Hadithi: Mmhh! Hata wewe mwanangu?

Hadithi: Mmhh! Hata wewe mwanangu?

Ngwananzengo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2012
Posts
1,911
Reaction score
1,320
Othmani anajilaza kitandani akiwa na lengo la kumsubiri rafiki yake Shukuru. Taratibu mawazo yanamrudisha nyuma miaka miwili iliyopita. Wakati akija kuanza masomo yake ya shahada ya Soshologi katika church cha MT. Augustino. Hakutegemea kama Muda ungeenda kwa kasi kiasi kile kiasi cha kufumba na kufumbua tayari yupo mwaka wa Tatu.

Mawazo yake yanakubaliana na ile methali ya wahenga, "Ukiona nyani Mzee porini basi jua kakwepa mikuki mingi". Ni mengi yametokea, yapo ya kutia moyo na kukatisha tamaa. Lakini kama ilivyo Ada ni wajibu wa kila mmoja kuyakabiri. Othmani akiwa katika kuwaza taratibu usingizi unampitia.

******* ******** *********

Ni siku nyingine inayowakutanisha Othmani, Shukuru na Rahabu. Wote hawa wapi mwaka wa Tatu wakisoma shahada ya Soshologi. Wamekaa kikao ili kupanga jinsi gani ya kuukabiri mwaka wao wa mwisho wa masomo. Pamoja na kwamba wote wanasoma pamoja Kuna kingine cha zaidi kinachowaunganisha wawe karibu. Othmani na Shukuru night marafiki wa dhati. Kwa sababu ya tabia zao kuendana urafiki wao uliongezeka na kuwa mithili ya ndugu.

Rahabu ambae ni mrembo kwa maana halisi ya urembo. Yeye ni mpenzi wa Shukuru. Rahabu ni binti mwenye sifa tele, macho yake mithili ya goroli, mwanya wa kishikaji bila kusahau "deenpose", umbo zuri lenye mvuto wa mahaba na nywele zake. Vyote kwa ujumla vimekuwa vikiwatia kiwewe wanaume na vijana wakwale.

Rahabu pamoja na uzuri ambao amejaaliwa anaamini elimu ndiyo inayoweza kumpa heshima. Anajituma kadri awezavyo ili aweze kufanikiwa.

******* ********* ********

Muafaka wa kikao chao ni kuongeza juhudi zaidi. Hii ni upande mmoja wa shilingi, upande wa pili Othmani ni mnyonge na hakuwa na amani rohoni. Aliwaza na kuwazua bila kupata jibu. Mapenzi ya Shukuru na Rahabu yalimfanya na yeye atamani kuwa na mpenzi. Amejitahidi kumpata ampendae lakini maskini hana bahati. Kila anapojaribu huwa anaangukia pua "Jamani nina mkosi gani mie". Kila Mara Othmani hujiuliza bila kupata jibu.

Tatizo hili ni kama kidonda ndugu katika moyo wa Othmani. Lakini nini Tatizo? Othmani amezaliwa na kukulia Kinondoni mtaa wa Mwinjuma karibu na Mango Garden. Fujo zote anazijua. Anajishangaa iweje aangukie pua kila Mara.

Mawazo yanamkumbusha jinsi Rhoda yule binti anaesoma sheria mwaka wa pili alivyomfanyia. Alianza vizuri kwa kupewa namba za simu, lakini cha kusikitisha na kushangaza alipoanza mashambulizi hakuamini yaliyomkuta. Yote tisa lakini kumi ni ule ujumbe aliotumiwa na Rhoda baada ya kuwa amefunguka. Ujumbe ule ulimtia simanzi na unyonge mwingi. Ndani ya ujumbe huo Rhoda aliamua kumpa za uso. Ujumbe ulikuwa hivi, "Wewe ni mtu wa aina gani usiejua kukataliwa. For me to be with you is a shame because I'm in next level"

Ilibidi akubaliane na hali halisi japo aliona kadharauliwa pakubwa. Hata hivyo hakuyumba katika masomo yake. Hasira zake alizimalizia katika kusoma.

******* ITAENDELEA.
 
SEHEMU YA PILI.

Shukuru na Rahabu wao mambo yao ni mazuri. Penzi lao kila uchao linazidi kuchanua. Kila mwisho wa juma wanapenda kwenda kutembelea sehemu tofauti tofauti. Shukuru na Othmani wanakaa chumba kimoja katika hosteli za Mkulima.

Ni majira ya saa tisa alasiri Rajabu amempitia mpenzi wake Shukuru ili wakatembee. Jumapili hii ni tulivu kabisa yenye jua kiasi. Nguo alizovaa Rahabu zimemkaa vizuri mithili ya mwanamitindo. Kafanya hivyo makusudi kuwachoma mioyo viforokwinyo ambao ni wabaya wake. Kila siku iendayo kwa Mungu hawaachi si tu kumsema bali kumwombea mabaya bali pia kumwingilia katika penzi lake. Japo hana ushahidi lakini wakati mwingine macho huwa yanaongea. Macho ya kina dada yamekuwa yakisema wazi kumtaka Shukuru.

Kwa jinsi Rahabu anavyompenda Shukuru wake hataki kabisa kuona hilo linatokea. Ndio maana yupo karibu na mtu wake akikaba hadi penalti. Anapofika kwenye mlango anabisha hadi.
"Hodi ndani ".
Rahabu anapoingia wote wanapigwa na butwaa. Ni kweli Rahabu ni mrembo wa nguvu kama sio haja. Lakini kwa namna alivyoupala leo amejiongezea 'credit'.
" Mbona hivyo jamani, hamnijui? " Rahabu anauliza.
" Tunakujua ila hongera sana, umependeza mno ndio maana tumekaa kimya kidogo kukuangalia " Othmani anajibu.
" Basi msinishangae, mkinishangaa nyinyi wengine itakuwaje? "
Baada ya mazungumzo kidogo Shukuru na Rahabu wanaafikiana waende Lakairo Hotel. Wanamuaga Othmani na kumwambia wataonana usiku.

******** ********** ***********

Usongo wa mawazo unamzidi Othmani baada ya rafiki yake kutoka na mpenzi wake wakiwa wamependeza na wenye furaha tele. Mawazo yanaanza kumsumbua. "Iweje Shukuru afanikiwe katika mapenzi yeye ashindwe?".

Anakumbuka likizo ya mwaka wa kwanza alivyomwomba Shukuru waende wote Dar es salaam. Shukuru hata Dar hakuwahi kufika kabla. Ni yeye ndie alimtembeza na kumwonyesha jiji. Alimtembeza maeneo yote muhimu Ikulu, Mlimani city, uwanja mkuu wa Taifa, soko la Kariakoo bila kusahau Bilicanas, San-siro, Travertine uwanja wa nyumbani wa mfalme na Jahazi yake na sehemu zingine. Lakini mbona yeye anachekelea ingali yeye akinuna.

Othmani anazidi kutafakari na kujiona kama mjinga. Anajidharau kutaka kumchukia rafiki yake bila sababu. Rafiki yake hajachangia kwa lolote linalofanya yeye kuangukia pua. Hiyo hali inajitokeza bila kupangwa. Anaanza kuyakemea mawazo yake, anaona ni mawazo mabaya yanayoweza kujenga chuki kati yao.

******** *********** ************

Shukuru na Rahabu wanapofika Lakairo Hotel wanaagiza vinywaji na utumbo wa kuchoma. Hotel hii inasifika sana kwa chakula Safi hasa mishikaki ya utumbo na samaki wa kuchoma. Wakiwa wanaendelea kunywa vinywaji anakuja bwana mmoja ambae anaonekana kiumri anatoka kwenye ujana, anaelekea kwenye utu uzima.
"Habari zenu jamani?" Anauliza.
"Nzuri " Shukuru anajibu.
" Samahani naomba niongee na wewe japo kidogo" Yule bwana anaongea
Shukuru anainuka na wanafuatana hadi pembeni.
"Samahani Kaka, yule dada nani yako? ".
" Yule ni rafiki yangu, tumekuja kujipumzisha"
"Hongera sana, anaonekana ni msichana mrembo "
" ahsante nashukuru "
" Wewe ni mwanaume kama mimi, naomba usijisikie vibaya kwa swali nililokuuliza "
" Hapana usijali " Shukuru anajibu.
Shukuru anarudi kwenye Meza yake na kukaa.
" Alikuwa anakwambia nini?" Rahabu anamuuliza Shukuru kwa hamu kubwa yenye kutaka kufahamu.

Kabla Shukuru hajajibu yule bwana anarudi kwenye meza yao na kusema "Nashukuru sana kuwafahamu, chukueni hiki kidogo mtaagiza mnachopenda". Ghafla yule bwana anatoa rundo la pesa na kuziweka mezani. Taratibu anaondoka na kuwaacha wakiwa wanashangaa.

Baada ya kupita sekunde kadhaa Shukuru anazichukua pesa na kuzihesabu. Haamini! ni laki tano. Anamueleza Rahabu namna alivyoongea nae. "Kuna nini nyuma ya hizi pesa?" Wote wanaanza kufikiri. Wanajifariji kwa kuamini hawajafanya lolote baya.

Baada ya dakika tano kupita wanaamua kukodi gari na kurudi chuo. Pamoja na kuianza siku yao vizuri wanaona wanaweza kuimaliza vibaya. Wote bado hawaelewi nia na dhamira ya yule bwana.
 
SEHEMU YA TATU.

Yule bwana aliewapa Shukuru na Rahabu laki tano ni Afisa Afisa mikopo wa benki moja maarufu hapa nchini. Jina lake ni Martini. Martini night mtu mwenye kupenda wasichana warembo. Kwa kutumia uwezo wake kifedha na kazi aliyonayo amekuwa akiwapata kwa ulahisi, mithili ya kusukuma mlevi. Wakati Shukuru na Rahabu wanaingia hotelini alikuwa wa kwanza kuwaona. Moyo wake uliwaka kwa tamaa ya kumtaka Rahabu. Hata hivyo alivyomwangalia Shukuru alimwona ni kijana mdogo, dhamira yake ya kumtaka Rahabu ilififia kwani kufanya hivyo aliona ni sawa na kumnyanyasa. Alihisi bado ni mwanachuo hivyo hivyo hakuona kama ni vizuri kushindana na mtu asie saizi yake.

Baadae nafsi ilimtuma walau awasalimie na kuwapa hongera. Na ndivyo alivyofanya. Pesa alizowapa alizitoa kwa moyo mweupe bila kinyongo chochote. Lengo lake lilikuwa ni kuona wanafurahia maisha. Na kama angekuwa anamfahamu Shukuru basi angehamia mezani kwao kwa kampani. Alisita kufanya hivyo kwa kuhisi atawaboa.

Kwa kifupi pamoja na ufedhuli wake Martin ni mtu anaependa mafanikio ya wengine. Kwake kuona mtu anafanikiwa iwe kiuchumi au hata katika masuala ya kijamii kama ilivyo kwenye mapenzi ni furaha kubwa. Kumwona Shukuru akiwa na mrembo wa kiwango cha Rahabu aliyachukulia ni mafanikio na alistahili kupigiwa makofi. Na kweli alimpigia makofi ya nguvu. Kitita cha laki tano alichowapa mithili ya mana si kidogo. Japo Shukuru hakujua kama anapigiwa makofi. Yeye aliamini kuna nia na dhamira mbaya iliyojificha nyuma ya hizo pesa. Hakuamini kwa hali ya maisha ilivyo mtu anaweza kutoa kitita chote hicho bila kuwa na kitu anachofaidi.

******** ******** **********
Siku zinazidi kwenda kwa kasi. Pamoja na kuzidi kufanya vizuri katika masomo yake Othman hana amani ndani ya nafsi yake. Hitaji la msingi ni kuwa na rafiki wa kike. Anaamini akimpata atakuwa amepata faraja kubwa. "Nianzie wapi safari hii?" anajiuliza ndani ya nafsi.

Kama wahenga walivyosema 'macho hayana pazia'. Jicho la Othman tayari lilikuwa limeshatua kwa binti mmoja anaesoma shahada ya uhasibu. Pamoja na kuangukia pua kila Mara,hakuwa mtu wa kumtaka yeyote atakae tokea. Yeye si mtu wa kupenda ligi ndogo. Anapenda mtu mwenye viwango. Binti ambae by ameanza kumvutia ni binti mrembo kweli kweli. Umbo lake ni la namba nane lenye mvuto unaokubali nguo na kila aina. Hips za nguvu, kiuno cha nyigu na kifua kisichochosha kukitazama ambacho kimebeba chuchu zenye kusisimua.

Binti huyu anaitwa Bhoke Nyangi na kwao ni Dar. Anaishi mtaa wa Mazongera nyuma ya TTC Chang'ombe karibu kabisa na Kivulini Pub.

******** ********* ******
 
SEHEMU YA NNE.

Kama ilivyo Ada Shukuru na Rahabu ni lazima watoke wakatembee kila jumapili Jumapili hii wameamua wakapumzike Tilapia hotel. Tilapia hotel ni karibu na Ziwa, lengo la kwenda hapo ni kuondoa uchovu wa wiki nzima kwa kupunga upepo. Rahabu kumuomba Shukuru wapitie ATM ya CRDB iliyopo barabara ya Nyerere. Bahati mbaya wanakuta mstari mrefu wa watu wenye kuhitaji huduma. Anaamua kupanga mstari huku mwenzie akisimama pembeni.

Rahabu akiwa amebakiza watu watatu aingie kwenye ATM, ghafla anavutwa pembeni ya mstari. "Samahani dada na pole kwa usumbufu. Nina haraka kidogo naomba unichukulie pesa. Kadi yangu hii hapa na password ni 6118". Kaka huyu alitamka maneno yenye kuomba lakini kauli yake ilionyesha ni amri.
"Unataka nikutolee kiasi gani? "
" Nitolee milioni moja ". Yule kaka akajibu.
Rahabu akaichukua kadi yake na kurudi kwenye mstari.
Aliingia kwenye ATM akatoka pesa kwenye akaunti yake kisha akamtolea yule kaka pesa yake. Alipotoka akasogea mbali kidogo na ATM. Yule kaka akamsogelea Rahabu sehemu aliposimama.
"Pesa na kadi yako hivi hapa" akaongea huku akikabidhi.
"Ahsante, una moyo mzuri kama sura yako" akajibu huku akimsifia.
"Samahani hivi unaitwa nani?"
"Naitwa Rahabu " Rahabu akajibu.
" Nashukuru kukufahamu, kama huna haraka naomba twende Golden Crest tukanywe japo juisi "
" Nashukuru sana, ratiba yangu imebana " Rahabu anajibu.
"Nakuomba upokee japo hii pesa utakunywa huko uendako" Kaka anatoa kiasi fulani cha na kumpa Rahabu. Anapoona anasita kuzichukua, anaziweka kwenye mkono wake na kukwambia, "Hii ni ahsante yangu". Pesa anamkabidhi pamoja na business card yake. Kwa hatua za taratibu anaenda kupanda gari.

Bila kuziweka hela kwenye pochi anatembea hadi kwa Shukuru. Anamkabidhi pesa alizopewa na yule kaka. Wanaondoka na kwenda kupanda taksi.

********* ********** ***********

Yule kaka aliempa Rahabu pesa anaitwa Rashid. Wakati Rashid akimtoa Rahabu kwenye mstari na kuongea nae Shukuru alikuwa akiona. Aliona pia jinsi Rashid alivyotoa pesa na kumkabidhi Rahabu.

Kwa kawaida Shukuru si mtu mwenye papara. Siku zote hujiamini na hakurupuki. Hakupenda kuyaingilia maongezi ya Rashid na mpenzi wake. Aliamua kutulia ili aone mwisho nini kitatokea. Aliona ni busara kusubiri ili baadae aje kuuliza, maana aliamini, "ukiishi karibu na bandari, usiogope honi za meli"

******** ******** ***********
Kutoka ilipo ATM hadi Tilapia hotel ni mwendo wa dakika tano. Wakiwa ndani ya gari Rahabu anatarajia kuulizwa na Shukuru yule kaka ni nani. Kwa bahati mbaya inakuwa kinyume chake. Shukuru haulizi chochote zaidi ya kushangaa jinsi watu walivyojaa stesheni ya gari Moshi.

Tilapia hoteli, wanapomaliza kumlipa dreva taksi wanaingia ndani na kwenda kukaa kwenye meza iliyo karibu na Ziwa. Baada ya kuagiza vinywaji Shukuru anaamua kuondoa ukimya kwa kuuliza swali.
"Zile pesa ulizonipa ni za nini? "
" Nilikupa uzitunze ili tukifika huku tuone ni za nini. "
" Kwani ni kiasi gani? "
" Sijui ni shilingi ngapi, labda uzihesabu. Mie nimezipokea na sikuzihesa "
" We, unadhani amekupa za nini? "
" Sijui,ila mwenyewe kasema ni ahsante ya kumtolea pesa ATM ". Shukuru anazitoa pesa na kuanza kuzihesabu.
" Ni laki mbili na nusu. " Anamwambia Rahabu.

********* ********* ********
 
SEHEMU YA TANO

Ni kweli Rashid alikuwa ameamua kumpa Rahabu laki mbili na nusu. Lakini Rashid ni mtu tofauti mno na Martin yule afisa mikopo. Martin alitoa pesa zake kwa lengo la kumpongeza mwanaume mwenzake kwa kung'oa binti mrembo wa nguvu. Hakuwa na nia nyingine zaidi.

Rashid kwa upande alitoa pesa kwa Nia ya kurusha chambo. Kwa mawazo na fikra anaamini pesa ndio kila kitu. Hategemea katika maisha ya kileo Kuna binti anaweza kuwa shujaa au jasiri dhidi ya pesa. Siku zote hujiuliza ni nani alie shujaa wa kukivuka kigingi hiki.

Rashid ana haki ya kuamini kile anachofikiri. Akiwa ni kijana mdogo mwenye umri wangu miaka the thelathini, ana mafanikio makubwa. Mwenyezi Mungu amemfungulia milango ya neema.

ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom