ndipo kwenye tatizo. Baba ameendelea kushikilia msimamo kuwa nioe mwanamke kutoka kijijini kwetu. Kuna kitu tunatakiwa kufanya mpenzi wangu ili tuweze kufanikisha jambo hili.”
“Mh! Kweli kuna kazi, kwa hiyo hutanioa Chris kwa sababu hiyo? Kumbuka mimi nakupenda na nimekuwa tayari kufanya kila kitu kwa ajili yako. Sipo tayari kukupoteza.”
“Najua, ndiyo maana nimekuambia, kuna jambo inabidi lifanyike ili tufanikishe.”
“Ni jambo gani mpenzi wangu?”
“Nimeshamwambia baba kuwa nimepata mchumba kijijini, sasa unachotakiwa kufanya.
Itabidi nikazungumze na baba mdogo kuhusu jambo hili ili wewe uende kijijini, ukakae kwa muda, mzee ajue unatokea kule. Lengo langu ili mambo yaweze kwenda bila matatizo, itawezekana kweli mpenzi wangu?” akasema Chris.
“Kwa nini ishindikane wakati nakupenda baba?”
“Sasa itakuwa lini?”
“Panga wewe. Wiki mbili zijazo tunamalizia muhula, tunafunga chuo kabla ya kurudi tena kumalizia chuo kabisa.”
“Safi kabisa, ngoja nijipange ndani ya muda huo mama. Vipi, nyumbani hakutakuwa na tatizo?”
“Hapana, nitajua cha kufanya. Niamini mimi.”
“Sawa mpenzi wangu, angalau sasa nina amani. Naweza kupata usingizi wangu vizuri nashukuru sana mama, usiku mwema.”
“Nawe pia.”
Mwanga wa ndoa yake na Laura ulionekana wazi kabisa. Moyo wake ukagubikwa na furaha ya ajabu. Haikuwa kazi ngumu tena kupata usingizi. Kilichobaki ilikuwa ni utekelezaji tu!

Itaendelea....kesho
 
SEHEMU YA 21



ILIPOISHIA...Mwanga wa ndoa yake na Laura ulionekana wazi kabisa. Moyo wake ukagubikwa na furaha ya ajabu. Haikuwa kazi ngumu tena kupata usingizi. Kilichobaki ilikuwa ni utekelezaji tu!
SASA ENDELEA...

DK. Chris aliandika maneno fulani kwenye kadi alilokuwa nalo mkononi kisha akayarudisha tena macho yake kwa mgonjwa aliyekuwa ameketi mbele yake. Alikuwa mwanamke anayeelekea kuwa na umri si zaidi ya miaka 30. Alikuwa mpole, mkimya na anayeonekana kuhitaji huduma ya haraka sana. Hiyo ilikuwa ni muda mfupi baada ya kwenda maabara kutoa vipimo

. Aliitwa Sandra.

“Kuna tatizo kwenye mkojo wako. Una maambukizi. Kitaalamu tunaita Urinary Tract Infection, kwa kifupi UTI. Pia una malaria kali. Kwa namna hali yako ilivyo, ni lazima tukulaze ili tukuanzishie drip za kwinini mara moja ambayo inaweza kutibu malaria vizuri na haraka zaidi. Nitakupa na Antibiotics kali kwa ajili ya UTI.

“Hata hivyo lazima uwe makini sana matumizi ya vyoo, ambavyo hasa ndiyo chanzo kikuu cha maambuzi ya UTI. Pole sana Sandra,” alisema kwa sauti tulivu sana Dk. Chris.

“Ahsante dokta.”
“Ngoja nimuite sista aje kukuchukua,” akasema Dk. Chris.
Akainua mkonga wa simu iliyokuwa mezani kisha akabonyeza namba fulani na kuanza kuzungumza na upande wa pili. Muda mfupi baadaye alifika na kukabidhiwa kadi la Sandra, kisha akaongozana naye wodini. Mgonjwa mwingine akaingia.

Ndivyo siku ya Dk. Chris ilivyokuwa kazini kwake, Hospitali ya Kinondoni siku hiyo. Ilikuwa siku ambayo alidili na wagonjwa wa kawaida tu. Hakuwa na ratiba ya upasuaji siku hiyo.
***
Ilikuwa lazima apange safari ya Singida haraka iwezekavyo. Baba yake mzee Shila asingemwelewa hata kidogo kama angeendelea kuchelewa kuoa. Tayari alishatengeneza mazingira mazuri ofisini kwake.
Ni muda ambao hata Laura naye alikuwa ameshafunga chuo baada ya kumaliza mitihani. Ilikuwa ni kipindi cha likizo fupi ya wiki mbili. Hizo zilitosha kabisa kukamilisha mpango waliokubaliana.

Chris alisafiri hadi Singida ambapo alikutana na Laura na kuweka mipango yao sawa. Hakuwa na hofu tena, alishaamini kabisa kuwa Laura hakuwa mke wa mtu kama alivyojulishwa awali.
Hata hivyo kwa hofu ya usalama wake, hakuwa tayari kukutana naye katika hoteli ileile ya awali. Alifikia hoteli nyingine iliyokuwa nje kidogo ya mji.

“Laura unanipenda kweli? Kumbuka hapa nakwenda kufanya usaliti lakini ni kwa ajili ya penzi letu.”
“Najua baba, nakupenda, niamini.”
“Ahsante mama, sidhani kama tunatakiwa kutoka, maana kesho asubuhi tunakwenda kijijini. Mipango yote nitakuambia hukohuko, sawa mpenzi wangu?”

“Nimekuelewa baba.”
Walilala wakiwa na matumani makubwa ya kufanikisha mpango uliokuwa mbele yao; mpango wa ndoa. Safari haikuwa mbali sana.
Ni kesho tu!
***
Walishuka katika kituo cha Ibaga saa kumi jioni ikiwa ni safari ya takribani saa tano kutoka Singida Mjini hadi hapo katika mji mdogo wa Ibaga.
Kama miundombinu ingekuwa mizuri, ni safari ya saa mbili tu tena kwa mwendo wa kawaida. Walikuwa wachovu sana kwa safari hiyo. Walitafuta nyumba ya wageni na kulipia. Hapo ndipo filamu ilipotakiwa kuanza rasmi.

“Lazima mavazi yako yabadilike sasa, utavaa zile nilizokununulia mjini. Unapaswa kufanana na watu wa huku. Mchezo ulivyo ni kwamba, leo mimi nitakwenda nyumbani - Mkalama, wewe utalala hapa hadi kesho.
“Nitakwenda kuzungumza na baba mdogo ambaye anajua kila kitu kuhusu wewe, halafu yeye atazungumza na bibi kwamba, wewe utakuja kututembelea. Pale ndiyo sehemu ya kuchukua pointi, usilaze damu, ujitahidi kuendana na kila kitu cha pale nyumbani.

“Kwa bahati nzuri, hakuna shida sana, halafu kipindi hiki si cha kilimo kwa hiyo hawatakupeleka shamba. Kifupi uonyeshe heshima na mwonekano wa mtu wa kijijini usiyejua mambo ya mjini sana.
“Lakini itabidi tudanganye kuwa, hufahamu vizuri lugha yetu kwa sababu wazazi wako walihamia Mwanza tangu ukiwa mdogo lakini sasa wameamua kurudi tena kijijini. Mambo mengine utaniachia mimi.

Umenipata?” akasema Chris.
“Nimekuelewa vizuri sana.”
Mpango mzima ukawa umekamilika, ilibaki utekelezaji tu!
***
Chris alikodi baiskeli kutokea Ibaga hadi Mkalama, kijijini kwao. Alifika baada ya nusu saa tu. Alipokelewa vizuri na baba yake mdogo ambaye alimpa mpango mzima ulivyokuwa.
“Wazo zuri sana Chris, acha nizungumze na bibi. Naamini naye atafurahi. Hatajua mchezo wetu na inabidi iwe siri yetu tu,” akasema Shamakala.
“Sawa baba mdogo.”

“Zoezi linafanyika lini?”
“Hakuna kusubiri, ni kesho tu baba mdogo.”
“Sawa.” Itaendelea
 
SEHEMU YA 22



ILIPOISHIA...ILIPOISHIA...
“Zoezi linafanyika lini?”
“Hakuna kusubiri, ni kesho tu baba mdogo.”
“Sawa.”
SASA ENDELEA...

CHRIS hakutaka kupoteza muda, kilichokuwa akilini mwake ni mke tu. Hakutaka mwanamke mwingine zaidi ya Laura. Baba yake mdogo, Shamakala alikubaliana na wazo lake.
Hakuwa na sababu ya kupoteza muda. Alimfuata mama yake, alipokuwa amekaa kisha akaketi kwenye kigoda jirani yake.

“Mkombi...” (Mama) Shamakala aliita kwa Kinyiramba.
“Shamakala unasemaje?”
“Kuna jambo zuri nataka kukuambia.”
“Zuri? Hebu nikae vizuri sasa. Haya niambie ni nini?”
“Ni kuhusu Chris... anataka kuoa.”

“Jambo zuri sana hilo. Ameshapata huyo mwali mwenyewe sasa?”
“Ndiyo, tena ni mtu wa hukuhuku kwetu.”
“Wa wapi?”

“Anatokea Kijiji cha Mpambala.”
“Safi sana, sasa mmefikia wapi?”
“Anataka kesho amlete hapa nyumbani aje kututembelea, kama tena taratibu zetu, tukikaa naye hapa japo kwa siku mbili tutaweza kumchunguza japo kidogo unavyojua na sisi ili tujiridhishe kuwa anafaa kuingia kwenye familia yetu.”

“Ni wazo zuri, utaongozana naye sasa au?”
“Ndiyo... mimi ndiyo mwenyeji wake pale, lazima niende naye.”
“Mimi naunga mkono mwanangu, sina matatizo na hilo.”

“Sawa mama, nilisema nikujulishe tu maana ungeshangaa kuona mtu amekuja nyumbani bila taarifa yako, tukaona si busara.”
“Mmefanya vizuri.”

Shamakala alifurahishwa sana na majibu ya mama yake. Alimfuata Chris na kumweleza kila kitu kilivyokuwa, akafurahi sana.
Usiku ulikuwa mrefu sana, alitamani asubuhi ifike haraka ili Laura afike nyumbani kwao. Alitaka kuona namna ambavyo bibi yake angemchukulia.
***
Chris alikuwa wa kwanza kuamka asubuhi hiyo. Alidamka saa moja kasoro, muda ambao kwa kipindi hicho ambacho hakikuwa cha kilimo, ilikuwa mapema sana.
Kwa kawaida wakati wa kilimo wanakijiji hadaamka mapema na kwenda mashambani. Si katika kipindi hicho cha kiangazi. Alifanya shughuli ndogondogo za nyumbani hadi saa mbili ndipo baba yake mdogo alipoamka.

Chris alifurahi sana alipomuona baba yake mdogo akitoka nje. Baada ya salamu, wakaanza kupanga namna ya kufanya.

“Hapa hakuna cha kujadili sana, twende tu juu kule juu tukachukue pikipiki tuondoke,” akasema Chris.
“Sawa... lakini tupate kifungua kinywa kwanza.”
“Hapana, tutakunywa supu Ibaga.”
“Sawa.”

Hawakuwa na muda wa kupoteza, walikwenda barabarani walipochukua pikipiki moja ambayo walipanda kwa mtindo wa mshikaki, safari ya kwenda Ibaga ikaanza.

Kwa pikipiki ulikuwa ni mwendo wa dakika kumi tu, walikuwa wameshafika Ibaga. Chris ndiye aliyemlipa dereva, kisha wakatembea na kuelekea kwenye mgahawa mmoja maarufu eneo hilo.
“Sasa dingi, we’ nisubiri hapa, ngoja nikamchukue.”
“hivi ni wapi kwani?”

“Tumefikia Sayuni Lodge.”
“Sawa.”
Shamakala na Chris walikuwa na umri unaokaribiana sana, Shamakala alikuwa mtoto wa mwisho katika uzao wa baba yake na Chris. Sababu hiyo iliwafanya wazoeane kwa kiasi kikubwa.

Hata mazungumzo yao yalikuwa ya ujana zaidi kutokana na umri wao kukaribiana. Hata hivyo, hilo halikuvunja heshima waliyokuwa nayo. Bado Chris aliendelea kumheshimu Shamakala kama baba yake.
Chris alifika Sayuni na kwenda kugonga katika chumba alichomuacha Laura jana yake. Aligonga mara moja tu, Laura alifungua. Chris alishangaa sana.

Alikutana na Laura mpya kabisa. Laura alikuwa amevaa mavazi ambayo kwa kumwangalia tu unajua kuwa, alikuwa msichana aliyeishi kijijini. Alifafana nao kwa kila kitu.
“Daah! Kweli umefunika mpenzi wangu. Hapo umepatia kabisa.”

“Nashukuru mpenzi, nini kinaendelea?”
“Kama uko tayari, tuondoke. Hakuna kitu cha kusubiri zaidi.”

Ndivyo ilivyokuwa, walitoka na kwenda mgahawani alipokuwa Shamakala. Utambulisho mfupi ukafanyika kisha wote wakaagiza supu ya mbuzi. Walitumia dakika kumi tu kumaliza kula, kisha wote kwa pamoja wakainuka na kwenda kukodisha pikipiki iliyowafikisha kijijini Mkalama.

Safari hii walifikishwa hadi nyumbani kwao kabisa. Walishuka kwenye pikipiki kisha wakapiga hatua za taratibu huku nyuso zao zikiwa zimepambwa na tabasamu pana. Bahati nzuri bibi alikuwa nje ameketi kibarazani.

Bibi alipowaona, alionekana kuukunja uso wake. Hata Chris alipojaribu kutabasamu, bado bibi aliendelea kukunja uso wake.

Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia hapa hapa
 
SEHEMU YA 23



ILIPOISHIA...Bibi alipowaona, alionekana kuukunja uso wake. Hata Chris alipojaribu kutabasamu, bado bibi aliendelea kukunja uso wake.
SASA ENDELEA...

HAKUaliyejua kilichokuwa moyoni mwa bibi, hakuwa ameukunja uso wake kwa hasira. Uso ulikunjamana kwa mshangao wa kumuona mjukuu wake sasa alifikia uamuzi sahihi wa kuachana na ukapera.

Chris na baba yake mdogo walipiga hatua za taratibu kumfuata bibi. Shamakala alikaa pembeni, bibi akawasogelea, wakakutana katikati. Alichokifanya bibi ilikuwa ni kuinama kidogo.

Haraka Shamakala akamwonyesha Laura ishara kuwa apige magoti chini. Akafanya hivyo. Bibi akamshika mkono Chris. Akatema mate kidogo mkononi mwake kisha akampaka Chris usoni.

Akamsogelea Laura, akamshika mikono yote miwili na kumwonyesha ishara asimame. Akafanya hivyo; akamvutia kwake na kumkumbatia, kisha akamtemea mate kidogo kwenye paji lake la uso.
Laura akatabasamu!

Kwao ilikuwa heshima kubwa sana, kutemewa mate na bibi, ilimaanisha baraka na kukubalika katika familia. Bibi akamshika mkono na kumwongoza hadi sebuleni, kwenye nyumba ile ya zamani ya tembe.
“Karibu sana mjukuu wangu,” bibi akamkaribisha Laura.

“Ahsante bibi.”
Tayari kifungua kinywa kilikuwa kimeshaandaliwa na mke wa Shamakala. Chai ilitengwa na vitafunwa vya maboga na mahindi ya kuchemsha. Wakaketi kwenye jamvi na kuanza kula. Wanaume walikula nje, wanawake ndani.

Ilikuwa siku mpya kwa Chris. Siku ya utambulisho wa ‘Laura wa Kijijini!’. Ukweli wa mambo ulijulikana na Laura, Chris na Shamakala pekee.

***
Moto ulikuwa unawaka huku moshi ukitoka. Ulikuwa usiku wa mbalamwezi. Watu wawili walikuwa wameuzunguka moto uliowashwa kwa kutumia kinyesi cha ngo’mbe. Ndani ya moto huo kulikuwa na karanga zikichomwa.

Kazi yao ilikuwa ni kuchomoa na kuendelea kula taratibu. Hapakuwa na mazungumzo. Muda kidogo bibi alifika.

“Hivi huyu msichana ni wa hapa Mkalama kweli?” bibi akamwuliza Chris.
“Hapana bibi. Ni kutoka Mpambala kama tulivyokuambia,” Chris akajibu.
“Lakini mbona hafahamu kinyumbani?”

“Bibi hajakulia hapa, wazazi wake walihamia Mwanza muda mrefu sana, tangu akiwa mdogo, amesomea huko na sasa hivi anamalizia masomo yake Singida Mjini ndiyo maana hajui vizuri kinyumbani. Ni kama mimi tu.”

“Hapo sawa.”
“Vipi lakini bibi, umegundua tatizo lolote kutoka kwake?”
“Tatizo? Hapana... ni msichana mzuri sana, mchapakazi na anayejua kujituma. Hana tatizo kabisa. Naweza kusema kwamba, mjukumuu wangu pale umepata mke sahihi.”

“Ahsante sana bibi.”
“Sasa lini mipango yako?”
“Bado kidogo, nasubiri amalizie masomo yake tu. Amebakiza miezi sita. Hatutakuwa na muda wa kusubiri zaidi. Akimaliza kinachofuata ni ndoa.”

“Sawa. Nyie endeleeni kuota moto lakini chakula kipo tayari, sasa hivi kinakuja.”
“Sawa bibi.”

***
Siku tatu zilitosha kabisa kwa Laura kuthibitishwa kuwa mke mtarajiwa wa Chris. Bibi alishatoa baraka zote. Ilikuwa furaha kubwa sana kwao. Waliagana wakiwa wenye furaha sana.

“Karibu kwenye ukoo wetu mjukuu wangu, hakuna atakayepinga uamuzi huu. Hata kama nikifika leo, kabla ya ndoa yenu, watu wote wanaonihusu watambue kuwa nimeridhia ndoa yenu,” akasema bibi.
“Ahsante sana bibi, nimefurahi sana kusikia hivyo,” Chris akasema.

Chris na Laura wakaondoka. Walikwenda hadi kituoni ambapo walichukua pikipiki iliyowapeleka moja kwa moja hadi mji mdogo wa Ibaga. Walifikia kwenye gesti ileile, Sayuni.

Walipoingia tu chumbani, wote walikumbatiana kwa furaha ya ushindi. Laura machozi yalimtoka kama maji yanavyotiririka kwenye mfereji uliopo bondeni.

“Tulia mpenzi, najua ni kiasi gani una furaha moyoni mwako. Ni furaha yetu sote na ni haki yetu kufurahi,” akasema Chris.

“Sikutegemea kama mambo yangeisha kwa wepesi kiasi hiki.”
“Najua lakini usijali. Sasa tumebakiza eneo moja tu. Nyumbani kwenu. Lazima hili jambo lijulikane mpenzi wangu kama kweli tuna lengo la kuoana. Kuna kitu lazima kifanyike mpenzi.”

“Ni kweli baba, nakuamini kwa mawazo yako, tunaanzia wapi?”
“Nashauri tukitoka hapa, wewe usikae kabisa mjini, nenda moja kwa moja Mwanza, kazungumze na wazazi wako kuhusu hili suala ili nao pia wawe wanajua.

Maadamu tunapendana na bibi amesharidhia, naamini ni jambo jepesi sana kumhadaa mzee Shila!”
“Kweli dear?”“Kabisa!”“Sawa.”

Ikawa asubuhi nyingine yenye kupendeza zaidi. Furaha yao haikubaki mioyoni mwao pekee, ilitoa msukumo mkali na kuchemsha damu za miili yao. Wote wakawaka!
Walijua namna ya kukitumia chumba kile vizuri kabisa!

Usikose leo saa moja usiku hapa hapa
 
SEHEMU YA 24



ILIPOISHIA...Furaha yao haikubaki mioyoni mwao pekee, ilitoa msukumo mkali na kuchemsha damu za miili yao. Wote wakawaka! Walijua namna ya kukitumia chumba kile vizuri kabisa!
SASA ENDELEA...
ILIONEKANA kama ni siku mpya kwao. Ilikuwa kama ndiyo kwanza wamekutana kwa mara ya kwanza katika mazingira waliyokuwa asubuhi hiyo.
Kila mmoja alijitahidi kumfanya mwenzake aone hakukosea kuwa naye katika muunganiko huo. Walionyeshana kazi!
Asubuhi hiyo upepo ulipuliza kwa kasi na kukifanya chumba kiwe baridi kabisa kama vile waliwasha kiyoyozi!
Hawakuhitaji blangeti! Wenyewe walitosha kwa kila kitu. Wote wakamiminiana misifa, ahadi kibao zikawatoka vinywani mwao.
Waliwaza ndoa tu!
Walishinda siku nzima ndani ya chumba hicho. Jioni, Chris alilazimika kuondoka na kurudi Mkalama. Mazungumzo ya usiku huo yaliendelea kuwa yaleyale. Laura alitawala.
“Mjukuu wangu, usiache kumuoa huyo msichana. Ni mzuri na anakufaa kwa maisha yako,” alisema bibi.
“Usijali bibi, hilo nakuahidi. Halafu kesho ndiyo narudi Dar. Najua unataka kusema kitu... bibi kazi nyingi lazima niondoke ila nitakuacha vizuri,” akasema Chris akitoa bahasha ya khaki na kumkabidhi.
“Ni laki moja bibi, tena nimezichenji kabisa. Zipo noti za elfu mbilimbili, najua hizi zitakusaidia mpaka siku nitakapokuja tena huku kijijini.”
Bibi aliachia mdomo wazi kwa furaha. Alisimama kwa tabu na kumkumbatia mjukuu wake.
“Mungu akubariki mume wangu, kwenye riziki zako kuongezeke,” akasema bibi.
“Ahsante sana bibi, nashukuru sana.”
Chris aliachana na bibi, akatenga muda wa kutosha kuzungumza na baba yake mdogo, Shamakala. Kama ilivyokuwa kwa bibi, ndivyo alivyofanya kwa Shamakala.
Alimpatia kiasi cha shilingi laki moja kama ahsante ya mambo yote aliyomsaidia.
“Kuondoka?” akauliza Shamakala.
“Kesho.”
“Sasa mwenzako?”
“Nimeshampa maelekezo, nimemwambia mhudumu wa pale amwamshe usiku saa tisa, hata mimi nitampigia. Huyo atamsaidia kumpakia kwenye gari ambapo atanikuta kituoni Mkalama.”
“Wazo zuri.”
Uzuri ni kwamba, gesti aliyokuwa amefikia Laura ilikuwa barabarani kabisa. Ilikuwa ni kiasi cha kuamshwa na kuwa barabarani mapema.
Kwa kawaida, magari ya kwenda mjini hutoka kituo cha Ibaga, usiku wa saa tisa na nusu. Kila siku kulikuwa na gari moja tu, likikukuacha, inabidi usibiri mpaka kesho yake au ukodi pikipiki, gharama yake wengi huikimbia.
Usafiri wa kutokea Ibaga, huwa ni kwenda Singida Mjini, Arusha kupitia Hydom, Igunga na Meatu kwa magari tofauti. Jambo hilo Laura alijulishwa mapema na mpenzi wake, kwa hiyo alijiandaa!
***
Chris alidamka mapema sana. Saa nane na nusu, tayari alikuwa macho. Haraka akampigia Laura ambaye alipokea na kumjulisha kuwa ameshaamka muda mrefu uliopita.
Alijiandaa haraka kisha akatoka na kwenda kumgongea baba yake mdogo, ambaye alitoka nje haraka. Tayari ilikuwa nimeshafika saa tisa kamili usiku.
Kwa msaada wa tochi, waliweza kutembea taratibu kuelekea barabarani. Walitumia robo saa kufika eneo hilo. Ilipotimia saa kumi kasorobo usiku, mlio wa gari ulianza kusikika kwa mbali, walikuwa na uhakika kuwa basi la kwenda mjini lilikuwa linakaribia kufika.
“Gari hilo linakuja,” akasema Chris.
“Ni kweli, ndiyo mida yake hii. Mimi nakutakia kila la kheri, hakikisha unatimiza yote tuliyokubaliana.”
“Sawa baba mdogo, nakutegemea.”
Basi lilisimama mbele yao, Chris akaingia. Hakupata shida kujua alipokuwa amekaa mpenzi wake, maana tayari alikuwa ameshakata tiketi mapema.
“Pole na usingizi mpenzi,” akasema Chris.
Laura akatabasamu, akamjibu: “Ahsante.”
Ni kama alikuwa anasubiri shuka katikati ya usiku wenye baridi kali. Alijitupa kifuani mwa Chris, akatulia. Robo saa baadaye, alikuwa ameshapitiwa na usingizi.
Alishtuka walipofika Iguguno! Tayari kulikuwa kumekucha! Muda mfupi baadaye walishuka Singida Mjini. Hapo ndipo walipoachana kwa majonzi mazito.
Chris alipanda basi lililotoka Kahama kwenda Dar na Laura akapanda basi lililotoka Dodoma kwenda Mwanza. Walishindwa kuficha hisia zao, muda mfupi kabla hawajaachana, walikumbatiana kwa muda mrefu. Kila mmoja alimhitaji mwenzake.
Mapenzi matamu kiasi gani?
Itaendelea?
 
SEHEMU YA 25


ILIPOISHIA...WALISHINDWA kuficha hisia zao, muda mfupi kabla hawajaachana, walikumbatiana kwa muda mrefu. Kila mmoja alimhitaji mwenzake.
Mapenzi matamu kiasi gani?
SASA ENDELEA...
WA kwanza kuingia kwenye basi alikuwa Chris aliyeingia kwenye Basi la NBS. Chris alitoa kichwa dirishani, akampungia mkono Laura, naye akafanya hivyo. Chris alisisimka alipoona mashavu ya mpenzi wake yakitiririsha machozi!
Hakuweza kuvumilia zaidi, akarudisha kichwa chake ndani kisha haraka akachukua simu yake na kumwandikia ujumbe uliosomeka: “Usilie mama, unanifanya nijisikie vibaya. Najua unanipenda sana Laura, nakupenda pia!”
“Najua Chris, lakini maumivu. Nimekuzoea sana, kwa siku chache nilizokaa nawe kijijini zimekuwa za tofauti sana kwangu, nahisi kama tayari umeshanioa. Nakupenda sana.”
“Nakupenda pia.”
Waliendelea kuwasiliana kwa muda mrefu. Tayari Laura alishangia kwenye Basi la Mohammed lililotokea Dodoma kuelekea Mwanza.
Safari nzima kwao ilikuwa yenye furaha kubwa. Ni kama walikuwa wakisafiri umbali mfupi tu kutokana na kuwekana karibu kwa mawasiliano.
Ahadi yao ilikuwa moja tu; ndoa. Wote waliazimia kuungana katika ndoa takatifu.
***
Chris aliingia Dar es Salaam saa mbili usiku akiwa amechoka sana. Alichokifanya ni kuchukua teksi iliyompeleka nyumbani kwake Kijitonyama.
Kweli alikuwa na hamu sana ya kukutana na wasanii wenzake akina Jaybee, Ramsey na Chika lakini kwa uchovu aliokuwa nao ilikuwa lazima apumzike kwanza.
Alijimwagia maji, akatafuta chakula kwenye mgahawa wa jirani, kisha akarudi nyumbani alipofungua jokofu lake na kutoa kinywaji. Ilikuwa lazima ajitoe uchovu kidogo!
Bia tatu zilitosha kumwondolea uchovu aliokuwa nao awali. Akajilaza kitandani akiendelea kutafakari siku yake mpya itakayofuata!
***
Mapokezi ya Laura nyumbani kwao Nyakato, Mwanza yalikuwa mazuri sana. Usiku mzima alikuwa akizungumza na ndugu zake ambao hakuonana nao kwa muda mrefu alipokuwa masomoni.
Sebule yao ilichangamka sana. Mpaka usiku sana, wengi walikuwa wameshaingia vyumbani kulala, wakabaki Laura na mama yake tu.
Hapo ndipo Laura alipoamua kutumia nafasi hiyo vizuri kwa ajili ya kuzungumza na mama yake. Walikuwa wawili tu.
“Mama kuna kitu nataka kukuambia!” akasema Laura akimwangalia mama yake usoni.
“Niambie mwanangu, ni nini tena hicho?”
“Nimepata mchumba... anataka kunioa.”
“Unasema?”
“Nimepata mchumba mama.”
“Ni nani?”
“Yupo Dar.”
“Umekutana naye wapi?”
“Singida.”
“Naye ni mwanafunzi?”
“Hapana mama. Nipe nafasi nikueleze vizuri, tatizo una haraka sana. Kwa nini hutaki kunisikiliza kwanza? Halafu tatizo si huyo mvulana, kuna shida kidogo kwa upande wa wazazi wake.”
“Shida kivipi?”
“Wazazi wake wamemwambia lazima aoe kijijini lakini sisi tumependana na yupo tayari kunioa.”
“Hata kama mmependana na yupo tayari kukuoa, itawezekana vipi wakati wazazi wake hawataki?”
“Kuna mpango tumeshafanya. Hivi ninavyoongea na wewe, tayari nimeshafika hadi kijijini kwao na wamenikubali.”
“Mh!”
“Usigune mama, ngoja nikueleze vizuri.”
Laura alimsimulia mchezo mzima ulivyokuwa, jinsi jambo hilo alivyoshirishwa baba yake mdogo na Chris, Shamakala, bila bibi na ndugu zake wengine kufahamu.
“Mh! Una hatari wewe mtoto. Enhee, huyo kijana mwenyewe ni nani hasa? Na kweli umri wake unamruhusu kuoa?” akauliza mama Laura.
“Hana shida, ni mtu mzima. Ana miaka 35 sasa, nayaamini maamuzi yake mama.”
“Anaitwa nani?”
“Ni Dk. Chris yule msanii wa filamu, kwa sababu ni maarufu najua utakuwa unamfahamu,” akasema Laura akitabasamu.
Alitegemea mama yake angefurahia jambo hilo, alichokutana nacho kilikuwa tofauti kabisa:
“Unasemaje wewe?” mama Laura akasema kwa sauti ya ukali sana.
“Vipi tena mama?”
“Sitaki matatizo na baba yako, unataka kuolewa na hao wahuni wa filamu? Huo ujinga wako uishie hapahapa,” alisema mama Laura kwa hasira kisha akaondoka sebuleni na kumuacha Laura peke yake!
Huzuni mpya!
Itaendelea.
 
SEHEMU YA 26


ILIPOISHIA...“Sitaki matatizo na baba yako, unataka kuolewa na hao wahuni wa filamu? Huo ujinga wako uishie hapahapa,” alisema mama Laura kwa hasira kisha akaondoka sebuleni na kumuacha Laura peke yake!
Huzuni mpya!
SASA ENDELEA...
ALIHISI moyo wake kama umeingiwa na ubaridi mkali, Laura alichanganyikiwa kwa hakika. Kwa urafiki wake na mama yake, alijua jambo lile angelipokea kwa urahisi sana.
Kinyume na matarajio hayo, mama yake aligeuka mbogo! Maneno yake yakamchanganya sana. Wasanii ni wahuni? Aliumia sana kichwani mwake.
“Wasanii ni wahuni? Mbona simwelewi mama lakini? Labda ni kweli ni wahuni lakini si kwa Chris wangu. Chris si mhuni. Kwanza ni daktari. Mama lazima akubaliane na mimi.
“Siwezi kukubali kuishi na mtu mwingine tofauti na Chris. Sijamwelewa mama hata kidogo. Hapo nitapingana naye,” aliwaza Laura.
Furaha aliyokuwa nayo moyoni mwake iliyeyuka ghafla. Alimtegemea mama yake ndiye angemuunga mkono na ugomvi na baba yake usingekuwepo lakini imekuwa tofauti.
Aliinuka kwa hasira na kwenda zake chumbani kwake. Hakufanya chochote zaidi ya kujitupa kitandani na kulala kama alivyotoka sebuleni.
Kitu pekee alichokumbuka ilikuwa ni kuchukua simu yake. Akaiweka karibu yake, pembeni ya mto. Alitakiwa kupunguza mawazo yake, mtu pekee ambaye angemsaidia kupunguza mawazo yaliyokuwa yamemvaa kwa kasi muda ule alikuwa ni mpenzi wake tu – Chris.
Lakini vipi kama angemwambia Chris kuhusu mama yake kugoma?
“Itakuwa tatizo lingine, sitakiwi kumwambia chochote,” akawaza.
“Pia sitakiwi kumpigia,” akawaza tena.
Sauti ya Chris pengine ingeweza kuwa dawa ya usingizi na kumpunguzia maumivu makali ya moyo lakini kwa namna hali ilivyokuwa, aliona ni bora aache kumpigia.
Alipitisha azimio hilo.
Akaamua kulala bila kuzungumza na mpenzi wake; si juu ya tukio lililotokea muda mfupi uliopita, bali hakutaka kuzungumza naye kitu chochote.
Akiwa anajitahidi kuubembeleza usingizi, simu yake iliita. Haraka akatupa macho yake kwenye kioo cha simu yake, akakutana na jina la ‘My Love’.
Alikuwa ni Chris. Alisita kupokea. Alishindwa kuelewa kama angepokea angezunguza nini na mpenzi wake. Habari alizokuwa nazo, hazikuwa nzuri hata kidogo. Ni habari ambazo asingependa kuzisikia kabisa.
“Lakini sijui anataka kuniambia nini...acha tu nimpokelee,” mwisho akapitisha uamuzi huo.
Akapokea.
“Hello darling,” ilikuwa sauti ya Chris.
“Niambie mpenzi wangu,” Laura alijitahidi kuzungumza kwa upendo akiweka pembeni tatizo lilitokea.
“Nimeshindwa kulala kabisa bila kuzungumza na wewe. Nimeshtuka muda huu mpenzi, nikakukumbuka,” akasema Chris.
“Kweli mpenzi wangu?”
“Kabisa dear.”
“Nashukuru kusikia hivyo, wazee hawajambo?”
“No! Kwa muda niliofika, ilikuwa vigumu sana kwenda nyumbani. Nipo kwangu Kijitonyama. Vipi huko, wewe?”
“Hawajambo.”
“Umewagusia suala letu?”
“Hapana mpenzi, nimeona nilale kwanza, niwaambie kesho. Ulipenda iwe leo mpenzi wangu?”
“Kabisa.”
“Mh! Una haraka? Unatamani hata hiyo ndoa yenyewe ingekuwa kesho. Mimi ni wako tu mpenzi, wala usiwe na wasiwasi wowote. Mimi ni mali yako.”
“Kweli?”
“Kwa nini usiamini maneno yangu?”
“Nakuamini mpenzi.”
“Nashukuru kusikia hivyo, nakutakia usiku mwema, nitakutafuta kesho mpenzi wangu sawa.”
“Sawa baba.”
“Usiache kunijulisha chochote kitakachotokea kuhusu mambo yetu.”
“Sawa mpenzi wangu.”
Wakakata simu zao.
Kitendo cha kukata tu simu, ilikuwa kama ndiyo tiketi ya Laura kuanza kulia. Alilia kuliko kawaida. Aliumizwa sana na maneno ya Chris ambaye hakujua kilichokuwa kikiendelea Mwanza!
Ukweli ni kwamba, Chris hakutakiwa kwa sababu tu alikuwa msanii wa filamu.
Kwa mama yake na Laura, msanii wa filamu ni mhuni tu, asiye na sifa ya kummiliki mwanaye.
Ulikuwa mwiba mkali sana kwa Laura ambaye aliugulia mwenyewe. Hakuwa na wa kumwambia kuhusu kilichokuwa kikiendelea.
Alilia sana.
Mto wote ulikuwa chapachapa! Ulilowanishwa na machozi ya Laura. Alikuwa na jeraha kubwa sana moyoni mwake. Jeraha bichi kabisa. Jeraha linalovuja damu!
***
“Niambie ulipofikia,” mzee Shila, baba yake na Chris alimwambia mwanaye jioni hiyo walipokuwa wamepumzika bustanini.
Siku nzima Chris aliamua kushinda nyumbani kwao, Mbezi Beach. Hakwenda kazini wala hakukutana na rafiki zake. Aliamua kujipumzisha na ndugu zake nyumbani.
“Hatua nzuri baba. Bibi ameshamaliza kila kitu. Imebaki ndoa tu,” akasema Chris.
“Kweli?”
 
SEHEMU YA 27


ILIPOISHIA...“Hatua nzuri baba. Bibi ameshamaliza kila kitu. Imebaki ndoa tu,” akasema Chris.
“Kweli?”
SASA ENDELEA...

MOYONI Chris alikuwa na woga ambao hauna kipimo, alijua wazi jibu ambalo angemjibu baba yake, lilikuwa la uongo lakini alilazimika kufanya hivyo kwa sababu ya kutimiza lengo lake.

Ni kweli alikuwa akidanganya lakini hata baba yake hakumtendea haki kumchagulia mahali na mtu wa kumuoa. Jambo hilo liligoma kabisa kuingia ubongoni mwake.
“Niamini baba, nasema kweli kabisa.”

Chris aliyatuliza macho yake usoni mwa baba yake, aliona milima midogomidogo iliyokuwa usoni mwa Mzee Shila ikiwa kama inaporomoka! Makunyanzi yake yakayeyuka taratibu.

Tabasamu likachanua!
Alitamani sana kuona mwanaye akioa! Siyo kuoa tu; aoe msichana kutoka kijijini! Kilichoendelea Mwanza, hakuna aliyejua!
Si Chris wala baba yake, mzee Shila.

Ni fumbo!
“Ahsante sana mwanangu. Naamini hujaniangusha, namwamini sana baba yako mdogo, najua hawezi kufanya makosa. Vipi, umeweza kuja na picha yake?”

“Hapana baba, ungependa kumuona?” akauliza Chris akitabasamu.
“Kabisa...natamani kumuona.”
“Nitafanya mpango wa picha, ngoja nifanye mawasiliano nitakujulisha.”
“Sawa mwanangu.”

Furaha ya mzee Shila ilikuwa wazi kabisa, ugomvi wa kwanza na mwanaye ulikuwa umeisha, ulibaki mmoja tu; kuigiza! Kwa mzee Shila, kuigiza ilikuwa ni uhuni na kujidhalilisha.

Kila alipokutana na skendo za wasanii mbalimbali katika magazeti, alijua kwa sababu mwanaye pia ni msanii, lazima angekuwa na tabia kama hizo. Siku zote alipata tabu sana kumfanya Chris akubaliane naye.

Hata hivyo, kwa hatua hiyo ya awali, kwa mzee Shila yalikuwa mafanikio makubwa. Moyoni akasema: “Acha kwanza hili lipite, mengine yataendelea. Hanishindi, huyu ni nimemzaa mwenyewe.”

Ilikuwa furaha kubwa sana kwa familia hiyo, siku nzima walishinda wakiwa wenye amani, kitu kikubwa kilichojadiliwa, ilikuwa ndoa ya Chris na Njile (Laura).

“Sikupatii picha mwanangu...siku hiyo, nakuona umevaa suti yako safi na mkeo amependeza, ukumbi mzima unasubiri kusikia utambulisho wa wazazi wako. MC sasa anasema: Baba mzaa chema, Profesa Shila naomba usimame watu wakuone....” alisema mzee Shila akicheka.

“Hatimaye Dk. Chris ameoa, ah! Mwanangu kwa kweli itakuwa furaha kubwa sana kwetu,” akadakia mama yake.

Hakutaka kabisa vurugu siku hiyo, vikao vyake vya pombe na rafiki zake akina Jaybee, Ramsey na Chika, alivisamehe kwa siku hiyo.
***
Usiku mzima, Laura hakupata usingizi. Mawazo yake yalikuwa kwa Chris ambaye sasa ndoto za kuoana zilikuwa zimeanza kuyeyuka. Tegemeo pekee wa kumsaidia katika hilo alikuwa ni mama yake ambaye hakutaka kuwa upande wake kabisa.

Asubuhi aliamka mapema na kukaa sebuleni akijifanya anaangalia taarifa ya habari ya Runinga ya ITV. Baba yake, mzee Moses Ngeleja alitoka akiwa ameshajiandaa kwenda kazini.
Alipomuona mwanaye sebuleni, alitabasamu...

“Morning dad!” Laura akasalimia kwa Kimombo.
“Morning to you daughter. Vipi za masomo?”
“Nzuri tu baba, nimebakiza kipindi kifupi cha mwisho nimalize masomo kabisa.”
“Ni kweli. Naona Singida si kubaya, kumekupenda sana mwanangu.”
“Mh! Baba bwana...”

“Laura, acha mimi nikimbie kazini, jioni nitawahi kurudi kwa ajili yako. Nina mengi ya kuzungumza na wewe mwanangu.”

Hayo yalimfanya Laura aamini kuwa mpaka muda huo, mama yake alikuwa hajamwambia chochote baba yake.
“Ila dad, natamani uniruhusu nije nikuone ofisini kwako mchana, naona jioni ni mbali, nami nina yangu ya kuzungumza na wewe.”
“Sawa...karibu mwanangu!”

Mzee Ngeleja akatoka nje. Akaingia kwenye gari yake aina ya Toyota VX, akaelekea kazini kwake, katikati ya Jiji la Mwanza, Jengo la Kaijage ilipokuwa ofisi yake.
***
Laura hakutaka kuzungumza na mama yake chochote kuhusiana na suala la Chris. Hata mchana alipotoka kwenda ofisini kwa baba yake, hakumwambia ukweli, zaidi ya kumdanganya kuwa anakwenda kumuona rafiki yake.

Akiwa mbele ya meza ya baba yake, Laura alijikaza na kumweleza baba yake ukweli: “Baba nimekua sasa, nimempata mkweo. Kuna mwanaume anataka kunioa.”
Mzee Ngeleja akatabasamu!

“Habari njema kiasi gani binti yangu. Vipi, umeshazungumza na mama yako kuhusu hili?” akasema mzee Ngeleja akiachia tabasamu mwanana usoni mwake.

Itaendelea
 
SEHEMU YA 28


ILIPOISHIA...
“Habari njema kiasi gani binti yangu. Vipi, umeshazungumza na mama yako kuhusu hili?” akasema mzee Ngeleja akiachia tabasamu mwanana usoni mwake.
SASA ENDELEA...

USO wa Laura ulisawagika. Alionekana dhahiri kuwa na hofu ya ghafla. Mabadiliko yake yalikuwa wazi. Mzee Ngeleja alijua kwa vyovyote vile, kuna jambo lilimsumbua mwanaye.
“Laura...” Mzee Ngeleja akaita.
“Abee baba.”
“Vipi, mbona kama umebadilika kidogo?”
“Hapana.”

“Mh!” mzee Ngeleja akaguna.
“Mbona unaguna baba?”
“Mimi nakujua vizuri mwanangu, kuna kitu unanificha.”
“Hakika hakuna kitu baba.”
“Sawa, hebu turudi katika suala lako. Umeshazungumza na mama yako?” akamwuliza tena.
“Yaani baba hiyo ndiyo sababu iliyonifanya nije kuzungumza na wewe huku kazini kwako.”
“Kivipi?”

“Jana usiku nilijaribu kumweleza juu ya jambo hilo lakini cha ajabu, akapingana na mimi. Amesema hataki kusikia hizo habari.”

“Hawezi kusema hivyo ikiwa hana sababu. Hebu kuwa wazi, niambie tatizo ni nini?”
“Ukweli baba tatizo ni juu ya mwanaume mwenyewe. Unajua baba, huyo jamaa anayetaka kunioa ni msanii wa filamu, lakini siyo mhuni kama mama anavyofikiri.
“Ni msomi, tena daktari na anafanya kazi hospitalini kabisa ila anafanya filamu kama sehemu yake ya kujifurahisha tu.”

“Ni nani?”
“Jina lake halisi ni Christopher Joseph Shila, kwenye kazi zake za filamu anajiita Dk. Chris. Tumechunguzana kwa muda mrefu sana, namjua vizuri baba. Nimewahi kufika hadi kijijini kwao.
“Ni mwanaume sahihi kabisa baba, lakini mama ananikataza kwa vile tu ni msanii wa filamu, ndiyo maana nimeamua kuja kukushirikisha hili suala ili unisaidie,” alisema Laura mfululizo, baba yake akiwa kimya akimsikiliza.
“Ok! Nimekuelewa vizuri sana. Umesema nyumbani kwao ulikwenda. Ilikuwaje?”

“Hiyo ni habari nyingine baba, unajua kwao, wazazi wake nao walimpa masharti kuhusu mwanamke wa kuoa. Wakamwambia ni lazima mkewe atokee kijijini tena vijiji vya nyumbani kwao. Lakini kwa sababu sisi tunapendana ikabidi atumie mbinu nyingine ili kuwafanya wazazi wake waamini kuwa mimi ni wa kijijini.”
“Mkafanyaje sasa?”

Laura akamsimulia kila kitu kilivyokuwa bila kumficha chochote. Mzee Ngeleja alikuwa kimya akimsiliza mwanaye ambaye hakuna alichodanganya. Alionekana kumuelewa binti yake.
“Kwa hiyo huyo kijana anaishi Dar?”
“Ndiyo.”

“Na wazazi wake?”
“Dar pia.”
“Anaishi nao?”
“Hapana. Chris yeye amepanga kwake.”
“Hoja za mama yako zinaweza kuwa na maana lakini na wewe pia maelezo yako ni ya msingi. Sitaki kuwa dikteta katika hili. Kitu pekee ambacho nakitaka, ni kukutana na huyo kijana kwanza. Anaweza kuja hapa Mwanza nikaonana naye?” akasema mzee Ngeleja.
Laura akashtuka sana!

Lilikuwa wazo zuri sana, kwa jinsi baba yake alivyozungumza, alionekana wazi kukubaliana naye lakini alitaka kuonana na Chris ili wazungumze na kufahamiana.
“Anaweza baba, hilo halina shida.”
“Sawa, nadhani hili tumemaliza, nenda zungumza naye, mpange siku ya kuja. Iwe mapema kabla hujarejea chuoni Singida.”

“Sawa baba, kazi njema.”
“Ahsante binti yangu.”
Laura akaondoka ofisini kwa baba yake, angalau kichwani akiwa amepunguza mawazo. Sasa alikuwa na mwanga kuwa Chris angeweza kuwa mwanaume wa maisha yake.

***
Aliposhuka chini ya Jengo la Kaijage, kitu cha kwanza Laura kufanya ilikuwa ni kumpigia Chris. Alipiga simu mara moja tu – ikapokelewa.
“Baby vipi?” Laura aliongea.
“Poa, mambo?”
“Safi kabisa.”

“Afadhali umenipigia, nilikuwa nakupigia sasa hivi.”
“Kuna nini tena?”
“Nilitaka unitumie picha zako kwenye WhatsApp. Nilizungumza na wazee kuhusu wewe, wanatamani kukuona japo katika picha tu,” akasema Chris.
“Mh! Haina shida mpenzi wangu, mimi nina kubwa zaidi.”
“Kubwa gani?”

“Ni stori ndefu sana mpenzi lakini kikubwa, baba yangu anataka kuonana na wewe. Nimeongea naye kwa kirefu sana kuhusu mimi na wewe!” akasema Laura.
“Dah! Kwani hukuzungumza na mama?”
“Mama ndiyo amesababisha yote hayo lakini hakuna tatizo, dalili ni nzuri,” akasema Laura.
“Unamaanisha nini?”

“Mama alianza kuleta vikwazo ndiyo maana nikaamua kumwambia baba, hivi tunavyoongea nimetoka ofisini kwake,” akasema Laura kwa sauti ya taratibu kabisa.
Chris alishtuka sana!

Itaendelea
 
SEHEMU YA 29

ILIPOISHIA...
“Habari njema kiasi gani binti yangu. Vipi, umeshazungumza na mama yako kuhusu hili?” akasema mzee Ngeleja akiachia tabasamu mwanana usoni mwake.
SASA ENDELEA...

USO wa Laura ulisawagika. Alionekana dhahiri kuwa na hofu ya ghafla. Mabadiliko yake yalikuwa wazi. Mzee Ngeleja alijua kwa vyovyote vile, kuna jambo lilimsumbua mwanaye.
“Laura...” Mzee Ngeleja akaita.
“Abee baba.”
“Vipi, mbona kama umebadilika kidogo?”
“Hapana.”

“Mh!” mzee Ngeleja akaguna.
“Mbona unaguna baba?”
“Mimi nakujua vizuri mwanangu, kuna kitu unanificha.”
“Hakika hakuna kitu baba.”
“Sawa, hebu turudi katika suala lako. Umeshazungumza na mama yako?” akamwuliza tena.
“Yaani baba hiyo ndiyo sababu iliyonifanya nije kuzungumza na wewe huku kazini kwako.”
“Kivipi?”

“Jana usiku nilijaribu kumweleza juu ya jambo hilo lakini cha ajabu, akapingana na mimi. Amesema hataki kusikia hizo habari.”

“Hawezi kusema hivyo ikiwa hana sababu. Hebu kuwa wazi, niambie tatizo ni nini?”
“Ukweli baba tatizo ni juu ya mwanaume mwenyewe. Unajua baba, huyo jamaa anayetaka kunioa ni msanii wa filamu, lakini siyo mhuni kama mama anavyofikiri.
“Ni msomi, tena daktari na anafanya kazi hospitalini kabisa ila anafanya filamu kama sehemu yake ya kujifurahisha tu.”

“Ni nani?”
“Jina lake halisi ni Christopher Joseph Shila, kwenye kazi zake za filamu anajiita Dk. Chris. Tumechunguzana kwa muda mrefu sana, namjua vizuri baba. Nimewahi kufika hadi kijijini kwao.
“Ni mwanaume sahihi kabisa baba, lakini mama ananikataza kwa vile tu ni msanii wa filamu, ndiyo maana nimeamua kuja kukushirikisha hili suala ili unisaidie,” alisema Laura mfululizo, baba yake akiwa kimya akimsikiliza.
“Ok! Nimekuelewa vizuri sana. Umesema nyumbani kwao ulikwenda. Ilikuwaje?”

“Hiyo ni habari nyingine baba, unajua kwao, wazazi wake nao walimpa masharti kuhusu mwanamke wa kuoa. Wakamwambia ni lazima mkewe atokee kijijini tena vijiji vya nyumbani kwao. Lakini kwa sababu sisi tunapendana ikabidi atumie mbinu nyingine ili kuwafanya wazazi wake waamini kuwa mimi ni wa kijijini.”
“Mkafanyaje sasa?”

Laura akamsimulia kila kitu kilivyokuwa bila kumficha chochote. Mzee Ngeleja alikuwa kimya akimsiliza mwanaye ambaye hakuna alichodanganya. Alionekana kumuelewa binti yake.
“Kwa hiyo huyo kijana anaishi Dar?”
“Ndiyo.”

“Na wazazi wake?”
“Dar pia.”
“Anaishi nao?”
“Hapana. Chris yeye amepanga kwake.”
“Hoja za mama yako zinaweza kuwa na maana lakini na wewe pia maelezo yako ni ya msingi. Sitaki kuwa dikteta katika hili. Kitu pekee ambacho nakitaka, ni kukutana na huyo kijana kwanza. Anaweza kuja hapa Mwanza nikaonana naye?” akasema mzee Ngeleja.
Laura akashtuka sana!

Lilikuwa wazo zuri sana, kwa jinsi baba yake alivyozungumza, alionekana wazi kukubaliana naye lakini alitaka kuonana na Chris ili wazungumze na kufahamiana.
“Anaweza baba, hilo halina shida.”
“Sawa, nadhani hili tumemaliza, nenda zungumza naye, mpange siku ya kuja. Iwe mapema kabla hujarejea chuoni Singida.”

“Sawa baba, kazi njema.”
“Ahsante binti yangu.”
Laura akaondoka ofisini kwa baba yake, angalau kichwani akiwa amepunguza mawazo. Sasa alikuwa na mwanga kuwa Chris angeweza kuwa mwanaume wa maisha yake.

***
Aliposhuka chini ya Jengo la Kaijage, kitu cha kwanza Laura kufanya ilikuwa ni kumpigia Chris. Alipiga simu mara moja tu – ikapokelewa.
“Baby vipi?” Laura aliongea.
“Poa, mambo?”
“Safi kabisa.”

“Afadhali umenipigia, nilikuwa nakupigia sasa hivi.”
“Kuna nini tena?”
“Nilitaka unitumie picha zako kwenye WhatsApp. Nilizungumza na wazee kuhusu wewe, wanatamani kukuona japo katika picha tu,” akasema Chris.
“Mh! Haina shida mpenzi wangu, mimi nina kubwa zaidi.”
“Kubwa gani?”

“Ni stori ndefu sana mpenzi lakini kikubwa, baba yangu anataka kuonana na wewe. Nimeongea naye kwa kirefu sana kuhusu mimi na wewe!” akasema Laura.
“Dah! Kwani hukuzungumza na mama?”
“Mama ndiyo amesababisha yote hayo lakini hakuna tatizo, dalili ni nzuri,” akasema Laura.
“Unamaanisha nini?”

“Mama alianza kuleta vikwazo ndiyo maana nikaamua kumwambia baba, hivi tunavyoongea nimetoka ofisini kwake,” akasema Laura kwa sauti ya taratibu kabisa.
Chris alishtuka sana!

Itaendelea leo saa moja usiku.
 
SEHEMU YA 30


ILIPOISHIA..“Ni Mkristo, sijawahi kuwa na mtoto na sina mke na sijawahi kuoa. Naamini nimejieleza vizuri kiasi mzee wangu, lakini kama utaona kuna kitu nimeacha unaweza kuniuliza,” akasema Chris.
“Ahsante sana, nimekuelewa vizuri Chris, napenda kukuita Dk. Chris. Naomba kwanza uniruhusu!”
“Ndiyo taaluma yangu mzee, ruksa kutumia.”
“Ahsante sana Dk. Chris, kwa hakika unajua kujieleza vizuri sana, nataka kukuambia kwa maelezo yako mafupi, nakuhakikishia kuwa binti yangu umempata!” akasema mzee Ngeleja.
Chris akatabasamu!SASA ENDELEA...
LAURA naye akafanya hivyo. Kwa furaha Chris alisimama na kunyoosha mkono wake kuelekea kwa mzee Ngeleja. Kitu cha ajabu ni kwamba, mzee huyo hakupokea mkono wake, zaidi akasema...
“Lakini kuna tatizo kidogo Dk. Chris.”
“Tatizo gani?” Chris akauliza haraka akionekana kushtuka sana.
Tayari matumaini ya kumpata Laura yalianza kufutika tena. Kitendo cha mzee Ngeleja ambaye ni kama alikuwa mtetezi wake kusema kuna tatizo kidogo, kulimaanisha kumkwamisha kwenye zoezi lililokuwa mbele yake.
Mzee Ngeleja alibaki kimya!
Chris alikuwa bado amesimama vilevile. Akamwuliza tena: “Kuna tatizo gani mzee wangu?”
“Tuliza moyo Dk. Chris,” akasema mzee Ngeleja akiachia tabasamu mwanana.
“Nimeshtuka sana.”
“Lazima iwe hivyo.”
“Lakini ni nini hasa?”
“Naona njia mliyotumia haikuwa sahihi. Kwa nini mliwadanganya wazazi?”
“Unamaanisha kule kijijini?”
“Ndiyo.”
“Kulikuwa hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya hivyo baba. Kumbuka msimamo wa baba yangu ulikuwa huo; kwamba lazima nioe kijijini. Laura siyo wa kijijini baba, ningefanyaje?”
Mzee Ngeleja akakaa kimya.
“Naomba utusamehe baba, lakini tulilazimika.”
“Tena baba, naomba uwe upande wetu katika hili. Sisi tunajua tunachotengeneza. Lengo letu ni zuri na najua litamfurahisha kila mmoja baadaye. Kwa sababu tumeshalianza kwa mtindo huu, naomba liishe hivyohivyo kwanza,” akadakia Laura.
“Wazo zuri sana Laura,” akasema Chris.
“Kwahiyo mnanishawishi nijiunge nanyi kusema uongo?” mzee Ngeleja akasema kwa hamaki.
“Si kwa maana hiyo baba. Lakini kama tulivyosema lengo letu ni zuri.”
Mzee Ngeleja akatulia tena.
“Sawa. Nimekubaliana nanyi, endeleeni na taratibu nyingine. Mimi kwa upande wetu huku mniachie sawa?”
“Sawa baba.”
“Basi sawa, yangu mimi yalikuwa ni hayo mwanangu Chris. Laura unaweza kumsindikiza mwenzako. Vipi ratiba yako? Utakuwa hapa leo ukiendelea kula sangara na sato au unaondoka leoleo?” akauliza mzee Ngeleja.
“Leo nipo, nina tiketi ya ndege ya kesho jioni maana sikujua mazungumzo yetu yangechukua muda gani.”
“Sawa, Laura msindikize mwenzako ili apate hoteli, maana najua kwa hapa mjini si mwenyeji.”
“Hakika baba, mimi nakwenda, ila nina zawadi yako!” akasema Chris akimkabidhi mzee Ngeleja begi dogo.
“Kuna nini humu?” akasema akitabasamu.
“Utaona ukifungua mwenyewe.”
“Ahsante sana dokta, nashukuru.”
Wakaagana.
**
Ilikuwa siku nyingine mpya kwa Chris na Laura. Waliongozana hadi hotelini ambapo mazunguzo ni kama yalianza upya kabisa. Chris hakuamini kama mambo yangekuwa rahisi kiasi kile hasa baada ya kuambiwa na Laura kuwa kulikuwa na tatizo kwa wazazi wake.
“Siamini dear,” akasema Laura.
“Siamini pia, lakini hapa mambo yanatakiwa kwenda harakaharaka kama ambavyo imepangwa. Mambo mengine yatajulikana baadaye.”
“Sawa baby.”
Chris alicharuka, Laura akasisimka. Ni kama damu zilikuwa zikiwaka moto. Ghafla walirukiana na kukutanisha ndimi zao. Kazi ya kufyonzana ikaanza. Waligalagala kitandani kwa muda mrefu kabla ya habari kuhamia kwenye upande wa kimataifa!
Wote walikuwa na uchu kama ndiyo kwanza walikuwa wamekutana siku hiyo. Jioni kabisa, Laura alirudi nyumbani kwao. Ilikuwa lazima awahi kabla baba yake hajarudi.
Chris alilala akiwa na uhakika wa kuingia kwenye ndoa na mwanamke wa maisha yake. Mwanamke ambaye alijihakikishia kumpenda kwa dhati ya moyo wake.
***
Mzee Ngeleja alirudi nyumbani akiwa na furaha sana. Alizungumza na mkewe chumbani kuhusu Chris na binti yao Laura. Mkewe hakuwa tayari kabisa kumwelewa kwa maelezo yaleyale; wasanii ni wahuni!
“Mke wangu achana na mawazo hayo, mimi nimekutana na Chris na kuzungumza naye.
Mimi ni mtu mzima, naelewa vizuri haya mambo. Yule kijana ni mtu mzuri sana, hana shida na anafaa kabisa kuoana na binti yetu,” akasema mzee Ngeleja.
Mkewe akashtuka!

Itaendelea leo leo
 
SEHEMU YA 31


ILIPOISHIA..““Mimi ni mtu mzima, naelewa vizuri haya mambo. Yule kijana ni mtu mzuri sana, hana shida na anafaa kabisa kuoana na binti yetu,” akasema mzee Ngeleja.
Mkewe akashtuka!
SASA ENDELEA...

MAMA Laura hakutegemea kuwa mumewe angeweza kuwa ameshakutana na Chris na kuzungumza naye. Kwake, Chris alikuwa kijana mhuni kwa vile tu alikuwa msanii wa filamu.
Kitendo cha kumwambia kuwa alikutana naye, kilimshangaza sana. Mama Laura alitoa macho na kumwuliza mumewe:

“Umekutana naye wapi?” akauliza kwa hamaki.
“Ofisini kwangu, leo hii amekuja Mwanza na kesho asubuhi anaondoka. Naomba ukubaliane na mimi, maana siwezi kukubali binti yangu akaolewa na kijana mpuuzi!”
Mama Laura akatulia.

Baadaye akasema: “Lakini mume wangu unapaswa kufikiri zaidi kuhusu hili. Naona kama utakuwa umeamua harakaharaka sana.”
“Hapana, mimi ni mtu mzima na nina uelewa mzuri. Najua ninachokifanya,” akasema mzee Ngeleja kwa kujiamini.

Mama Laura alikaa kimya tena. Safari hii utulivu ulikuwa wa hali ya juu zaidi.
Mzee Ngeleja akafungua lile begi na kutoa zawadi alizopewa na Chris. Kulikuwa na mashati mawili ya kitenge, saa, mkanda na tai mbili. Pia kulikuwa na doti tatu za vitenge vya gharama.

“Ona hizi ni zawadi alizotuletea. Ndiyo nafungua muda huu hapa. Chukua na vitenge vyako,” akasema mzee Ngeleja akimkabidhi mkewe.

Taratibu mama Laura akaonekana kuanza kuelewa somo, si kwa sababu ya zawadi bali utii alioanza kuhisi Chris anao.

“Nakubaliana na wewe mume wangu! Nakubali Chris amuoe binti yetu. Nimeanza kuhisi kitu tofauti sasa, bila shaka nimebadili uamuzi wangu.”
“Ahsante sana mke wangu!”

Wakakumbatiana kwa furaha. Tayari upande wa Laura hapakuwa na pingamizi. Ilibaki upande wa Chris tu.
***
Chris aliingia Dar es Salaam akiwa na matumaini mapya. Hakuwa na shaka yoyote kuhusu kumpata Laura. Alipozungumza na baba yake, alimwambia amwachie kila kitu yeye, anachotaka ni kuona anaoa!

“Zungumza na baba yako mdogo akamilishe kila kitu kuhusu ndoa. Kama mtaamua mnaweza kufunga ndoa ya kimila kijijini halafu kanisani mje mfunge huku Dar. Kutokana na majukumu yangu, namwachia jukumu hilo baba yako mdogo.

“Tafadhali lifanyike haraka sana. Mimi nimeshazungumza na marafiki zangu kuhusu ndoa yako. Wapo tayari kunisaidia. Wewe niachie mimi kila kitu, sawa?” akasema mzee Shila kwa kujiamini.
“Sawa baba, nimekuelewa!” akajibu Chris akiachia tabasamu.
Wasiwasi wa nini?
***
Siku zilikwenda haraka sana, hawakuwa na kitu cha kusubiri. Kwa kuwa Shamakala alikuwa anajua kila kitu kinachoendelea, kilichofanyika ilikuwa ni kupeleka posa kwa mzee Ngeleja.

Walilazimika kusafiri kutokea Singida mpaka Mwanza na kukamilisha zoezi la posa. Kila kitu kilikwenda sawa kabisa, posa ilikubaliwa na mahari ikapagwa. Vitu vidogovidogo vya kimila vilikamilishwa na mzee Ngeleja akawa tayari binti yake aende kufunga ndoa ya kimila kijijini.

Zoezi hilo lilifanyika bila wazazi wa pande zote mbili. Ndoa ilisimamiwa na Shamakala, baba mdogo wa Chris na wawakilishi wa mzee Ngeleja kutoka Mwanza. Baada ya hapo Laura alirudi chuoni kumalizia mitihani yake ya mwisho.

Mzee Shila alijulishwa na mdogo wake, Shamakala kuhusu mwenendo wa kila kitu kilivyokuwa kijijini. Alifurahi sana lakini kichwani mwake alijua kuwa, kijana wake alioa mwanamke wa nyumbani kwao jambo ambalo halikuwa la kweli.
***
Mipango yote ilivyokamilika, zoezi la mahari liliachwa mikononi mwa Shamakala. Yeye na washenga wa Chris ndiyo waliosafiri tena hadi Mwanza kulipa mahari kisha ikafanyika hafla fupi ya Laura kuvalishwa pete ya uchumba.

Kutokea hapo, Laura akawa mchumba rasmi wa Chris. Hadi kufikia muda huo, baba na mama wa Chris walikuwa hawajamuona Laura zaidi ya picha tu.

Mzee Shila hakutaka kusumbua watu, alikuwa ameshatayarisha fedha za kutosha kwa ajili ya sherehe ya mwanaye. Aliitisha kikao cha watu wachache tu, marafiki zake wa karibu kwa ajili ya kupeana mawazo ya namna harusi ya mwanaye itakavyokuwa na michango waliyoahidi.

Huko Mwanza vikao vya sherehe ya kumuaga Laura viliendelea. Taarifa ambazo mzee Shila alizipata ni kwamba, sherehe ya kumuaga Laura ingefanyika jijini Mwanza kwa baba yake mdogo ambapo aliishi na kusoma huko kwa muda mrefu.

Hata hivyo, baadaye siri ilivuja! Mzee Shila akagundua kuwa Laura hakuwa Mnyiramba, wala hakuwahi kuishi Mpambala kama ilivyoelezwa lakini pia hakuitwa Njile.
Ni Msukuma wa Mwanza!

Mzee Ngeleja alikasirika sana. Ilibaki wiki chache sana kabla ya ndoa. Alimwita Chris nyumbani kwake ambaye alimkuta baba yake amewaka kwa hasira.

“Chris unawezaje kunifanyia maigizo?” akafoka kwa hasira mbele ya mwanaye Chris.
“Kivipi baba?” Chris aliuliza lakini alianza kuhisi kuwa tayari mambo yalishaharibika.
“Huyo mchumba wako ni mtu wa wapi?”

“Baba jamani... si ni Singida!”
“Mpuuzi wewe! Singida ndiyo Mwanza siku hizi siyo? Halafu unanidanganya mimi kama mtoto mdogo? Pumbavu kabisa, sasa hiyo ndoa hesabu haipo.

Potelea mbali fedha nilizopoteza, lakini safari hii nitaongozana na wewe hadi kijijini na nitahakikisha unaoa mwanamke kutoka kijijini!” akasema mzee Shila kwa hasira.

Itaendelea kesho.
 
SEHEMU YA 32



ILIPOISHIA.. “Potelea mbali fedha nilizopoteza, lakini safari hii nitaongozana na wewe hadi kijijini na nitahakikisha unaoa mwanamke kutoka kijijini!” Akasema mzee Shila kwa hasira.
SASA ENDELEA...
CHRIS alichanganyikiwa sana, alimwangalia baba yake akiwa haamini kabisa kama tayari alikuwa ameshajua kila kinachoendelea. Alihisi kichwa kumuuma sana.
Alibaki amesimama palepale akimwangalia baba yake. Ndoa yake na Laura ilikuwa inayeyuka, jambo ambalo hakutaka kabisa litokee.
“Una jipya la kuniambia?” Mzee Shila akauliza kwa hasira.
“Baba tuliza hasira kwanza. Nahitaji kuzungumza na wewe.”
“Sitaki mazungumzo na wewe, naomba uondoke haraka sana mbele ya macho yangu. Toka tafadhali,” akasema mzee Shila kwa hasira.
Chris hakuwa na cha kufanya zaidi ya kuondoka. Baba yake alikuwa amekasirika katika kiwango cha mwisho kabisa. Aliingia garini kisha akapiga gia hadi nyumbani kwake Kijitonyama.
Alifikia sebuleni na kujitupa kwenye sofa kubwa, akijaribu kutafakari. Macho yake tayari yalishaanza kulengwalengwa na machozi. Bila hiyari yake akajikuta akianza kulia.
Hakuwa na msaada wowote kwa wakati ule. Alisimama ghafla na kuelekea kwenye jokofu kisha akatoa bia moja na kuifungua, akiwa palepale mbele ya jokofu lake, aliimimina kinywani mwake yote ikaishia humo!
Aliposhusha chupa, ilikuwa tupu kabisa. Akachukua bia nyingine, akafanya vilevile kisha akachukua tena ya tatu, safari hii akatembea hadi kwenye sofa na kuketi.
Akaendelea kunywa!
Ni kama alikuwa amechanganyikiwa kabisa. Jambo lile lilimuumiza sana na aliona kama dunia yote ilikuwa ikimuangukia yeye.
Amkose Laura?
Ni jambo ambalo hakutaka kabisa kuliruhusu litokee. Alihisi mwili wote ukitetemeka. Akiwa katika hali ile, akapata wazo la ghafla. Aliona usalama wake ulikuwa kwa mzee Ngeleja.
Lilikuwa wazo alilolipitisha moja kwa moja. Haraka akachukua simu kisha akabonyeza jina la mzee Ngeleja na kumpigia! Simu haikuita muda mrefu, tayari mzee Ngeleja alikuwa hewani!
“Shikamoo baba,” Chris akasalimia kwa heshima.
“Marahaba mwanangu, vipi mnaendeleaje na maandalizi huko?”
“Mambo yameharibika.”
“Kuna nini? Hebu niambie mwanangu, acha kuniweka roho juu mimi na huu utu uzima.”
“Baba amegundua kila kitu. Amejua mchezo wote. Amefahamu kuwa Laura siyo Mnyiramba. Hataki kusikia ndoa tena, amesema ataongozana na mimi hadi kijijini akanitafutie mke yeye mwenyewe!” Akasema Chris huku akilia.
Kimya cha sekunde kadhaa kilipita. Mzee Ngeleja alibaki kimya huku sauti ya kilio cha Chris ikisikika kwenye simu. Baadaye mzee Ngeleja akaanza tena kuzungumza...
“Mwanangu kwanza nataka kukuambia, ni afadhali jambo hilo limetokea!”
“Afadhali? Kwa nini baba?”
“Ingewasumbua sana baadaye!”
“Kwa hiyo mzee uko tayari kuona ndoa yangu na Laura inayeyuka?”
“Kwanza nataka kukutia moyo mwanangu. Hakuna ndoa inayoyeyuka hapo. Kwanza tayari ninyi ni wanandoa halali, maana mmefunga ya kimila. Hilo ondoa shaka kabisa.
“Jingine ni kwamba, hilo ni jambo dogo sana ambalo lipo ndani ya uwezo wangu. Najua naweza kulishughulikia.”
“Kivipi baba? Utafanyaje wakati wewe uko huko mbali?”
“Kesho nakuja Dar, naomba uwe na amani. Kwa sasa jambo hili lifanye siri kabisa. Usimwambie hata Laura kama kuna kitu kama hicho kimetokea.”
“Sawa baba.”
“Ok! Siku njema, naomba uwe na amani.”
“Ahsante.”
Wakakata simu zao.
Angalau sasa Chris alihisi amani moyoni mwake. Aliendea kunywa akiwa na matumaini ya ndoa yake kufungwa baada ya mzee Ngeleja kuahidi kumsaidia.
***
Saa 10:00 alasiri, mzee Ngeleja akiwa ameongozana na mchungaji wa kanisa lililotarajiwa ndoa ya Laura na Chris kufungwa na mwenyeji wao Chris, walikuwa mbele ya geti la mzee Shila, Mbezi Beach.
Kwa bahati nzuri, mzee Shila mwenyewe alikuwepo ndani. Chris aliwakaribisha na wote wakaingia hadi ndani. Sebuleni walimkuta mzee Shila amekaa na mkewe.
Aliwakaribisha kwa hofu akiwa hajui ni akina nani na walichofuata nyumbani kwake. Kwa utulivu mkubwa, mzee Ngeleja aliketi, kisha mchungaji.
“Karibuni jamani,” akasema mzee Shila akionesha wasiwasi kidogo.
“Ahsante, nafurahi tumewakuta, tena wote kwa pamoja. Labda tujitambulishe, mimi naitwa mzee Ngeleja natokea Mwanza, ni baba mzazi wa Laura ambaye kwa wewe unamfahamu pia kwa jina la Njile, mchumba wake na Chris,” mzee Ngeleja akasema kisha akatulia kidogo.
Mzee Shila akatoa macho, hakuweza kuzuia hasira yake.
“Nimeongozana na mchungaji Samatta, huyu tumempitia mimi na Chris kanisani wakati tunakuja hapa nyumbani,” akasema kwa hekima sana mzee Ngeleja.
“Karibuni sana.”
“Ahsante. Kikubwa ni kuhusu vijana wetu, nimetoka Mwanza kwa ajili ya jambo hilo. Nahitaji tuweke haya mambo sawa!” Akasema mzee Ngeleja.
“Mchungaji nakuheshimu sana, mzee mwenzangu nakuheshimu pia, lakini sijaona mtu wa kubadilisha maamuzi yangu. Nilichoamua nimeamua,” akasema mzee Shila.
“Lakini mume wangu...” akadakia mama Chris.
“Kaa kimya! Wakati wanaume wanazungumza unatakiwa kufunga bakuli lako!” akasema mzee Shila kwa ukali.

Itaendelea kesho.
 
SEHEMU YA 33


ILIPOISHIA.. “Kaa kimya! Wakati wanaume wanazungumza unatakiwa kufunga bakuli lako!” akasema mzee Shila kwa ukali.
SASA ENDELEA...

MAMA Chris alitulia. Alimjua vizuri sana mumewe na tabia zake. Ni wazi kuwa kama angeendelea kubishana naye, jambo lolote baya lingeweza kutokea, kitu ambacho hakukitaka kabisa.
Mchungaji alimwangalia mzee Shila ambaye uso wake ulijaa makunyanzi kutokana na hasira iliyokuwa imemkolea. Ilikuwa lazima afanye kitu kwa ajili ya kijana Chris ambaye alikuwa na jambo jema tu la kutaka kuoa.

“Mzee Shila, nakubaliana na wewe, lakini nakuomba usitumie maneno makali. Hebu tuzungumze kwa utaratibu ili tuone cha kufanya,” akasema Mchungaji kwa sauti ya kusihi sana.

“Kuna kipi cha kujadili hapa Mchungaji?” akauliza mzee Shila kwa sauti ya chini kidogo.
“Sababu hasa za kukataa kijana wako asimuoe huyo binti, maana maandiko yamefafanua wazi kuwa, mwanamke ataacha familia yake na kuungana na mwanaume, nao watakuwa mwili mmoja. Jambo ambalo vijana wetu wapo tayari kwa hilo.

“Sasa inawezekana kama mzazi ukawa na mawazo mazuri tu au sababu zinazosababisha uzuie, ni vyema basi ukasema mzee Shila,” akasema Mchungaji.

“Kikubwa ni kwamba nataka mwanangu aoe nyumbani kwetu, ndicho nilichomwagiza na alifanya hivyo lakini kumbe alikuwa ananidanganya. Amenifanya maigizo mimi. Mpaka ndoa ya kimila imeshafanyika nikijua ni binti wa nyumbani lakini kumbe haikuwa hivyo,” akasema mzee Shila kwa hasira.
Mchungaji akatulia.

Akamwangalia Chris, kisha akamtupia swali: “Anayosema mzee ni ya kweli?”
“Ndiyo Mchungaji.”
“Kwa nini umefanya hivyo?”

“Nakiri makosa Mchungaji. Unajua kubwa ni kwamba mimi nilikutana na Laura Singida, nikampenda sana. Nikajaribu kumchunguza, nikagundua kuwa ana mapenzi ya kweli kwangu, ndiyo maana nikafanya yote hayo.

“Najua nimekosea lakini namuomba baba anisamehe, ila namhakikishia kwa asilimia kubwa, mwanamke ambaye nataka kuoana naye ana tabia njema, anafaa kuwa mke wangu, hilo namhakikishia baba,” akasema Chris kwa sauti ya upole.“Labda mimi niongezee hapo kidogo,” akasema mzee Ngeleja baada

ya ukimya wa muda mrefu.
Wote wakamgeukia.
“Binti yangu alikuja nyumbani na kuzungumza na mama yake kuhusiana na suala hili. Mke wangu alikataa kabisa. Alikataa binti yake asiolewe na Chris kwa sababu ni msanii wa filamu.

“Alisema wasanii wote ni wahuni, hawana tabia nzuri na hawezi kuwa mwaminifu kwenye ndoa. Mwanangu alishindwa kulala siku hiyo, maana alizungumza na mama usiku usiku akiwa ameingia tu kutokea chuoni Singida.

“Baadaye alifikia uamuzi wa kuja ofisini kwangu kuzungumza nami kuhusu jambo hilo. Nilimsikiliza, hoja za mama yake sikuzidharau lakini kama mzazi nilitakiwa kufanya uchunguzi.
“Nilichofanya, nilimwagiza Laura amwambie Chris aje Mwanza aonane na mimi. Kweli akaja. Nikazungumza naye na kumwuliza maswali. Niseme ukweli, kama mzazi ambaye nimemlea mwanangu kwa maadili, nilivutiwa na Chris.

“Mawazo ya mama yake nikaona hayakuwa na uchunguzi. Nilikubaliana na Chris, akaondoka akiwa hajui kama kuna jambo lolote lililotokea. Nilipofika nyumbani nikazungumza na mwenzangu na nilimweleza yote hayo bila kumficha.

“Alinielewa lakini baada ya mvutano wa muda mrefu sana. Hata hili lilipotokea huku Dar, Chris alinishirikisha na niliamua kuja ili nizungumze na mzee mwenzangu tuweke haya mambo sawa.

“Nashauri, tuwaache hawa watoto waoane. Tuwape baraka zetu kama wazazi. Wanapendana kwa dhati na nakuhakikishia mzee mwenzangu, binti yangu nimemlea kwa malezi bora,” akasema mzee Ngeleja.
Ukimya ukatanda!

Mzee Shila akavuta pumzi ndefu sana, kisha akazishusha taratibu kabisa. Akamwangalia mwanaye... ni wazi kuwa kuna kitu alitaka kuzungumza...
“Ni kweli ulikwenda Mwanza kuonana na huyu mzee?”
“Ndiyo baba.”

Maneno ya mzee Ngeleja yalimwingia sana. Alionekana dhahiri kutaka kukubaliana naye. Mzee Ngeleja alizungumza maneno ya msingi sana. Ghafla mzee Shila alisimama, akasogea alipokuwa amekaa mwanaye Chris.

Akamwonyesha ishara kuwa asimame. Chris akasimama. Akamvutia kwake na kumkumbatia.
“Mwanangu nimekubaliana na wewe, tuachane na yote yaliyopita...” akasema mzee Shila.
Mama Chris akasimama, mzee Ngeleja akafuata, wote wakaunda duara dogo na kushikana mikono. Mchungaji akaanza maombi!
Kikao kikaisha!
***
Mazungumzo yaliyofuata yalikuwa ya kifamilia zaidi yaliyojaa upendo. Mzee Ngeleja alikaribishwa rasmi nyumbani na alipewa heshima zote. Alikaa hapo hadi jioni kabisa, wakizungumza mipango mbalimbali ya ndoa ya Laura na Chris.

Usiku, Chris ndiye aliyempeleka mzee Ngeleja uwanja wa ndege kwa safari ya kurudi nyumbani kwake Mwanza. Ilikuwa furaha kubwa sana kwa Chris.
***
Ilikuwa kama ndoto lakini ndivyo ilivyokuwa. Chris alikuwa na Laura mbele ya Kanisa la KKKT, Azania Front akifunga ndoa na mwanamke aliyempenda kutoka moyoni mwake.

Kanisa lilikuwa limejaa, wazazi, ndugu, jamaa na wasanii wakubwa wa Bongo Movies kama Jaybee, Ramsey, Thaiyway na wengine wengi.

Mchungaji Massawe alianza kwa kumwuliza Chris: “Christopher Joseph Shila, upo tayari kuoana na huyu Laura John Ngeleja awe mke wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
Chris hakujibu kitu!
Itaendelea...
 
SEHEMU YA 34


ILIPOISHIA..Mchungaji Massawe alianza kwa kumwuliza Chris: “Christopher Joseph Shila, upo tayari kuoana na huyu Laura John Ngeleja awe mke wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
Chris hakujibu kitu!
SASA ENDELEA...
HISIA kali ilimshika Chris. Ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kusisimua. Hakuamini kama ni yeye alikuwa mbele ya kanisa akiwa amevaa suti kali nyeusi na shati jeupe huku shingoni akiwa amevaa tai fupi nyekundu!
Laura alitingisha! Alivaa gauni jeupe na shela iliyoburuzika hadi chini. Furaha ikamfanya asahau kuwa yupo kanisani na alitakiwa kujibu swali la Mchungaji ili kukamilisha uhalali wa ndoa yao.
Kanisa zima lilikuwa kimya. Wengine walianza kuogopa, wakahisi huenda Chris aliamua kubadilisha mawazo. Kwamba aliamua kuachana na suala la ndoa na Laura.
Haikuwa hivyo.
Chris alimpenda sana Laura, alichanganywa na tukio lililokuwa mbele yake ambalo lilikuwa kama sinema ya kusisimua.
“Christopher...” Mchungaji akaita.
“Naam!”
“Hujaona sehemu ya kusoma kijana wangu?” akauliza Mchungaji.
“Nimeona.”
“Sawa, nami nitakuuliza tena: “Christopher Joseph Shila, upo tayari kuoana na huyu Laura John Ngeleja awe mke wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
“Ndiyo Mungu anisaidie,” akajibu Chris.
Ukumbi mzima ukalipuka kwa shangwe na nderemo. Matarumbeta nayo hayakuwa nyuma, yalisikika yakipulizwa na hivyo kuamsha shangwe ukumbini humo.
Mchungaji akamgeukia Laura kisha akamwuliza: “Laura John Ngeleja, upo tayari kuoana na huyu Christopher Joseph Shila awe mume wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
“Ndiyo Mungu anisaidie,” akajibu Laura.
Kelele zikazidi kuwa kubwa, kanisa zima lilishangilia. Ilikuwa furaha kwa wote. Zoezi lililofuata baada ya hapo ilikuwa ni kuvalishana pete.
Ndoa ikawa imefungwa!
Chris na Laura wakawa mume na mke rasmi.
***
Sherehe ilikuwa katika Ukumbi wa Mlimani City. Hiyo ilikuwa ni baada ya maharusi na ndugu wengine kuzunguka sehemu mbalimbali za jiji na kupiga picha.
Waandishi wa habari walikuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanapata picha nzuri za kupamba magazeti yao. Chris kuoa ilikuwa habari kubwa sana kwa magazeti Pendwa Bongo.
Waandishi na wapigapicha maarufu, Issa Mnally, Richard Bukos na Shakoor Jongo walikuwa wanashindana kutafuta picha bora zaidi ambayo ingependekezwa kutokea kwenye ukurasa wa mbele wa Gazeti la Ijumaa Wikienda siku ya Jumatatu.
Achana na hao, wapigapicha wa magazeti mengine ya kila siku na michezo walipigana vikumbo kupata picha nzuri. Msanii wa Bongo Muvi kuoa halikuwa jambo dogo!
Ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, wasanii walikuwa wengi sana. Walialikwa watu maalum tu. Viongozi kadhaa wa kiserikali walikuwemo, wabunge, mawaziri, wakuu wa wilaya na madaktari.
Ilikuwa sherehe yenye heshima kubwa sana. Chris alijisikia mwanaume kamili kati ya wanaume. Wapambe wao walikuwa ni wasanii wa filamu, Jaybee na mkewe Vanessa.
MC wa shughuli hiyo alikuwa ni Chika, ambaye siku zote amekuwa akiongoza hafla mbalimbali za wasanii na watu wengine. Kwa Chris ilikuwa siku mpya ya kipekee ambayo ilikamilisha haja ya moyo wake.
Wenye kunywa walikunywa sana. Chakula kililiwa hadi kikabaki. Fungakazi ilikuwa zawadi, watu walitoa zawadi nyingi sana, achilia mbali wazazi wa pande zote ambao waliwazidi wote.
Alianza mzee Shila: “Umefanya kitu kikubwa sana mwanangu. Leo umenifanya nijisikie baba yako kamili. Nakupenda sana mwanangu. Kuhusu namna ya kuishi na mwenzako tumeshazungumza mengi, najua umeyashika.
“Kuna kitu ambacho nataka kukisema mbele ya watu wote hapa. Kwa tendo hili, nasema kwamba nimebadili fikra zangu. Nilichukia sana mwanangu kutokuoa mapema, lakini sikutaka kusikia anaoa mjini.
“Akilini mwangu niliamini wasanii wote ni wahuni, wana tabia mbaya na ni watu wasiofaa kwenye jamii. Kumbe nilikuwa nawaza tofauti. Nikadhani mke sahihi lazima atokee kijijini, kumbe siyo kweli.
“Leo hii mwanangu amepata mke mwema, sahihi na mzuri ambaye atamsaidia kama vitabu vinavyosema. Ninawabariki wanangu, mkaishi kwa amani na upendo. Kuanzia sasa, sina kinyongo na kazi ya mwanangu Chris. Pamoja na kwamba nilikulazimisha kusomea udaktari, nashukuru unaifanya kazi hiyo vizuri.
“Unasaidia kuokoa maisha ya Watanzania wengi kupitia taaluma yako. Wakati ukifanya yote hayo, bado pia unafanya sanaa kama sehemu ya kipato na fani uliyoichagua na kuipenda.
Kuhusu zawadi, najua una gari la kutembelea, lakini mimi nimekununulia jingine, litakalofanana na hadhi yako ya ubaba, maana sasa umekuwa baba. Nimekununulia Toyota Range Rover, iko hapo nje. Funguo zake hizi hapa,” akasema mzee Shila na kwenda kumkabidhi.
Shangwe zikaibuka upya!
Chris alipokea funguo za gari, kisha akanyanyua mkono juu na kuwaonyesha wageni ukumbini. Ghafla akagonganisha macho na mtu ambaye hakutarajia kabisa kumuona!
Chris alishtuka sana!
Itaendelea.
 
SEHEMU YA 35


ILIPOISHIA......Mchungaji Massawe alianza kwa kumwuliza Chris: “Christopher Joseph Shila, upo tayari kuoana na huyu Laura John Ngeleja awe mke wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
Chris hakujibu kitu!
SASA ENDELEA...
HISIA kali ilimshika Chris. Ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kusisimua. Hakuamini kama ni yeye alikuwa mbele ya kanisa akiwa amevaa suti kali nyeusi na shati jeupe huku shingoni akiwa amevaa tai fupi nyekundu!
Laura alitingisha! Alivaa gauni jeupe na shela iliyoburuzika hadi chini. Furaha ikamfanya asahau kuwa yupo kanisani na alitakiwa kujibu swali la Mchungaji ili kukamilisha uhalali wa ndoa yao.
Kanisa zima lilikuwa kimya. Wengine walianza kuogopa, wakahisi huenda Chris aliamua kubadilisha mawazo. Kwamba aliamua kuachana na suala la ndoa na Laura.
Haikuwa hivyo.
Chris alimpenda sana Laura, alichanganywa na tukio lililokuwa mbele yake ambalo lilikuwa kama sinema ya kusisimua.
“Christopher...” Mchungaji akaita.
“Naam!”
“Hujaona sehemu ya kusoma kijana wangu?” akauliza Mchungaji.
“Nimeona.”
“Sawa, nami nitakuuliza tena: “Christopher Joseph Shila, upo tayari kuoana na huyu Laura John Ngeleja awe mke wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
“Ndiyo Mungu anisaidie,” akajibu Chris.
Ukumbi mzima ukalipuka kwa shangwe na nderemo. Matarumbeta nayo hayakuwa nyuma, yalisikika yakipulizwa na hivyo kuamsha shangwe ukumbini humo.
Mchungaji akamgeukia Laura kisha akamwuliza: “Laura John Ngeleja, upo tayari kuoana na huyu Christopher Joseph Shila awe mume wako, ushirikiane naye katika shida na raha, hadi kifo kiwatenganishe? Kama ndivyo, sema ndiyo Mungu anisaidie.”
“Ndiyo Mungu anisaidie,” akajibu Laura.
Kelele zikazidi kuwa kubwa, kanisa zima lilishangilia. Ilikuwa furaha kwa wote. Zoezi lililofuata baada ya hapo ilikuwa ni kuvalishana pete.
Ndoa ikawa imefungwa!
Chris na Laura wakawa mume na mke rasmi.
***
Sherehe ilikuwa katika Ukumbi wa Mlimani City. Hiyo ilikuwa ni baada ya maharusi na ndugu wengine kuzunguka sehemu mbalimbali za jiji na kupiga picha.
Waandishi wa habari walikuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanapata picha nzuri za kupamba magazeti yao. Chris kuoa ilikuwa habari kubwa sana kwa magazeti Pendwa Bongo.
Waandishi na wapigapicha maarufu, Issa Mnally, Richard Bukos na Shakoor Jongo walikuwa wanashindana kutafuta picha bora zaidi ambayo ingependekezwa kutokea kwenye ukurasa wa mbele wa Gazeti la Ijumaa Wikienda siku ya Jumatatu.
Achana na hao, wapigapicha wa magazeti mengine ya kila siku na michezo walipigana vikumbo kupata picha nzuri. Msanii wa Bongo Muvi kuoa halikuwa jambo dogo!
Ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, wasanii walikuwa wengi sana. Walialikwa watu maalum tu. Viongozi kadhaa wa kiserikali walikuwemo, wabunge, mawaziri, wakuu wa wilaya na madaktari.
Ilikuwa sherehe yenye heshima kubwa sana. Chris alijisikia mwanaume kamili kati ya wanaume. Wapambe wao walikuwa ni wasanii wa filamu, Jaybee na mkewe Vanessa.
MC wa shughuli hiyo alikuwa ni Chika, ambaye siku zote amekuwa akiongoza hafla mbalimbali za wasanii na watu wengine. Kwa Chris ilikuwa siku mpya ya kipekee ambayo ilikamilisha haja ya moyo wake.
Wenye kunywa walikunywa sana. Chakula kililiwa hadi kikabaki. Fungakazi ilikuwa zawadi, watu walitoa zawadi nyingi sana, achilia mbali wazazi wa pande zote ambao waliwazidi wote.
Alianza mzee Shila: “Umefanya kitu kikubwa sana mwanangu. Leo umenifanya nijisikie baba yako kamili. Nakupenda sana mwanangu. Kuhusu namna ya kuishi na mwenzako tumeshazungumza mengi, najua umeyashika.
“Kuna kitu ambacho nataka kukisema mbele ya watu wote hapa. Kwa tendo hili, nasema kwamba nimebadili fikra zangu. Nilichukia sana mwanangu kutokuoa mapema, lakini sikutaka kusikia anaoa mjini.
“Akilini mwangu niliamini wasanii wote ni wahuni, wana tabia mbaya na ni watu wasiofaa kwenye jamii. Kumbe nilikuwa nawaza tofauti. Nikadhani mke sahihi lazima atokee kijijini, kumbe siyo kweli.
“Leo hii mwanangu amepata mke mwema, sahihi na mzuri ambaye atamsaidia kama vitabu vinavyosema. Ninawabariki wanangu, mkaishi kwa amani na upendo. Kuanzia sasa, sina kinyongo na kazi ya mwanangu Chris. Pamoja na kwamba nilikulazimisha kusomea udaktari, nashukuru unaifanya kazi hiyo vizuri.
“Unasaidia kuokoa maisha ya Watanzania wengi kupitia taaluma yako. Wakati ukifanya yote hayo, bado pia unafanya sanaa kama sehemu ya kipato na fani uliyoichagua na kuipenda.
Kuhusu zawadi, najua una gari la kutembelea, lakini mimi nimekununulia jingine, litakalofanana na hadhi yako ya ubaba, maana sasa umekuwa baba. Nimekununulia Toyota Range Rover, iko hapo nje. Funguo zake hizi hapa,” akasema mzee Shila na kwenda kumkabidhi.
Shangwe zikaibuka upya!
Chris alipokea funguo za gari, kisha akanyanyua mkono juu na kuwaonyesha wageni ukumbini. Ghafla akagonganisha macho na mtu ambaye hakutarajia kabisa kumuona!
Chris alishtuka sana!
 
SEHEMU YA 36



ILIPOISHIA...Chris alipokea funguo za gari kisha akanyanyua mkono juu na kuwaonesha wageni ukumbini. Ghafla akagonganisha macho na mtu ambaye hakutarajia kabisa kumuona!
Chris alishtuka sana!
SASA ENDELEA...
MSHTUKO ulikuwa mkubwa kwa hakika, kumuona mtu yule ambaye pia hakumwalika na alikuwa na uhakika kuwa Laura naye hakumwalika, kulimchanganya sana.
Akajitahidi kujikaza. Akaweka zile funguo za gari alizokabidhiwa na baba yake mfukoni. Baba yake akarudi kwenda kukaa sehemu yake. Chris alipomwangalia Laura akagundua kuwa, naye alikuwa amemuoana yule mtu.
Alikuwa ni Julius.
Jully, yule mwanafunzi aliyekuwa akisoma na Laura chuo Singida. Ni Jully ndiye aliyesaidia kuwaunganisha. Kwa maneno mengine kama si yeye, usiku ule pale club, kulikuwa na uwezekano mkubwa kwa Chris kumkosa kabisa Laura.
Zoezi la zawadi likaendelea ambapo Mzee Ngeleja alitangaza kutoa ekari 50 za mashamba ya mpunga, yaliyopo Mbarali, Mbeya. Ilipofika zamu ya wageni waalikwa, Jully naye alikwenda.
Alitoa bahasha ya kaki kwenye sehemu ya kuwekea zawadi kisha akamsogelea Chris na kumpatia karatasi ndogo.
“Hongera sana kaka, usijiulize ningekujaje hapa, ila naomba unitafute baada ya fungate, namba zangu zipo humu kwenye karatasi, kuna jambo lazima nikuambie.”
“Poa.”
Akatoka hapo na kwenda kwa Laura. Akamkumbatia na kumpongeza.
***
Tayari mipango yote ya fungate ilikuwa imefanyika. Wazazi wa bwana na bibi harusi waliamua kuchangia fedha kwa ajili ya safari ya watoto wao.
Ulikuwa muunganiko mzuri sana wa familia hizo mbili. Wazazi waliwataka watoto wao wachague kisiwa chochote duniani, waende wakastarehe kwa wiki mbili katika kufurahia ndoa yao mpya.
Kitu cha kushangaza ni kwamba, wote kwa pamoja walikubaliana kwenda Zanzibar. Wazazi walishangaa.
“Kwa nini Zanzibar?” Mzee Ngeleja aliuliza.
“Kwanza ni hapahapa Tanzania, tunapenda kufanya utalii wa ndani baba. Lakini pia tuna mambo mengi sana ya kufanya kama wanandoa, hatutaki kwenda mbali wala kutumia muda mrefu kwa ajili ya fungate.
“Wiki moja itatosha sana mjini Zanzibar kwa mapumziko ya fungate yetu, wiki nyingine tutakwenda Singida, halafu tutarudi Dar kuendelea na mambo mengine.”
Hakuna aliyepinga, Mzee Ngeleja na Mzee Shila wakakubaliana kwa pamoja na watoto wao. Walilala The Atriums Hotel iliyopo Sinza–Afrika Sana ambapo asubuhi ya saa 4:00 waliondoka hadi uwanja wa ndege walipopanda ndege na kuelekea visiwani Zanzibar.
***
Wakiwa wamejipumzisha kwenye bustani ndani ya Hoteli ya Karafuu mjini Unguja wakicheza michezo ya kimapenzi, Chris akamkumbuka Jully.
“Mh! Lakini Jully anaonekana ana jambo muhimu la kuniambia, lakini sijajua ni nini. Ngoja nikachukue ile namba yake ya simu ndani,” akasema Chris.
“Hapana dear, ngoja nikachukue. Umeweka wapi?”
Chris akamwelekeza.
Laura akanyanyuka na kwenda ndani, baadaye aliporejea alikuwa na karatasi yenye namba ya simu, akampa mumewe. Chris palepale akampigia Jully.
“Kaka ulisema nikutafute baada ya fungate lakini naona kama nachelewa sana kujua, ndiyo maana nimekutafuta mapema,” akasema Chris mara baada ya Jully kupokea simu.
“Usijali kaka, uko wapi?”
“Zanzibar, tunaweza kuzungumza sasa?”
“Siyo ya kwenye simu kaka, halafu napenda nikizungumza uwe na Laura.”
“Njoo Zanzibar basi, kila kitu nitagharamia mimi.”
“Kweli?”
“Ndiyo, tena ikiwezekana leo. Sema nifanye mpango wa ndege ya jioni mara moja.”
“Nakubaliana na wewe.”
Ndivyo ilivyokuwa, mipango ikafanyika vyema, jioni yake Jully aliingia Zanzibar. Aliungana nao kwenye hoteli ileile waliyofikia. Jioni wakiwa wanapata chakula, Jully akaanzisha mazungumzo...
“Kwanza hongereni kwa kufanikisha kufunga ndoa. Nataka kuwahakikishia kuwa, kila mmoja ni muhimu na maalum kwa mwenzake. Muishi kwa upendo, amani na kusikilizana.
“Pia nimefurahi kwamba, mimi ni mtu pekee mliyeniamini na kunipa heshima ya kuwatembelea hadi kwenye fungate yenu, ahsanteni sana ndugu zangu,” akaanza kusema Jully.
“Usijali kaka, tupo pamoja. Wewe ni mtu muhimu, maana bila wewe ilikuwa vigumu sana kumpata Laura.”
“Ni kweli. Ila kuna jambo ambalo lazima niliseme kwa ukweli wa moyo wangu, maana nisipofanya hivyo nitabaki na mateso makubwa sana moyoni. Hiyo ndiyo sababu iliyonifanya nifunge safari kutoka Moshi hadi Dar kufuatilia kuhusu harusi yenu na hatimaye nikahudhuria.
“Kuna jambo nimewafanyia, siyo zuri. Siyo la kiungwana hata kidogo, nataka kuwa mkweli kwenu, lakini nawaomba kabla sijaanza kusema, mkubali kunisamehe kwa nilichowafanyia kwanza,” akasema Jully, sasa akianza kutokwa machozi.
Wote wakamshangaa.
Jully akamgeukia Laura, akamwambia: “Laura tafadhali naomba unisamehe!”
Laura hakumjibu, akamgeukia mumewe na kumwangalia kwa makini, akamwonesha ishara kuwa, akubali kumsamehe ili wamsikilize mpaka mwisho.
Laura akatingisha kichwa.
“Ahsante. Je, Chris nawe utanisamehe?” Akauliza Jully.

Je, Jully amefanya jambo gani? Usikose siku ya kesho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom