HADITHI: FATINAH (Kama Kuna Njia Ya Kuingia, Kuna Njia Ya Kutokea)

SEHEMU YA 6
Na Gwamaka Mwamasage 'Maestro'

SURA YA KUMI:RAHA NA KARAHA

Siku mbili mbele kama ilivyo ada nilikuwa ofisini kwangu nikipanga hili na lile ili mradi tu kutekeleza wazo la kibiashara nililopewa na Fatinah. Ilikuwa asubuhi tulivu kabisa yenye bashasha tele zilizonadiwa na kukuru kakara za vyombo vya moto vikienda na kurudi huku na huko, waenda kwa miguu pia hawakuwa nyuma katika harakati mbalimbali zenye kuwaletea mkate wao wa kila siku mezani mwao. Yote niliyashuhudia kupitia dirisha kubwa kiasi la ofisi yangu.
Mara nilipotuliza macho kwa mbali nikamuona Alex, ndio Alex Fyumagwa Afisa Masoko wa Kakakuona akishuka katika usafiri wa bajaji na kushika uelekeo kuielekea ofisi yangu. Nikajua huu mguu ni wangu.
Akajingia moja kwa moja na kukutana na Jully ofisi ya mapokezi, niliyasikia mazungumzo yao. Wakasalimiana na kabla Alex hajazungumza zaidi nikatoa amri ya ukaribisho kwa sauti kubwa toka ofisini kwangu. Akanisikia na kuingia.
"Almas...!!" Akasema baada ya kuingia
"Alex...!!" Nikamjibu nikimkaribisha kwa tabasamu pana na kusimama nikimpa mkono
"Ulijuaje ni mimi"
"Nimekuona tangu mbali Alex, tafadhali karibu uketi" nikamjibu nikimkaribisha naye akanipa mkono wa salamu na kuketi. Na baada ya soga mbili tatu;
"Ehee!!...jipya!!?" Nikafungua mazungumzo.
"Ni Bosi Said....Said Soud Mabrouk!" Akasema kwa mkato
"Ana jipya gani tena mwarabu wenu hahahaha" nikachagiza kwa masikhara
"Bosi Said amefurahishwa sana na biashara iliyofanyika baina yetu...baina yetu wewe, sisi na yeye!"
"Nashukuru..." Nikajibu nikijiweka sawa kitini tayari kupokea habari kamili huku tabasamu pana bado halijaachana na uso wangu. Kisha akaendelea;
"Bwana Said ameamua asikusumbue, safari hii atasimamia suala zima la manunuzi ya mazao, kwa pesa yake. Hataki utumie hata senti tano kutoka mifukoni mwako. Atatoa pesa, wewe ndio utajua ununue kwa bei gani na kiasi gani kitabaki ambacho ndio faida yako"
Sikutia neno lolote, nilimuacha aendelee.
Akaweka wazi pesa aliyotoa Bosi Said pamoja na muda ambao zoezi lingetakiwa kukamilika. Haikutakiwa kuzidi wiki moja tangu makubaliano ya kimkataba yakamilike.
"Na nyinyi mnajilipa vipi?" Hatimaye nikamtupia swali.
"Hii pesa niliyokutajia tumeshachukua pesa zetu na yeye anafahamu kwamba alitupatia pesa kiasi gani, tumechukua kiasi gani na wewe zimekufikia kiasi gani...tukikubaliana nitaandika barua pepe kumfahamisha ambapo nakala nitakutumia pia"
Nikatikisa kichwa kukubaliana na biashara. Biashara ya pesa nzuri kabisa. Niliridhika nayo.
"Kazi?"
"Kazi!"
Aliniuliza kama nakubali na mimi nikamjibu nakubali.
Kabla hajaondoka nikakumbuka jambo. Kwamba nakwenda kufanya maamuzi ya kibiashara bila uwepo wa mwanasheria wangu, Fatinah.
Alex akataka kuaga nikamzuia kwa ishara ya mkono huku mkono mwingine nimekamata simu, nikabofya namba za Fatinah nikampigia. Akapokea.
Baada ya nusu saa akafika ofisini kwangu. Nikamjulisha juu ya biashara aliyokuja nayo Alex.
"Kazi!?" Nikamuuliza Fatinah
"Kazi bosi" Akanijibu,Kama kawaida ndio hutumia lugha hii kuafikiana katika shughuli zetu. Tulishaizoea. Alex akaaga na kuondoka ili kuendelea na utaratibu wa miamala.
Tukabaki wawili mimi na Fatinah tu ofisini.
"Kwahiyo tunaendelea na ile biashara uliyonishauri ama nishughulike na hii kwanza" Nikazungumza mara tu baada ya Alex kutoka
"Almas...bosi wangu hakuna kulala, fanya kazi kama mtumwa uishi kama mfalme. Hizi biashara zote mbili ni lazima ziende pamoja" Akasema kwa msisitizo
Nilimsikiliza kwa makini sana, kwa kuwa nilitokea kumuamini sana huyu mlimbwende hivyo anapozungumza mara zote huwa namzingatia sana.
Akaendelea;
"Umeshafikiria japo kidogo tu ni kwa namna gani utaingiza faida kwa mkupuo?"
"Mama...mimi kwako nilishakuwa mfupa kwa fisi, wewe sema mimi nitafanya" Niliropokwa kwa utani lakini nikiwa makini zaidi.
"Nunua mzigo kwa pesa yako, kisha nunua mwingine kwa pesa yake, huo ulionunua kwa pesa yako unamuuzia kwa bei ile ile uliyomwambia umenunulia mzigo ule wa pesa yake" Akasema mwanasheria wangu.
Kama nilivyosema tangu mwanzo mpaka sasa sijapatapo kupingana na mawazo ya Fatinah, yuko sahihi siku zote.
"Kazi Bosi!?" Akaniuliza
"Kazi" Nikamjibu.
Jioni ya siku hiyo muamala ukaingizwa katika akaunti zangu za benki, na baada ya wiki mzigo ukatumwa, ule aliotuma hela ukaenda bure na ule nilioulipia akanilipa pesa zangu.
Maisha yalikuwa yanakwenda vizuri, maisha chini ya Fatinah yalikuwa matamu sana. Ungeweza kuona ni namna gani Almas natereza kama napita juu ya maganda ya ndizi.
Mwisho wa wiki ujao nikapanga kuwapeleka mahali yeye na Fatinah kama nilivyowaahidi mwanzo tukajipongeze kidogo, sehemu za starehe. Maana katikati ya wiki iliyokuwa inafuata ndio kuna siku ambayo mama angekuja kwa ajili ya kujipatia huduma ya afya yake ya kila baada ya miezi mitatu.
Na tangu wakati ule inapotokea nikiwa na Fatinah nikiongea na Mama basi Fatinah naye angeongea naye. Wakazoeana kabla hawajaonana.
Tulipanga tutoke siku ya jumamosi ili watu wapumzike siku ya jumapili kwa ajili ya kazi siku ya jumatatu. Hivyo jumamosi hiyo tulivu kabisa ilitukuta South Beach Kigamboni tukila, kunywa na kuogelea.
Jully na Fatinah waliutumia muda mwingi majini, mimi nilibaki nchi kavu nikifakamia vilevi, bahati mbaya huwa sinywi pombe mara kwa mara kwahiyo ilinichota akili haraka. Nilichangamka mapema sana.
Ilipofika alasiri nilikuwa hoi kwa kilevi.

