Hadithi : Singidani (A Story From My Heart)

Hadithi : Singidani (A Story From My Heart)

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,638
Image may contain: 1 person, close-up

CHRIS hakuweza kuvumilia zaidi, akatembea kwa haraka akitetemeka miguu. Alipowafikia akasimama na kuwaangalia kwa kuwakazia macho. Si Davis wala Pamela walioshtuka.
Ni kama hawakuona chochote wala yeyote. Wakaendelea na shughuli zao. Muda huohuo, kwa ghafla sana, Chris akasikia kibao cha nguvu mgongoni mwake...
“Nani?” akasema akipaza sauti.
“Cut...” Director Mushi akasema akiwaamrisha wasitishe kuigiza.
Chris akiwa amefura akageuza uso wake. Hamad! Alikutana na uso wa baba yake mzazi ukiwa umekunjamana!
Mzee Joseph Shila.
“Kweli unaweza kuzaa watoto lakini si wote watakuwa watoto bora. Daktari mzima, tena niliyepoteza mamilioni yangu kukusomesha nje ya nchi, unakaa na hawa wajinga wamevaa vichupi mnaigiza?
“Hivi Christopher mwanangu utakua lini wewe? Lini utakuwa mtu mzima na kuelewa ninayokuambia? Pumbaaf, endelea na ujinga wako,” akasema mzee Shila kisha akaondoka zake.
Chris akabaki ameduwaa.
Mushi alibaki anashangaa tu asijue cha kufanya. Neno moja likamponyoka kwa haraka: “What is going on Chris?”
Chris hakujibu.
“Kwa nini tunaharibiana kazi? Hivi kweli scene moja inaweza kutuchukulia siku nzima? Jana ulisema unaumwa kichwa, leo umechelewa location ukasema ulikuwa kwenye upasuaji, baadaye tena sijui unamwita mtu aje kutuharibia kazi ili iweje?
“Kama unaona hutaki kufanya hii sinema si uache kaka? Unadhani wewe ni staa sana siyo? Ni bora kufanya kazi na chipukizi wenye nidhamu kuliko kuhangaika na nyie mastaa mnaotusumbua vichwa kila siku,” akasema Mushi kwa hasira.
Scene hiyo ilimsumbua sana kutokana na ugumu wake...tena siku hiyo walipatia kwa kiasi kikubwa sana kuvaa uhalisia katika kiwango cha juu. Kosa la mzee Shila lilimuumiza sana, maana liliwatoa wasanii katika mwendelezo mzuri wa kuvutia.
“Samahani kaka, unanifikiria vibaya. Yule ni baba yangu.”
“Baba yako?” akauliza Mushi kwa sauti ya upole.
“Ndiyo...ni baba yangu.”
“Imekuwaje?”
“Ni habari ndefu.”
“Samahani sana kaka.”
“Usijali.”
“Upo kwenye mood nzuri na tunaweza kuendelea?” akauliza Mushi.
“Bila shaka.”
“Kweli?”
“Nitajitahidi...”
“Sawa...usijali, tutaendelea palepale...kaeni tayari...kamera upo sawa? Boom please...light...Ok! Action...” akasema Mushi.
“Pamela!!!” neno hilo likamtoka Chris huku machozi yakimiminika kwa kasi sana.
Ilikuwa sauti iliyojaa huzuni na kitetemeshi cha hali ya juu. Kweli alivaa uhusika sawasawa. Ni kweli, tukio lile alitakiwa kutoa machozi, alipaswa kuonyesha huzuni kama alivyofanya.
Hakuna aliyejua ila ukweli ni kwamba alifanikiwa zaidi kutokana na machungu ya kero za mzee wake na si kwa sababu ya tukio lililokuwa ndani ya scene ile.
***
Mzigo mzito ulimjaa Chris kichwani. Mwanamke yule mrembo aliuteka mtima wake. Alikuwa mweusi, mrefu wa wastani mwenye umbo namba nane. Alisuka nywele zake katika mtindo wa rasta nene.
Alivaa sketi fupi ya khaki, iliyofanya miguu yake ya bia ionekane vizuri zaidi. Chris akasahau mawazo yote, akatembea hadi kwenye mlango wa kuingilia chooni na kusimama hapo.
Dakika mbili baadaye yule mrembo alitoka msalani na kumpita Chris pale alipokuwa amesimama. Yule msichana alimwangalia Chris ambaye alijitahidi kutabasamu lakini hakuonyesha kama alimuona! Akapita na hamsini zake. Chris akakasirika!
Na umaarufu wote huo?
Tanzania nzima ilimfahamu kutokana na umaarufu wake kwenye filamu za Kibongo. Mara zote amekuwa mstaarabu na kamwe huwa hatumii umaarufu wake kuwapata wasichana lakini safari hii alitamani sana kutumia silaha hiyo.
Jambo la kusikitisha ni kwamba, silaha hiyo ni kama ilikuwa butu au haiwezi kabisa kutumika. Pengine ingeweza kutumika na ilikuwa na nguvu mujarabu lakini siyo kwa msichana yule!
Itaendelea.
 
MARA kadhaa watu walikuwa wakimwangalia na kumnyooshea vidole wakisemezana ndani ya ukumbi huo. Wengine walimfuata na kumsalimia huku wengine wakitaka hata kupiga naye picha tu.
Kwa msichana huyu ni tofauti. Hana muda naye kabisa. Pengine silaha ya kwanza haikuwa na nguvu au msichana yule si mpenzi wa filamu kwa hiyo hamfahamu.
Labda!
Bado alikuwa na silaha nyingine. Mavazi ya gharama aliyokuwa amevaa yalikuwa ni silaha kwa msichana yeyote wa mjini. Chris alikuwa amependeza sana. Alivaa kawaida tu, lakini alipendeza vilivyo.
Silaha hiyo nayo imeshindikana!
Chris akabaki akimsindikiza kwa macho mpaka alipoishilia. Akaanza kupiga hatua za taratibu kurudi alipokuwa amekaa awali. Lengo likiwa ni kuendelea na mawazo yake yaleyale!
***
Macho ya Chris ni kama yalizingirwa na ukungu. Akaamua kuyapekecha kidogo ili kuuondoa ili aweze kuangalia vizuri. Kweli kabisa...alichokiona ni sahihi.
Ni yule msichana alikuwa anacheza na kundi la vijana watano. Wale vijana walikuwa wamemzunguka, yeye akawa katikati yao. Kuna wakati, walianza kuingia katikati mmojammoja na kucheza na yule mrembo kwa zamu.
Lilikuwa onesho la bure lililovutia ambalo lilisababisha wengine waache kucheza, wabaki kuwaangalia wao. Chris akafura!
“Yaani wale watoto ndiyo wanaweza kushindana na mimi? Haiwezekani. Mimi ni mtoto wa mjini...” akawaza Chris akiinuka kusogea karibu na lile duara la vijana watano wakicheza na msichana yule mrembo!
Yule anayeusumbua moyo wake.
Mtikisiko wa moyo ulimvaa Chris. Hasira zikamkaba rohoni. Aliumizwa na msichana yule mrembo ambaye alikataa hata kumsalimia tu wakati tayari alikuwa ameshaufanya moyo wake mateka. Hasira zake sasa zilihamia kwa wale vijana.
Chris akajikaza na kusimama kisha akasogea karibu na wale vijana. Akatoa macho. Hata yeye alijishangaa ni kwa nini alikuwa na hasira kiasi kile.
Yule msichana hakuwahi kumfahamu kabla na hakuwa mpenzi wake. Kwa nini achanganyikiwe? Labda ni mapenzi, lakini kwa nini awakasirikie watu wengine ambao hawafahamu?
Alikiri moyoni mwake kwamba alifanya makosa.
“Nakosea sasa...nadhani huu umaarufu wangu unataka kunidanganya. Natakiwa kuwa mpole kwanza...” akawaza.
Kitu alichogundua kwa haraka ni kwamba alitakiwa kupata liwazo kidogo. Ingekuwa rahisi zaidi kuliwazwa na msichana yule lakini kwa sababu anajifanya anamkataa, Chris alikuwa na kitulizo kingine.
Alichepuka haraka hadi kwenye kaunta ndogo ya pembeni katika ukumbi ule. Akamvaa msichana aliyekuwa akihudumia.
“Nataka toti tatu za Grant’s haraka tafadhali,” akasema Chris akiweka noti moja ya elfu kumi mezani.
“Kaka Chris hata salamu?” yule mrembo akamwambia.
Chris akageuza uso, akakutana na msichana mrembo, mweupe, mrefu, mwenye macho makubwa ya kung’ara. Alijilaumu sana.
“Wakati mwingine unaweza kupoteza cast hivihivi...huyu msichana anafaa kuigiza,” akawaza akitabasamu.
“Habari yako dada yangu?”
“Salama, sasa mambo si hayo? Kwani ulivyonisalimia umekufa?”
Chris akacheka.
“Wewe utakuwa unatoka katika makabila mawili tu ya hapa Singida, kama siyo Mnyaturu utakuwa Mnyisanzu.”
“Mh! Wewe umejuaje? Mimi Mnyaturu.”
“Umeona sasa! Nilisema tu, nimefurahi kuwa mtabiri mzuri,” alisema Chris huku akiondoka zake.
Anarudi kulekule! Msichana hana jipya kwake, anamtaka yule ya mwanzo. Kadiri muda unavyozidi kwenda anazidi kuwaza tofauti. Si kwamba alimtaka msichana yule kwa usiku mmoja tu; aliwaza ndoa kabisa.
Ilikuwa mapema sana kwake kuanza kuwaza mambo makubwa kama yale lakini ndicho kilichokuwa kichwani mwake. Potelea mbali, hata kama akigombana na baba yake mzee Shila, bora aishi na yule mrembo!
“Nimeshajua cha kufanya!” akajisemea Chris akipiga funda moja dogo, akachanganya na mate, akameza.
Itaendelea.....
 
SEHEMU YA 03


ILIPOISHIA...
“Nimeshajua cha kufanya!” akajisemea Chris akipiga funda moja dogo, akachanganya na mate, akameza.
SASA ENDELEA...
SASA alipata wazo jipya. Wazo ambalo kwa hakika lingeweza kumsaidia kumpata yule msichana. Alianza kumfuatilia kijana mmoja ambaye alionekana kama wangeweza kuelewana kidogo. Aliachana na wote, akabaki akimwangalia huyo tu. Mara yule kijana akajitoa pale na kutembea akielekea chumba maalum cha kuvutia sigara. Chris na glasi yake, akamfuata yule kijana.
“Oyaa mambo vipi?” Chris akamsalimia.
“Aaaaah! Mkubwa, bora nimekuona nitapona. Inakuwaje mwana?”
“Salama.”
“Umeingia lini Singapore?”
“Jioni ya leo...samahani huu ni mguu wako lakini kama hutajali kachukue kwanza kinywaji. Unakunywa nini?”
“Ngumu bro.”
“Ngumu?”
“Ndiyo.”
“Unamaanisha nini?”
“Kitu cha konya ndo mzuka.”
“Sawa, kachukue kubwa na pakiti nzima ya fegi,” akasema Chris akimkabidhi noti mbili za elfu kumikumi.
Yule jamaa akaondoka na dakika mbili tu baadaye alirudi akiwa na chupa kubwa ya pombe kali aina ya konya na pakiti ya sigara. Akamrudishia chenji Chris ambaye alimshika mkono na kumtoa katika kile chumba cha kuvutia sigara.
“Vipi?”
“Njoo huku.”
Waliishia kwenye sofa kubwa ndani ya ukumbi ule, pembeni na meza ya Pool Table ambapo bila kupoteza muda, Chris alianza kumwuliza kuhusu yule msichana.
“Nimewaona muda mrefu mkicheza na yule dada. Vipi unamfahamu vizuri?” akauliza Chris.
“Tunasoma naye.”
“Kati yenu pale kuna mtu wake?”
“Mtu wa wapi? Yule msichana ni mwanafunzi mwenzetu tu, hakuna mwenye kisu kikali pale kaka. Yule demu ni mkali chuo kizima.”
“Mnasoma chuo gani?”
“Uhasibu.”
“Oke! Sikia nikuambie mdogo wangu, yule mtoto mimi nimempenda..siyo kwamba nakuambia kwakuwa sijui kutongoza laah! Nataka tu unisaidie kunikutanisha naye, maana naona kama ananata fulani hivi...mambo mengine nitajua mwenyewe.”
“Usiogope mwanajeshi wangu, hilo limepita.”
“Kweli?”
“Wewe sema unataka aje sasa hivi?”
“Ndiyo...”
“Nakuja naye.”
“Sawa.”
“Njoo kwanza....” Chris akamwita yule kijana ambapo mara moja alirudi.
“Hujaniambia jina lako bado.”
“Naitwa Julius.”
“Poa.”
Julius akaondoka. Kama mchezo hivi, dakika moja baadaye, alifika alipokuwa amekaa Chris akiwa amemshika mkono yule msichana. Akamkalisha kwenye sofa kubwa, akamuweka katikati. Pembeni wakamzunguka na Chris.
“Huyu ni kaka yangu...anaitwa Chris. Nimesoma na mdogo wake JK Nyerere Sekondari, Moshi. Tunaheshimiana sana lakini nimechukizwa na tabia yako ya dharau kwake,” Julius akamwambia yule msichana huku akimkazia macho.
Chris akashtuka.
“Mbona huyu dogo anataka kuharibu sasa?” akawaza.
“Nimemfanyaje?” yule msichana akauliza.
“Hujui? Najua unanata na una dharau lakini kwani wewe humfahamu Chris? Utakuja kupoteza bahati bure wewe mtoto wa kike...si kila mwanaume ni mhuni,” akasema Julius kwa hasira.
Pamoja na kwamba kile alichokuwa akikifanya ilikuwa ni maigizo tu ili kumuunganisha na Chris lakini pia pombe aliyokunywa ilikuwa inafanya kazi yake sawasawa.
“Samahani bro Jully.”
“Siyo mimi, wa kumuomba msamaha ni huyu hapa...mimi nawaacha, naamini utafanya hivyo.”
Yule msichana akatingisha kichwa kukubaliana naye. Julius akasimama na kurudi zake ‘Smoking Room’.
Yule msichana alitulia kwa muda, Chris bila kupoteza muda, akamsogelea kidogo. Naye akaanza kumwangalia kwa macho yanayozungumza. Chris alikuwa akifikisha ujumbe wake moja kwa moja.
 
SEHEMU YA 03


ILIPOISHIA...
“Nimeshajua cha kufanya!” akajisemea Chris akipiga funda moja dogo, akachanganya na mate, akameza.
SASA ENDELEA...
SASA alipata wazo jipya. Wazo ambalo kwa hakika lingeweza kumsaidia kumpata yule msichana. Alianza kumfuatilia kijana mmoja ambaye alionekana kama wangeweza kuelewana kidogo. Aliachana na wote, akabaki akimwangalia huyo tu. Mara yule kijana akajitoa pale na kutembea akielekea chumba maalum cha kuvutia sigara. Chris na glasi yake, akamfuata yule kijana.
“Oyaa mambo vipi?” Chris akamsalimia.
“Aaaaah! Mkubwa, bora nimekuona nitapona. Inakuwaje mwana?”
“Salama.”
“Umeingia lini Singapore?”
“Jioni ya leo...samahani huu ni mguu wako lakini kama hutajali kachukue kwanza kinywaji. Unakunywa nini?”
“Ngumu bro.”
“Ngumu?”
“Ndiyo.”
“Unamaanisha nini?”
“Kitu cha konya ndo mzuka.”
“Sawa, kachukue kubwa na pakiti nzima ya fegi,” akasema Chris akimkabidhi noti mbili za elfu kumikumi.
Yule jamaa akaondoka na dakika mbili tu baadaye alirudi akiwa na chupa kubwa ya pombe kali aina ya konya na pakiti ya sigara. Akamrudishia chenji Chris ambaye alimshika mkono na kumtoa katika kile chumba cha kuvutia sigara.
“Vipi?”
“Njoo huku.”
Waliishia kwenye sofa kubwa ndani ya ukumbi ule, pembeni na meza ya Pool Table ambapo bila kupoteza muda, Chris alianza kumwuliza kuhusu yule msichana.
“Nimewaona muda mrefu mkicheza na yule dada. Vipi unamfahamu vizuri?” akauliza Chris.
“Tunasoma naye.”
“Kati yenu pale kuna mtu wake?”
“Mtu wa wapi? Yule msichana ni mwanafunzi mwenzetu tu, hakuna mwenye kisu kikali pale kaka. Yule demu ni mkali chuo kizima.”
“Mnasoma chuo gani?”
“Uhasibu.”
“Oke! Sikia nikuambie mdogo wangu, yule mtoto mimi nimempenda..siyo kwamba nakuambia kwakuwa sijui kutongoza laah! Nataka tu unisaidie kunikutanisha naye, maana naona kama ananata fulani hivi...mambo mengine nitajua mwenyewe.”
“Usiogope mwanajeshi wangu, hilo limepita.”
“Kweli?”
“Wewe sema unataka aje sasa hivi?”
“Ndiyo...”
“Nakuja naye.”
“Sawa.”
“Njoo kwanza....” Chris akamwita yule kijana ambapo mara moja alirudi.
“Hujaniambia jina lako bado.”
“Naitwa Julius.”
“Poa.”
Julius akaondoka. Kama mchezo hivi, dakika moja baadaye, alifika alipokuwa amekaa Chris akiwa amemshika mkono yule msichana. Akamkalisha kwenye sofa kubwa, akamuweka katikati. Pembeni wakamzunguka na Chris.
“Huyu ni kaka yangu...anaitwa Chris. Nimesoma na mdogo wake JK Nyerere Sekondari, Moshi. Tunaheshimiana sana lakini nimechukizwa na tabia yako ya dharau kwake,” Julius akamwambia yule msichana huku akimkazia macho.
Chris akashtuka.
“Mbona huyu dogo anataka kuharibu sasa?” akawaza.
“Nimemfanyaje?” yule msichana akauliza.
“Hujui? Najua unanata na una dharau lakini kwani wewe humfahamu Chris? Utakuja kupoteza bahati bure wewe mtoto wa kike...si kila mwanaume ni mhuni,” akasema Julius kwa hasira.
Pamoja na kwamba kile alichokuwa akikifanya ilikuwa ni maigizo tu ili kumuunganisha na Chris lakini pia pombe aliyokunywa ilikuwa inafanya kazi yake sawasawa.
“Samahani bro Jully.”
“Siyo mimi, wa kumuomba msamaha ni huyu hapa...mimi nawaacha, naamini utafanya hivyo.”
Yule msichana akatingisha kichwa kukubaliana naye. Julius akasimama na kurudi zake ‘Smoking Room’.
Yule msichana alitulia kwa muda, Chris bila kupoteza muda, akamsogelea kidogo. Naye akaanza kumwangalia kwa macho yanayozungumza. Chris alikuwa akifikisha ujumbe wake moja kwa moja.
Gijaa
 
SEHEMU YA 04


Yule msichana alitulia kwa muda, Chris bila kupoteza muda, akamsogelea kidogo. Naye akaanza kumwangalia kwa macho yanayozungumza. Chris alikuwa akifikisha ujumbe wake moja kwa moja.
SASA ENDELEA...
ILA kilichotokea ukumbini mle alihisi ni kama alikuwa ndotoni. Ukweli haukuwa huo, hakuwa anaota. Kila kitu kilikuwa yakinifu kwa hakika kabisa.
Akaufaidi uzuri wa yule msichana kwa karibu kabisa. Moyoni alikuwa na furaha akijua kuwa angalau alikuwa akielekea kutimiza lengo lake. Kukaa naye pale pekee kulimpa matumaini mapya.
“Samahani kaka Chris,” akasema yule msichana kwa sauti iliyojaa utulivu na unyenyekevu.
“Achana na samahani...unaitwa nani mrembo?”
“Naitwa Laura.”
“Nice name...sikia...sitaki kukupotezea muda wako. Kikubwa ni kwamba nahitaji kuzungumza na wewe. Si hapa club na ujue kabisa ni mambo ya kazi,” akasema Chris kwa uhakika kabisa.
Laura akatulia kwa muda.
Muda huu sasa, Laura alipata nafasi nzuri ya kumwangalia Chris kwa ukaribu. Aliyafumbua macho yake makubwa yaliyozungushwa na wanja hafifu mweusi na kuyatuliza usoni mwa Chris.
Kuna kitu kipya aligundua; Chris alikuwa mwanaume mwenye wivu na aibu kidogo. Ukimya na uso wake uliojaa bashasha ulizidi kumpa matumaini kuwa amekutana na mwanaume makini.
“Umesema kazi?” akauliza haraka kama aliyegutuliwa mawazoni.
“Ndiyo.”
“Mimi nasoma.”
“Najua lakini unaweza kufanya kazi nje ya masomo yako.”
“Mh! Kazi gani?”
“Sanaa.”
“Unamaanisha filamu?”
“Ndiyo! Wewe ni msanii mkali sana, hujapata nafasi tu. Unaweza kuwapindua wasanii wote wanaotamba Bongo Movies sasa hivi. Niamini mimi. Unaweza sana ni kiasi cha kupewa nafasi na kuelekezwa kidogo sana, utakuwa mkali.”
“Unataka tuzungumze lini?”
“Leo, maana kesho nasafiri kwenda Mkalama.”
“Mkalama ni wapi?”
“Yaani hujui wilaya ambayo ipo katika mkoa unaoishi?”
“Mimi ni mwanafunzi tu hapa, natokea Mwanza. Kule ndiyo kwetu. Niambie kuhusu Ilemela, Sengerema, Kwimba, Ukerewe, Magu, Nyamagana na Misungwi nitakuambia lakini hapa najua hapahapa mjini tu labda sana Ikungi na Manyoni.”
Chris akacheka.
“Haya mama, nimekuelewa vizuri sana. Namaanisha usiku huu.”
“Tukazungumzie wapi sasa?”
“Hotelini.”
Laura akafura!
Macho ya Laura ni kama yalijitokeza yote yalipojificha. Yalizidi kuwa makubwa na kuchambua kope zake zilizotingishika kwa kasi kutokana na kufumba macho na kufumbua mara kwa mara.
Sura ya Laura ilionekana wazi kabisa kuchukizwa na maneno aliyoyasikia kutoka kwa Chris. Alimwangalia kwa dharau kidogo, akimchambua kuanzia chini hadi juu.
“Chris kumbe uko hivyo?” akauliza Laura kwa hamaki.
“Nikoje?”
“Sikia nikuambie, mimi siyo malaya kama unavyonichukulia. Nimekuja club kwa pesa yangu na nitaondoka mwenyewe baadaye kwa muda wangu lakini huwezi kunipata kirahisi hivyo kwa sababu sijui ya pesa zako au kwa vile unajulikana. Mimi siyo wa hivyo. Umekosea njia!”
“Unanifikiria vibaya Laura. Mimi si mwanaume wa namna hiyo. Tafadhali usinipe sifa ambayo si yangu. Naomba unielewe, lengo langu ni kazi tu, hakuna kitu kingine.
“Inawezekana hujajua thamani ya kipaji ulichonacho au hakuna aliyewahi kukuambia kuwa kuna kitu kama hicho ndani yako. Lakini pia inawezekana umeathiriwa na tabia ya wanaume wengi, wakitaka kumsaidia mwanamke lazima wawe wapenzi kwanza...that’s not me!”
“Sasa kwa nini unataka iwe hotelini?” Laura akamwuliza akimkazia macho.
“Vizuri sana. Kwanza ni kwa sababu ndipo nilipofikia lakini pia kuna utulivu mkubwa zaidi ya hapa.”
“Lakini mbona hata hapa tunaweza kwenda kuzungumzia nje?”
“Laura tafadhali heshimu mawazo yangu na unatakiwa kujua kuwa utakuwa salama kwa kila kitu. Tafadhali naomba ukubali.”
“Sawa tutakwenda kuzungumza hotelini lakini kwa masharti!” akasema Laura sasa kwa utulivu.
“Paaaaaa!” moyo wa Chris ukapiga kwa nguvu.
Itaendelea wiki ijayo.

TOA MAONI
 
SEHEMU A 05


SHINDI ulianza kunukia. Kukubaliwa tu na msichana yule kwenda naye hotelini kwa mazunguzo ilikuwa sehemu ya ushindi. Potelea mbali kuhusu masharti aliyosema angempa, yasingemshinda!
“Kwanza masharti yapi?” akajiuliza Chris.
“Hana cha kunishinda huyu,” akazidi kuwaza.
Tabasamu changa lilichanua usoni mwa Chris wakati akizidi kufaidi uzuri wa macho ya msichana yule wa kuvutia; Laura! Kama kungekuwa na mashindano ya kumsaka mwanamke mwenye mvuto hasa wa kike, Laura lazima angeshinda.
Nini hana?
Angalia miguu yake. Hebu mtazamo anavyozungumza kwa mpangilio mzuri. Ona nyusi zake, angalia kiuno. Mwone hata mikono yake laini, mizuri inayoshawishi.
Laura ni mwanamke wa haja. Hana upungufu wowote kwa kumwangalia. Chris alivuta pumzi ndefu sana, kisha akazishusha taratibu. Akanyanyua glasi yake yenye pombe kali na kuipeleka kinywani.
Ilikuwa kali lakini hakujali. Aliifuta yote, aliposhusha glasi chini, ilikuwa tupu! Laura akawa anaangalia sinema ya bure. Akaachia tabasamu changa la kupendeza.
“Sawa kaka Chris?” Laura akauliza.
“Bila shaka Lau.”
“Mbona hujauliza kuhusu masharti?”
“Sina shaka kabisa na masharti yako, najua nitayamudu tu.”
“Unajua ni nini?”
“Kwanza utanirudisha chuo...” akasema Laura kwa sauti ya kudeka.
“Hilo limepitishwa bila kupingwa....lingine?”
“Hatutafanya chochote.”
“Wewe! Chochote lazima tufanye, maana tunakwenda kuzungumza.”
“Mi’ sitaki!”
“Hutaki?”
“Ndiyo sitaki.”
“Sasa mbona umekubali kwenda hotelini?”
“Nimekubali kwa ajili ya mazungumzo tu.”
“Sasa kwani hayo mazungumzo siyo chochote?” akauliza Chris.
Sura ya Laura iliyokuwa imekunjamana sasa ikarudi kawaida kabisa. Tabasamu likaonekana. Uzuri wake ukazidi kuchanua.
“Tuondoke zetu basi!” akasema Chris.
“Poa, twende.”
Waliongozana hadi nje, wakashikana mikono kama vile walikuwa wakifahamiana kabla. Laura alijishangaa sana kumzoea Chris kwa muda mfupi kiasi hicho.
Macho ya watu wote yalikuwa kwao. Tatizo ni umaarufu wa Chris. Moja kwa moja hadi kwenye taksi. Wakaingia.
“Wapi brother?”
“Aqua Vitae Resort.”
“Buku tano tu.”
“Endesha gari kaka.”
Dereva ni kama alikuwa amechanganyikiwa. Haraka akawasha gari na kuliondoa kwa kasi kuelekea Aqua Resort.
***
Chumba kilikuwa kikubwa, kizuri chenye hewa safi iliyochanganyika na manukato hafifu yasiyokera pua. Chris alikuwa amekaa kitandani na Laura kwenye sofa kubwa! Taa chumbani mle ilikuwa ya rangi hivyo kumfanya Laura azidi kuonekana katika mwonekano wa kuvutia zaidi.
Kitanda kilikuwa kikubwa, chenye mito mikubwa minne iliyopangwa vizuri kitandani. Mashuka meupe nayo yalizidi kukifanya chumba kionekane nadhifu zaidi.
Ni saa nane za usiku!
“Karibu sana Laura,” akasema Chris.
“Ahsante sana.”
“Kikubwa nilichotaka kukuambia ni kwamba wewe ni mrembo sana na unaweza kufanya vizuri kwenye sanaa kama ukiwezeshwa na kupewa mwongozo mzuri. Nakuambia ukweli, kuna uwezekano mkubwa sana wa kumfunika hata Wema au Johari.
“Niamini mimi, uwezo wako ni mkubwa sana Laura. Kubali nikusaidie tafadhali. Isitoshe nina sinema yangu mpya ambayo naiandaa, kuna sehemu ndani yake inahitaji sana msichana kama wewe. Nakuhakikikishia wewe ni staa na maisha yako yanaweza kubadilika ukitumia kipaji chako ipasavyo,” akasema Chris kwa sauti ya taratibu sana.
Shoti ya umeme wa mapenzi ilimwingia moyoni. Ilikuwa nafasi kubwa na muhimu sana kwake. Hakutakiwa kufanya ajizi katika nafasi ile ya pekee. Msichana mrembo kama Laura kuingia chumbani kwake halafu aondoke hivihivi?
“Kaka Chris, kweli mimi naweza kuwa msanii? Naweza kuwazidi hata mastaa?”
“Kabisa...niamini mimi. Ni marekebisho madogomadogo tu.”
Chris aliwaza kwa muda, alitakiwa kuwa na mbinu za kisasa ili aweze kumpata Laura. Lakini alijihakikishia moyoni kwamba alimpenda kwa dhati ya moyo wake. Kumpata kwa usiku ule tu halikuwa jambo muhimu kwake, alimtaka kwa maisha yake yote!
“Lakini nikimkosa usiku huu, sitaeleweka. Anaweza kuniona sijakamilika,” akazidi kuwaza Chris.
Itaendelea kesho

TOA MAONI
 
SEHEMU YA 06



ILIPOISHIA...
“Lakini nikimkosa usiku huu, sitaeleweka. Anaweza kuniona sijakamilika,” akazidi kuwaza Chris.
SASA ENDELEA...
HRIS aliinuka kitandani lakini akiwa tayari ameshainuka, akajishangaa maana hakujua aliinuka ili kufanya nini! Hakutaka kuonekana kama alikuwa hajui cha kufanya.
Akamwangalia Laura kwa jicho lililojaa ubembe, kisha akamsogelea na kukaa kwenye sofa kubwa lililotosha kukaliwa na watu wawili tu, akapiga magoti chini yake.
Bado hakujua alichotaka kumwambia. Bahati nzuri, Chris alikuwa na utajiri wa maneno kwa hiyo haikumpa shida sana. Laura akashangazwa na namna Chris alivyopiga magoti mbele yake.
“Sikia nikuambie Laura. Mimi ni mwanaume wa tofauti sana. Mara zote nimekuwa mkweli na ninayeheshimu hisia zangu. Kila kinachotoka kinywani mwangu, huwa yakinifu kabisa,” akasema Chris, kisha akatulia kidogo.
Ni kama alikuwa akifikiria jambo. Kichwani Laura akaanza kuona hisia za mapenzi kutoka kwa Chris kwenda kwake. Pamoja na kwamba alikuwa ameonja kidogo kilevi, hakuwa tayari kumpa Chris mwili wake kwa sababu tu ni staa wa filamu.
Alifika pale hotelini kwa heshima tu. Alimwamini ghafla sana. Hakutegemea kama angetongozwa na hata kama angetongozwa, hakuwa tayari kujiachia kwa siku hiyohiyo!
“Ameanza....nilijua tu. Wanaume bwana!” akawaza Laura.
“Lakini hapati kitu hapa,” akawaza tena.
Chris akaendelea: “Shika haya maneno yangu Laura. Nayaona maisha yako miaka miwili ijayo, jinsi utakavyokuwa staa na maisha yako yatakavyobadilika.
“Acha nikutengeneze. Najua ninaweza kukufanya ukawa juu kuliko unavyowaza. Unacho kipaji kikubwa sana Laura.”
Chris alikuwa akizungumza kwa hisia kali sana. Hata hivyo si kweli kwamba, Laura alikuwa na kipaji cha kuigiza – alikuwa mrembo! Hiyo ilikuwa gia tu ya kumwingiza kwenye kumi na nane zake.
Laura aliachia tabasamu pana. Moyoni Chris akaugulia maumivu ya shoti ya mapenzi. Alizidi kuchanganyikiwa. Kila dakika, kila sekunde, uzuri wa Laura uliongezeka.
Pamoja na kuelezwa yote hayo, Laura hakuzungumza chochote. Alibaki kimya tu akimwangalia Chris. Macho yao kuna wakati yaligongana na wote hawakuweza kuhimili kuangaliana japo kwa sekunde tano tu mfululizo.
Tayari kuna kitu kilianza kuingia moyoni mwa Laura lakini hakukiamini sana. Eti ameanza kumpenda Chris!
“Siyo kweli. Hizi si hisia zangu. Ni pombe tu,” akawaza.
Ghafla Chris akasimama. Alifanya kitendo hicho kwa haraka sana kama aliyeamrishwa. Alirudi nyuma kidogo hadi alipofikia kitandani. Akachukua taulo kubwa pale kitandani kisha akalitupa begani mwake.
“Samahani...” akasema Chris.
“Ndiyo!”
“Naingia bafuni kidogo.”
“Sawa.”
Chris akapiga hatua nyingine fupi, akaufikia mlango wa kuingia bafuni. Akashika kitasa na kukinyonga kidogo. Mlango ukafunguka. Mara moja akaingia, halafu akaufunga.
Punde tu maji yalianza kusikika yakichuruzika. Chris alikuwa anaoga. Alipomaliza, alijikausha vizuri kisha akajifunga taulo yake kiunoni. Akabeba zile nguo zake na kutoka mle bafuni.
Kwa Laura lilikuwa tukio la ajabu sana. Chris aliingia chumbani na taulo tu. Ajabu kubwa ni Chris kutoka na taulo lakini lingine ni mshangao wa mwili wa Chris.
Kutoka moyoni, Laura alikiri kuvutiwa na mwonekano wa Chris. Taulo lilimfanya mwili wake uonekane kwa ukamilifu wake. Kifua cha mazoezi kilionekana dhahiri, huku tumbo lake likiwa limefunikwa na bustani nzuri ya kupendeza!
Siku zote Laura amekuwa akichanganywa zaidi na miili ya wanaume wa namna hiyo. Shoti ya umeme wa mapenzi ikahamia kwa Laura. Bado alikiri kuwa hajampenda Chris lakini angalau kwa usiku ule angemfaa sana!
“Oooooh! Kumbe yupo hivi? Hebu angalia jamani. Chris ananipa mateso sasa,” akawaza Laura alipomwangalia Chris tumbo lake.
“Samahani kwa mara nyingine, sikujali kutoka na taulo kwa sababu najua hakuna tatizo. Wewe ni rafiki yangu. Au nimekosea?” Chris akasema.
“Uko sawa.”
Chris akafungua begi lake kisha akatoa bukta na tisheti, akarudi tena bafuni. Huko alivaa kisha akarudi tena chumbani. Mawazo yalimjaa Chris. Ni kweli alimtaka sana yule mrembo usiku ule lakini aliogopa angeweza kumkosa kama angemwambia mambo ya mapenzi mapema.
Wazo lake kichwani alijua amepata mke, siyo demu wa kuzugia! Mwisho aliamua kuzishinda hisia zake ili aweze kutengeneza kitu chenye manufaa mengine makubwa zaidi mbele yake.
Angejua!!!
Laura yeye aliumizwa sana na mwili wa Chris. Alitamani sana asikie akimwambia angehitaji kuwa naye usiku ule. Ni kwa usiku ule tu! Laura hakuwa na chembe ya mapenzi ya kudumu na Chris.
Hakuna aliyejua kilichokuwa moyoni mwa mwenzake.
Itaendelea siku ya keshooooooooo

TOA MAONI
 
SEHEMU YA 07


ILIPOISHIA...
ILIKUWA hisia kali za mapenzi lakini kila mmoja alikuwa na hofu ya kumweleza mwenzake kwa hofu ya kuonekana malaya. Chris aliugulia akiwa bado amemkumbatia kwa nguvu akiendelea kuhisi joto zuri la kusisimua la Laura.
Laura aliumia sana, hisia za mapenzi ziliwaka kama moto wa kifuu. Alitaka kusema chochote lakini yeye ni mwanamke; ingewezekanaje? Lilikuwa jambo gumu sana kwake.
Ghafla, kwa msukumo wa hisia ambazo hazikuwa na majibu. Laura alijitoa kifuani mwa Chris. Akasimama hatua mbili kutoka kwa Chris.
“Usiku mwema dada Laura!” Chris akasema kwa sauti ya chini.
“Dada!” neno hilo likajirudia kichwani mwa Laura.
Kuitwa dada pekee kulitosha kabisa kumfanya agundue kuwa, Chris hakuwa akimtaka. Bado moyoni mwake alisimamia jambo moja kubwa; hampendi Chris hata kidogo ila hisia za mapenzi za usiku ule pekee ndizo zilizokuwa zikimpelekesha puta!
Akamwangalia Chris kwa makini, kisha akamwambia: “Hunitoi?”
Lilikuwa swali la mtego sana. Kwa usiku ule, saa tisa kasoro za usiku ilikuwa vigumu kwa mtoto wa kike kutoka mwenyewe katika hoteli ile kubwa. Kutoka kwenye chumba walichokuwepo hadi kufika getini ilikuwa ni mwendo wa dakika tatu, kutokana ukubwa wa hoteli ile.
“Nitakusindikiza usijali. Siyo kukusindikiza tu, nitahakikisha unafika salama.”
“Unamaana unataka kunipeleka?”
“Sina maana hiyo, nitamwita dereva akupeleke.”
Wakatoka nje, Chris akafunga mlango na kuanza kutembea wakiwa wameshikana mikono. Wakiwa katikati ya safari yao kuelekea getini, Chris akatoa simu yake na kumpigia dereva wake aitwaye Maulanga. Akamwambia afike haraka sana Aqua Hotel usiku ule.
Kwa kuwa bado alikuwa Skyway Club, ilikuwa rahisi sana, dakika kumi tu zilitosha kumfikisha Maulanga Aqua Hotel. Chris akamwambia Mulanga ahakikishe anamfikisha Laura anapoishi.
“Mambo ya pesa hayo tufanye kesho lakini hakikisha anafika salama ndugu yangu.”
“Sawa kaka.”
Laura akamsogelea tena Chris ambaye alimvutia kwake. Akamkumbatia na kumbusu. Wakaagana. Akaingia kwenye gari na baada ya muda mfupi sana, Maulanga aliingiza gia namba moja.
Gari likayoyoma!
***
Kwa mbali Chris alijilaumu na kujiona mjinga kwa kumkosa Laura. Taratibu kila kilichotokea chumbani akiwa na mrembo yule, kikaanza kujirudia kichwani mwake.
Kulikuwa na kila dalili za Laura kumwelewa somo lake lakini akajisahau na kuamua kuachana na jambo hilo.
Chris aliumia sana. Hata hivyo alijipa moyo akiamini kwamba, lengo lake hasa halikuwa kumtumia kwa usiku mmoja, bali awe mke wa maisha yake yote.
Jambo hilo ndilo lililompa moyo na kuamini kuwa, bado Laura angekuwa wake! Uchovu wa pombe, mawazo ya mapenzi na baridi kali ya Singida usiku huo, vilimfanya Chris asichukue muda mrefu kupata usingizi!
Akapotelea usingizini.
***
Aliamka akiwa mchovu sana, bado mning’inio wa ulevi uliendelea kumsumbua. Alijimwagia maji kisha akatoka na kwenda mgahawani kupata kifungua kinywa, akarudi tena chumbani kwake.
Kwa kuwa alipanga kusafiri kwenda kijijini Mkalama siku iliyofuata, aliamua kuhama hoteli na kwenda Kibaoni, jirani na Stendi Kuu ya Mabasi ya Mikoani Singida, Misuna.
Maulanga ndiye aliyemsaidia kupata hoteli nzuri iliyokuwa barabara kuu ya Dodoma – Mwanza. Akampigia Laura na kumwelekeza. Akaahidi kufika hapo saa kumi jioni.
***
Laura hakuwa mwongo, alifika pale hotelini kama walivyokubaliana na Chris ingawa alichelewa kwa saa nzima mbele. Alimpigia Chris aliyemwelekeza hadi chumbani kwake.
Akaingia.
Mazungumzo ya hapa na pale yakaendelea, huku jambo kubwa lililotawala likiwa ni kumsaidia Laura ili aweze kuwa msanii mkubwa wa filamu za Kibongo.
Mwisho Chris hakuweza kuvumilia. Mazoea ya muda mrefu yalimfanya amweleze ukweli Laura kuhusu maisha yake yote na lengo la safari yake kuelekea kijijini Mkalama.
“Tafadhali usinifananishe na wahuni, moyo wangu umetuama kwako. Hapa natakiwa kuoa, baba amenipa miezi mitatu tu ya kukamilisha jambo hilo. Najua siwezi kukutana na mwanamke wa hadhi yangu kijijini.
“Nimekupenda wewe na naamini hisia zangu. Ndiyo maana hata jana sikutaka kufanya chochote na wewe kwa sababu najua ninachohitaji kwako ni kikubwa zaidi ya tendo la usiku mmoja tu.
“Tafadhali naomba unisaidie kwa hilo. Nipe nafasi moyoni mwako. Nakupenda sana Laura,” Chris akasema kwa hisia kali sana.
Itaendelea kesho...

TOA MAONI
 
SEHEMU YA 08


“Tafadhali naomba unisaidie kwa hilo. Nipe nafasi moyoni mwako. Nakupenda sana Laura,” Chris akasema kwa hisia kali sana.
SASA ENDELEA...
HUMBA kilikuwa kikubwa chenye kila kitu. Giza jepesi la jioni lilianza kuchukua nafasi chumbani mle. Taratibu jua liliendelea kuzama na kufanya ukimya wa jioni uanze kuingia taratibu.
Ndani ya chumba hiki, watu wawili walikuwa wamezama katika mazungumzo muhimu sana. Dk. Chris anajaribu kueleza namna anavyougulia mapenzini kwa msichana mrembo Laura.
Kwa hakika Chris aliamua kujitutumua. Alijihisi mpweke na hakutaka kabisa kumkosa. Tayari alishakatisha safari yake ya kijijini kwao ambako alitakiwa aende kutafuka mke huko.
Laura alimtosha kabisa.
Laura ni kama hakusikia vizuri kauli ya Chris. Kama alisikia basi alikuwa hajaamini maneno ya kijana huyo ambaye anasumbua katika ulimwengu wa filamu za Kibongo.
“Chris una hakika na unachokizungumza?” Laura aliuliza kwa sauti laini, tamu ambayo ilikuwa burudani tosha kwa Chris.
Jibu lilikuwa rahisi sana: “Nina zaidi ya hakika Laura. Nipe nafasi. Nitaumia sana nikikukosa. Moyo wangu umeniambia unakupenda wewe tu. Tafadhali usiniumize wala kuniadhibu.”
“Siamini maneno yako Chris.”
“Kwa nini mama?”
“Sikuamini tu. Nyie wanaume maneno mengi sana, hasa ninyi wasanii. Mh! Hapo utasema maneno yote lakini ukinipata tu, mapenzi yanaishia hapo. Kwa kweli nimeondoa kabisa imani na wanaume.”
“Kuna tofuati kubwa sana kati ya wanaume na Chris. Mimi ni tofauti na wengine wote unaowajua au uliowahi kukutana nao. Mimi ni kweli ni mwanaume, lakini ni Chris. Nipe nafasi tafadhali.”
Kama ni filamu basi Chris alikuwa kwenye kipande cha mapenzi na aliweza kuvaa uhusika wake kisawasawa. Unaweza kudhani hivyo, lakini safari hii Chris hakuwa mbele ya kamera.
Alikuwa akizungumza kutoka ndani na kueleza hisia za kweli za moyoni mwake. Laura alimteka kwa hakika.
“Hata kama nikikubali Chris, kumbuka baba yako ameshasema anataka mke wako atoke kijijini. Angalia... kwanza mimi siishi kijijini, pia siyo Mnyiramba kama baba yako anavyotaka. Mimi ni Msukuma. Itakuwaje?”
“Najua cha kufanya Laura. Ninalo wazo.”
“Wazo gani?” Laura akauliza harakaharaka.
“Lipo lakini nataka kujua kwanza kutoka kwako. Wewe unanipenda?” Chris akamwuliza Laura.
“Ndiyo... kwa nini nimchukie binadamu mwenzangu? Nawapenda watu wote.”
“Tafadhali Laura, usiniumize hisia zangu. Usiutese moyo wangu tafadhali. Nazungumzia mapenzi hapa. Tunajadiliana kuhusu maisha mama. Tafadhali chukulia kwa uzito huohuo Laura.”
“Nakupenda Chris,” Laura akasema mara moja tu, akanyamaza.
“Kweli?”
“Ndiyo... lakini bado kuna mambo nahitaji kuzungumza kidogo na wewe. Kuna vitu nataka kujua zaidi kuhusu wewe. Nadhani tukutane Club jioni, tuzungumze zaidi.”
Chris alisimama alipokuwa amekaa, akapiga hatua fupi nne, akamfikia Laura. Akamnyooshea mikono yake miwili kama ambaye alitaka kupokewa. Laura akaipokea.
Taratibu Chris akamwinua Laura, akasogea mzimamzima. Akamlaza kifuani mwake. Miili yao ikakutana. Wote kwa pamoja wakapata msisimko mkali sana.
“Nakupenda sana Laura,” Chris akatokwa na maneno hayo huku akimwaga machozi.
“Nakupenda pia Chris, sikutegemea kama ningekupenda kwa kiwango hiki. Ngoja niwe mkweli... sikukupenda hata kidogo lakini sasa naona ni kwa namna gani ningepoteza mtu muhimu sana maishani mwangu.
“Nimekupa kila kitu mpenzi wangu. Nakupa moyo wangu. Chukua mwili wangu. Nichukue baba. Nichukue mpenzi. Mimi ni wako kwa kila kitu. Nifanye upendavyo!”
Chris akasisimka!
Sheria yake ilikuwa ileile. Ndani ya nafsi yake, huba zito lilimlemea. Kamwe hakutaka kuonekana mhuni. Pamoja na maneno yale ya Laura kuashiria kwamba alikuwa tayari kwa lolote, moyoni Chris alikataa!
“Ahsante dear. Nami nimekukabidhi kila kitu mpenzi wangu. Nakupenda sana.”
“Nitoe baba niondoke, jioni tukutane Club sawa?”
“Sawa mama.”
Wakatoka nje wakiwa wameshikana mikono. Laura akaingia kwenye taksi na kuondoka zake. Ahadi ilikuwa kukutana Club usiku.
***
Ni saa nne na dakika zake usiku. Chris alikuwa anatoka kwenye Baa ya G8, Kibaoni. Kutoka hapo hadi ilipo hoteli yake ni jirani mno, ni mwendo wa dakika mbili tu kwa miguu. Njiani akakutana na mmoja wa wahudumu wa hoteli aliyofikia.
Akamwambia: “Kaka unatafutwa na maaskari. Kumbe yule mwanamke uliyekuwa naye chumbani ni mke wa polisi, tena ni mkuu pale Central. Wamekuja maaskari wanne na silaha wanakutafuta. Mimi nakushauri usirudi tena. Tafuta mahali ulale mpaka asubuhi wakati tukitafuta ufumbuzi wa hili jambo,” alisema akionekana kujawa na wasiwasi mwingi.
Itaendelea siku ya kesho

TOA MAONI
 
SEHEMU YA 09


ILIPOISHIA...“Kaka unatafutwa na maaskari. Kumbe yule mwanamke uliyekuwa naye chumbani ni mke wa polisi, tena ni mkuu pale Central. Wamekuja maaskari wanne na silaha wanakutafuta. Mimi nakushauri usirudi tena. Tafuta mahali ulale mpaka asubuhi wakati tukitafuta ufumbuzi wa hili jambo,” alisema dada yule harakaharaka huku akionekana kujawa na wasiwasi mwingi.
Pombe yote ilimruka!
SASA ENDELEA...
I kama alikuwa hajanywa hata tone moja la pombe. Kichwa kilikuwa tupu kabisa. Bado alikuwa na maswali mengi kichwani mwake; inawezekana kweli Laura akawa mke wa mtu? Labda inawezekana lakini vipi amwache mumewe na kwenda kujirusha klabu?
Kichwa kiliwaka moto. Aliumizwa na mengi. Achana na kukamatwa na pengine kufunguliwa mashitaka lakini alijilaumu kwa kujichelewesha kumpata. Angalau angekuwa amefaidi uzuri wake, kidogo ingepooza maumivu ya kile alichoelekea kukikabilia.
Alimwangalia yule msichana kwa jicho lenye maswali lukuki, lakini alionekana kama ambaye hana majibu sahihi ya maswali yaliyozunguka kichwani mwake.
“Sikia dada, mimi huwa sipendi mizaha kabisa. Hebu niambie ukweli, kuna maaskari wamekuja pale?”
“Ndiyo!”
“Wamevaa nguo za polisi?”
“Ndiyo, tena kuna mwingine amevaa koti jeusi.”
Moyo wa Chis ukalipuka.
“Wamenitaja jina?”
“Ndiyo. Wamesema wanamtaka Dk. Chris. Tena alitaka tuwafungulie mlango ili wakague chumba chako, tukakataa. Kwa inavyoonekana itakuwa ni kweli. Hili ni tatizo kaka yangu, tafuta mahali pengine pa kulala.”
Chris akatulia kidogo.
Mawazo yakazidi kumwandama. Kuna kitu aliwaza; iweje leo hii Laura awe mke wa mtu? Mbona hakuwa na pete kidoleni? Laura si mwanafunzi?
“Au kuna mchezo nachezewa?” akajiuliza Chris.
“Halafu kama ni mchezo mtu wa kunisaidia hapa ni mmoja tu, Maulanga.”
Ni kweli Maulanga, dereva taksi aliyekuwa akimtumia kwa mizunguko yake pale mjini ndiye ambaye angeweza kumsaidia kujua ukweli wa tukio lile. Ni Maulanga huyohuyo ndiye aliyempeleka Laura kwenye nyumba anayoishi.
“Kwahiyo dada unanishauri nisije kabisa pale?”
“Huna haja ya kufanya hivyo, lakini kama unaona nakudanganya nenda. Wamesema watarudi tena baadaye, maana wameagizwa na mkuu wao, ukamatwe kabla ya asubuhi.”
Moyo wa Chris ukapiga.
“Sawa, ahsante kwa taarifa. Ngoja nitulize kichwa, nitajua cha kufanya. Kwa sasa naomba tu unisaidie namba yako ya simu tafadhali,” akasema Chris, yule dada akatekeleza.
“Unaitwa nani vile?”
“Mwanjaa.”
“Ok.”
Palepale Chris akaamua kubadilisha kiwanja ili atulize kichwa chake wakati akitafakari cha kufanya. Mwanjaa alirudi zake alipotoka, Chris akachukua bodaboda na kumwambia dereva ampeleke Baa ya Serengeti iliyokuwa katikati ya mji.
***
Chris akiwa Serengeti Bar, alimpigia simu Maulanga na kumwambia amfuate pale haraka sana. Maulanga hakuwa mbali na eneo, alikuwa ameegesha jirani na Benki ya CRDB, lilipo Jengo la TRA la Mkoa wa Singida. Dakika mbili baadaye alikuwa pale.
“Hivi yule msichana uliyempeleka hosteli jana usiku unamfahamu?”
“Namuona sana klabu karibu kila wikiendi, huwa anakuja na rafiki zake.”
“Unajua kuwa ni mke wa mtu?”
“Mke wa mtu? Sina hakika kwa kweli.”
“Kivipi?”
“Yaani sifahamu chochote ingawa nahisi kwamba atakuwa ni mwanafunzi. Si anasoma chuo?”
“Kwanini unasema unahisi? Kwani siku ile hukumfikisha hosteli?”
“Kuna nyumba aliingia, akasema anaishi hapo na dada yake.”
“Lakini mimi aliniambia anaishi hosteli. Dah! Sijui hii ishu ikoje! Nasikia wamekuja maaskari pale gesti, wananitafuta.. eti wanasema niliingia na mke wa mtu mle ndani na mumewe ni askari.”
“Mh! Mbona majanga haya kaka. Sasa unafanyaje?”
“Niachie mwenyewe, nitajua cha kufanya. Wewe nenda, nitakuita baadaye.”
“Poa.”
Chris alianza kunywa upya kabisa. Baadaye akapata wazo. Alitakiwa kupumzika ili siku inayofuata aweze kwenda zake kijijini kwao. Wazo la Laura alishalifuta kabisa. Aliona tatizo likiwa mbele yake waziwazi kabisa!
Akatoka pale Serengeti Bar na kutafuta gesti nyingine jirani na eneo lile, akalala. Katikati ya usiku, simu yake ikapigwa. Alipoangalia kwenye kioo cha simu, alishtuka sana.
Alikuwa ni Laura anampigia!
Itaendelea.

TOA MAONI
 
SEHEMU YA 10


MACHO ya mshangao yalimtoka. Woga ukamjaa moyoni mwake. Alibaki akiingalia ile simu bila kuipokea. Mara simu ikakatika. Hapo sasa akapata nafasi ya kuangalia simu yake vizuri.
Alikuta meseji nne, zote zilitoka kwa Laura. Alipoifungua ya kwanza tu, simu ikaanza kuita tena. Chris akazidi kuogopa. Akili yake ilimtuma kwamba, huenda aliyekuwa akipiga alikuwa ni mume wa Laura au walikuwa pamoja na alilazimishwa kufanya hivyo ili aingie mtegoni.
Hakuwa tayari!
Simu ilipokatika, mara moja akaanza kusoma ile meseji. Maneno aliyoyasoma yalimchanganya sana. Hakuamini alichokiona. Meseji ile iliandikwa: “Kwa muda mfupi sana umeuteka moyo wangu, tafadhali Chris usinitese. Mbona hujanitafuta wakati tulikubaliana tukutane klabu?”
Inawezekana vipi mwanamke ambaye aliambiwa ni mke wa mtu ampigie simu usiku ule tena akimwambia kuwa anatakiwa kwenda kukutana naye klabu? Jambo hilo lilimchanganya sana kichwa chake.
Akaendelea kusoma nyingine mfululizo: “Baba vipi jamani? Mbona kimya? Acha kunitesa.”
“Chris nimekuwa tayari kukukabidhi moyo wangu wote kwako, mbona sasa huonyeshi kuwa upo tayari?”
“Sikia, tayari mimi nipo klabu hapa, kama huji niambie nirudi zangu hosteli nikapumzike. Nimekuja hapa kwa ajili yako Chris.”
Meseji ya mwisho ndiyo iliyomchanganya zaidi. Anamwambia anataka kwenda hosteli? Ni hosteli gani wakati alishaambiwa kuwa ni mke wa mtu?
Kwa hakika usingizi wote ulipotea. Pamoja na yote hayo, alijua alikuwa mtegoni na kama angejibu chochote angeweza kukamatwa mara moja. Kwa mtu mkubwa kama mkuu wa kituo cha polisi, maana yake ni kwamba, kama angeamua kumfanyia chochote kwa kosa la kutembea na mke wake, angeweza!
Wazo moja la haraka likamvamia kichwani mwake; alitakiwa kuvunja kabisa line yake. Hakutakiwa kupatikana tena kwa namba ile. Hilo ndilo wazo lililomwingia kwa kasi sana. Hakutaka kufikiria sana kuhusu hilo.
Akavunja ile line na kuitupilia mbali!
“Shiiit! Tuone sasa, watanipata wapi! Kwanza mimi sijafumaniwa. Najua wakiamua kunitafuta watanipata, lakini natakiwa kuwa mjanja sana kwenye eneo hilo. Hawawezi kunikamata asilani.”
Hasira ilimjaa moyoni. Alishindwa kuelewa ni kwa nini Laura aliamua kumdanganya kuwa hajaolewa wakati alikuwa mke wa mtu, tena wa askari kabisa. Jambo hilo lilimuumiza sana.
Akajilazimisha kulala.
***
Nani asiyemjua Dk. Chris, msanii wa filamu za Kibongo? Kila kona alijulikana. Hilo lilimaanisha kuwa, kama polisi mkoani Singida wangeamua kumtafuta kwa dhati kabisa, wangemkamata mapema sana asubuhi hiyo.
Chris alilijua hilo. Mara baada ya kuamka, alikwenda moja kwa moja mapokezi na kumuomba mhudumu akamnunulie kofia ya kapero. Yule mhudumu hakuwa na maswali mengi, alichukua fedha kwa Chris kisha akaenda kununua kofia na kumpelekea.
Chris akaichukua na kuivaa baada ya kujiandaa kikamilifu. Alitoka nje ya gesti hiyo na kutembea kwa mwendo wenye tahadhari zote. Taratibu akiwa ameuficha uso wake kwa kapero, alikodi teksi na kumtaka dereva ampeleke stendi kuu ya mabasi mkoani Singida, Misuna.
Dakika tano tu zilitosha kumfikisha kituoni hapo. Alishuka na kumlipa dereva kisha akatembea hadi katika ofisi za basi la Beffe, linalofanya safari zake kutoka mjini kwenda wilayani Mkalama kupitia Iguguno na Nduguti.
“Gari linaondoka saa ngapi?” Chris akamwuliza dada aliyekuwa akimkatia tiketi.
“Saa tano kamili, kwa sababu leo tunapita hadi Meatu.”
“Sawa, nipatie tiketi lakini kuna shughuli zangu nazifanya hapa mjini, sitapandia hapa. Mtanikuta kwenye mizani huo muda.”
“Tafadhali usije kulalamika umeachwa, saa tano juu ya alama uwe pale, sisi tutakukuta hapo.”
“Haina shida dada.”
Chris akalipa kisha akaondoka zake na kwenda kuchukua teksi nyingine iliyompeleka Kibaoni, ambapo ndipo gesti iliyokuwa na begi lake na vitu vyake vingine. Gari liliingia eneo hilo na kuegesha mbele ya geti.
“Naomba ukaniitie mhudumu tafadhali,” Chris akamwomba yule dereva ambaye alitii.
Sekunde chache sana, Mwanjaa alitokea, akakutana na swali kutoka kwa Chris: “Vipi, jamaa walirudi tena jana?”
Chris alisubiria jibu la Mwanjaa akiwa mwenye wasiwasi mwingi sana. Bado hakuijua hatma yake.
Itaendelea kesho.
 
SEHEMU YA 11


Chris akalipa kisha akaondoka zake na kwenda kuchukua taksi nyingine iliyompeleka Kibaoni, ambapo ndipo gesti iliyokuwa na begi lake na vitu vyake vingine. Gari liliingia eneo hilo na kuegesha mbele ya geti.
“Naomba ukaniitie mhudumu tafadhali,” Chris akamwomba yule dereva ambaye alitii.
Sekunde chache sana baadaye, Mwanjaa alitokea, akakutana na swali kutoka kwa Chris: “Vipi, jamaa walirudi tena jana?”
Chris alisubiria jibu la Mwanjaa akiwa mwenye wasiwasi mwingi sana. Bado hakujua hatma yake.
SASA ENDELEA....
WASIWASI ulimjaa moyoni akiwa hajui kabisa kilichotokea usiku wa kuamkia siku hiyo. Macho yake aliyatuliza usoni mwa Mwanjaa akisubiri kusikia jibu lake. Mwanjaa alionekana kusita kidogo.
“Vipi... walikuja? Naomba uniambie haraka maana natakiwa kuondoka.”
“Hapana,” Mwanjaa akajibu.
“Asubuhi hii?”
“Pia hawajaja.”
“Sikia... naomba unichukulie begi langu pale ndani, kuna vitu vyangu vingine vidogovidogo vipo kwenye kabati.”
“Sawa kaka.”
Mwanjaa akatoka haraka na kwenda ndani. Dakika tatu baadaye, alitoka ndani akiwa na begi la Chris. Ghafla Mwanjaa akaonekana kusimama na kuonyesha kuwa na mshangao mkubwa sana.
Chris alipoangalia barabarani, akashtuka sana baada ya kuwaona maaskari wanne wenye silaha wakivuka mfereji mdogo uliokuwa pembeni mwa barabara kuu ya Dodoma – Mwanza. Pembeni waliegesha karandinga lao. Kufumba na kufumbua, taksi ilikuwa imezungukwa na maaskari wale.
“Nimekwisha!” Chris akajisemea moyoni.
“Hamtakiwi kufanya chochote kwa sasa,” mmoja wa maaskari wale akasema.
“Tumefanya nini?” Chris akauliza.
“Haya mikono juu,” akasema yule askari.
Wakafanya hivyo.
Maaskari wawili kati yao, waliingia garini na kuanza upekuzi, baadaye wakamuamuru dereva afungue buti. Wakakagua lakini pia hawakuona walichokuwa wakikitafuta ambacho pia hawakusema ni nini.
“We’ dada, hiyo mizigo ni ya nani?” mmoja wao akauliza.
“Wa huyo hapo...” Mwanjaa akajibu haraka akimsonza kidole Chris.
“Lete.”
Mizigo ikapelekwa.
Haraka ikaanza kukaguliwa, Chris alikuwa akipewa maelekezo na kuambiwa atoe nguo moja baada ya nyingine na vitu vingine vilivyokuwa ndani ya begi lake.
“Wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Dk. Christopher.”
“Unatokea wapi?”
“Dar es Salaam.”
“Unaelekea wapi?”
“Nakwenda Kiomboi,” akadanganya Chris.
“Tunaweza kuona kitambulisho chako?”
“Bila shaka.”
Mara moja Chris akatoa na kuwapa. Wasiwasi ulikuwa moyoni lakini kwa namna fulani ulianza kuondoka akiwa na imani kuwa walichokuwa wakikifuatilia kwake hakikuwa kuhusu Laura tena.
Wakakagua kitambulisho chake kisha wakamrudishia.
“Wewe dada ni nani?” askari mmoja akamwuliza Mwanjaa.
“Mhudumu.”
“Nahitaji kuona kitabu chako cha wageni,” akasema yule askari akiongozana na Mwanjaa ndani.
Alipofika getini yule askari ambaye alionekana ndiye kiongozi wao, aligeuka na kusema: “Ninyi mnaweza kwenda.”
Chris akaingia kwenye gari, dereva akawasha moto, akaondoa gari.
***
Maswali yalikuwa mengi kuliko majibu, lakini jambo kubwa kwa Chris wakati ule ni kwamba alikuwa amefanikiwa kuondoka mikononi mwa hatari ya kuingizwa kwenye kashfa ya kutembea na mke wa mtu. Yaliyoendelea nyuma hayakuwa na maana kwake.
Ndani ya Basi la Beffe, Chris alikuwa kimya kabisa, akitafakari mtihani wake uleule; kwenda kuoa kijijini.

***
Laura alikuwa akitengeneza nywele zake saluni iliyokuwa Ginnery. Hisia zake za ndani bado ziliendelea kumhakikishia kuwa Chris ndiye angekuwa mwanaume wa maisha yake. Hakutaka kusikia mwanaume mwingine zaidi yake.
Alijiuliza, kwanini hakupokea simu yake? Kwanini hakuonekana klabu kama walivyokubaliana? Kwanini hapatikani hewani?
“Kwanini naingia kwenye mateso makubwa kiasi hiki? Nampenda Chris, nina hakika na hisia zangu. Sikutegemea kama hili lingetokea kirahisi hivi, lakini inanipasa nikubali kuwa nimeshatekwa na ninampenda. Nitahakikisha nampata Chris, lazima,” aliwaza Laura.

Itaendelea.
 
SEHEMU YA 14


ILIPOISHIA...
Alikuwa akimfuata msanii mwenzake Ramsey.
SASA ENDELEA...

ALIKANYAGA mafuta kisawasawa, foleni ni kama ilikuwa hakuna kabisa usiku huo. Dakika kumi tu zilitosha kabisa kumfikisha Mzalendo Pub. Akaegesha gari lake kisha akapanda hadi ghorofa ya kwanza ilipo Pub hiyo.

Hakupata shida kujua Ramsey alipokuwa amekaa maana walikuwa na kawaida ya kukaa sehemu moja ndani ya Pub hiyo kila walipokwenda. Alimfuata akiwa ameachia tabasamu mwanana.
“Vipi kaka?” Ramsey akamsalimia.
“Poa, mambo?”

“Fresh kabisa... vipi za kijijini?”
“Daaah! Huko acha tu. Yaani habari ndefu sana kaka. Nimekutana na mengi sana huko.”
“Usiniambie umepata mwanamke wa ukweli tayari... ni Mnyiramba au Mnyaturu?” akauliza Ramsey.
“Mh! Wapi ndugu yangu? Majanga tu mzee.”
“Imekuwaje?”

“Ngoja nikusimulie.”
Chris akakaa sawasawa... ni muda huo mhudumu alifika mezani kwake na kutaka kumsikiliza. Aliagiza pombe kali. Wakati mhudumu anakwenda kaunta kumchukulia kinywaji chake, Chris alianza kumsimulia Ramsey.

Hakuna alichomficha, alimweleza yote yaliyotokea Singida Mjini. Mipango waliyopanga na baba yake mdogo, Shamakala na namna alivyozugumza na baba yake baada ya kuingia Dar usiku huo.
“Aisee una kazi kaka. Yote hayo nimekusikia lakini sasa nahisi mzee mzima unaweza kuingia kwenye skendo!”

“Skendo?” Chris akahamaki.
“Ndiyo! Kama huyo mwanamke wa Singida kweli ni mke wa mtu, tena wa polisi, kuna nini tena kaka? Utachafuka!” Ramsey akasema kwa msisitizo.
Chris akabaki kimya.

Maneno yale yalimwingia akilini. Alitulia akifikiria kwa kina, akajikuta akipoteza furaha. Ni kweli alikuwa maarufu kiasi kwamba, mtu yeyote akitaka kumpata muda wowote ingekuwa rahisi tu.
“Lakini kaka, ukweli ni kwamba sikutembea naye!” Chris akamwambia Ramsey.
“Sawa ila si ulikuwa naye chumbani?”

“Kaka kuna mambo ya kisheria hapo. Hata kama nilikuwa naye chumbani, hakuna mtu aliyenikuta nikiwa naye huko chumbani. Kama ningekuwa nimefumaniwa ingekuwa sawa, lakini maneno tu ya mtaani yanaweza kunikamatisha na kuniweka ndani?”
“Kaka tunywe tu bwana!” akasema Chris kwa sauti ya kilevi.

“Ndicho kilichobaki mkubwa. Aisee nina majukumu mengi sana wiki hii. Sijui itakuwaje lakini nitajipanga,” akasema Chris.
Pombe zikaendelea. Haikuwa rahisi kwa Chris kukaa pale muda mrefu hasa kwa sababu ndiyo kwanza alikuwa ameingia Dar. Bado mawazo juu ya Laura yaliendelea kumzonga.
Alitamani sana Laura asingekuwa mke wa mtu!

***
Laura alipoteza amani ya moyo kabisa... mwanaume aliyempenda ghafla haonekani tena mbele yake. Alifikiria sana namna ya kumpata lakini alikosa majibu.
Alijiuliza maswali mengi sana, lakini mwisho alipata wazo zuri. Lilikuwa jambo gumu sana kwake lakini alikuwa tayari mradi ampate Chris.

“Lazima niende Dar es Salaam...” akawaza Laura.
Lilikuwa wazo zuri lakini lingetumia muda mwingi sana kukamilika. Alikuwa tayari kupoteza masomo japo kwa wiki moja ili aweze kumpata Chris, mwanaume wa maisha yake.
Mara moja akaanza kupanga mipango ya safari ya kwenda Dar es Salaam.

***
Laura alikuwa amedhamiria hasa. Wiki moja baadaye alikuwa jijini Dar es Salaam. Saa 11:00 jioni alikuwa anashuka ndani ya Basi la ABC katika kituo kikuu cha mabasi ya mikoani na nchi jirani, Ubungo jijini Dar es Salaam.

Alikuwa amechoka sana. Hakuwa mgeni wa Dar es Salaam. Alikuwa na ndugu zake wawili waliokuwa wakiishi jijini humo ambao kuna wakati huwa anakwenda kuwatembelea.
Mama yake mdogo aishiye Kurasini na mjomba wake anayeishi Gongo la Mboto ndiyo ndugu zake jijini Dar. Hakutaka kabisa wajue uwepo wake jijini Dar kwa sababu alikwenda kwa sababu maalum.

Alichukua taksi na kumwambia dereva ampeleke Manzese. Huko aliamini angepata gesti ya bei nafuu ambayo angeishi hapo kwa wiki nzima wakati akimtafuta Dk. Chris.
Wakiwa wanakaribia mataa ya Shekilango, Laura akavunja ukimya, alijua kwa kumtumia dereva yule angepata mwanga wa wapi pa kuanzia ili aweze kumpata Chris.

“Kaka hivi nawezaje kumpata Dk. Chris, yule mcheza filamu?” Laura aliuliza kwa sauti laini, akiyalegeza macho yake na kumfanya dereva apoteze umakini barabarani.
“Vipi unataka kumwa mwigizaji au umeshampenda bibie?” dereva yule akajibu huku akiachia tabasamu, macho yake akiwa ameyatuliza kwa Laura.

Aliporudisha macho yake barabarani, alishangazwa sana na kitu kilichotokea!
“Nakufaaa....” Laura akapiga kelele.

Usikose kufuatilia kesho.
 
SEHEMU YA 15


ILIPOISHIA...Aliporudisha macho yake barabarani, alishangazwa sana na kitu kilichotokea!
“Nakufaaa…” Laura akapiga kelele.
SASA ENDELEA…
UZURI wa Laura ulikuwa tishio, dereva alishachanganywa na uzuri wa Laura. Pamoja na urembo wa sura yake, hakuweza kuficha ushamba wake wa jiji kubwa la Dar es Salaam. Ingawa alikuwa na ndugu zake, lakini hakuwa akienda Dar mara kwa mara.
Macho ya kuangaza kila mahali, hakuweza kuyaepuka! Ni sababu hiyo ndiyo ilimfanya dereva achanganyikiwe na kutokuwa makini barabarani. Gari lilikuwa mbele yake kwenye mataa ya Shekilango hakuliona. Aliliona likiwa mita chache sana mbele yake.
Alifunga breki kwa nguvu... Laura akafumba macho ili asishuhudie ile ajali. Kwa bahati nzuri, akiwa anakaribia kabisa kuligonga lile gari, tayari magari yalishaanza kutembea... taa ya kijani ilishawaka! Hiyo ndiyo ikawa salama yao!
Taratibu wakateleza. Laura alifumbua macho, akahema kwa kasi sana.
“Weweee jamaniiii!” akasema kwa sauti dhaifu, akijaribu kuvuta pumzi ndefu sana...
Akazishusha taratibu kabisa!
“Kumbe wewe mwoga sana?” dereva yule akasema, safari hii akiwa makini sana barabarani.
“Kwani we huogopi?”
“Naogopa pia... lakini usijali. Tatizo ni wewe bwana!”
“Tatizo mimi, kivipi?”
“Tuachane na hayo, kuhusu hawa jamaa wa Bongo Movies, ukitaka kuwapata kwa urahisi ni Jumamosi mara nyingi wanakutana Leaders Club.”
“Kinondoni?”
“Ndiyo.”
“Huwa wanafanya nini hapo?”
“Si unajua tena mambo ya wasanii, wanakutana na kujadiliana mambo yao tu. Kiukweli sijui mambo yao vizuri zaidi ya hapo.”
“Ahsante, najua nitaweza kuanzia hapo. Ingia hapo kushoto, nataka kushukia hapo Tip Top.”
“Barabarani kabisa au unataka nikuingize ndani?”
“Hapana, hapo barabarani tu panatosha kabisa.”
Dereva akapinda kushoto na kuegesha nyuma kidogo ya kituo cha daladala, Tip Top. Laura akamlipa yule dereva na kubaki hapo amesimama kwa muda. Dereva akaondoa gari.
Laura aliangaza macho huku na huko, kisha akaamua kuifuata barabara ya vumbi iliyokuwa ikielekea Manzese – Uzuri. Alitembea taratibu kwa mtindo wa kuangaza huko na huko. Mbele kidogo akaona bango dogo juu ya nyumba limeandikwa Waridi Lodge.
Laura akatabasamu. Akaenda mpaka hapo, akapita moja kwa moja Mapokezi. Akapokelewa na dada mrembo sana, lakini alijihakikishia kuwa, pamoja na urembo wa dada huyo, bado hakufua dafu mbele yake! Yeye alikuwa mzuri kuliko huyo msichana!
“Nahitaji chumba,” akasema Laura.
“Umepata mrembo!”
Laura akaandikisha kwenye kitabu cha wageni. Kisha akepelekwa kwenye chumba chake.
***
Ilikuwa Jumamosi, wasanii wengi wa filamu walikuwa wamekaa kwenye viti vya plastiki, pembeni mwa uwanja wa mpira wa pete katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Eneo karibu lote lilikuwa na watu wengi sana.
Mapema sana!
Saa tano asubuhi!
Supu ilinywewa kwa fujo, wengine nyama choma na bia. Kifupi watu walikuwa kwenye mapumziko ya mwisho wa wiki. Wengi wa wasanii wale walikuwa ni wanachama wa klabu yao ya Bongo Film. Wasanii wa klabu hiyo hukutana hapo kila Jumamosi kwa ajili ya kuweka mikakati yao ya kisanii.
Ilibaki nusu saa tu kikao rasmi kianze.
***
Aliteremsha mguu wa kwanza chini kutoka kwenye gari alilokuwa amepanda. Kisha ukafuata mwingine. Baadaye, mwili mzima ulitoka ndani ya gari. Akasimama na kusukuma mlango kwa nguvu wa gari kwa nguvu. Akapunga mkono kumuaga dereva, ambaye aligeuza gari na kuondoka.
Alikuwa msichana mrembo kuliko kawaida. Namna yake ya kutembea ikawa kivutio kingine kwa watu waliokuwa wakimtazama wakati akitembea kwa madaha. Macho yote yalikuwa kwake. Si wanaume wala wanawake.
Wote walishangazwa na uzuri wa msichana yule. Kwa alivyoonekana alijua alichokuwa akikifanya. Alijua alipokuwa anakwenda na alimjua aliyekuwa akimfuata. Alinyoosha moja kwa moja hadi walipokuwa wamekaa wasanii wa filamu.
Wasanii wote wakapagawishwa na uzuri wake. Akasimama katikati yao, akawaangalia kwa zamu, kisha akavua miwani yake myeusi iliyokuwa usoni mwake. Macho yake mazuri yakawa tatizo lingine!
“Samahanini jamani... samahani sana ndugu zangu. Nimekuja hapa kwa sababu ya mtu mmoja tu; Chris!” akasema msichana yule.
Alikuwa ni Laura.
Dk. Chris alishtuka sana alipomuona Laura eneo lile. Akasimama na kumwangalia kwa hasira.
“Kaa mbali kabisa na maisha yangu. Sitaki matatizo. Kama umetumwa, mnajidanganya, mimi ni daktari kitaaluma, tena nimesoma nje ya nchi, mimi siyo bwege!” alisema Dk. Chris kwa hasira.
 
SEHEMU YA 16


ILIPOISHIA..ILIPOISHIA...
“Mimi ni daktari kitaaluma. Tena nimesoma nje ya nchi, mimi siyo bwege!” alisema Dk. Chris kwa hasira.
SASA ENDELEA...
CHRIS alikuwa anatetemeka kwa hasira. Kichwani mwake aliamini kwamba, Laura alikuwa akimchezea mchezo. Aliamini alikuwa kwenye mtego ili atapeliwe. Hakuwa tayari kwa jambo hilo hata kidogo. Chris alikuwa amefura kwa hasira.
Kitu ambacho hakukijua ni namna msichana yule alivyokuwa akimpenda. Alikuwa akimpenda kwa moyo wake wote, ndiyo maana alifunga safari kutokea Singida kumfuata yeye. Kilichompeleka Dar kilikuwa ni mapenzi tu!
Dk. Chris!
Hilo tu!
Hakutaka kulipa nafasi jambo hilo kichwani mwake. Alidhamiria kukaa naye mbali kabisa. Hisia za mapenzi zilishahama. Hakutaka kumuendekeza. Ramsey rafiki yake kipenzi, akamwangalia yule msichana kwa makini.
Alishawishika sana na urembo wake. Kwa stori za Chris kuhusu mwanamke aliyetaka kumwingiza kwenye matatizo mjini Singida, alianza kuamini kuwa ndiye aliyekuwa mbele yao. Alichokifanya ilikuwa ni kumtuliza rafiki yake kwanza...
“Kaka tulia tafadhali... lakini ni nani huyu msichana?” Ramsey akauliza kwa sauti ndogo.
“Ni yule mwanamke wa Singida niliyekuambia. Anataka kuniharibia maisha yangu huyu. Sikia wewe... umekosea njia, ondoka kwenye maisha yangu,” akasema Dk. Chris kwa hasira na sauti ya juu.
Laura alikuwa analia machozi. Hakuwa anaigiza, alikuwa analia machozi ya kweli kabisa...
Kama angekuwa mbele ya kamera akirekodi filamu, angekuwa amefanikiwa kuvaa uhusika katika kiwango cha mwisho kabisa. Laura aliweza kuonesha kilichotakiwa kufanyika. Lakini haikuwa hivyo... ilikuwa halisi.
Laura alikuwa analilia mapenzi!
“Chris nina kosa gani mimi? Wewe ndiye umekuja kwenye maisha yangu, ukasema unanipenda, nakiri kweli mwanzoni sikuwa na hisia hizo, lakini sasa nimegundua upendo wangu kwako, ndiyo maana nimetoroka chuoni na kuja huku kwa ajili yako.
“Nakupenda Chris. Nakupenda sana baba. Usinifikirie vibaya baba. Ni mapenzi tu. Nakupenda mpenzi wangu. Naomba unipe nafasi, nipe pumziko la moyo ndani yako...” maneno haya yalisikika huku machozi yakiendelea kutiririka machoni mwake.
“Acha uongo wewe... unajifanya mwanafunzi, wewe ni mwanafunzi au mke wa mtu? Nimesema sitaki mawasiliano yoyote na wewe.”
Laura akazidi kulia.
Chika, Katibu Mkuu wa Bongo Film Club, aliingilia kati. Alimshika mkono Laura, akamsihi anyamaze, akatulia kidogo. Chika akaanza kuzungumza: “Maneno ya huyu binti si ya kupuuzwa, anahitaji kusikilizwa. Tafadhali Chris, Ramsey na Jaybee naomba tuzungumze pembeni. Naamini tutapata ufumbuzi.”
“Sitaki!” Dk. Chris akajibu kwa hasira.
“Utataka!” Jaybee, mwenyekiti wa nidhamu wa klabu hiyo alisema.
Dk. Chris akanywea!
Isingekuwa rahisi hata kidogo kumpinga Jaybee, msanii mwenye jina kubwa na sauti Bongo Film Club. Heshima yake ndiyo hasa iliyosababisha akabidhiwe kofia ya kusimamia nidhamu klabuni hapo. Ramsey alijua alichotakiwa kufanya.
Alitoka na kusogea pembeni, Chika akafuta, Jaybee ndiye aliyekuwa wa kwanza akitangulizana na Laura. Dk. Chris akawa wa mwisho. Walitembea mpaka pembeni kidogo na kaunta iliyokuwa ndani. Wakaketi jirani na runinga.
“Wakati mwingine huwa inanilazimu kutumia ukali kidogo ili mambo yaende sawa. Sikuwa na lengo la kukudhalilisha ila nilipenda haya mambo yajadiliwe kwa staha na siri. Chris lazima tuzungumzie huku pembeni,” alisema Jaybee, safari hii kwa sauti tulivu.
“Nimekuelewa...” akasema Chris.
“Huyu msichana unamfahamu?”
“Ndiyo... lakini hafai huyu. Unajua...” akaanza kuzungumza kwa hasira lakini Jaybee akamkatiza.
“Tulia, swali nililokuuliza ni moja tu; unamfahamu?”
“Ndiyo.”
“Utapenda haya mambo tuzungumze pamoja au mtayajadili wenyewe?” akauliza tena Jaybee.
Dk. Chris alitulia kwa muda, alionekana akitafakari jambo kwa kina kidogo. Kichwa chake kilifanya kazi kama umeme. Pamoja na yote hayo, bado hakutaka mazungumzo yale yasikike na kila mtu. Haraka akajibu:
“Nataka tuzungumze mimi na yeye tu!”
“Si unaona mambo hayo?” Chika akasema na wote kwa pamoja wakasimama na kuwaacha Dk. Chris na Laura peke yao.
***
“Nataka uniambie ukweli, umeolewa au hujaolewa?”
Chris akamwuliza Laura.
“Mbona maajabu tena mpenzi wangu? Niolewe na nani sasa?”
“Jibu swali, wewe ni mke wa mtu au sivyo?”
“Sivyo. Sijaolewa mimi.”
“Ndiyo maana nakuambia unataka kunichezea mchezo... mbona mimi nilikuja kutafutwa na maaskari wakisema nimetembea na mke wa mtu... tena mke wa mkuu wa kituo?”
Itaendelea kesho....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom