INAENDELEA
"Mapenzi wivu bila wivu hakuna mapenzi ". Rahabu anaongea ndani ya nafsi. Hata yeye alitaka kuwa na wasiwasi iweje" baby "wake ashuhudie kitendo cha pale ATM kati yake na Rashid asishituke. Ndio maana alianza kuwa mdogo baada ya" baby" kuonyesha dalili za kutoguzwa na lolote. Lakini sasa anajiona yupo juu mithili ya kisoda. Maneno aliyoambiwa anayachukulia kama ushindi unaoashiria kwa kiasi gani mpenzi wake alivyomweka rohoni.
"Shukuru Kuna umuhimu wowote wa kurudi chuo?"
"Sikuelewi?"
"Namaanisha kwa nini tusiende kupumzika kwenye hotel usiku wa Leo. Mimi naona si vyema tukakaa na hizi pesa , ni vyema tuzitumie zote ziishe "
" Hilo neno, ila jiandae tusije tukafika nikajijukulia ushindi wa mezani maana kiwanja kigeni kisije kikawa kisingizio "
" Duuuhh, siku zote wewe si ndio hupoteza mechi na kuanza kutaja jina la Bibi yako leo unasema utashinda? "
" Haya tusubiri tuone nani zaidi " Shukuru anasema.
" Haya tutaona, maana leo nitazionyesha silaha zangu za maangamizi nilizozipata 'lukuledi' "
" Mimi nitakuonyesha kwa nini Kagera watu wazima kila siku wanaanika magodoro. Nitakuonyesha "katerero" na wazimu wake.
*************** ************ *********
Othman ameteseka mno. Moyo wake umezamilia kumweleza ukweli Bhoke. Kwa nini aumie kiasi hiki wakati dawa ipo. Kabla ya kwenda kwa Bhoke anaamua kutafuta undani wa Bhoke. Anaamua kumtumia Paul na Paul anakubali sababu wanasoma kozi moja na Bhoke.
Leo ndio siku ambayo Othman kaambiwa atapewa taarifa za Bhoke ili zimsaidie katika pambano lililo mbele yake.
"Hodi " Paul anagonga mlango wa chumba.
" Karibu " Othman anaitikia.
Paul anaingia ndani huku usoni wake ukiwa na bashasha. Baada ya kusalimia anaona asipoteze Muda
" Kaka hongera sana "
" Ahsante, lakini hongera ya nini? " Othman anaipokea na kuuliza.
" Habari nilizozipata ni kwamba Bhoke mbali ya kuwa ni binti mrembo hana makuu na anajiheshimu kwa namna ambayo sina Mfano wa kukupa. Lakini habari nzuri kwako ni kwamba kwa sasa yupo single. Huenda anafanya kwa siri tena siri kubwa. Hata hivyo naamini penzi ni kikohozi watu wangekuwa wanajua. Nakutia shime huenda wewe ndie ulieandaliwa kwa ajili yake " Paul anasema.
" Kwa maelezo yako huenda nafasi ikawa finyu ".
" Huenda ni kweli, huenda si kweli kweli. Mapenzi ni upofu, anaweza asione mwingine akawa kakuona wewe "
Paul anaendelea kumfahamisha Othman kuwa kuna Makuwadi wengi wanaowatafutia wenye hela zao viburudisho kwa Bhoke wamekwama. Si tu amewakatalia bali hata maneno yake yamekuwa mwiba mkali kwao. Wengi wamekuwa wakiondoka vichwa chini. Hali hii imewajaza hasira kubwa baadhi ya vibompa kiasi cha kuwa radhi kupanda Dau na kuweka mezani ofa kubwa kubwa kama gari na safari za Dubai, China na kwingine huko ughaibuni. Sijui anajiamini nini, labda masomo anayochukua. Maana watu wenye kusoma mambo yenye kuhusiana na hesabu "automatic" hali hii huwafanya wawe watu wa misimamo kama sio kusimamia kile wanacho kiamini.
Othman anamshukuru Paul na kumweleza atajipa ili ajue anatoka vipi. Paul anaaga na kuondoka. Anamwacha Othman akitafakari. Unyonge unaanza kumwingia. Maskini mie Sijui lini nitafanikisha. Duuuhh hii ligi ni ngumu na kweli mchezo huu hauhitaji hasira. Hata hivyo kwa mbali Kuna chembe chembe za ujasiri zinamwingia. Anasikia sauti kwa mbali inamwambia, "Siku zote Jemedali wa kweli hufia kwenye uwanja wa vita, ni aibu na fedheha kusita kufika uwanja wa mpambano.