Itaendelea...
 
Kwa hiyo baada ya kukosa wateja wa kununua kitabu UCHWARA umeamua kugawa Bure hadithi yako UCHWARA.
 
FATINAH

SEHEMU YA SANA

Inaendelea...

Saa 10 Alfajiri fahamu zilinirudia, nikafungua macho kwa kituo. Na kwa dakika kadhaa nikabaki nimetuamisha mwili wangu tu kuiruhusu akili yangu na mwili wangu vijipange katika utaratibu wake wa kawaida. Mwili ulijawa na uchovu tele. Mdomoni mwangu ilitawala harufu ya pombe za jana.
Kitambo kidogo kikapita nikitazama dari la chumba nilichokuwamo, haikuwa nyumba niliyoizoea, hapakuwa nyumbani kwangu, hakikuwa kitanda changu, halikuwa shuka langu na kila kilichokuwamo hakikuwa changu. Nikavuta kumbukumbu vizuri siku ya jana nilikuwa wapi na ikawaje. Matukio yakaanza kujipanga moja baada ya jingine. Nilipofikia moja ya tukio nikashtuka.
Nikatazama pembeni. Palikuwa na mtu mwingine. Mwanamke. Nikapigwa butwaa kama sio mshangao.
Nikajiinua kidogo sehemu ya kiwiliwili changu nimtambue huyo mwanamke.
"Fatinah...!!!" Nikajisemea kwa sauti ya chini. Tulikuwa ndani ya shuka moja!
"Khaa!" Kisha nikajikerehesha.
Yeye hakuwa na habari, alikuwa ametopea kwenye usingizi wa pono huku kageukia upande mwingine na kunipa mgongo. Nikafunua shuka kidogo kiasi cha kuruhusu sehemu ya miili yetu kuonekana kwa urahisi. Wote tulikuwa uchi wa mnyama.
"Tumefanya mapenzi!!" Yakanitoka tena kwa butwaa lililotukuka.
Nikamgusa bega kidogo ili kumuamsha, akashtuka toka usingizini akajinyoosha kidogo na kugeukia upande wangu. Kisha akafikicha kidogo macho yake kwa uchovu wa usingizi.
"Umemkaje kipenzi changu Almas..!" Akaongea kwa sauti ya chini bila kubabaika
"Kipenzi!!??" Mshangao ukaniponyoka kwa sauti ya chini vile vile huku nikiendelea kustaajabu, sikumjibu.
"Umeamka pensi la jeje?" Akasema, sikumuelewa.
"Pensi la jeje ndio nani?" Nikamuuliza nikiwa bado sielewi hali ya mambo ilivyo.
"Ulilewa Almas..." Akasema na kuinuka akaelekea maliwatoni. Hapo nikapata kulishuhudia lile umbo lake matata la kihaya lililositiriwa na ngozi nyeusi mororo kabisa, hakuwa japo na kipande cha khanga mwilini mwake na hakujali vile vile. Alijongea kuelekea maliwatoni kwa madaha yaliyotukuka. Kwa muda nikabaki nimesinyaa nikimtazama mpaka alipojongelea jumla. Kwisha kujisaidia akarudi na kujibwaga kitandani. Mimi bado nimeganda kama nyamafu tu, zumbukuku.
"Umesahau kuna jamaa alikuwa anaogelea amevaa bukta pana, ulicheka sana ukawa unamtania pensi la jeje?" Alisema huku anacheka sana.
"Pamoja na hayo Fatinah, Yaani kwako habari ya mimi kumtania mtu kuhusu bukta yake ndio habari kuliko hiki kilichotokea kati yangu na wewe hapa?" Nilizungumza kwa ukali karibia kumfokea.
"Kuna habari gani hapa Almas? Mimi na wewe? Kufanya mapenzi? Nilipanga, hainisumbui" akajibu akiwa mkavu kabisa, Niliingiwa na fadhaa kuu nisipate neno la kuzungumza.
"Kupanga au kutopanga sio habari sana, lakini hakuna mapenzi na kazi" Hatimaye nikabwata kwa hasira
"Tutaona" Fatinah hakuwa na mchecheto alinijibu kawaida kabisa.
"Almas mwanaume wangu kazi zilikuwepo kabla yako na utaziacha! Akaniongeza.
"Mwanaume wako? Tangu lini?" Hakujibu, akavuta shuka na kujifunika.
Mimi najijua, ghadhabu zinapopanda huziona tangu mbali na inapobidi kuzidhibiti huwa nafanya hivyo, labda niziruhusu tu. Kwa nafasi ya Fatinah kwangu sikutaka kuruhusu hasira, ilihitajika maamuzi ya busara, hivyo ilikuwa lazima nifanye jambo kisha nizungumze naye wakati mwingine nikiwa sina hasira tena. Halafu niliamini pia pengine anaendeshwa na kilevi, kikiisha tutazungumza lugha moja.
"Jully yuko wapi?" Nikamuuliza
"Chumba cha pili" akajibu akipiga miayo mfululizo kiasi kwamba nilitumia uzoefu tu kusikia alichosema. Nikamtazama kwa ghadhabu nikakosa maneno.
Baadae niligundua tulilala hapo hapo hotelini tuliposhinda siku nzima tukiburudika.
Nikatazama saa ya ukutani ilikuwa inakaribia saa 11 alfajiri. Nikazoa zoa mavazi yangu sakafuni nikavaa haraka bila kuzungumza jambo. Nikatoka na kuubamiza mlango, huko nyuma nikamsikia akiangua kicheko. Nikatamani nirudi ndani nimzabe japo kelbu mbili tatu, nikapiga moyo konde kuendelea na maamuzi yangu niliyoona ndio sahihi. Nikaondoka.

Itaendelea..

smart11 Panzi Mbishi moneytalk Duke Tachez Kelebe
 
FATINAH

SEHEMU YA SANA

Inaendelea...

Saa 10 Alfajiri fahamu zilinirudia, nikafungua macho kwa kituo. Na kwa dakika kadhaa nikabaki nimetuamisha mwili wangu tu kuiruhusu akili yangu na mwili wangu vijipange katika utaratibu wake wa kawaida. Mwili ulijawa na uchovu tele. Mdomoni mwangu ilitawala harufu ya pombe za jana.
Kitambo kidogo kikapita nikitazama dari la chumba nilichokuwamo, haikuwa nyumba niliyoizoea, hapakuwa nyumbani kwangu, hakikuwa kitanda changu, halikuwa shuka langu na kila kilichokuwamo hakikuwa changu. Nikavuta kumbukumbu vizuri siku ya jana nilikuwa wapi na ikawaje. Matukio yakaanza kujipanga moja baada ya jingine. Nilipofikia moja ya tukio nikashtuka.
Nikatazama pembeni. Palikuwa na mtu mwingine. Mwanamke. Nikapigwa butwaa kama sio mshangao.
Nikajiinua kidogo sehemu ya kiwiliwili changu nimtambue huyo mwanamke.
"Fatinah...!!!" Nikajisemea kwa sauti ya chini. Tulikuwa ndani ya shuka moja!
"Khaa!" Kisha nikajikerehesha.
Yeye hakuwa na habari, alikuwa ametopea kwenye usingizi wa pono huku kageukia upande mwingine na kunipa mgongo. Nikafunua shuka kidogo kiasi cha kuruhusu sehemu ya miili yetu kuonekana kwa urahisi. Wote tulikuwa uchi wa mnyama.
"Tumefanya mapenzi!!" Yakanitoka tena kwa butwaa lililotukuka.
Nikamgusa bega kidogo ili kumuamsha, akashtuka toka usingizini akajinyoosha kidogo na kugeukia upande wangu. Kisha akafikicha kidogo macho yake kwa uchovu wa usingizi.
"Umemkaje kipenzi changu Almas..!" Akaongea kwa sauti ya chini bila kubabaika
"Kipenzi!!??" Mshangao ukaniponyoka kwa sauti ya chini vile vile huku nikiendelea kustaajabu, sikumjibu.
"Umeamka pensi la jeje?" Akasema, sikumuelewa.
"Pensi la jeje ndio nani?" Nikamuuliza nikiwa bado sielewi hali ya mambo ilivyo.
"Ulilewa Almas..." Akasema na kuinuka akaelekea maliwatoni. Hapo nikapata kulishuhudia lile umbo lake matata la kihaya lililositiriwa na ngozi nyeusi mororo kabisa, hakuwa japo na kipande cha khanga mwilini mwake na hakujali vile vile. Alijongea kuelekea maliwatoni kwa madaha yaliyotukuka. Kwa muda nikabaki nimesinyaa nikimtazama mpaka alipojongelea jumla. Kwisha kujisaidia akarudi na kujibwaga kitandani. Mimi bado nimeganda kama nyamafu tu, zumbukuku.
"Umesahau kuna jamaa alikuwa anaogelea amevaa bukta pana, ulicheka sana ukawa unamtania pensi la jeje?" Alisema huku anacheka sana.
"Pamoja na hayo Fatinah, Yaani kwako habari ya mimi kumtania mtu kuhusu bukta yake ndio habari kuliko hiki kilichotokea kati yangu na wewe hapa?" Nilizungumza kwa ukali karibia kumfokea.
"Kuna habari gani hapa Almas? Mimi na wewe? Kufanya mapenzi? Nilipanga, hainisumbui" akajibu akiwa mkavu kabisa, Niliingiwa na fadhaa kuu nisipate neno la kuzungumza.
"Kupanga au kutopanga sio habari sana, lakini hakuna mapenzi na kazi" Hatimaye nikabwata kwa hasira
"Tutaona" Fatinah hakuwa na mchecheto alinijibu kawaida kabisa.
"Almas mwanaume wangu kazi zilikuwepo kabla yako na utaziacha! Akaniongeza.
"Mwanaume wako? Tangu lini?" Hakujibu, akavuta shuka na kujifunika.
Mimi najijua, ghadhabu zinapopanda huziona tangu mbali na inapobidi kuzidhibiti huwa nafanya hivyo, labda niziruhusu tu. Kwa nafasi ya Fatinah kwangu sikutaka kuruhusu hasira, ilihitajika maamuzi ya busara, hivyo ilikuwa lazima nifanye jambo kisha nizungumze naye wakati mwingine nikiwa sina hasira tena. Halafu niliamini pia pengine anaendeshwa na kilevi, kikiisha tutazungumza lugha moja.
"Jully yuko wapi?" Nikamuuliza
"Chumba cha pili" akajibu akipiga miayo mfululizo kiasi kwamba nilitumia uzoefu tu kusikia alichosema. Nikamtazama kwa ghadhabu nikakosa maneno.
Baadae niligundua tulilala hapo hapo hotelini tuliposhinda siku nzima tukiburudika.
Nikatazama saa ya ukutani ilikuwa inakaribia saa 11 alfajiri. Nikazoa zoa mavazi yangu sakafuni nikavaa haraka bila kuzungumza jambo. Nikatoka na kuubamiza mlango, huko nyuma nikamsikia akiangua kicheko. Nikatamani nirudi ndani nimzabe japo kelbu mbili tatu, nikapiga moyo konde kuendelea na maamuzi yangu niliyoona ndio sahihi. Nikaondoka.

Itaendelea..

smart11 Panzi Mbishi moneytalk Duke Tachez Kelebe
Nimefika bosi
 
FATINAH

SEHEMU YA SANA

Inaendelea...

Saa 10 Alfajiri fahamu zilinirudia, nikafungua macho kwa kituo. Na kwa dakika kadhaa nikabaki nimetuamisha mwili wangu tu kuiruhusu akili yangu na mwili wangu vijipange katika utaratibu wake wa kawaida. Mwili ulijawa na uchovu tele. Mdomoni mwangu ilitawala harufu ya pombe za jana.
Kitambo kidogo kikapita nikitazama dari la chumba nilichokuwamo, haikuwa nyumba niliyoizoea, hapakuwa nyumbani kwangu, hakikuwa kitanda changu, halikuwa shuka langu na kila kilichokuwamo hakikuwa changu. Nikavuta kumbukumbu vizuri siku ya jana nilikuwa wapi na ikawaje. Matukio yakaanza kujipanga moja baada ya jingine. Nilipofikia moja ya tukio nikashtuka.
Nikatazama pembeni. Palikuwa na mtu mwingine. Mwanamke. Nikapigwa butwaa kama sio mshangao.
Nikajiinua kidogo sehemu ya kiwiliwili changu nimtambue huyo mwanamke.
"Fatinah...!!!" Nikajisemea kwa sauti ya chini. Tulikuwa ndani ya shuka moja!
"Khaa!" Kisha nikajikerehesha.
Yeye hakuwa na habari, alikuwa ametopea kwenye usingizi wa pono huku kageukia upande mwingine na kunipa mgongo. Nikafunua shuka kidogo kiasi cha kuruhusu sehemu ya miili yetu kuonekana kwa urahisi. Wote tulikuwa uchi wa mnyama.
"Tumefanya mapenzi!!" Yakanitoka tena kwa butwaa lililotukuka.
Nikamgusa bega kidogo ili kumuamsha, akashtuka toka usingizini akajinyoosha kidogo na kugeukia upande wangu. Kisha akafikicha kidogo macho yake kwa uchovu wa usingizi.
"Umemkaje kipenzi changu Almas..!" Akaongea kwa sauti ya chini bila kubabaika
"Kipenzi!!??" Mshangao ukaniponyoka kwa sauti ya chini vile vile huku nikiendelea kustaajabu, sikumjibu.
"Umeamka pensi la jeje?" Akasema, sikumuelewa.
"Pensi la jeje ndio nani?" Nikamuuliza nikiwa bado sielewi hali ya mambo ilivyo.
"Ulilewa Almas..." Akasema na kuinuka akaelekea maliwatoni. Hapo nikapata kulishuhudia lile umbo lake matata la kihaya lililositiriwa na ngozi nyeusi mororo kabisa, hakuwa japo na kipande cha khanga mwilini mwake na hakujali vile vile. Alijongea kuelekea maliwatoni kwa madaha yaliyotukuka. Kwa muda nikabaki nimesinyaa nikimtazama mpaka alipojongelea jumla. Kwisha kujisaidia akarudi na kujibwaga kitandani. Mimi bado nimeganda kama nyamafu tu, zumbukuku.
"Umesahau kuna jamaa alikuwa anaogelea amevaa bukta pana, ulicheka sana ukawa unamtania pensi la jeje?" Alisema huku anacheka sana.
"Pamoja na hayo Fatinah, Yaani kwako habari ya mimi kumtania mtu kuhusu bukta yake ndio habari kuliko hiki kilichotokea kati yangu na wewe hapa?" Nilizungumza kwa ukali karibia kumfokea.
"Kuna habari gani hapa Almas? Mimi na wewe? Kufanya mapenzi? Nilipanga, hainisumbui" akajibu akiwa mkavu kabisa, Niliingiwa na fadhaa kuu nisipate neno la kuzungumza.
"Kupanga au kutopanga sio habari sana, lakini hakuna mapenzi na kazi" Hatimaye nikabwata kwa hasira
"Tutaona" Fatinah hakuwa na mchecheto alinijibu kawaida kabisa.
"Almas mwanaume wangu kazi zilikuwepo kabla yako na utaziacha! Akaniongeza.
"Mwanaume wako? Tangu lini?" Hakujibu, akavuta shuka na kujifunika.
Mimi najijua, ghadhabu zinapopanda huziona tangu mbali na inapobidi kuzidhibiti huwa nafanya hivyo, labda niziruhusu tu. Kwa nafasi ya Fatinah kwangu sikutaka kuruhusu hasira, ilihitajika maamuzi ya busara, hivyo ilikuwa lazima nifanye jambo kisha nizungumze naye wakati mwingine nikiwa sina hasira tena. Halafu niliamini pia pengine anaendeshwa na kilevi, kikiisha tutazungumza lugha moja.
"Jully yuko wapi?" Nikamuuliza
"Chumba cha pili" akajibu akipiga miayo mfululizo kiasi kwamba nilitumia uzoefu tu kusikia alichosema. Nikamtazama kwa ghadhabu nikakosa maneno.
Baadae niligundua tulilala hapo hapo hotelini tuliposhinda siku nzima tukiburudika.
Nikatazama saa ya ukutani ilikuwa inakaribia saa 11 alfajiri. Nikazoa zoa mavazi yangu sakafuni nikavaa haraka bila kuzungumza jambo. Nikatoka na kuubamiza mlango, huko nyuma nikamsikia akiangua kicheko. Nikatamani nirudi ndani nimzabe japo kelbu mbili tatu, nikapiga moyo konde kuendelea na maamuzi yangu niliyoona ndio sahihi. Nikaondoka.

Itaendelea..

smart11 Panzi Mbishi moneytalk Duke Tachez Kelebe
Mkuu imekuwaje tena??? Naona mzigo umekata..... T11
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom